Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 17 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 20...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu, na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkipo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kila wakati ninaposali, nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu, maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo. Ndugu, upendo wako umeniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

1Divai huleta dhihaka na kileo huleta ugomvi;
yeyote anayevutiwa navyo hana hekima.
2Ghadhabu kali ya mfalme ni kama simba angurumaye;
anayemkasirisha anayahatarisha maisha yake.
3Ni jambo la heshima kuepa ugomvi;
wapumbavu ndio wanaogombana.
4Mvivu halimi wakati wa kulima;
wakati wa mavuno atatafuta asipate chochote.
5Fikira za mtu zimefichika kama kilindi cha maji;
lakini mtu mwenye busara ajua kuzichota humo.
6Watu wengi hujivunia kuwa wema,
lakini mwaminifu wa kweli apatikana wapi?
7Mtu mwadilifu akiishi kwa unyofu;
watoto wake atakaowaacha watabarikiwa.
8Mfalme mwema aketipo kutoa hukumu,
huupepeta uovu wote kwa macho yake.
9Nani athubutuye kusema: “Nimeutakasa moyo wangu;
mimi nimetakasika dhambi yangu?”
10Mizani ya udanganyifu na vipimo vya udanganyifu,
vyote ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu.
11Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake,
kama tabia yake ni njema na aminifu.
12Sikio lisikialo na jicho lionalo,
yote mawili kayafanya Mwenyezi-Mungu.
13Usipende kulala tu usije ukawa maskini;
uwe macho nawe utakuwa na chakula kingi.
14“Hakifai, hakifai”, mnunuzi hulalamika,
lakini akiondoka hujisifu amepunguziwa bei.
15Kuna dhahabu na wingi wa mawe ya thamani kubwa;
lakini cha thamani kubwa zaidi ni maneno ya busara!
16Mtu akiahidi mbele yako kumdhamini mgeni,
chukua nguo yake;
mfanye awajibike kwa kuwadhamini wageni.
17Chakula kipatikanacho kwa udanganyifu ni kitamu,
lakini baadaye huwa kama mchanga kinywani.
18Mipango mizuri hufanyika kwa kushauriana;
ukitaka kuanza vita lazima kutafakari kwanza.
19Mpiga domo hafichi siri,
kwa hiyo mwepe mtu wa kuropoka.
20Anayemlaani baba yake au mama yake,
mwanga wa uhai wake utazimwa kama taa gizani.
21Mali iliyopatikana kwa haraka mwanzoni,
haitakuwa ya heri mwishoni.
22Usiseme, “Nitalipiza ubaya niliotendewa.”
Mtegemee Mwenyezi-Mungu naye atakusaidia.
23Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,
na vipimo visivyo halali ni kitu kibaya.
24Hatua za mtu huongozwa na Mwenyezi-Mungu;
awezaje binadamu kujua njia ya kwenda?
25Ni hatari kusema kwa mzaha “Usiahidi kumpa Mungu kitu bila kufikiri,
la sivyo utaanza kusikitika baada ya nadhiri yako.”
26Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu;
huwaadhibu bila huruma.
27Dhamiri ya mtu ni taa ya Mwenyezi-Mungu;
huchunguza nafsi yake mtu mpaka ndani kabisa.
28Wema na uaminifu humkinga mfalme;
utawala wake huimarishwa kwa uadilifu.
29Fahari ya vijana ni nguvu zao,
uzuri wa vikongwe ni mvi za uzee.
30Mapigo yanayoumiza ni dawa ya kuondoa uovu;
viboko husafisha nafsi mpaka ndani kabisa.

Methali20;1-30

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 16 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 19...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...

