Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 17 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 13....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Enyi watumishi wa nyumbani, watiini wakuu wenu kwa heshima yote, wawe wema na wapole au wenye kuchukiza. Maana kama mnavumilia maumivu ya mateso msiyostahili kwa sababu mwajua kwamba Mungu anataka hivyo, basi Mungu atawafadhili. Maana, mtapata tuzo gani mkivumilia mapigo mnayostahili kwa sababu ya makosa yenu? Lakini kama mnavumilia mateso hata ingawa mmetenda mema, Mungu atawapeni baraka kwa ajili hiyo.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Hayo ndiyo mliyoitiwa; maana Kristo mwenyewe aliteseka kwa ajili yenu, akawaachieni mfano, ili mfuate mwenendo wake. Yeye hakutenda dhambi, wala neno la udanganyifu halikusikika mdomoni mwake. Alipotukanwa yeye hakujibu kwa tukano; alipoteseka yeye hakutoa vitisho, bali aliyaweka matumaini yake kwa Mungu, hakimu mwenye haki.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Yeye mwenyewe alizibeba dhambi zetu katika mwili wake juu ya msalaba, tupate kufa kuhusu dhambi, na kuishi kwa ajili ya uadilifu. Kwa majeraha yake, nyinyi mmeponywa. Nyinyi mlikuwa kama kondoo waliokuwa wamepotea; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mlinzi wa roho zenu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Mungu ataiadhibu Babuloni
1 13:1--14:23 Taz Isa 47:1-15; Yer 50:1--51:64 
Kauli ya Mungu dhidi ya Babuloni ambayo Isaya, mwana wa Amozi, alipewa katika maono:
2Mungu asema:
“Twekeni bendera juu ya mlima usio na miti.
Wapaazieni sauti askari
wapungieni watu mkono
waingie malango ya mji wa wakuu.
3Mimi nimewaamuru wateule wangu,
nimewaita mashujaa wangu,
hao wenye kunitukuza wakishangilia,
waje kutekeleza lengo la hasira yangu.”
4Sikilizeni kelele milimani
kama za kundi kubwa la watu!
Sikilizeni kelele za falme,
na mataifa yanayokusanyika!
Mwenyezi-Mungu wa majeshi
analikagua jeshi linalokwenda vitani.
5Wanakuja kutoka nchi za mbali,
wanatoka hata miisho ya dunia:
Mwenyezi-Mungu na silaha za hasira yake
anakuja kuiangamiza dunia.
6 13:6 Taz Yoe 1:15 Lieni maana siku ya Mwenyezi-Mungu imekaribia;
inakuja kama maafa kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu.
7Kwa hiyo mikono ya kila mtu italegea,
kila mtu atakufa moyo.
8Watu watafadhaika,
watashikwa na hofu na maumivu,
watakuwa na uchungu kama mama anayejifungua.
Watatazamana kwa mashaka,
nyuso zao zitawaiva kwa haya.
9Siku ya Mwenyezi-Mungu inakuja,
siku kali, ya ghadhabu na hasira kali.
Itaifanya nchi kuwa uharibifu,
itawaangamiza wenye dhambi wake.
10 13:10 Taz Eze 32:7; Mat 24:29; Marko 13:24-25; Luka 21:25; Ufu 6:12-13 Nyota na vilimia vyake angani hazitaangaza;
jua linapochomoza litakuwa giza,
na mwezi hautatoa mwanga wake.
11Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Nitauadhibu ulimwengu kwa uovu wake,
waovu kwa sababu ya makosa yao.
Nitakikomesha kiburi cha wenye majivuno,
na kuporomosha ubaradhuli wa watu katili.
12Nitawafanya watu kuwa wachache kuliko dhahabu safi;
binadamu watakuwa wachache kuliko dhahabu ya Ofiri.
13Nitazitetemesha mbingu
nayo nchi itatikisika katika misingi yake
kwa sababu ya ghadhabu yangu Mwenyezi-Mungu
siku ile ya hasira yangu kali.
14“Kama swala anayewindwa,
kama kondoo wasio na mchungaji,
kila mmoja atajiunga na watu wake
kila mtu atakimbilia nchini mwake.
15Yeyote atakayeonekana atatumbuliwa,
atakayekamatwa atauawa kwa upanga.
16Watoto wao wachanga watapondwapondwa mbele yao,
watanyanganywa nyumba zao,
na wake zao watanajisiwa.
17“Ninawachochea Wamedi dhidi yao;
watu ambao hawajali fedha
wala hawavutiwi na dhahabu.
18Mishale yao itawaua vijana,
hawatakuwa na huruma kwa watoto,
wala kuwahurumia watoto wachanga.
19 13:19 Taz Mwa 19:24 Babuloni johari ya falme zote
na umaarufu wa kiburi cha Wakaldayo
utakuwa kama Sodoma na Gomora,
wakati Mungu alipoiangamiza.
20Kamwe hautakaliwa tena na watu,
watu hawataishi humo katika vizazi vyote.
Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake humo,
wala mchungaji atakayechunga wanyama wake humo.
21 13:21 Taz Isa 34:14; Sef 2:14; Ufu 18:2 Badala yake watakuwamo wanyama wakali wa porini,
bundi watajaa katika nyumba zake.
Mbuni13:21 Mbuni: Au pepo wabaya. wataishi humo,
na majini13:21 majini: Au Ibilisi; namna ya pepo wa hadithi za Babuloni. yatachezea humo.
22Mbwamwitu watalia ndani ya ngome zake,
mbweha wataonekana ndani ya nyumba zao za anasa.
Wakati wa Babuloni umekaribia,
wala siku zake hazitaongezwa.”

