Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 11 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 52....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Yesu aliondoka mahali hapo akaenda kukaa katika sehemu za Tiro na Sidoni. Basi, mama mmoja Mkanaani wa nchi hiyo alimjia, akapaza sauti: “Bwana, Mwana wa Daudi, nionee huruma! Binti yangu anasumbuliwa na pepo.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Lakini Yesu hakumjibu neno. Basi, wanafunzi wake wakamwendea, wakamwambia, “Mwambie aende zake kwa maana anatufuatafuata akipiga kelele.” Yesu akajibu, “Sikutumwa ila kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.” Hapo huyo mama akaja, akamsujudia, akasema, “Bwana, nisaidie.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Yesu akamjibu, “Si vizuri kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.” Huyo mama akajibu, “Ni kweli, Bwana; lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka meza ya bwana wao.” Hapo Yesu akamjibu, “Mama, imani yako ni kubwa; basi, ufanyiwe kama unavyotaka.” Yule binti yake akapona wakati huohuo.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


Maangamizi ya Yerusalemu
(2Fal 24:18-25:7)
1Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala. Alitawala kwa muda wa miaka kumi na mmoja huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, mkazi wa mji wa Liba. 2Alitenda maovu mbele ya Mwenyezi-Mungu kama mabaya yote aliyotenda Yehoyakimu. 3Mwenyezi-Mungu aliwakasirikia sana watu wa Yerusalemu na Yuda hata akawafukuza mbali naye.
Sedekia alimwasi mfalme wa Babuloni. 4Ikawa katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, mwaka wa tisa wa kutawala kwake Sedekia, Nebukadneza mfalme wa Babuloni, alifika na jeshi lake lote kuushambulia Yerusalemu, wakauzingira kila upande. 5Mji uliendelea kuzingirwa mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia. 6Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ilikuwa kali sana mjini hata hapakuwa na chakula chochote kwa ajili ya wakazi wake. 7Basi, sehemu ya ukuta wa mji ilibomolewa, nao askari walikimbia wakatoka nje ya mji wakati wa usiku wakipitia njia ya lango katikati ya kuta mbili, kwenye bustani ya mfalme, wakaenda upande wa Araba, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji wote. Waisraeli walikimbia kuelekea bonde la mto Yordani. 8Lakini jeshi la Wakaldayo lilimfuatia mfalme na kumteka katika tambarare za Yeriko, jeshi lake lote likatawanyika na kumwacha. 9Basi Wakaldayo walimteka mfalme, wakampeleka kwa mfalme wa Babuloni, huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, naye akamhukumu. 10Hukohuko Ribla, mfalme wa Babuloni aliwaua wana wa Sedekia mbele ya baba yao. Aliwaua pia maofisa wote wa Yuda. 11Kisha aliyangoa macho ya Sedekia na kumfunga pingu, akamchukua Sedekia Babuloni na kumtia kizuizini mpaka siku alipokufa.
Kuharibiwa kwa hekalu
(2Fal 25:8-17)
12Katika siku ya kumi ya mwezi wa tano, mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza, mfalme wa Babuloni, Nebuzaradani kapteni wa walinzi wa mfalme ambaye alimtumikia mfalme wa Babuloni, aliingia Yerusalemu. 13Alichoma moto nyumba ya Mwenyezi-Mungu, ikulu na nyumba zote za Yerusalemu; kila nyumba kubwa ilichomwa moto. 14Askari wote wa Wakaldayo waliokuwa pamoja na kapteni wa walinzi, walizibomoa kuta zote zilizouzunguka mji wa Yerusalemu. 15Nebuzaradani kapteni wa walinzi wa mfalme, aliwachukua uhamishoni watu waliokuwa wamebakia mjini na wale waliokuwa wamejisalimisha kwa mfalme wa Babuloni pamoja na mafundi. 16Lakini Nebuzaradani kapteni wa walinzi wa mfalme, aliwaacha baadhi ya watu waliokuwa maskini kabisa nchini, wawe watunza mizabibu na wakulima.
17Wakaldayo walivunja vipandevipande nguzo za shaba nyeusi ambazo zilikuwa katika nyumba ya Mwenyezi-Mungu pamoja na vikalio na birika kubwa la shaba nyeusi lililokuwamo katika nyumba ya Mwenyezi-Mungu, wakaichukua shaba nyeusi yote mpaka Babuloni. 18Kadhalika, walichukua vyungu, sepetu, mikasi, makarai, vijiko vikubwa na vyombo vyote vya shaba nyeusi vilivyotumiwa katika huduma ya hekalu. 19Pia kapteni wa walinzi wa mfalme alichukua vibakuli, vyetezo, mabirika, vyungu, vinara vya taa, vijiko vikubwa na mabakuli ya sadaka za vinywaji, vyombo hivyo vikiwa vya dhahabu au vya fedha. 20Kuhusu vitu Solomoni alivyotengeneza: Nguzo mbili, birika kubwa moja na sanamu za fahali kumi na mbili za shaba nyeusi ambazo zilikuwa chini ya hilo birika kubwa pamoja na vikalio, shaba nyeusi ya vitu hivi vyote ilikuwa na uzito mwingi sana. 21Kila moja ya nguzo hizo mbili ilikuwa na urefu wa mita 8, mzingo wake mita 5.25, na unene wa milimita 75, zote zilikuwa wazi ndani. 22Juu ya kila nguzo kulikuwa na kichwa cha shaba nyeusi; urefu wa kila kichwa ulikuwa mita 2 na sentimita 20. Kila kichwa kilizungushiwa mapambo ya wavu ya makomamanga, yote ya shaba nyeusi. 23Kulikuwa na makomamanga tisini na sita ubavuni mwa nguzo hizo; jumla ya makomamanga yote ilikuwa 100 na mapambo kandokando yake.
Watu wa Yuda wanapelekwa Babuloni
(2Fal 25:18-21,27-30)
24Kisha Nebuzaradani kapteni wa walinzi wa mfalme, alimchukua mateka Seraya kuhani mkuu, na Sefania kuhani wa pili, pamoja na walinda mlango watatu; 25na kutoka mjini alimchukua ofisa mmoja ambaye alikuwa akiongoza askari vitani, pamoja na watu saba washauri wa mfalme ambao aliwakuta mjini. Kadhalika alimchukua katibu wa kamanda mkuu wa jeshi ambaye alitunza kumbukumbu za jeshi pamoja na watu mashuhuri sitini ambao aliwakuta mjini Yerusalemu. 26Nebuzaradani kapteni wa walinzi wa mfalme, aliwachukua watu hao na kuwapeleka kwa mfalme wa Babuloni huko Ribla. 27Mfalme Nebukadneza wa Babuloni aliwapiga na kuwaua watu hao huko Ribla katika nchi ya Hamathi.
Basi, watu wa Yuda walikwenda uhamishoni nje ya nchi yao. 28Ifuatayo ni idadi ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua uhamishoni mnamo mwaka wa saba wa utawala wake: Alichukua Wayahudi 3,023; 29mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, alichukua kutoka Yerusalemu mateka 832; 30mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Nebukadneza, Nebuzaradani kapteni wa walinzi wa mfalme, alichukua mateka Wayahudi 745. Jumla ya mateka wote ilikuwa watu 4,600.
31Mnamo mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda alipopelekwa uhamishoni, siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili, Evil-merodaki mfalme wa Babuloni, mwaka uleule alipofanywa mfalme, alimsamehe Yehoyakini mfalme wa Yuda, akamtoa gerezani. 32Aliongea naye vizuri na kumpa nafasi ya heshima kuliko wafalme wengine waliokuwa pamoja naye uhamishoni huko Babuloni. 33Basi, Yehoyakini alibadili mavazi yake ya kifungoni, akawa anapata chakula chake daima mezani kwa mfalme. 34Daima alipewa posho na mfalme wa Babuloni kulingana na mahitaji yake ya kila siku, mpaka alipofariki.


