Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 1 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 8...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki/mwezi mwingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Basi, tuzingatie kwa makini imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka mbinguni; Yesu, Mwana wa Mungu.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...
Huyu Kuhani Mkuu wetu anaelewa kabisa unyonge wetu; yeye mwenyewe alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu mwenye neema, tupokee huruma na neema ya kutusaidia wakati wa shida.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Wito wa Hekima
1 Taz Meth 1:20-21 Sikilizeni! Hekima anaita!
Busara anapaza sauti yake!
2Juu penye mwinuko karibu na njia,
katika njia panda ndipo alipojiweka.
3Karibu na malango ya kuingilia mjini,
mahali wanapoingia watu anaita kwa sauti:
4“Enyi watu wote, nawaita nyinyi!
Wito wangu ni kwa ajili ya binadamu.
5Enyi wajinga, jifunzeni kuwa na akili;
sikilizeni kwa makini enyi wapumbavu.
6Sikilizeni maana nitakachosema ni jambo muhimu;
midomoni mwangu mtatoka mambo ya adili.
7Kinywa changu kitatamka kweli tupu;
uovu ni chukizo midomoni mwangu.
8Kinywa changu kitatamka maneno ya kweli,
udanganyifu ni haramu midomoni mwangu.
9Kwa mtu mwelewa kila kitu ni wazi,
kwa mwenye maarifa yote ni sawa.
10Chagua mafundisho yangu badala ya fedha;
na maarifa badala ya dhahabu safi.
11“Mimi Hekima nina thamani kuliko johari;
chochote unachotamani hakiwezi kulingana nami.
12Mimi Hekima ninao ujuzi;
ninayo maarifa na busara.
13Kumcha Mwenyezi-Mungu ni kuchukia uovu.
Nachukia kiburi, majivuno na maisha mabaya;
nachukia na lugha mbaya.
14Nina uwezo wa kushauri na nina hekima.
Ninao ujuzi na nina nguvu.
15Kwa msaada wangu wafalme hutawala,
watawala huamua yaliyo ya haki.
16Kwa msaada wangu viongozi hutawala,
wakuu na watawala halali.8:16 tafsiri nyingine: Wakuu, mahakimu wa dunia.
17Nawapenda wale wanaonipenda;
wanaonitafuta kwa bidii hunipata.
18Utajiri na heshima viko kwangu,
mali ya kudumu na fanaka.
19Matunda yangu ni mazuri kuliko dhahabu safi,
faida yangu yashinda ile ya fedha bora.
20Natembea katika njia ya uadilifu;
ninafuata njia za haki.
21Mimi huwatajirisha wanaonipenda,
huzijaza tele hazina zao wanipendao.
22 Taz Ufu 3:14 “Mwenyezi-Mungu aliniumba mwanzoni mwa kazi yake,8:22 kazi yake: Makala ya Kiebrania: Njia yake.
zama za zama kabla ya kuwako kitu chochote.
23Nilifanywa mwanzoni mwa nyakati,
nilikuwako kabla ya dunia kuanza.
24Nilizaliwa kabla ya vilindi vya bahari,
kabla ya chemchemi zibubujikazo maji.
25Kabla ya milima haijaumbwa,
na vilima kusimamishwa mahali pake,
mimi nilikuwako tayari.
26Kabla Mungu hajaumba dunia na mashamba yake,
wala chembe za kwanza za mavumbi ya dunia.
27Nilikuwako wakati alipoziweka mbingu,
wakati alipopiga duara juu ya bahari;
28wakati alipoimarisha mawingu mbinguni,
alipozifanya imara chemchemi za bahari;
29wakati alipoiwekea bahari mpaka wake,
maji yake yasije yakavunja amri yake;
wakati alipoiweka misingi ya dunia.
30Nilikuwa pamoja naye kama fundi stadi,8:30 fundi stadi: Au Mtoto mdogo.
nilikuwa furaha yake kila siku,
nikishangilia mbele yake daima,
31nikifurahia dunia na wakazi wake,
na kupendezwa kuwa pamoja na wanadamu.
32“Sasa basi wanangu, nisikilizeni:
Heri wale wanaofuata njia zangu.
33Sikilizeni mafunzo mpate hekima,
wala msiyakatae.
34Heri mtu anayenisikiliza,
anayekaa kila siku mlangoni pangu,
anayekesha karibu na milango yangu.
35Anayenipata mimi amepata uhai,
amepata upendeleo kwa Mwenyezi-Mungu.
36Asiyenipata anajidhuru mwenyewe;
wote wanaonichukia wanapenda kifo.”