Asante kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Mtakusanya nyara zake zote katika uwanja wa hadhara wa mji na kuzichoma kwa moto kama sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana Mungu wenu; mji huo utakuwa rundo la magofu milele, nao hautajengwa tena.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Msichukue kitu chochote kilichotolewa kiteketezwe, ili Mwenyezi-Mungu aache ile hasira yake kali, awaoneshe rehema na huruma, na kuwafanya muwe wengi sana kama alivyowaahidi babu zenu,
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

kama tu mtaitii sauti ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, mkishika amri zake zote ninazowapa hivi leo, na kufanya yaliyo sawa mbele yake Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Afadhali maskini aishiye kwa unyofu,
kuliko mtu mpotovu wa maneno na mpumbavu.
2Haifai mtu kuwa bila akili;
mwenda harakaharaka hujikwaa.
3Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake,
huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu.
4Mali huvuta marafiki wengi wapya,
lakini maskini huachwa bila rafiki.
5Shahidi mwongo hataacha kuadhibiwa;
asemaye uongo hataepa adhabu.
6Watu wengi hujipendekeza kwa wakuu;
kila mtu hutaka kuwa rafiki ya mtu mkarimu.
7Maskini huchukiwa na ndugu zake;
marafiki zake ndio zaidi: Humkimbia!
Hata awabembeleze namna gani hatawapata.19:7 Hata … hatawapata: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
8Ajipatiaye hekima anaipenda nafsi yake;
anayezingatia busara atastawi.
9Shahidi mwongo hatakosa kuadhibiwa;
asemaye uongo ataangamia.
10Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa,
tena ni vibaya zaidi mtumwa kuwatawala wakuu.
11Mwenye busara hakasiriki upesi;
kusamehe makosa ni fahari kwake.
12Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba,
lakini wema wake ni kama umande juu ya majani.
13Mtoto mpumbavu ni balaa kwa baba yake;
na ugomvi wa mke ni kama matone ya mvua yasiyoisha.
14Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa wazee wake,
lakini mke mwenye busara hutoka kwa Mwenyezi-Mungu.
15Uzembe ni kama usingizi mzito;
mtu mvivu atateseka kwa njaa.
16Anayeshika amri anasalimisha maisha yake;
anayepuuza agizo atakufa.
17Anayemsaidia maskini anamkopesha Mwenyezi-Mungu;
Mwenyezi-Mungu atamlipa kwa tendo lake jema.
18Mrudi mwanao kungali bado na tumaini,
lakini usimwadhibu kiasi cha kumwangamiza.
19Mtu wa hasira kali lazima apate adhabu;
ukimwachia mara moja itakubidi kumwachia tena.19:19 ukimwachia … tena: Au ukimtoa kwenye matatizo hali yake huwa mbaya zaidi.
20Sikiliza shauri na kupokea mafundisho,
upate hekima ya kukufaa siku zijazo.
21Kichwani mwa mtu mna mipango mingi,
lakini anachokusudia Mwenyezi-Mungu ndicho kitakachofanyika.
22Kinachotakiwa kwa mtu ni uaminifu;
afadhali mtu maskini kuliko mtu mwongo.
23Kumcha Mwenyezi-Mungu kunaleta uhai;
amchaye hujaliwa pumziko la kutosheleza,
wala hatapatwa na baa lolote.
24Mvivu ni kama mtu atiaye mkono katika sahani ya chakula,
lakini hana nguvu ya kuuinua hadi mdomoni.
25Mwadhibu mwenye mzaha naye mjinga atapata akili;
mwonye mwenye busara naye atapata maarifa.
26Anayemdhulumu baba yake na kumfukuza mama yake,
ni mtoto asiyefaa na mpotovu.
27Mwanangu, ukiacha kusikiliza mafundisho,
utapotea mara mbali na maneno ya hekima.
28Shahidi asiyefaa kitu huidhihaki haki;
na kinywa cha mwovu hubugia uovu.
29Adhabu iko tayari kwa wenye mzaha,
mijeledi imetayarishwa kuchapa migongo ya wapumbavu.