Yeremia52;1-34

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 10 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 51....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Petro akasema, “Tufafanulie huo mfano.” Yesu akasema, “Hata nyinyi hamwelewi? Je, hamwelewi kwamba kila kinachoingia kinywani huenda tumboni na baadaye hutolewa nje chooni?
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....
Lakini mambo yatokayo kinywani hutoka moyoni, na hayo ndiyo yanayomtia mtu unajisi.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Maana moyoni hutoka mawazo ya uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na kashfa. Hayo ndiyo yanayomtia mtu unajisi. Lakini kula chakula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


1Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Nitachochea upepo wa kuangamiza dhidi ya Babuloni,
dhidi ya wakazi wa Kaldayo.
2Nitawapeleka wapepetaji Babuloni,
nao watampepeta;
watamaliza kila kitu katika nchi yake
watakapofika kuishambulia toka kila upande
wakati wa maangamizi yake.”
3Usiwape nafasi wapiga mshale wa Babuloni;
usiwaache wavute upinde,
wala kuvaa mavazi yao ya vita.
Usiwahurumie vijana wake;
liangamize kabisa jeshi lake.
4Wataanguka na kuuawa katika nchi ya Wakaldayo,
watajeruhiwa katika barabara zake.
5Lakini Israeli na Yuda hawakuachwa na Mungu wao Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
ingawa nchi yao imejaa hatia mbele yake yeye Mtakatifu wa Israeli.
6Kimbieni kutoka Babuloni,
kila mtu na ayaokoe maisha yake!
Msiangamizwe katika adhabu yake,
maana huu ndio wakati wa Mungu wa kulipa kisasi,
anaiadhibu Babuloni kama inavyostahili.
7Babuloni ilikuwa kikombe cha dhahabu
mkononi mwa Mwenyezi-Mungu,
ambacho kiliilewesha dunia nzima.
Mataifa yalikunywa divai yake,
hata yakapatwa wazimu.
8Ghafla Babuloni imeanguka na kuvunjikavunjika;
ombolezeni kwa ajili yake!
Leteni dawa kutuliza maumivu yake;
labda utaweza kuponywa.
9Tulijaribu kuuponya Babuloni,
lakini hauwezi kuponywa.
Uacheni, twendeni zetu,
kila mmoja katika nchi yake,
maana hukumu yake ni kuu mno
imeinuka mpaka mawinguni.
10Mwenyezi-Mungu amethibitisha kuwa hatuna hatia.
Twendeni Siyoni tukatangaze
matendo ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu.
11Mwenyezi-Mungu amezichochea roho za wafalme wa Media, kwa maana amenuia kuiangamiza Babuloni. Naam, hicho ndicho kisasi cha Mwenyezi-Mungu; analipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake.
Noeni mishale yenu!
Chukueni ngao!
12Twekeni bendera ya vita
kushambulia kuta za Babuloni.
Imarisheni ulinzi;
wekeni walinzi;
tayarisheni mashambulizi.
Mwenyezi-Mungu amepanga na kutekeleza
mambo aliyosema juu ya wakazi wa Babuloni.
13Nchi hiyo imejaa mito na hazina tele,
lakini mwisho wake umefika,
uzi wa uhai wake umekatwa.
14Mwenyezi-Mungu wa majeshi ameapa kwa nafsi yake:
“Hakika nitakujaza majeshi mengi kama nzige,
nayo yatapiga vigelegele vya ushindi juu yako”
15Mwenyezi-Mungu ndiye aliyeumba dunia kwa nguvu yake,
aliyeuimarisha ulimwengu kwa hekima yake,
na kwa maarifa yake akazitandaza mbingu.
16Anapotoa sauti yake maji hutitima mbinguni,
hufanya ukungu upande kutoka mipaka ya dunia.
Hufanya umeme umulike wakati wa mvua
huvumisha upepo kutoka ghala zake.
17Kila mtu ni mpumbavu bila maarifa,
kila mhunzi anaaibishwa na vinyago vyake;
maana sanamu zake ni udanganyifu mtupu,
wala hazina pumzi ndani yake.
18Hazina thamani, ni udanganyifu mtupu;
wakati watakapoadhibiwa,
nazo zitaangamia.
