Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 9 August 2013

Tamasha kubwa la muziki wa Injili kufanyika Washington DC kesho!!!!


 Waimbaji wanaofanya vema kwenye muziki wa Injili Afrika Mashariki, Upendo Kilahiro na Christina Shusho, watatumbuiza katika Tamasha kubwa la Injili litakalofanyika Jumamosi hii jijini Washington DC

 Kama walivyoongea kwenye VIDEO HII, waimbaji hao wamekamilisha maandalizi ya tamasha hilo ambalo pia litashirikisha waimbaji wenyeji wa hapa Marekani.
 

 Tamasha hilo kubwa lililo sehemu ya Maadhimisho ya miaka mitano ya kanisa la The Way of The Cross Gospel Ministries litafanyika siku ya Jumamosi kuanzia saa kumi kamili mpaka saa tatu usiku (6:00pm - 9:00pm) na kiingilio kwenye tamasha hilo kitakuwa ni dola kumi ($10) kwa watu wazima, bure kwa watoto.

 Anwani ambapo litapofanyika tamasha hilo ni

 The Way of the Cross Gospel Ministries 

 (at University United Methodist Church) 

 3621 Campus Drive 

 College Park, MD 20740 

 Kwa maelezo zaidi unaweza kuwasiliana na

 Mch. Ferdnand Shideko +1 240 476 6718 ama

 Ms Flora Mnkande +1 240 217 6335

 Waimbaji hawa wote watatumbuiza nyimbo zao za zamani na mpya na wanawaalika watu wote kujumuika nao na waimbaji wenyeji kuweza kupata BARAKA kwa njia hii ya uimbaji

   

   
Zaidi utayapata; http://www.changamotoyetu.blogspot.com
 http://www.youtube.com/user/mutwiba

No comments: