Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 14 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Maombolezo 3....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!


Yesu alianza kufundisha tena akiwa kando ya ziwa. Umati mkubwa wa watu ulimzunguka hata ikambidi aingie katika mashua na kuketi. Watu wote wakawa wamekaa katika nchi kavu, kando ya ziwa. Aliwafundisha mambo mengi kwa mifano, na katika mafundisho yake aliwaambia,
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


“Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu. Alipokuwa akipanda mbegu, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila. Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi, zikaota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina. Jua lilipochomoza, zikateketea; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga, nazo hazikuzaa nafaka. Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikamea, zikakua na kuzaa: Moja punje thelathini, moja sitini na nyingine mia.” Kisha akawaambia, “Mwenye masikio na asikie!”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Adhabu, toba na tumaini
1Mimi ni mtu niliyepata mateso
kwa fimbo ya ghadhabu yake Mungu.
2Amenichukua akanipeleka
mpaka gizani kusiko na mwanga.
3Amenyosha mkono wake dhidi yangu mimi tu,
akanichapa tena na tena mchana kutwa.
4Amenichakaza ngozi na nyama,
mifupa yangu ameivunja.
5Amenizingira na kunizungushia
uchungu na mateso.
6Amenikalisha gizani
kama watu waliokufa zamani.
7Amenizungushia ukuta nisitoroke,
amenifunga kwa minyororo mizito.
8Ingawa naita na kulilia msaada
anaizuia sala yangu isimfikie.
9Njia zangu ameziziba kwa mawe makubwa
amevipotosha vichochoro vyangu.
10Yeye ni kama dubu anayenivizia;
ni kama simba aliyejificha.
11Alinifukuza njiani mwangu,
akanilemaza na kuniacha mkiwa.
12Aliuvuta upinde wake,
akanilenga mshale wake.
13Alinichoma moyoni kwa mishale,
kutoka katika podo lake.
14Nimekuwa kitu cha dhihaka kwa watu wote,
mchana kutwa nimekuwa mtu wa kuzomewa.
15Amenijaza taabu,
akanishibisha uchungu.
16Amenisagisha meno katika mawe,
akanifanya nigaegae majivuni.
17Moyo wangu haujui tena amani,
kwangu furaha ni kitu kigeni.
18Nimewaza “Nimekata tamaa kabisa,
tumaini langu kwa Mwenyezi-Mungu limetoweka.”
19Kukumbuka taabu na kutangatanga kwangu
kwanipa uchungu kama wa nyongo.
20Nayafikiria hayo daima,
nayo roho yangu imejaa majonzi.
21Lakini nakumbuka jambo hili moja,
nami ninalo tumaini:
22Kwamba fadhili za Mwenyezi-Mungu hazikomi,
huruma zake hazina mwisho.
23Kila kunapokucha ni mpya kabisa,
uaminifu wake ni mkuu mno.
24Mwenyezi-Mungu ndiye hazina yangu
hivyo nitamwekea tumaini langu.
25Mwenyezi-Mungu ni mwema kwa wanaomtegemea,
ni mwema kwa wote wanaomtafuta.