Isaya13;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 16 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 12....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...
Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Wapenzi wangu, nawasihi nyinyi kama wageni na wakimbizi hapa duniani! Achaneni na tamaa za mwili ambazo hupingana na roho. Mwenendo wenu kati ya watu wasiomjua Mungu unapaswa kuwa mwema kabisa, ili hata watakapowasingizieni kwamba mnatenda mabaya, waweze kutambua matendo yenu mema na hivyo wamtukuze Mungu siku ya kuja kwake.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Basi, jiwekeni chini ya mamlaka yote ya kibinadamu, kwa ajili ya Bwana: Utii kwa mfalme aliye mtawala mkuu, utii kwa wakuu wa mikoa ambao wameteuliwa naye kuwaadhibu wahalifu na kuwasifu watendao mema. Maana Mungu anataka muweze kuyakomesha maneno ya kijinga ya watu wasio na akili kwa matendo mema mnayofanya.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Ishini kama watu huru; lakini msiutumie uhuru wenu kuuficha ubaya, bali ishini kama watumishi wa Mungu. Waheshimuni watu wote, wapendeni ndugu zenu waamini, mcheni Mungu, mheshimuni mfalme.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Wimbo wa shukrani
1Siku hiyo mtasema:
“Nakushukuru, ee Mwenyezi-Mungu,
maana ingawa ulinikasirikia,
hasira yako imetulia,
nawe umenifariji.
2 12:2 Taz Kut 15:2; Zab 118:14
 Mungu ndiye mwenye kuniokoa,
nitamtegemea yeye, wala sitaogopa;
Mwenyezi-Mungu hunijalia nguvu;
yeye mwenyewe ndiye aniokoaye.”
3Mtachota maji kwa furaha
kutoka visima vya wokovu.
4Siku hiyo mtasema:
“Mshukuruni Mwenyezi-Mungu
mwombeni kwa jina lake.
Yajulisheni mataifa matendo yake,
tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
5Mwimbieni Mwenyezi-Mungu sifa
kwa kuwa ametenda mambo makuu;
haya na yajulikane duniani kote.
6Pazeni sauti na kuimba kwa furaha,
enyi wakazi wa Siyoni,
maana aliye mkuu miongoni mwenu
ndiye Mungu, Mtakatifu wa Israeli.”


Isaya12;1-6

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 13 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 11....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Lakini nyinyi ni ukoo mteule, makuhani wa Mfalme, taifa takatifu; watu wake Mungu mwenyewe, mlioteuliwa kutangaza matendo makuu ya Mungu aliyewaiteni kutoka gizani, akawaingizeni katika mwanga wake mkuu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Wakati mmoja nyinyi hamkuwa watu wa Mungu, lakini sasa nyinyi ni watu wake; wakati mmoja hamkupewa huruma ya Mungu, lakini sasa mmepokea huruma.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Ufalme wa amani

1 11:1 Taz Ufu 5:5; 22:16 
Kutatokea chipukizi katika kisiki cha Yese,
tawi litachipua mizizini mwake.
2Roho ya Mwenyezi-Mungu itakaa kwake,
roho ya hekima na maarifa,
roho ya shauri jema na nguvu,
roho ya ujuzi na ya kumcha Mwenyezi-Mungu.
3Atafurahia kumcha Mwenyezi-Mungu.
Hatahukumu kadiri ya mambo ya njenje,
wala kuamua kufuatana na yale anayosikia.
4 11:4 Taz 2Thes 2:8 Atawapatia haki watu maskini,
atawaamulia sawasawa wanyonge nchini.
Kwa neno lake ataiadhibu dunia,
kwa tamko lake atawaua waovu.
5 11:5 Taz Efe 6:14 Haki itakuwa kama mkanda wa kujifunga,
uaminifu utakaa naye kama mkanda kiunoni.
6 11:6-9 Taz Isa 65:25 Mbwamwitu ataishi pamoja na mwanakondoo,
chui watapumzika pamoja na mwanambuzi.
Ndama na wanasimba watakula pamoja,
na mtoto mdogo atawaongoza.
7Ngombe na dubu watakula pamoja,
ndama wao watapumzika pamoja;
na simba atakula majani kama ng'ombe.
8Mtoto mchanga atacheza kwenye shimo la nyoka
mtoto ataweza kutia mkono shimoni mwa nyoka wa sumu.
9 11:9 Taz Hab 2:14 Katika mlima mtakatifu wa Mungu
hakutakuwa na madhara wala uharibifu.
Maana kumjua Mwenyezi-Mungu kutaenea pote nchini,
kama vile maji yajaavyo baharini.
Walio uhamishoni watarudi
10 11:10 Taz Roma 15:12 Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa ishara kwa mataifa; mataifa yatamtafuta na makazi yake yatatukuka. 11Siku hiyo, Bwana ataunyosha mkono wake tena kuwarejesha watu wake waliosalia huko Ashuru, Misri, Pathrosi, Kushi, Elamu, Shinari, Hamathi na sehemu za pwani.
12Naye atatweka bendera kuwaashiria mataifa,
kuwakusanya Waisraeli waliodharauliwa,
kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa,
na kuwarudisha toka pembe nne za dunia.
13Wivu wa Efraimu juu ya Yuda utakoma,
hakutakuwa tena na uadui kati ya Yuda na Efraimu.
14Wote pamoja watawavamia Wafilisti walio magharibi,
pamoja watawapora watu wakaao mashariki.
Watawashinda Waedomu na Wamoabu,
nao Waamoni watawatii.
15Mwenyezi-Mungu atakausha ghuba ya bahari ya Shamu,11:15 bahari ya Shamu: Kiebrania: Bahari ya Misri.
kwa pumzi yake ichomayo atakausha mto Eufrate,
nao utagawanyika katika vijito saba,
watu wavuke humo miguu mikavu.
16Tena, kutakuwa na barabara kuu toka Ashuru
kwa ajili ya watu wake waliobaki humo
kama ilivyokuwa kwa Waisraeli
wakati walipotoka nchini Misri.

Isaya11;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 12 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 10....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Tazama! Naweka jiwe huko Siyoni, jiwe la msingi, teule na la thamani. Mtu atakayemwamini huyo hataaibishwa.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kwenu nyinyi mnaoamini, jiwe hilo ni la thamani kubwa; lakini kwa wale wasioamini, “Jiwe walilolikataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Tena Maandiko yasema: “Jiwe hilo ni jiwe la kujikwaa, mwamba wa kuwaangusha watu.” Watu hujikwaa kwa sababu hawauamini ule ujumbe; na ndivyo walivyopangiwa tangu mwanzo.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.