Methali19;1-29

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 15 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 18...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Mpigeni mawe mpaka afe! Kwa sababu amejaribu kukuvutia mbali na Mwenyezi-Mungu, Mungu wako, aliyekutoa utumwani nchini Misri. Hivyo, Waisraeli wote watasikia na kuogopa, na kamwe hawatafanya uovu kama huo.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

“Mtakapoishi katika miji ambayo Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, anawapa, huenda mkasikia kuwa watu fulani mabaradhuli miongoni mwenu, wamewashawishi watu wa mji wakisema, ‘Twende tukaabudu miungu mingine,’ miungu ambayo bado hamjawahi kuijua,
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

basi mtapeleleza na kufanya uchunguzi na kuuliza kwa makini; na kama ni kweli kuwa jambo la kuchukiza limetendeka kati yenu, hamna budi kuwaua kwa upanga watu wa mji huo; mtauangamiza kabisa mji huo na kuwaua ng'ombe wote kwa upanga.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

1Anayetafuta yake tu hujitenga na wenzake;
hukasirika akipewa shauri lolote jema.
2Mpumbavu hapendezwi na busara;
kwake cha maana ni maoni yake tu.
3Ajapo mwovu huja pia dharau;
pamoja na aibu huja fedheha.
4Maneno yaweza kuwa chemchemi ya hekima;
yenye kilindi kama bahari, kama kijito kinachobubujika.
5Si vizuri kumpendelea mtu mwovu,
na kumnyima haki mtu mwadilifu.
6Maneno ya mpumbavu huleta ugomvi;
kila anachosema husababisha adhabu.
7Kinywa cha mpumbavu humwangamiza mwenyewe;
mdomo wake ni mtego wa kumnasa yeye mwenyewe.
8Maneno ya msengenyaji ni kama kitoweo kitamu;
ambacho hushuka moja kwa moja mpaka tumboni.
9Mtu mvivu kazini mwake
ni ndugu yake mharibifu.
10Jina la Mwenyezi-Mungu ni mnara imara;
mwadilifu huukimbilia akawa salama.
11Lakini tajiri hudhani mali ni ngome yake;
anafikiri hayo ni ukuta mrefu unaomlinda.
12Majivuno ya moyoni huleta maangamizi,
lakini unyenyekevu huleta heshima.
13Kujibu kabla ya kusikiliza
ni upumbavu na jambo la aibu.
14Roho ya mtu huweza kustahimili ugonjwa,
lakini ukiwa umevunjika moyo, utastahimilije?
15Mtu mwenye akili hujipatia maarifa,
sikio la mwenye busara hutafuta maarifa.
16Zawadi humfungulia mtu milango;
huweza kumfikisha mtu mbele ya mkuu.
17Ajiteteaye kwanza huonekana msema kweli,
mpaka hapo mpinzani wake atakapoanza kumhoji.
18Kura hukomesha ubishi;
huamua kati ya wakuu wanaopingana.
19Ndugu aliyeudhiwa ni mgumu kuliko mji wa ngome;18:19 Ndugu … ngome: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
magomvi hubana kama makufuli ya ngome.
20Maneno ya mtu yaweza kumshibisha;
hutosheka kwa matokeo ya maneno yake.
21Ulimi una nguvu ya kufanya hai na kuua;
wanaopenda kuutumia watakula matunda yake.
22Anayempata mke amepata bahati njema;
hiyo ni fadhili kutoka kwa Mwenyezi-Mungu.
23Maskini huomba kwa unyenyekevu,
bali tajiri hujibu kwa ukali.
24Marafiki wengi waweza kumwangusha mtu,18:24 Marafiki wengi … kumwangusha mtu: Maana yake katika makala ya Kiebrania si dhahiri.
lakini wapo marafiki waaminifu kuliko ndugu.