26Ni vema mtu kungojea kwa saburi
ukombozi utokao kwa Mwenyezi-Mungu.
27Ni vema mtu kujifunza uvumilivu
tangu wakati wa ujana wake.
28Heri kukaa peke na kimya,
mazito yanapompata kutoka kwa Mungu.
29Yampasa kuinama na kujinyenyekesha,
huenda ikawa tumaini bado lipo.
30Yampasa kumgeuzia shavu mwenye kumpiga,
na kuwa tayari kupokea matusi yake.
31Mwenyezi-Mungu hatatutupa milele.
32Ingawa atufanya tuhuzunike,
atakuwa na huruma tena
kadiri ya wingi wa fadhili zake.
33Yeye hapendelei kuwatesa
wala kuwahuzunisha wanadamu.
34Wafungwa wote nchini
wanapodhulumiwa na kupondwa;
35haki za binadamu zinapopotoshwa
mbele yake Mungu Mkuu,
36kesi ya mtu inapopotoshwa mahakamani,
je, Mwenyezi-Mungu haoni hayo?
37Nani awezaye kuamuru kitu kifanyike
Mwenyezi-Mungu asipopanga iwe hivyo?
38Maafa na mema hutokea tu
kwa amri yake Mungu Mkuu.
39Kwa nini mtu anung'unike,
ikiwa ameadhibiwa kwa dhambi zake?
40Na tupime na kuchunguza mwenendo wetu,
tupate kumrudia Mwenyezi-Mungu.
41Tumfungulie Mungu huko mbinguni
mioyo yetu na kumwomba:
42“Sisi tulikukosea na kukuasi
nawe bado hujatusamehe.
43“Umejizungushia hasira yako ukatufuatia,
ukatuua bila huruma.
44Umejizungushia wingu zito,
sala yeyote isiweze kupenya humo.
45Umetufanya kuwa takataka na uchafu
miongoni mwa watu wa mataifa.
46“Maadui zetu wote wanatuzomea.
47Kitisho na hofu vimetuandama,
tumepatwa na maafa na maangamizi.
48Macho yangu yabubujika mito ya machozi
kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu.
49“Machozi yatanitoka bila kikomo,
50mpaka Mwenyezi-Mungu kutoka huko mbinguni
aangalie chini na kuona.
51Nalia na kujaa majonzi,
kuona yaliyowapata kina mama wa mji wangu.
52“Nimewindwa kama ndege
na hao wanichukiao bila sababu.
53Walinitupa shimoni nikiwa hai
na juu yangu wakarundika mawe.
54Maji yalianza kunifunika kichwa,
nami nikafikiri, ‘Huu ni mwisho wangu.’
55“Kutoka chini shimoni
nilikulilia ee Mwenyezi-Mungu.
56Wewe umenisikia nikikulilia:
‘Usiache kusikia kilio changu cha msaada
bali unipatie nafuu.’
57Nilipokuita ulinijia karibu
ukaniambia, ‘Usiogope!’
58“Umenitetea katika kisa changu ee Mwenyezi-Mungu,
umeyakomboa maisha yangu.
59Umeuona uovu niliotendewa ee Mwenyezi-Mungu,
uniamulie kwa wema kisa changu.
60Umeuona uovu wa maadui zangu,
na mipango yao yote ya hila dhidi yangu.
61“Umesikia matukano yao ee Mwenyezi-Mungu,
na mipango yao yote ya hila dhidi yangu.
62Maneno na mawazo ya maadui zangu siku nzima
ni juu ya kuniangamiza mimi.
63Wakati wote, wamekaa au wanakwenda,
mimi ndiye wanayemzomea.
64Uwalipize, ee Mwenyezi-Mungu
kadiri ya hayo matendo yao,
kadiri ya mambo waliyotenda wenyewe.
65Uipumbaze mioyo yao,
na laana yako iwashukie.
66Uwafuatie kwa hasira, uwaangamize,
uwafanye watoweke ulimwenguni.”