1Ole wao wanaotunga sheria zisizo za haki,
watu wanaopitisha sheria za kukandamiza.
2Huwanyima maskini haki zao,
na kuwaibia maskini wa watu wangu maslahi yao.
Wajane wamekuwa nyara kwao;
yatima wamekuwa mawindo yao.
3Je, mtafanya nini siku ya adhabu,
siku dhoruba itakapowajieni kutoka mbali?
Mtamkimbilia nani kuomba msaada?
Mtakwenda wapi kuweka mali yenu?
4Litakalowabakia ni kujikunyata kati ya wafungwa
na kuangamia pamoja na wanaouawa vitani.
Hata hivyo, hasira ya Mwenyezi-Mungu haijatulia,
bado ameunyosha mkono wake.
Onyo kwa mfalme wa Ashuru
5 10:5-34 Taz Isa 14:24-27; Nah 1:1--3:19; Sef 2:13-15 
Ole wake Ashuru, fimbo ya hasira yangu,
yeye ashikaye kiboko cha hasira yangu!
6Nilimtuma kuliadhibu taifa ovu,
nilimwamuru kuwaadhibu watu niliowakasirikia,
kuwapora na kuteka nyara,
na kuwakanyaga chini kama tope njiani.
7Lakini Ashuru hakudhamiria hivyo,
yeye alikuwa na nia nyingine;
alikusudia kuharibu kabisa,
kuangamiza mataifa mengi iwezekanavyo.
8Maana alisema:
“Je, si kweli majemadari wangu ni wafalme?
9Je, si kweli kwamba Kalno nitautenda kama Karkemishi,
mji wa Hamathi kama mji wa Arpadi,
Samaria kama Damasko?
10Kama nimefaulu kuunyosha mkono wangu
dhidi ya falme zenye sanamu za miungu
kubwa kuliko sanamu za Yerusalemu na Samaria;
11je, nitashindwa kuutenda Yerusalemu na sanamu zake,
kama nilivyoutenda Samaria na sanamu zake?”
12Wakati Mwenyezi-Mungu atakapomaliza kazi zake zote mlimani Siyoni na mjini Yerusalemu, atamwadhibu mfalme wa Ashuru, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.
13Maana mfalme wa Ashuru alisema:
“Kwa nguvu zangu mwenyewe nimetenda hayo,
na kwa hekima yangu, maana mimi ni mwerevu!
Nimeondoa mipaka kati ya mataifa,
nikazipora hazina zao;
kama fahali nimewaporomosha walioketia viti vya enzi.
14Kama mtu anyoshaye mkono kwenye kiota,
ndivyo nilivyochukua mali yao;
kama mtu aokotavyo mayai yaliyoachwa kiotani,
ndivyo nilivyowaokota duniani kote,
wala hakuna mtu aliyeweza kupiga bawa,
au aliyefungua kinywa kunipigia kelele.”
Lakini Mwenyezi-Mungu asema hivi:
15“Je, shoka litajigamba dhidi ya anayelitumia?
Msumeno waweza kujivuna dhidi ya mwenye kukata nao?
Ni kana kwamba fimbo ingeweza kumwinua anayeishika,
au mkongojo kumwinua mwenye kuutumia!”
16Kwa hiyo, Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
atawaletea askari wao ugonjwa wa kuwakondesha,
na fahari yao itateketezwa kama kwa moto.
17Mungu aliye mwanga wa Israeli atakuwa kama moto,
Mtakatifu wa Israeli atakuwa mwali wa moto
ambao kwa siku moja utateketeza kila kitu:
Miiba yake na mbigili zake pamoja.
18Misitu yake ya fahari na mashamba yake mazuri,
Mwenyezi-Mungu atayaangamiza yote;
itakuwa kama mtu aliyemalizwa na ugonjwa.
19Miti itakayobaki msituni mwake itakuwa michache sana
hata mtoto mdogo ataweza kuihesabu.

Wachache watarudi
20Siku ile wazawa wa Yakobo watakaobaki, naam, Waisraeli watakaosalia hawatalitegemea tena taifa lililowaadhibu, bali watamtegemea kabisa Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wa Israeli. 21Wazawa wa Yakobo wachache watakaobaki watamrudia Mungu Mkuu. 2210:22 Taz Roma 9:27 Maana, hata kama sasa Waisraeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaorudi. Maangamizi yamepangwa yafanyike, nayo yatafanyika kwa haki tupu. 23Naam! Bwana, Mwenyezi-Mungu wa majeshi, atakamilisha kabisa katika nchi yote jambo aliloamua kutenda.
Mwenyezi-Mungu ataiadhibu Ashuru
24Kwa hiyo, Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: “Enyi watu wangu mnaokaa Siyoni msiwaogope Waashuru ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua mikongojo yao dhidi yenu kama walivyofanya Wamisri. 25Maana bado kitambo, nayo hasira yangu itapita na ghadhabu yangu itawageukia Waashuru. 26Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi na nitawachapa kama nilivyowachapa Wamidiani kwenye jabali la Orebu. Nitanyosha fimbo yangu juu ya bahari kuwachapa kama nilivyowafanya Wamisri. 27Wakati huo, mzigo waliowabebesha nitauondoa na nira waliyowatia shingoni mwenu itavunjwa.”
Adui anakaribia
Adui amepanda kutoka Rimoni,
28amefika mjini Ayathi.
Amepitia huko Migroni,
mizigo yake ameiacha Mikmashi.
29Amekwisha pita kivukoni,
usiku huu analala Geba.
Watu wa Rama wanatetemeka kwa hofu,
wakazi wa Gibea, mji wa Shauli, wamekimbia.
30Pazeni sauti enyi watu wa Galimu!
Tegeni sikio enyi watu wa Laisha!
Jibuni enyi wenyeji wa Anathothi!
31Watu wa Madmena wako mbioni,
wakazi wa Gebimu wanakimbilia usalama.
32Leo hii, adui atatua Nobu,
atatikisa ngumi yake dhidi ya mlima Siyoni;
naam, atautikisia ngumi mji wa Yerusalemu.
33Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi
atakata matawi yake kwa ukatili;
miti mirefu itaangushwa chini,
walio juu wataaibishwa.
34Atakata vichaka vya msituni kwa shoka,
Lebanoni na mierezi yake maarufu itaanguka.

Isaya10;1-34

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.