Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 14 May 2018

Kikombe Cha Asubuhi ; 1Mambo ya Nyakati 3...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana...
Ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua
na kutupa kibali cha kuendelea tena kuiona leo hii
Si kwamba sisi ni wema sana,si kwamba sisi ni wazuri mno,
si kwa nguvu zetu wala si kwa akili zetu si kwa uwezo wetu
sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa neema/rehema ni kwa mapenzi yake Mungu wetu..
Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, wilayani Galilaya. Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa naye.

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Utukuzwe ee Mungu wetu,Usifiwe Baba wa Mbinguni,Uhimidiwe Jehovah
Uabudiwe Yahweh...!
Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho ni Alfa na Omega
Matendo yako ni makuu mno,Matendo yako ni ya ajabu
Neema yako yatutosha Mungu wetu...!

Yahweh tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na
kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe
wale wote waliotukosea
Jehovah utuepushe katika majaribu Mungu wetu tunaomba utuokoe
na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba
utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Wazazi wake walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka. Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi. Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari. Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki. Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza kuwabariki
wenye kuhitaji
Baba wa Mbinguni tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Jehovah ukatupe kama inavyokupendeza wewe.....

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,watoto,wazazi wetu
Familia/ndugu na wote wanao tuzunguka
Jehovah tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Yahweh tunaomba ukabariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Mungu wetu ukavitakase na kuvifunika kwa Damu ya Bwana wetu
Yesu Kristo
Baba wa Mbinguni ukatamalaki na kutuatamia
Mungu wetu tukawe salama rohoni
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatupe macho ya kuona na masikio ya 
kusikia sauti yako na kuitii
Mungu wetu tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Baba wa Mbinguni tukasimamie Neno lako amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu
Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Jehovah tukanene yaliyo yako
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema yako na Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Mfalme wa amani amani yako ikatawale na upendo ukadumu kati yetu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike
kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi

Siku ya tatu, walimkuta hekaluni kati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali. Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima. Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutendea hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.” Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?” Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia. Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake. Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.

Baba wa Mbinguni tunawaweka mikononi mwako wote
wanaokutafuta/kukuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
Jehovah tunaomba ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Yahweh tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Mungu wetu tunaomba ukawape macho ya rohoni na masikio ya kusikia
Baba wa Mbinguni ukaonekane katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukasikie na ukapokee sala/maombi yetu
Baba wa Mbinguni ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kutendea kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Krisro na Upendo wa Mungu Baba
ukawe nanyi daima.....
Nawapenda.





Wana wa mfalme Daudi

1Hawa ndio wana wa mfalme Daudi waliozaliwa wakati alipokuwa huko Hebroni:
Amnoni, mzaliwa wake wa kwanza; mama yake aliitwa Ahinoamu, Myezreeli; wa pili Danieli ambaye mama yake alikuwa Abigaili, Mkarmeli; 2wa tatu alikuwa Absalomu, ambaye mama yake alikuwa Maaka, bintiye Talmai mfalme wa Geshuri; wa nne alikuwa Adoniya, ambaye mama yake alikuwa Hagithi; 3wa tano alikuwa Shefatia, ambaye mama yake alikuwa Abitali; na wa sita alikuwa Ithreamu, ambaye mama yake alikuwa Egla.
4Wote sita, walizaliwa Hebroni ambako Daudi alitawala kwa muda wa miaka saba na nusu. Huko Yerusalemu, alitawala kwa muda wa miaka thelathini na mitatu. 5Wafuatao ni wana wa mfalme Daudi alipokuwa Yerusalemu: Mkewe Bathshua, bintiye Amieli, alimzalia wana wanne: Himea, Shobabu, Nathani na Solomoni.
6Na mbali na hao alikuwa na wana wengine tisa: Ibhari, Elishua, Elifaleti, 7Noga, Nefegi, Yafia, 8Elishama, Eliada na Elifeleti. 9Hao wote walikuwa wana wa Daudi, mbali na wale wengine waliozaliwa na masuria wake. Daudi alikuwa na binti pia, aliyeitwa Tamari.