19Mungu aliye hazina ya Yakobo si kama hizo,
maana yeye ndiye aliyeviumba vitu vyote,
na Israeli ni kabila lililo mali yake;
Mwenyezi-Mungu wa Majeshi, ndilo jina lake.
Mwisho wa Babuloni
20Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Wewe Babuloni ni rungu na silaha yangu ya vita;
nakutumia kuyavunjavunja mataifa,
nakutumia kuangamiza falme.
21Nakutumia kuponda farasi na wapandafarasi,
magari ya kukokotwa na waendeshaji wake.
22Ninakutumia kuwaponda wanaume na wanawake,
wazee na vijana,
wavulana na wasichana.
23Ninakutumia kuponda wachungaji na makundi yao,
wakulima na wanyama wao wa kulimia,
wakuu wa mikoa na madiwani.
24“Nitaiadhibu Babuloni na wakazi wote wa Kaldayo mkiona kwa macho yenu wenyewe, kwa sababu ya uovu wote walioufanya katika Siyoni. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
25Mimi ninapingana nawe ewe mlima mharibifu,
mlima unaoharibu dunia nzima!
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
Nitanyosha mkono wangu dhidi yako,
nitakuangusha kutoka miambani juu
na kukufanya kuwa mlima uliochomwa moto;
26hata hamna jiwe lako litakalochukuliwa kujengea,
hakuna jiwe litakalochukuliwa kuwekea msingi!
Utakuwa kama jangwa milele.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
27Tweka bendera ya vita duniani,
piga tarumbeta kati ya mataifa;
yatayarishe mataifa kupigana naye;
ziite falme kuishambulia;
falme za Ararati, Mini na Ashkenazi.
Weka majemadari dhidi yake;
walete farasi kama makundi ya nzige.
28Yatayarishe mataifa kupigana naye vita;
watayarishe wafalme wa Medi, watawala na mawakili wao,
tayarisheni nchi zote katika himaya yake.
29Nchi inatetemeka na kugaagaa kwa maumivu,
maana nia ya Mwenyezi-Mungu kuhusu Babuloni ni thabiti:
Ataifanya nchi ya Babuloni kuwa jangwa,
ataifanya iwe bila watu.
30Askari wa Babuloni wameshindwa kupigana,
wamebaki katika ngome zao;
nguvu zao zimewaishia,
wamekuwa kama wanawake.
Nyumba za Babuloni zimechomwa moto,
malango yake ya chuma yamevunjwa.
31Tarishi baada ya tarishi wanapiga mbio,
mjumbe mmoja anamfuata mjumbe mwingine,
kumpasha habari mfalme wa Babuloni
kwamba mji wake umevamiwa kila upande.
32Vivuko vya mto vimetekwa,
ngome zimechomwa moto,
askari wamekumbwa na hofu.
33Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli asema hivi:
“Babuloni ni kama uwanja wa kupuria nafaka
wakati unapotayarishwa.
Lakini bado kidogo tu,
wakati wa mavuno utaufikia.”
34Mfalme Nebukadneza wa Babuloni
aliuharibu na kuuponda mji wa Yerusalemu
aliuacha kama chungu kitupu;
aliumeza kama joka.
Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri,
akautupilia mbali kama matapishi.
35Watu wa Yerusalemu na waseme:
“Babuloni na ulipizwe ukatili uleule,
tuliotendwa sisi pamoja na jamaa zetu!
Babuloni ipatilizwe
kwa umwagaji wa damu yetu.”
Mwenyezi-Mungu atasaidia
36Kwa hiyo asema hivi Mwenyezi-Mungu:
“Nitawatetea kuhusu kisa chenu,
na kulipiza kisasi kwa ajili yenu.
Nitaikausha bahari ya Babuloni
na kuvifanya visima vyake vikauke.
37Babuloni itakuwa rundo la magofu,
itakuwa makao ya mbweha,
itakuwa kinyaa na kitu cha kuzomewa;
hakuna mtu atakayekaa huko.
38Wababuloni watanguruma pamoja kama simba;
watakoroma kama wanasimba.