Maombolezo3;1-66

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 13 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Maombolezo 2....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Saba na visamaki vichache.” Basi, Yesu akawaamuru watu wakae chini.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, akamshukuru Mungu, akavimega, akawapa wanafunzi, nao wakawagawia watu. Wote wakala, wakashiba. Kisha wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu saba.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Hao waliokula walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto. Basi, Yesu akawaaga watu, akapanda mashua, akaenda katika eneo la Magadani.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Adhabu ya Yerusalemu
1Mwenyezi-Mungu, kwa hasira yake,
amewaweka watu wa Siyoni gizani.
Fahari ya Israeli ameibwaga chini.
Siku ya hasira yake
alilitupilia mbali hata hekalu lake.
2Mwenyezi-Mungu ameharibu bila huruma
makazi yote ya wazawa wa Yakobo.
Kwa ghadhabu yake amezibomoa ngome za watu wa Yuda.
Ufalme wao na watawala wake
ameuporomosha chini kwa aibu.
3Nguvu yote ya Israeli ameivunja kwa hasira.
Hakunyosha mkono kuwasaidia
walipokutana na adui;
amewawakia watu wa Yakobo kama moto,
akateketeza kila kitu.
4Amevuta upinde wake kama adui,
na kuuweka mkono wake wa kulia tayari,
amewaua wote tuliowaonea fahari
katika maskani yetu watu wa Siyoni.
Ametumiminia hasira yake kama moto.
5Mwenyezi-Mungu amekuwa kama adui,
ameangamiza watu wa Israeli;
majumba yake yote ameyaharibu,
ngome zake amezibomoa.
Amewazidishia watu wa Yuda
matanga na maombolezo.
6Hekalu lake amelibomoa kama kitalu bustanini,
maskani yake ameiharibu.
Amefutilia mbali sikukuu na Sabato huko Siyoni,
kwa hasira yake kuu amewakataa mfalme na makuhani.
7Mwenyezi-Mungu ameipuuza madhabahu yake
na hekalu lake amelikataa.
Kuta za majumba mjini amewaachia maadui wazibomoe,
wakapiga kelele humo nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu
kama kelele za wakati wa sikukuu.
8Mwenyezi-Mungu alipania kuubomoa ukuta wa mji wa Siyoni;
aliupima na kuhakikisha kila kitu kimeharibiwa;
minara na kuta za nje ya mji akazifanya ukiwa,
zote kwa pamoja zikaangamia.
9Malango yake yameanguka chini,
makomeo yake ameyaharibu na kuyavunjavunja.
Mfalme na wakuu wake wako uhamishoni kati ya mataifa.
Mwongozo wa sheria umetoweka kabisa,
manabii wake hawapati tena maono
kutoka kwake Mwenyezi-Mungu.
10Wazee wa Siyoni wameketi chini kimya,
wamejitia mavumbi vichwani
na kuvaa mavazi ya gunia.
Wasichana wa Yerusalemu wameinamisha vichwa.
11Macho yangu yamevimba kwa kulia,
roho yangu imechafuka.
Moyo wangu una huzuni nyingi
kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu
kwa sababu watoto wachanga wanazirai katika barabara za mji.
12Wanawalilia mama zao:
“Wapi chakula, wapi kinywaji?”
Huku wanazirai kama majeruhi
katika barabara za mjini,
na kukata roho mikononi mwa mama zao.
13Nikuambie nini ee Yerusalemu?
Nikulinganishe na nini?
Nikufananishe na kitu gani
ili niweze kukufariji,
ee Siyoni uliye mzuri?
Maafa yako ni mengi kama bahari.
Ni nani awezaye kukuponya?
14Manabii wako wamekuonea maono madanganyifu,
hawakufichua wazi uovu wako
ili wapate kukurekebisha,
bali walikuonea kauli ya uongo na ya kupotosha.
15Wapita njia wote wanakudhihaki;
wanakuzomea, ee Yerusalemu,
wakitikisa vichwa vyao kwa dharau na kusema:
“Je, huu ndio ule mji uliofikia upeo wa uzuri,
mji uliokuwa furaha ya dunia nzima?”
16Maadui zako wote wanakuzomea,
wanakufyonya na kukusagia meno,
huku wakisema, “Tumemwangamiza!
Kweli, siku ile tuliyoingojea kwa hamu
sasa imefika na tumeiona!”
17Mwenyezi-Mungu amefanya yale aliyokusudia,
ametekeleza yale aliyotishia;
kama alivyopanga tangu kale
ameangamiza bila huruma yoyote;
amewafanya maadui wafurahie adhabu yako,
amewakuza mashujaa wa maadui zako.
18Kuta zako, ee mji wa Siyoni, zimlilie Mwenyezi-Mungu!
Machozi na yatiririke kama mto mchana na usiku!
Lia na kuomboleza bila kupumzika!
19Usiku kucha uamkeamke ukalie.
Mfungulie Mwenyezi-Mungu yaliyo moyoni mwako.
Mwinulie mikono yako kuwaombea watoto wako,
watoto wanaozirai kwa njaa popote barabarani.
20Tazama ee Mwenyezi-Mungu uone!
Je, kuna yeyote uliyemtendea ulivyotutendea sisi?
Je, hata kina mama wawale watoto wao?
Je, nao makuhani wauawe hekaluni mwako?
21Maiti za vijana na wazee zimelala vumbini barabarani,
wasichana na wavulana wangu wameuawa kwa upanga;
umewaua bila huruma siku ya hasira yako.
22Umewaalika kama kwenye sikukuu
maadui zangu walionitisha kila upande.
Katika siku ya hasira yako ee Mwenyezi-Mungu,
hakuna aliyetoroka au kunusurika.
Wale niliowazaa na kuwalea
adui zangu wamewaangamiza.