Wazawa wa mfalme Solomoni

10Wazawa wa mfalme Solomoni: Solomoni alimzaa Rehoboamu, aliyemzaa Abiya, aliyemzaa Asa, aliyemzaa Yehoshafati, 11aliyemzaa Yehoramu, aliyemzaa Ahazia, aliyemzaa Yoashi, 12aliyemzaa Amazia, aliyemzaa Uzia, aliyemzaa Yothamu, 13aliyemzaa Ahazi, aliyemzaa Hezekia, aliyemzaa Manase, 14aliyemzaa Amoni, aliyemzaa Yosia. 15Yosia alikuwa na wana wanne: Yohanani, mzaliwa wake wa kwanza, wa pili Yehoyakimu, wa tatu Sedekia na wa nne Shalumu. 16Yehoyakimu alikuwa na wana wawili: Yekonia na Sedekia.
17Wana wa Yekonia aliyechukuliwa mateka na Wababuloni walikuwa saba: Shealtieli, 18Malkiramu, Pedaya, Shenazari, Yekamia, Hoshama na Nedabia. 19Wana wa Pedaya walikuwa Zerubabeli na Shimei. Zerubabeli alikuwa na wana wawili: Meshulamu na Hanania, na binti mmoja, jina lake Shelomithi. 20Zerubabeli pia alikuwa na wana wengine watano: Hashuba, Oheli, Berekia, Hasadia na Yushab-hesedi. 21Wana wa Hanania walikuwa Pelatia na Yeshaya. Yeshaya alimzaa Refaya, aliyemzaa Arnani, aliyemzaa Obadia, aliyemzaa Shekania.3:21 aya hii Kiebrania si dhahiri. 22Shekania alimzaa Shemaya. Wana wa Shemaya walikuwa sita: Hatushi, Igali, Baria, Nearia na Shafati. 23Nearia alikuwa na wana watatu: Eliehonai, Hizkia na Azrikamu. 24Eliehonai alikuwa na wana saba: Hodavia, Eliashibu, Pelaya, Akubu, Yohanani, Delaya na Anani.



1Mambo ya Nyakati3;1-24


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 11 May 2018

Kikombe Cha Asubuhi ; 1Mambo ya Nyakati 2...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana
Tumshukuru Mungu katika yote....

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majuku yetu
Utukuzwe ee Mungu wetu,Usifiwe Baba wa Mbinguni
Uhimidiwe Jehovah,Uabudiwe Yahweh...
Matendo yako ni makuu mno,Matendo yako ni ya ajabu,
Matendo yako yanatisha...
Neema yako yatutosha ee mungu wetu...!!


Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na sheria, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele za Bwana. Katika sheria ya Bwana imeandikwa: “Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana.” Pia walikwenda ili watoe sadaka: Hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika sheria ya Bwana. Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye. Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Kristo wa Bwana. Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na sheria, Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu, akisema: “Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, umruhusu mtumishi wako aende kwa amani. Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu ulioleta, ambao umeutayarisha uonekane na watu wote: Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli.”


Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Jehovah nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe 
wale wote waliotukosea
Mungu wetu utuepushe katika majaribu Yahweh utuokoe na 
yule mwovu na kazi zake zote
Ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni
utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo 
wa Nazareti,yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..

Baba yake Yesu na mama yake walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto. Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu; na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako.”


Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Yahweh nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Jehovah tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwabariki
wenye kuhitaji
Baba wa Mbinguni tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,watoto,wazazi wetu
familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Yahweh tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Jehovah tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukabariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase na kuvifunika kwa Damu 
ya Bwana wetu Yesu Kristo
Yahweh ukatamalaki na kutuatamia
Mungu wetu tukawe salama rohoni
Baba wa Mbinguni ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Jehovah ukatupe neema ya kufuata njia zako Mungu wetu
tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote za maisha yetu
Mfalme wa amani tunaomba amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Baba wa Mbinguni ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Yahweh tukanene yaliyo yako,ukatupe hekima na busara Mungu wetu
Baba wa Mbinguni ukatufanye chombo chema Mungu wetu
nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi


Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa. Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana. Saa hiyohiyo, alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na kueleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.

Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wote 
wanaokutafuta na kukuomba kwa bidii na imani
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
Yahweh tunaomba ukawaponye kimwili na kiroho pia
Jehovah ukaonekane katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea na kufuata njia zako
nazo zikawaweke huru
Ukawape macho ya kuona Mungu wetu na amasikio ya kusikia sauti yako
Ee Baba tunaomba ukasikie na ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukajibu sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Yesu Kristo kwakuwa nami
Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea kama inavyompendeza yeye
Nawapenda.