Methali8;1-36

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 28 June 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 7...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa “Leo,” akasema baadaye kwa njia ya Daudi maneno yaliyokwisha tajwa: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiwe wakaidi.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kama Yoshua angekuwa amewapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine. Kwa hiyo, basi, bado kuna kupumzika kwa watu wa Mungu. Maana, kila aingiaye mahali pa pumziko la Mungu atapumzika kutoka katika kazi yake kama vile pia Mungu alivyopumzika kutoka kazi yake. Basi, tujitahidi kuingia katika pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwetu atakayekataa kutii kama walivyofanya wao.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na uboho. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu. Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake yeye ambaye kwake tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

1Mwanangu, yashike maneno yangu,
zihifadhi kwako amri zangu.
2Zifuate amri zangu nawe utaishi;
yalinde mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
3Yafunge vidoleni mwako;
yaandike moyoni mwako.
4Iambie Hekima: “Wewe ni dada yangu”,
na Busara “Wewe ni rafiki yangu”.
5Vitakulinda mbali na mwanamke mbaya,
vitakuepusha na maneno matamu ya mwanamke mgeni.

Mwanamke mwasherati
6Siku moja dirishani mwa nyumba yangu,
nilichungulia nje kupitia viunzi vya dirisha,
7nikawaona vijana wengi wajinga,
na mmoja hasa aliyekuwa mpumbavu.
8Huyo alikuwa akitembea kwenye barabara ile,
karibu na kona alikoishi mwanamke fulani.
Basi akashika njia iendayo nyumbani kwa mwanamke huyo.
9Ilikuwa yapata wakati wa jioni,
giza na usiku vilikuwa vimeanza kuingia.
10Punde kijana akakutana na huyo mwanamke;
amevalia kama malaya, ana mipango yake.
11Alikuwa mwanamke wa makelele na mkaidi;
miguu yake haitulii nyumbani:
12Mara barabarani, mara sokoni,
katika kila kona ya njia hakosekani akivizia.
13Alimkumbatia kijana huyo na kumbusu,
na kwa maneno matamu, akamwambia:
14“Ilinilazimu kutoa tambiko zangu;
leo hii nimekamilisha nadhiri yangu.
15Ndio maana nimetoka ili nikulaki,
nimekutafuta kwa hamu nikakupata.
16Nimetandika kitanda changu vizuri,
kwa shuka za rangi za kitani kutoka Misri.
17Nimekitia manukato, manemane, udi na mdalasini.
18Njoo tulale pamoja mpaka asubuhi;
njoo tujifurahishe kwa mahaba.
19Mume wangu hayumo nyumbani,
amekwenda safari ya mbali.
20Amechukua bunda la fedha;
hatarejea nyumbani karibuni.”
21Alimshawishi kwa maneno mengi ya kubembeleza;
kijana akashawishika kwa maneno yake matamu.
22Hapo akamfuata huyo mwanamke moja kwa moja,
kama ng'ombe aendaye machinjioni,
kama paa arukiaye mtegoni.
23Hakutambua kwamba hiyo itamgharimu maisha yake,
mpaka alipojikuta amekuwa kama amechomwa mshale moyoni,
amekuwa kama ndege aliyenaswa wavuni.
24Sasa wanangu, nisikilizeni;
yategeeni sikio maneno ya kinywa changu.
25Msikubali kuongozwa na mwanamke kama huyo,
wala msipitepite katika mapito yake.
26Maana amewaangusha wanaume wengi;
ni wengi mno hao aliowachinja.
27Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu,
ni mahali pa kuteremkia mautini.