39Wakiwa na uchu mkubwa
nitawaandalia karamu:
Nitawalewesha mpaka wapepesuke;
nao watalala usingizi wa daima
na hawataamka tena.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
40Nitawashusha chini kama kondoo wa kuchinjwa,
kama vile kondoo dume na beberu.
41Ajabu kutekwa kwa Babuloni;
mji uliosifika duniani kote umechukuliwa!
Babuloni umekuwa kinyaa kati ya mataifa!
42Bahari imefurika juu ya Babuloni,
Babuloni imefunikwa mawimbi yaliyochafuka.
43Miji yake imekuwa kinyaa,
nchi ya ukavu na jangwa,
nchi isiyokaliwa na mtu yeyote,
wala kupitika na binadamu yeyote.
44Nitamwadhibu mungu Beli huko Babuloni,
nitamfanya akitoe alichokimeza.
Mataifa hayatamiminika tena kumwendea.
Ukuta wa Babuloni umebomoka.
45“Tokeni humo enyi watu wangu!
Kila mtu na ayasalimishe maisha yake,
kutoka hasira kali ya Mwenyezi-Mungu.
46Msife moyo wala msiwe na hofu,
kwa sababu ya uvumi mnaosikia nchini.
Mwaka huu kuna uvumi huu,
mwaka mwingine uvumi mwingine;
uvumi wa ukatili katika nchi,
mtawala mmoja dhidi ya mtawala mwingine.
47Kweli siku zaja,
nitakapoadhibu sanamu za Babuloni;
nchi yake yote itatiwa aibu,
watu wake wote watauawa humohumo.
48Kisha mbingu, dunia na vyote vilivyomo
vitaimba kwa furaha kuhusu kuanguka kwa Babuloni,
waangamizi watakapofika kutoka kaskazini kuushambulia.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
49Babuloni umesababisha vifo duniani kote;
sasa wenyewe utaangamizwa kwa mauaji ya Israeli.
50“Nyinyi mlinusurika kifo,
ondokeni sasa, wala msisitesite!
Ingawa mko nchi ya mbali mkumbukeni Mwenyezi-Mungu,
ukumbukeni pia mji wa Yerusalemu.
51Mnasema: ‘Tumeaibishwa na kufadhaishwa;
aibu imezifunika nyuso zetu,
kwa sababu wageni wameingia
katika sehemu takatifu za nyumba ya Mwenyezi-Mungu.’
52“Kwa hiyo, wakati unakuja,
nasema mimi Mwenyezi-Mungu,
ambapo nitaviadhibu vinyago vya Babuloni,
na majeruhi watapiga kite katika nchi yake yote.
53Ingawa Babuloni atapanda mpaka mbinguni,
na kuziimarisha ngome zake ndefu,
waangamizi watakuja kutoka kwangu kumvamia.
2Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
Maangamizi zaidi juu ya Babuloni
54“Sikiliza! Kilio kinasikika kutoka Babuloni!
Kishindo cha maangamizi makubwa
kutoka nchi ya Wakaldayo!
55Maana mimi Mwenyezi-Mungu naiangamiza Babuloni,
na kuikomesha kelele yake kubwa.
Adui ananguruma kama mawimbi ya maji mengi,
sauti ya kishindo chao inaongezeka.
56Naam, mwangamizi anaijia Babuloni;
askari wake wametekwa,
pinde zao zimevunjwavunjwa.
Mimi Mwenyezi-Mungu ni Mungu mwenye kuadhibu,
hakika mimi nitalipiza kisasi kamili.
57Nitawalewesha wakuu na wenye hekima wake,
watawala wake, madiwani na askari wake;
watalala usingizi wa milele wasiinuke tena.
Nasema mimi mfalme ambaye jina langu ni Mwenyezi-Mungu wa Majeshi.
58“Mimi Mwenyezi-Mungu wa Majeshi nasema:
Ukuta mpana wa Babuloni
utabomolewa mpaka chini,
na malango yake marefu
yatateketezwa kwa moto.
Watu wanafanya juhudi za bure,
mataifa yanajichosha maana mwisho wao ni motoni!”