Wazawa wa Yuda

1Israeli alikuwa na wana wa kiume kumi na wawili: Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuluni, 2Dani, Yosefu, Benyamini, Naftali, Gadi na Asheri. 3Wana wa Yuda waliozaliwa na Bethshua, mkewe Mkanaani, walikuwa Eri, Onani na Shela. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu mbele ya Mwenyezi-Mungu, basi Mwenyezi-Mungu akamuua. 4Na Tamari, mkwewe, alimzalia wana wawili: Peresi na Zera. Jumla, wana wa Yuda walikuwa watano.
5Peresi alikuwa na wana wawili: Hesroni na Hamuli. 6Zera nduguye alikuwa na wana watano: Zimri, Etheni, Hemani, Kalkoli na Dara. 7Mwana wa Karmi, alikuwa Akari. Huyu aliwaletea Waisraeli taabu kwa sababu alijiwekea nyara zilizokuwa zimewekwa wakfu. 8Ethani alikuwa na mwana mmoja, jina lake Azaria.

Nasaba ya mfalme Daudi

9Wana wa Hesroni walikuwa Yerameeli, Ramu na Kelubai. 10Ramu alimzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Nashoni, mkuu wa kabila la Yuda. 11Nashoni alimzaa Salma, Salma akamzaa Boazi, 12Boazi akamzaa Obedi, Obedi akamzaa Yese. 13Yese aliwazaa Eliabu, mwanawe wa kwanza, wa pili Abinadabu, wa tatu Shimea, 14wa nne Nethaneli, wa tano Radai, 15wa sita Osemu na wa saba Daudi. 16Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa watatu: Abishai, Yoabu na Asaheli. 17Abigaili alimzaa Amasa ambaye baba yake alikuwa Yetheri, Mwishmaeli.

Wazawa wa Hesroni

18Kalebu, mwana wa Hesroni, kutokana na wake zake wawili, Azuba na Yeriothi, aliwazaa Yesheri, Shaobabu na Ardoni. 19Azuba alipofariki, Kalebu alimwoa Efratha aliyemzalia Huri. 20Huri alimzaa Uri, naye Uri akamzaa Besaleli.
21Hesroni alipokuwa na umri wa miaka sitini, alimwoa binti Makiri, dada yake Gileadi. Huyo alimzalia mwana jina lake Segubu. 22Segubu alimzaa Yairi ambaye alitawala miji mikubwa ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi. 23Lakini falme za Geshuri na Aramu ziliwashambulia na kuwanyanganya miji ya Haroth-yairi, Kenathi na vijiji vyake, jumla miji sitini. Hao wote walikuwa wazawa wa Makiri, baba yake Gileadi. 24Baada ya Hesroni kufariki, Kalebu alimwoa Efratha,2:24 Kalebu alimwoa Efratha: Kiebrania: Huko Kalebu Efratha. mjane wa Hesroni, baba yake. Efratha alimzalia Kalebu mwana jina lake Ashuri, aliyekuwa mwanzilishi wa mji wa Tekoa.

Wana wa Yerameeli

25Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, alikuwa na wana watano: Ramu, mzaliwa wake wa kwanza, Buna, Oreni, Osemu na Ahiya. 26Yerameeli alikuwa na mke mwingine jina lake Atara. Huyu alimzalia Yerameeli mwana, jina lake Onamu. 27Wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, Yamini na Ekeri. 28Wana wa Onamu walikuwa Shamai na Yada. Nao wana wa Shamai walikuwa Nadabu na Abishuri.
29Abishuri alioa mke, jina lake Abihaili, naye akamzalia wana wawili: Abani na Molidi. 30Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu; lakini Seledi alifariki bila watoto.
31Apaimu alikuwa na mwana mmoja aliyeitwa Ishi. Ishi alimzaa Sheshani, na Sheshani akamzaa Alai. 32Yada, nduguye Shamai, alikuwa na wana wawili: Yetheri na Yonathani. Lakini Yetheri alifariki bila watoto. 33Yonathani alikuwa na wana wawili: Pelethi na Zaza. Wote hao ni wazawa wa Yerameeli. 34Sheshani hakuwa na watoto wa kiume; alikuwa na binti tu. Hata hivyo, alikuwa na mtumwa wa Kimisri, jina lake Yarha. 35Hivyo, Sheshani akamwoza Yarha mtumwa wake, mmoja wa binti zake, naye akamzalia mwana jina lake Atai. 36Atai alimzaa Nathani, Nathani akamzaa Zabadi. 37Zabadi akamzaa Eflali, Eflali akamzaa Obedi, 38Obedi akamzaa Yehu, Yehu akamzaa Azaria, 39Azaria akamzaa Helesi, Helesi akamzaa Eleasa, 40Eleasa akamzaa Sismai, Sismai akamzaa Shalumu, 41Shalumu akamzaa Yekamia, na Yekamia akamzaa Elishama.