Maombolezo2;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 12 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Tunamshukuru Mungu kwa kumaliza Kitabu cha Yeremia,Leo Tunaanza Kitabu cha Maombolezo 1....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tunamshukuru Mungu kwa kutupa kibali cha
 kupitia kitabu cha "YEREMIA
"
Ni matumaini yangu kuna mengi tumejifunza/kufaidika
na kutupa mwanga/kuelewa kwenye kitabu hiki...


Leo tunapokwenda anza kupitia Kitabu cha"MAOMBOLEZO"tunamuomba Mungu wetu akatupe kibali,macho ya rohoni
 na akili ya kuelewa katika kujifunza NENO lake...
Ee Mungu  tunaomba ukatuongoze...!!

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Yesu alitoka hapo akaenda kando ya ziwa Galilaya, akapanda mlimani, akaketi. Watu wengi sana wakamjia wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaweka mbele ya miguu yake, naye Yesu akawaponya.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Umati ule wa watu ulishangaa sana ulipoona bubu wakiongea, waliokuwa wamelemaa wamepona, viwete wakitembea na vipofu wakiona; watu wakamsifu Mungu wa Israeli.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Basi, Yesu aliwaita wanafunzi wake, akasema, “Nawaonea huruma watu hawa kwa sababu wamekuwa nami kwa siku tatu, wala hawana chakula. Sipendi kuwaacha waende zao bila kula, wasije wakazimia njiani.” Wanafunzi wakamwambia, “Hapa tuko nyikani; tutapata wapi chakula cha kuwatosha watu wengi hivi?”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.