Ujumbe wa Yeremia unapelekwa Babuloni
59Mnamo mwaka wa nne wa utawala wake, mfalme Sedekia alikwenda Babuloni pamoja na ofisa wa askari wake aitwaye Seraya mwana wa Neria na mjukuu wa Maseya. Kutokana na fursa hiyo mimi Yeremia nilimpa Seraya ujumbe. 60Nilikuwa nimeandika kitabuni maafa yote niliyotangaza juu ya Babuloni na pia maneno mengine kuhusu Babuloni. 61Nilimwambia Seraya: “Utakapofika Babuloni ni lazima uwasomee wote ujumbe huu. 62Kisha umalizie na maneno haya: ‘Ee Mwenyezi-Mungu, wewe umesema kwamba utapaharibu mahali hapa hata pasikaliwe na kiumbe chochote, mwanadamu au mnyama, na kwamba nchi hii itakuwa jangwa milele.’ 63Utakapomaliza kusoma kitabu hiki, kifungie jiwe, kisha ukitumbukize katikati ya mto Eufrate, ukisema: 64‘Hivi ndivyo mji wa Babuloni utakavyozama, wala hautainuka tena, kwa sababu ya maafa ambayo Mwenyezi-Mungu anauletea.’”51:64 anauletea: Kiebrania: Anayouletea, nao watachoka. Mwisho wa maneno ya Yeremia.


Yeremia51;1-64

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 7 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 50....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

‘Mungu asema: Watu hawa huniheshimu kwa maneno tu, lakini mioyoni mwao wako mbali nami. Kuniabudu kwao hakufai, maana mambo wanayofundisha ni maagizo ya kibinadamu tu.’”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Yesu aliuita ule umati wa watu, akawaambia, “Sikilizeni, mkaelewe! Kitu kinachomtia mtu unajisi si kile kiingiacho kinywani, bali kile kitokacho kinywani. Hicho ndicho kimtiacho mtu unajisi.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Kisha wanafunzi wakamwendea, wakamwambia, “Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa waliposikia maneno yako?” Lakini yeye akawajibu, “Kila mmea ambao Baba yangu aliye mbinguni hakupanda, utangolewa. Waacheni wenyewe! Wao ni vipofu, viongozi wa vipofu; na kipofu akimwongoza kipofu, wote wawili hutumbukia shimoni.”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Babuloni
1Neno la Mwenyezi-Mungu alilosema kwa njia ya nabii Yeremia kuhusu nchi ya Babuloni na nchi ya Wakaldayo:
2“Tangazeni kati ya mataifa,
twekeni bendera na kutangaza,
Msifiche lolote. Semeni:
‘Babuloni umetekwa,
Beli ameaibishwa.
Merodaki amefadhaishwa;
sanamu zake zimeaibishwa,
vinyago vyake vimefadhaishwa.’
3“Kwa maana, taifa kutoka kaskazini limefika kuushambulia; litaifanya nchi yake kuwa uharibifu. Hakuna atakeyeishi humo; watu na wanyama watakimbia mbali.
Kurudi kwa Israeli
4“Siku hizo na wakati huo, nasema mimi Mwenyezi-Mungu, watu wa Israeli na watu wa Yuda watakusanyika pamoja na kurudi wakilia huku wananitafuta mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao. 5Watauliza njia ya kwenda Siyoni, huku nyuso zao zimeelekea huko, wakisema, ‘Njoni!’ Nao watajiunga na Mwenyezi-Mungu katika agano la milele ambalo kamwe halitasahauliwa.
6“Watu wangu walikuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha, wakawageuza kuelekea milimani; walitembea toka mlima hadi kilima, wakasahau zizi lao. 7Watu wote waliowakuta waliwaua, na maadui zao wamesema, ‘Hatuna hatia sisi’, maana hao wamemkosea Mwenyezi-Mungu aliye malisho yao ya kweli; Mwenyezi-Mungu ambaye ni tegemeo la wazee wao!