Wazawa wengine wa Kalebu

42Mzaliwa wa kwanza wa Kalebu, nduguye Yerameeli, aliitwa Mesha. Mesha alimzaa Zifu, Zifu akamzaa Maresha, Maresha akamzaa Hebroni.2:42 Hebroni: Kiebrania si dhahiri. 43Hebroni alikuwa na wana wanne: Kora, Tapua, Rekemu na Shema. 44Shema alikuwa baba yake Rahamu na babu yake Rekemu. Rekemu nduguye Shema alimzaa Shamai, 45Shamai akamzaa Maoni, na Maoni akamzaa Beth-suri. 46Kalebu alikuwa na suria, jina lake Efa. Huyu alimzalia wana wengine watatu: Harani, Mosa na Gazezi. Harani alimzaa Gazezi. 47Yadai alikuwa na wana sita: Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa na Shaafu. 48Kalebu alikuwa na suria mwingine jina lake Maaka. Huyu alimzalia wana wawili: Sheberi na Tirhana. 49Maaka alimzalia Kalebu wana; Shaafu mwanzilishi wa mji wa Madmana, na Sheva, mwanzilishi wa mji wa Makbena na Gibea. Kalebu alikuwa pia na binti, jina lake Aksa.
50Kalebu alikuwa na wazawa wengine pia kwa mkewe Efratha. Huri, mzaliwa wake wa kwanza, alikuwa na wana watatu: Shobali, mwanzilishi wa mji wa Kiriath-yearimu, 51wa pili Salma, mwanzilishi wa mji wa Bethlehemu, na wa tatu Herefu, mwanzilishi wa mji wa Bethi-gaderi. 52Shobali, mwanzilishi wa mji wa Kiriath-yearimu, alikuwa pia babu yao watu wa Haroe, na nusu ya wakazi wa mji wa Menuhothi, 53pamoja na koo zifuatazo zilizoishi Kiriath-yearimu: Waithri, Waputhi, Washumathi na Wamishrai. (Wasorathi na Waeshtaoli walitokana na watu hao).
54Salma, mwanzilishi wa mji wa Bethlehemu alikuwa babu ya Wanetofathi, Waatroth-beth-yoabu na nusu ya Wamenahathi yaani Wasori.
55Jamaa zifuatazo za waandishi ziliishi katika mji wa Yabesi: Watirathi, Washimeathi na Wasukathi. Wao ndio Wakeni waliotoka katika uzao wa Hamathi, aliyekuwa babu yao waliokuwa wa ukoo wa Warekabu.




1Mambo ya Nyakati2;1-55


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 10 May 2018

Maisha-Lifestyle;[Wanawake na imani]-Majibu ya da'Rose wa Mbeyela-Ni neema ya Mungu..


Maisha yangu mimi ni Mungu....




Asante sana da'Rose, kwanza kwakupokea na kuchukua wakati wako kutujibu
Mungu aendelee kukubariki pamoja na familia yako..
Utukufu tumrudishie Mungu wetu Muumba wa vyote....

Wapendwa nafikiri kunakitu tumejifunza kupitia video hii

Unaweza kumfuta -YouTube;Rose Mwinuka

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Kikombe Cha Asubuhi ; Tumemaliza Kitabu cha -2 Wafalme ,Leo tunaanza kitabu Cha 1Mambo ya Nyakati 1...




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana...
Tunamshukuru Mungu wetu kwa kutupa neema ya kuweza
kupitia kitabu cha "Wafalme" Asante sana Mungu wetu kwa nafasi hii
Kwa imani yote tuliyojifunza kupitia kitabu hiki yatakuwa ndani yetu
pia na faida kwetu na kwa wengine....