1Ajabu mji uliokuwa umejaa watu,

sasa wenyewe umebaki tupu!
Ulikuwa maarufu kati ya mataifa;
sasa umekuwa kama mama mjane.
Miongoni mwa miji ulikuwa kama binti mfalme;
sasa umekuwa mtumwa wa wengine.
2Walia usiku kucha;
machozi yautiririka.
Hakuna hata mmoja wa wapenzi wake wa kuufariji.
Rafiki zake wote wameuhadaa;
wote wamekuwa adui zake.
3Watu wa Yuda wamekwenda uhamishoni
pamoja na mateso na utumwa mkali.
Sasa wanakaa miongoni mwa watu wa mataifa,
wala hawapati mahali pa kupumzika.
Waliowafuatia wamewakamata wakiwa taabuni.
4Barabara za kwenda Siyoni zinasikitisha;
hakuna wapitao kwenda kwenye sikukuu.
Malango ya mji wa Siyoni ni tupu;
makuhani wake wanapiga kite,
wasichana wake wana huzuni,
na mji wenyewe uko taabuni.
5Adui zake ndio wanaoutawala na wanafanikiwa,
kwani Mwenyezi-Mungu ameutesa
kwa sababu ya makosa mengi.
Watoto wake wametekwa na kupelekwa mbali.
6Fahari yote ya watu wa Siyoni imewatoweka;
wakuu wake wamekuwa kama kulungu wasio na malisho.
Bila nguvu waliwakimbia watesi wao.
7Ukiwa sasa magofu matupu,
Yerusalemu wakumbuka fahari yake.
Ulipoangukia mikononi mwa maadui zake,
hakuna aliyekuwako kuusaidia.
Washindi wake walichekelea kuanguka kwake.
8Yerusalemu ulitenda dhambi mbaya,
ukawa mchafu kwa dhambi zake.
Wote waliousifia wanaudharau,
maana wameuona uchi wake.
Wenyewe wapiga kite na kujificha kwa aibu.
9Uchafu wake ulionekana waziwazi,
lakini wenyewe haukujali mwisho wake.
Anguko lake lilikuwa kubwa mno;
hakuna awezaye kuufariji.
Wasema:
“Tazama ee Mwenyezi-Mungu mateso yangu,
maana adui yangu ameshinda.”
10Maadui wamenyosha mikono yao,
wanyakue vitu vyake vyote vya thamani.
Naam umeona watu wa mataifa wakiingia hekaluni,
watu ambao Mwenyezi-Mungu aliwakataza
kujumuika na jumuiya ya watu wake.
11Watu wa Yerusalemu wote wanahangaika kutafuta chakula;
hazina zao wanazitoa kupata chakula,
wajirudishie nguvu zao.
Nao mji unalia,
“Hebu niangalie, ee Mwenyezi-Mungu,
ona jinsi nilivyogeuka kuwa duni.
12“Enyi wapita njia, hivi hamjali kitu?
Tazameni! Hakuna aliyepatwa na uchungu kama mimi,
uchungu alioniletea Mwenyezi-Mungu,
siku ya hasira yake kali.
13“Aliteremsha moto kutoka juu,
ukanichoma hata mifupani mwangu.
Alinitegea wavu akaninasa,
kisha akanirudisha nyuma,
akaniacha nimeduwaa na kuzirai mchana kutwa.
14“Aliyahesabu makosa yangu yote
akayakusanya mahali pamoja;
aliyafunga shingoni mwangu kama nira,
nikafyonzwa nguvu zangu kwa uzito wake.
Mwenyezi-Mungu aliniweka mikononi mwao
watu ambao siwezi kuwapinga.
15“Mwenyezi-Mungu aliwakataa askari walionilinda,
alitangaza wakati maalumu wa kuniadhibu
kuwaponda vijana wangu wa kiume.
Aliwaponda kama katika shinikizo
watu wangu wa Yuda.
16“Kwa sababu ya hayo ninalia,
machozi yanitiririka,
sina mtu yeyote wa kunifariji;
hakuna yeyote wa kunitia moyo.
Watoto wangu wameachwa wakiwa,
maana adui yangu amenishinda.
17“Nainyosha mikono yangu
lakini hakuna wa kunifariji.
Mwenyezi-Mungu ametoa amri dhidi yangu mimi Yakobo,
jirani zangu wawe maadui zangu.
Naam, mimi Yerusalemu nimekuwa kinyaa kwao.
18“Lakini Mwenyezi-Mungu amefanya sawa
kwa maana nimeliasi neno lake.
Nisikilizeni enyi watu wote,
yatazameni mateso yangu.
Wasichana wangu na wavulana wangu,
wamechukuliwa mateka.
19“Niliwaita wapenzi wangu,
lakini wao wakanihadaa.
Makuhani na wazee wangu
wamefia mjini
wakijitafutia chakula,
ili wajirudishie nguvu zao.
20“Ona, ee Mwenyezi-Mungu nilivyo taabuni.
Roho yangu imechafuka,
moyo wangu unasononeka
kwani nimekuasi vibaya.
Huko nje kumejaa mauaji,
ndani nako ni kama kifo tu.
21“Sikiliza ninavyopiga kite;
hakuna wa kunifariji.
Maadui zangu wote wamesikia juu ya taabu yangu:
Wanafurahi kwamba umeniletea maafa.
Uifanye ile siku uliyoahidi ifike,
uwafanye nao wateseke kama mimi.
22“Uwapatilize kwa ajili ya uovu wao wote.
Uwatende kama ulivyonitenda mimi
kwa sababu ya makosa yangu yote.
Nasononeka sana kwa maumivu
na moyo wangu unazimia.”