Methali18;1-24

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 12 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 17...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Lakini nabii huyo au mtabiri wa ndoto atauawa, kwa sababu atakuwa amewafundisha uasi dhidi ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, aliyewatoa katika nchi ya Misri na kuwakomboa kutoka utumwani, ili muiache njia ambayo Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu aliwaamuru muifuatea. Hivyo ndivyo mtakavyokomesha uovu miongoni mwenu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

“Ikiwa ndugu yako wa tumbo moja, au mtoto wako wa kiume au wa kike, au mke wako umpendaye sana, au rafiki yako mwandani, atakushawishi kwa siri akisema, ‘Twende tukaabudu miungu mingine’, miungu ambayo wewe wala babu zenu hamuijui, au baadhi ya miungu ya watu wanaoishi karibu nanyi, au miungu ya watu waishio mbali toka ncha moja ya dunia hadi nyingine,
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

usikubali kushawishiwa, wala usimsikilize au kumhurumia, wala usimwachilie wala kumficha; bali utamuua. Wewe utakuwa wa kwanza kuchukua hatua ya kumuua, kisha watu wengine wote watafuata.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

1Afadhali mkate mkavu kwa amani,
kuliko karamu katika nyumba ya ugomvi.
2Mtumwa mwenye busara atachukua nafasi ya mwana mpumbavu,
atapata sehemu ya urithi wa jamaa hiyo.
3Ubora wa dhahabu ama fedha hupimwa kwa moto,
lakini Mwenyezi-Mungu ndiye apimaye mioyo ya watu.
4Mtenda maovu husikiliza maneno mabaya,
mwongo hutegea sikio ulimi mdanganyifu.
5Anayemdhihaki maskini anamtukana Muumba wake;
anayefurahia maafa hatakosa kuadhibiwa.
6Wazee huwaonea fahari wajukuu zao;
watoto huwaonea fahari wazazi wao.
7Maneno mazuri si kawaida kinywani mwa mpumbavu,
sembuse maneno ya uongo kinywani mwa kiongozi!
8Kwa mhongaji, hongo ni kama hirizi;
kila afanyacho hufanikiwa.
9Anayesamehe makosa hujenga urafiki,
lakini anayekumbusha makosa hutenga rafiki.
10Onyo kwa mwenye busara lina maana,
kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
11Afanyalo mtu mwovu ni kuasi tu;
mjumbe mkatili atatumwa dhidi yake.
12Afadhali kukutana na dubu jike aliyenyanganywa watoto wake,
kuliko kukutana na mpumbavu katika upumbavu wake.
13Mwenye kulipiza mema kwa mabaya,
mabaya hayataondoka nyumbani mwake.
14Kuanzisha ugomvi ni kama kufanya ufa kwenye bwawa;
achana na ugomvi kabla haujafurika.
15Kumsamehe mwenye hatia na kumwadhibu asiye na hatia
yote mawili ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu.
16Ya nini mpumbavu kuwa na fedha mkononi kununulia hekima,
wakati yeye mwenyewe hana akili?
17Rafiki wa kweli ni rafiki siku zote,
ndugu huzaliwa asaidie wakati wa taabu.
18Si jambo la akili kuweka rehani,
na kuwa mdhamini wa mtu mwingine.
19Anayependa ugomvi anapenda dhambi;
anayejigamba17:19 anayejigamba: Neno kwa neno; ainuaye sana mlango wake. anajitafutia maangamizi.
20Mwenye moyo mpotovu hafanikiwi,
na msema uongo hupatwa na maafa.
21Mtoto mpumbavu ni huzuni kwa baba yake,
na baba wa mpumbavu hana furaha.
22Moyo mchangamfu ni dawa,
bali moyo wenye huzuni hudhoofisha mwili.
23Mtu mbaya hupokea hongo kwa siri
ili apate kupotosha haki.
24Mtu mwenye busara lengo lake ni hekima,
lakini mpumbavu hupania kila kitu duniani.
25Mtoto mpumbavu ni huzuni kwa baba yake,
na uchungu kwa mama yake mzazi.
26Si vizuri kumtoza faini mtu asiye na hatia;
ni kosa kumchapa viboko muungwana.
27Asiyesema sana ana maarifa;
mtu mtulivu ni mwenye busara.
28Hata mpumbavu akinyamaza huonekana ana hekima;
akifunga mdomo wake huonekana kuwa mwenye akili.

Methali17;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.