8“Kimbieni kutoka Babuloni! Tokeni nje ya nchi ya Wakaldayo, muwe kama mabeberu mbele ya kundi. 9Maana, mimi nitachochea mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini washambulie Babuloni. Watajiandaa kuishambulia Babuloni na kuiteka. Mishale yao ni kama shujaa hodari asiyerudi mikono mitupu. 10Nchi ya Wakaldayo itaporwa, na hao watakaoipora wataridhika. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
Kuanguka kwa Babuloni
11“Enyi waporaji wa mali yangu!
Japo mnafurahi na kushangilia,
mnarukaruka kama mtamba wa ng'ombe anayepura nafaka,
na kulia kama farasi dume,
12nchi yenu ya kuzaliwa itaaibishwa;
hiyo nchi mama yenu itafedheheshwa.
Lo! Babuloni itakuwa ya mwisho kati ya mataifa,
itakuwa nyika kame na jangwa.
13Kwa sababu ya ghadhabu yangu Mwenyezi-Mungu,
Babuloni haitakaliwa kabisa na watu,
bali itakuwa jangwa kabisa;
kila atakayepita karibu nayo atashangaa
ataizomea kwa sababu ya majeraha yake.
14“Enyi nyote wapiga mishale stadi,
shikeni nafasi zenu kuuzingira mji wa Babuloni;
upigeni, msibakize mshale hata mmoja,
maana umenikosea mimi Mwenyezi-Mungu.
15Upigieni kelele za vita pande zote,
sasa Babuloni umejitoa ukamatwe.
Ngome zake zimeanguka,
kuta zake zimebomolewa.
Ninalipiza kisasi juu ya Babuloni
Basi jilipizeni kisasi,
utendeeni kama ulivyowatenda wengine.
16Zuieni watu wasipande mbegu Babuloni,
wala wasivune wakati wa mavuno.
Kutokana na upanga wa udhalimu,
kila mmoja atawarudia watu wake
kila mmoja atakimbilia nchini mwake.
17“Israeli ni kondoo wanaowindwa na kufukuzwa na simba. Kwanza waliangamizwa na mfalme wa Ashuru, na sasa Nebukadneza mfalme wa Babuloni, amevunjavunja mifupa yake. 18Kwa hiyo, mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, nasema hivi: Nitamwadhibu mfalme wa Babuloni na nchi yake, kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru. 19Nitawarudisha Waisraeli nchini mwao, nao watakula mavuno yatakayolimwa juu ya mlima Karmeli na Bashani na watatosheka kwa chakula kutoka milima ya Efraimu na Gileadi. 20Siku hizo na wakati huo, uovu utatafutwa nchini Israeli, lakini hautapatikana; dhambi itatafutwa nchini Yuda, lakini haitapatikana; maana mimi nitawasamehe wale ambao nimewabakiza. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
21“Pandeni, mwiendee nchi ya Merathaimu,
nendeni kuishambulia;
washambulieni wakazi wa Pekodi
na kuwaangamiza kabisa watu wake.
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
22Kelele za vita zinasikika nchini,
kuna uharibifu mkubwa.
23Jinsi gani huo mji uliokuwa nyundo ya dunia nzima
unavyoangushwa chini na kuvunjika!
Babuloni umekuwa kinyaa
miongoni mwa mataifa!
24Ewe Babuloni, nilikutegea mtego ukanaswa,
wala hukujua juu yake;
ulipatikana, ukakamatwa,
kwa sababu ulishindana nami Mwenyezi-Mungu.
25Nimefungua ghala yangu ya silaha,
nikatoa humo silaha za ghadhabu yangu,
maana mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi
nina kazi ya kufanya
katika nchi ya Wakaldayo.
26Njoni mkamshambulie kutoka kila upande;
zifungueni ghala zake za chakula;
mrundikieni marundo ya nafaka!
Iangamizeni kabisa nchi hii;
msibakize chochote!
27Waueni askari wake hodari;
waache washukie machinjoni.
Ole wao, maana siku yao imewadia,
wakati wao wa kuadhibiwa umefika.
28“Sikiliza! Wakimbizi na watoro kutoka nchi ya Babuloni wanakuja kutangaza huko Siyoni jinsi Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, alivyolipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake.