Maombolezo1;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 11 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 52....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Yesu aliondoka mahali hapo akaenda kukaa katika sehemu za Tiro na Sidoni. Basi, mama mmoja Mkanaani wa nchi hiyo alimjia, akapaza sauti: “Bwana, Mwana wa Daudi, nionee huruma! Binti yangu anasumbuliwa na pepo.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Lakini Yesu hakumjibu neno. Basi, wanafunzi wake wakamwendea, wakamwambia, “Mwambie aende zake kwa maana anatufuatafuata akipiga kelele.” Yesu akajibu, “Sikutumwa ila kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.” Hapo huyo mama akaja, akamsujudia, akasema, “Bwana, nisaidie.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Yesu akamjibu, “Si vizuri kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.” Huyo mama akajibu, “Ni kweli, Bwana; lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka meza ya bwana wao.” Hapo Yesu akamjibu, “Mama, imani yako ni kubwa; basi, ufanyiwe kama unavyotaka.” Yule binti yake akapona wakati huohuo.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


Maangamizi ya Yerusalemu
(2Fal 24:18-25:7)
1Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala. Alitawala kwa muda wa miaka kumi na mmoja huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, mkazi wa mji wa Liba. 2Alitenda maovu mbele ya Mwenyezi-Mungu kama mabaya yote aliyotenda Yehoyakimu. 3Mwenyezi-Mungu aliwakasirikia sana watu wa Yerusalemu na Yuda hata akawafukuza mbali naye.
Sedekia alimwasi mfalme wa Babuloni. 4Ikawa katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, mwaka wa tisa wa kutawala kwake Sedekia, Nebukadneza mfalme wa Babuloni, alifika na jeshi lake lote kuushambulia Yerusalemu, wakauzingira kila upande. 5Mji uliendelea kuzingirwa mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia. 6Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ilikuwa kali sana mjini hata hapakuwa na chakula chochote kwa ajili ya wakazi wake. 7Basi, sehemu ya ukuta wa mji ilibomolewa, nao askari walikimbia wakatoka nje ya mji wakati wa usiku wakipitia njia ya lango katikati ya kuta mbili, kwenye bustani ya mfalme, wakaenda upande wa Araba, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji wote. Waisraeli walikimbia kuelekea bonde la mto Yordani. 8Lakini jeshi la Wakaldayo lilimfuatia mfalme na kumteka katika tambarare za Yeriko, jeshi lake lote likatawanyika na kumwacha. 9Basi Wakaldayo walimteka mfalme, wakampeleka kwa mfalme wa Babuloni, huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, naye akamhukumu. 10Hukohuko Ribla, mfalme wa Babuloni aliwaua wana wa Sedekia mbele ya baba yao. Aliwaua pia maofisa wote wa Yuda. 11Kisha aliyangoa macho ya Sedekia na kumfunga pingu, akamchukua Sedekia Babuloni na kumtia kizuizini mpaka siku alipokufa.
Kuharibiwa kwa hekalu
(2Fal 25:8-17)
12Katika siku ya kumi ya mwezi wa tano, mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza, mfalme wa Babuloni, Nebuzaradani kapteni wa walinzi wa mfalme ambaye alimtumikia mfalme wa Babuloni, aliingia Yerusalemu. 13Alichoma moto nyumba ya Mwenyezi-Mungu, ikulu na nyumba zote za Yerusalemu; kila nyumba kubwa ilichomwa moto. 14Askari wote wa Wakaldayo waliokuwa pamoja na kapteni wa walinzi, walizibomoa kuta zote zilizouzunguka mji wa Yerusalemu. 15Nebuzaradani kapteni wa walinzi wa mfalme, aliwachukua uhamishoni watu waliokuwa wamebakia mjini na wale waliokuwa wamejisalimisha kwa mfalme wa Babuloni pamoja na mafundi. 16Lakini Nebuzaradani kapteni wa walinzi wa mfalme, aliwaacha baadhi ya watu waliokuwa maskini kabisa nchini, wawe watunza mizabibu na wakulima.