Methali7;1-27

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 27 June 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 6...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, kwa vile ahadi ya kuingia mahali pa pumziko bado ipo, na tuogope ili yeyote kati yenu asije akashindwa kupata pumziko hilo. Maana Habari Njema imehubiriwa kwetu kama vile ilivyohubiriwa kwa hao watu wa kale. Lakini ujumbe huo haukuwafaa chochote, maana waliusikia lakini hawakuupokea kwa imani.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, sisi tunaoamini tunapata pumziko hilo aliloahidi Mungu. Kama alivyosema: “Nilikasirika, nikaapa: ‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko.’” Mungu alisema hayo ingawa kazi yake ilikuwa imekwisha malizika tangu alipoumba ulimwengu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Maana Maandiko yasema mahali fulani kuhusu siku ya saba: “Mungu alipumzika siku ya saba, akaacha kazi zake zote.” Tena jambo hili lasemwa pia: “Hawataingia mahali pangu pa pumziko.” Basi, hiyo ahadi ya kuingia bado ipo, maana wale waliohubiriwa Habari Njema pale awali walishindwa kuingia humo kwa sababu walikosa kutii.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Maonyo manne
1Mwanangu, kama umejitolea kumdhamini jirani yako,
ikiwa umetoa ahadi yako kwa ajili ya mtu huyo,
2umejibana kwa maneno yako mwenyewe,
umejinasa kwa ahadi uliyofanya.
3Ujue kwamba uko chini ya mamlaka ya mwenzio,
lakini mwanangu, ukitaka kujiokoa, basi fanya hivi:
Mwendee mtu huyo mara moja umsihi akupe uhuru wako.
4Jitahidi usiache macho yako yapate usingizi,
wala kope za macho yako zisinzie.
5Jiokoe kwa kujitoa katika mtego huo,
mithili ya paa ama ndege amtorokavyo mwindaji.
6Ewe mvivu! Hebu ukamchungulie sisimizi,
fikiria namna yake ya kuishi ukapate hekima.
7Sisimizi hana kiongozi, ofisa, wala mtawala;
8lakini hujiwekea chakula wakati wa kiangazi,
hujikusanyia akiba wakati wa mavuno.
9Ewe mvivu, utalala hapo mpaka lini?
Utaamka lini katika usingizi wako?
10Wasema: “Acha nilale kidogo tu,
acha nisinzie kidogo!
Niache nikunje mikono nipumzike kidogo!”
11Wakati huo umaskini utakuvamia kama mnyanganyi,
ufukara utakufuata kama jambazi.6:11 Taz pia 24:33-34
12Mtu mwovu, mtu asiyefaa kitu,
huzururazurura akisema maneno mapotovu.
13Hukonyeza jicho kuwakosesha wengine,
huparuza kwa nyayo,
na kuashiria watu kwa vidole.
14Akiwa amejaa ulaghai moyoni hutunga maovu,
huzusha ugomvi kila mahali.
15Kutokana na hayo maafa yatamvamia ghafla,
ghafla atadhurika vibaya asiweze kupona tena.
16Kuna vitu sita anavyochukia Mwenyezi-Mungu;
naam, vitu saba ambavyo ni chukizo kwake:
17Macho ya kiburi,
ulimi mdanganyifu,
mikono inayoua wasio na hatia,
18moyo unaopanga mipango miovu,
miguu iliyo mbioni kutenda maovu,
19shahidi wa uongo abubujikaye uongo,
na mtu achocheaye fitina kati ya ndugu.

Onyo dhidi ya uasherati
20Mwanangu, shika maagizo ya baba yako,
wala usisahau mafundisho ya mama yako;
21yaweke daima moyoni mwako,
yafunge shingoni mwako.
22Yatakuongoza njiani mwako,
yatakulinda wakati ulalapo,
yatakushauri uwapo macho mchana.
23Maana amri hiyo ni taa,
na sheria hiyo ni mwanga.
Maonyo hayo na nidhamu yatuweka njiani mwa uhai.
24Yatakulinda mbali na mwanamke mbaya,
yatakuepusha na maneno matamu ya mwanamke mgeni.6:24 Taz 5:5 maelezo.
25Usimtamani mwanamke huyo kwa uzuri wake,
wala usikubali kunaswa kwa kope za macho yake.
26Mtu hupoteza kipande cha mkate kwa malaya,
lakini kwa mke wa mtu mwingine utapoteza uhai wako wote.
27Je, waweza kuweka moto kifuani
na nguo zako zisiungue?
28Je, waweza kukanyaga makaa ya moto
na nyayo zako zisiungue?
29Ndivyo alivyo mwanamume alalaye na mke wa mwenzake;
yeyote anayemgusa mwanamke huyo hataacha kuadhibiwa.
30Watu hawambezi sana mtu akiiba kwa sababu ya njaa;
31lakini akipatikana lazima alipe mara saba;
tena atatoa mali yote aliyo nayo.
32Mwanamume anayezini na mke wa mtu hana akili kabisa;
huyo hujiangamiza yeye mwenyewe.
33Atapata majeraha na madharau;
fedheha atakayopata haitamtoka.
34Maana wivu wa mume humfanya kuwa mkali kabisa;
wakati atakapolipiza kisasi hana cha kuhurumia.
35Hatakubali fidia yoyote;
wala kutulizwa na zawadi zako nyingi.