29“Waiteni wapiga mishale waishambulie Babuloni. Pelekeni kila mtu ajuaye kuvuta upinde. Uzingireni mji pasiwe na yeyote atakayetoroka. Ulipizeni kadiri ya matendo yake yote; utendeeni kama ulivyowatendea wengine, maana kwa kiburi ulinidharau mimi Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wa Israeli. 30Kwa hiyo, vijana wake watauawa katika mitaa yake, na majeshi yake yote yataangamizwa siku hiyo. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
31“Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
napigana nawe ewe mwenye kiburi,
maana siku yako ya adhabu imefika,
wakati nitakapokuadhibu umewadia.
32Mwenye kiburi atajikwaa na kuanguka,
wala hapatakuwa na mtu wa kumwinua.
Nitawasha moto katika miji yake,
nao utateketeza kila kitu kandokando yake.”
33Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: “Watu wa Israeli wanakandamizwa; hali kadhalika na watu wa Yuda. Wale waliowachukua mateka wamewabana sana na wanakataa kuwaachia. 34Lakini mimi, Mkombozi wao ni mwenye nguvu. Mwenyezi-Mungu wa Majeshi ndilo jina langu. Hakika nitatetea kisa chao ili nilete amani katika nchi yao, lakini taabu kwa wakazi wa Babuloni.
35“Kifo kwa Wakaldayo,
kwa wakazi wa Babuloni
na maofisa na wenye hekima wake!
36Kifo kwa waaguzi,
wanachotangaza ni upumbavu tu!
Kifo kwa mashujaa wake,
ili waangamizwe!
37Kifo kwa farasi wake na uharibifu kwa magari yake,
kifo kwa majeshi yake yote ya kukodiwa,
ili wawe na woga kama wanawake!
Uharibifu kwa hazina zake zote
ili zipate kuporwa.
38Ukame uyapate maji
ili yapate kukauka!
Maana Babuloni ni nchi ya sanamu za miungu,
watu ni wendawazimu juu ya vinyago vyao.
39“Kwa hiyo wanyama wa porini, mbwamwitu pamoja na mbuni, watakaa Babuloni. Hapatakaliwa kamwe na watu vizazi vyote vijavyo. 40Kama vile mimi Mwenyezi-Mungu nilivyoiangamiza miji ya Sodoma na Gomora na miji ya jirani, vivyo hivyo hapatakuwa na mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakeyekaa huko. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
41“Tazama! Watu wanakuja kutoka kaskazini;
taifa lenye nguvu na wafalme wengi
wanajitayarisha kutoka miisho ya dunia.
42Wameshika pinde zao na mikuki;
ni watu wakatili na wasio na huruma.
Vishindo vyao ni kama mvumo wa bahari,
wamepanda farasi.
Wamejipanga tayari kwa vita,
dhidi yako wewe Babuloni!
43Mfalme wa Babuloni amesikia habari zao,
nayo mikono yake ikawa kama kamba.
Ameshikwa na dhiki na uchungu kama mama anayejifungua.
44“Tazama, mimi nitakuwa kama simba anayechomoza kutoka msitu wa mto Yordani na kuingia kwenye malisho mazuri: Mimi Mwenyezi-Mungu nitawafukuza ghafla watu wake kutoka kwake. Nami nitamweka huko kiongozi yeyote nitakayemchagua. Maana, ni nani anayeweza kulinganishwa nami? Nani awezaye kunishtaki? Ni mchungaji gani awezaye kunipinga? 45Kwa hiyo, sikilizeni mpango ambao mimi Mwenyezi-Mungu nimepanga dhidi ya Babuloni pamoja na mambo niliyokusudia kuitendea nchi ya Wakaldayo: Hakika watoto wao wataburutwa na kuchukuliwa; kweli kutakuwa na mshangao mkubwa katika makao yao. 46Kwa kishindo cha kutekwa kwa Babuloni dunia itatetemeka, na kilio chake kitasikika miongoni mwa mataifa mengine.”


Yeremia50;1-46

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.