17Wakaldayo walivunja vipandevipande nguzo za shaba nyeusi ambazo zilikuwa katika nyumba ya Mwenyezi-Mungu pamoja na vikalio na birika kubwa la shaba nyeusi lililokuwamo katika nyumba ya Mwenyezi-Mungu, wakaichukua shaba nyeusi yote mpaka Babuloni. 18Kadhalika, walichukua vyungu, sepetu, mikasi, makarai, vijiko vikubwa na vyombo vyote vya shaba nyeusi vilivyotumiwa katika huduma ya hekalu. 19Pia kapteni wa walinzi wa mfalme alichukua vibakuli, vyetezo, mabirika, vyungu, vinara vya taa, vijiko vikubwa na mabakuli ya sadaka za vinywaji, vyombo hivyo vikiwa vya dhahabu au vya fedha. 20Kuhusu vitu Solomoni alivyotengeneza: Nguzo mbili, birika kubwa moja na sanamu za fahali kumi na mbili za shaba nyeusi ambazo zilikuwa chini ya hilo birika kubwa pamoja na vikalio, shaba nyeusi ya vitu hivi vyote ilikuwa na uzito mwingi sana. 21Kila moja ya nguzo hizo mbili ilikuwa na urefu wa mita 8, mzingo wake mita 5.25, na unene wa milimita 75, zote zilikuwa wazi ndani. 22Juu ya kila nguzo kulikuwa na kichwa cha shaba nyeusi; urefu wa kila kichwa ulikuwa mita 2 na sentimita 20. Kila kichwa kilizungushiwa mapambo ya wavu ya makomamanga, yote ya shaba nyeusi. 23Kulikuwa na makomamanga tisini na sita ubavuni mwa nguzo hizo; jumla ya makomamanga yote ilikuwa 100 na mapambo kandokando yake.
Watu wa Yuda wanapelekwa Babuloni
(2Fal 25:18-21,27-30)
24Kisha Nebuzaradani kapteni wa walinzi wa mfalme, alimchukua mateka Seraya kuhani mkuu, na Sefania kuhani wa pili, pamoja na walinda mlango watatu; 25na kutoka mjini alimchukua ofisa mmoja ambaye alikuwa akiongoza askari vitani, pamoja na watu saba washauri wa mfalme ambao aliwakuta mjini. Kadhalika alimchukua katibu wa kamanda mkuu wa jeshi ambaye alitunza kumbukumbu za jeshi pamoja na watu mashuhuri sitini ambao aliwakuta mjini Yerusalemu. 26Nebuzaradani kapteni wa walinzi wa mfalme, aliwachukua watu hao na kuwapeleka kwa mfalme wa Babuloni huko Ribla. 27Mfalme Nebukadneza wa Babuloni aliwapiga na kuwaua watu hao huko Ribla katika nchi ya Hamathi.
Basi, watu wa Yuda walikwenda uhamishoni nje ya nchi yao. 28Ifuatayo ni idadi ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua uhamishoni mnamo mwaka wa saba wa utawala wake: Alichukua Wayahudi 3,023; 29mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, alichukua kutoka Yerusalemu mateka 832; 30mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Nebukadneza, Nebuzaradani kapteni wa walinzi wa mfalme, alichukua mateka Wayahudi 745. Jumla ya mateka wote ilikuwa watu 4,600.
31Mnamo mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda alipopelekwa uhamishoni, siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili, Evil-merodaki mfalme wa Babuloni, mwaka uleule alipofanywa mfalme, alimsamehe Yehoyakini mfalme wa Yuda, akamtoa gerezani. 32Aliongea naye vizuri na kumpa nafasi ya heshima kuliko wafalme wengine waliokuwa pamoja naye uhamishoni huko Babuloni. 33Basi, Yehoyakini alibadili mavazi yake ya kifungoni, akawa anapata chakula chake daima mezani kwa mfalme. 34Daima alipewa posho na mfalme wa Babuloni kulingana na mahitaji yake ya kila siku, mpaka alipofariki.


Yeremia52;1-34

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.