Methali6;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 26 June 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 5...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Shauli akajibu, “Nimefanya dhambi. Hata hivyo, unistahi sasa mbele ya wazee wa watu wangu na Waisraeli. Niruhusu nirudi pamoja nawe ili nikamwabudu Mwenyezi-Mungu, Mungu wako.” Basi, Samueli akarudi pamoja naye mpaka Gilgali na Shauli akamwabudu Mwenyezi-Mungu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kisha Samueli akasema, “Nileteeni hapa Agagi mfalme wa Waamaleki.” Agagi akamwendea Samueli akiwa mwenye furaha kwani alifikiri, “Uchungu wa kifo umepita.” Samueli akasema, “Kwa kuwa upanga wako umewafanya akina mama wengi wasiwe na watoto, ndivyo na mama yako atakavyokuwa bila mtoto miongoni mwa akina mama.” Akamkatakata Agagi vipandevipande mbele ya Mwenyezi-Mungu huko Gilgali.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kisha, Samueli akaenda Rama; na mfalme Shauli akarudi nyumbani kwake huko Gibea. Tangu siku hiyo, Samueli hakumwona tena Shauli, mpaka siku alipofariki. Hata hivyo Samueli alimlilia Shauli. Naye Mwenyezi-Mungu alisikitika kwamba alikuwa amemtawaza Shauli mfalme juu ya Israeli.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Onyo dhidi ya uasherati
1Mwanangu, sikia hekima yangu,
tega sikio usikilize elimu yangu.
2Ndipo utakapoweza kuhifadhi busara,
na midomo yako izingatie maarifa.
3Mdomo wa mwanamke mpotovu ni mtamu kama asali,
maneno yake ni laini kuliko mafuta;5:3-5 Kuhusu aya 3-5 Taz pia 2:16; 7:6-27; 22:14; Mhu 7:26
4lakini hatimaye ni mchungu kama pakanga,
ni mkali kama upanga wenye makali kuwili.
5Nyayo zake zaelekea chini mautini,
hatua zake zaenda kuzimu.
6Yeye haijali njia ya uhai,
njia zake ni za kutangatanga, wala hajui.
7Sasa enyi wanangu, nisikilizeni,
wala msisahau maneno ya kinywa changu.
8Iepushe njia yako mbali naye,
wala usiukaribie mlango wa nyumba yake.
9Usije ukawapa wengine heshima yako,
na wakatili miaka yako;
10wageni wasije wakajishibisha kwa mali yako,
na jasho lako likaishia nyumbani kwa mgeni.
11Mwishoni mwa maisha yako utaomboleza
wakati mwili wako utakapoangamizwa.
12Hapo utasema, “Jinsi gani nilivyochukia nidhamu,
na kudharau maonyo moyoni mwangu!
13Sikuisikiliza sauti ya waalimu wangu,
wala kuwategea sikio wakufunzi wangu.
14Sasa niko karibu kuangamia kabisa
mbali na jumuiya ya watu.”
15Mkeo ni kama kisima cha maji safi:
Kunywa maji ya kisima chako mwenyewe.
16Ya nini chemchemi zako zitawanywe mbali,
na vijito vya maji barabarani?
17Hiyo ni yako wewe mwenyewe,
wala usiwashirikishe watu wengine.
18Chemchemi yako na ibarikiwe,
umfurahie mke uliyemwoa ukiwa kijana.
19Ni mzuri kama ayala, apendeza kama paa.
Mahaba yake yakufurahishe kila wakati,
umezwe daima na pendo lake.
20Mwanangu, ya nini kutekwa na mwanamke mwasherati?
Ya nini kumkumbatia kifuani mwanamke mgeni?
21Kumbuka njia za mtu zi wazi mbele ya Mwenyezi-Mungu;
yeye anaona kila hatua anayochukua binadamu.
22Mtu mwovu hunaswa kwa uovu wake mwenyewe;
hukamatwa katika tanzi za dhambi yake mwenyewe.
23Yeye hufa kwa utovu wa nidhamu,
huangamia kwa sababu ya upuuzi wake mkuu.

Methali5;1-23

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.