 Leo tunaanza Kitabu cha "1Mambo ya Nyakati"Mungu wetu tunaomba
tunapoanza kusoma Neno lako kupitia kitabu hiki,ukatupe macho
ya rohoni,masikio,uelewa na kutambua..
Mungu wetu tukasome na kuhifadhi pia elimu hii ikawafae na wengine
Ee Baba tunaomba ukatuongoze...!!

Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote nchini kote wahesabiwe. Sensa hiyo ilikuwa mara ya kwanza, wakati Kurenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria. Basi, wote waliohusika walikwenda kuhesabiwa kila mtu katika mji wake. Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya, na kwa vile alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi, alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yudea, alikozaliwa mfalme Daudi. Alikwenda kuhesabiwa pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mjamzito. Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia, akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.

Tunakushukuru Mungu wetu kwa siku hii pia
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa kibali
cha kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana,wala si kwamba sisi 
ni wazuri mno,si kwa nguvu zetu wala utashi wetu
Si kwa uwezo wala akili zetu sisi kuwa hivi tulivyo
Ni kwa neema/rehema zako ni kwa mapenzi yako Mungu wetu
Sifa na Utukufu tunakurudishia Baba wa Mbinguni...!!

Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao. Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana. Malaika akawaambia, “Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kubwa itakayowapata watu wote. Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana. Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini.” Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema: “Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu anaowafadhili!”


Tazama jana imepita Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho
ni siku nyingine Jehovah
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Yahweh nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe
wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuokoe na yule mwovu
na kazi zake zote
Baba wa Mbinguni tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Mungu wetu utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu
Yesu Kristo wa Nazareti,yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate
kupona...

Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: “Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha.” Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini. Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake. Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji. Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake. Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Yahweh nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Jehovah tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza kuwabariki
wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Mfalme wa amani tunaomba amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,watoto,wazazi wetu
familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Baba wa Mbinguni tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote
tunavyovimiliki
Jehovah tunaomba  ukatamalaki na kutuatamia
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase na kuvifunika kwa Damu ya Bwana 
wetu Yesu Kristo..
Mungu wetu tukawe salama rohoni
Baba wa Mbinguni ukatupe macho ya kuona na masikio ya 
kusikia sauti yako na kuitii
Jehovah ukatupe neema ya kufuata njia zako Mungu wetu tukasimamie
Neno lako amri na sheria zako siku zote za maisha yetu
Yahweh ukatupe akili ya kutamnbua mema na mabaya
Baba wa Mbinguni ukaonekane katika maisha yetu
Neema yako na Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
mkono wako wenye nguvu ukatuguse ee Mungu wetu
Ukatufanye chombo chema Baba wa Mbinguni nasi tukatumike
kama inavyokupendeza wewe..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi


Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
Tazama wenye shida/tabu Mungu wetu
Tazama watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
Yahweh tunaomba ukamguse kila mmoja na mahitaji yake
Jehovah ukaonekane katika maisha yao
Baba wa Mbinguni ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Mungu wetu tunaomba ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia
zako Mungu wetu ukawape macho ya rohoni
Yahweh tunaomba ukasikie kulia kwao Mungu wetu tunaomba
 ukawafute machozi yao
Baba wa Mbinguni tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukapokee sala/maombi yetu Jehovah ukawatendee
sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwa kuwanami/kunisoma
Baba wa Mbinguni akawabariki na kuwatendea kama inavyompendeza yeye..
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukawe nanyi Daima...
Nawapenda.

Toka Adamu hadi Abrahamu

(Mwa 5:1-32; 10:1-32; 11:10-26)

1Adamu alimzaa Sethi, Sethi akamzaa Enoshi, Enoshi akamzaa Kenani, 2Kenani akamzaa Mahalaleli, Mahalaleli akamzaa Yaredi, 3Yaredi akamzaa Henoki, Henoki akamzaa Methusela. Methusela alimzaa Lameki, 4Lameki akamzaa Noa. Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi.
5Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi. 6Wana wa Gomeri walikuwa Ashkenazi, Difathi na Togama. 7Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu. 8Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misri, Puti na Kanaani. 9Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani. 10Kushi alimzaa Nimrodi, aliyekuwa mtu shujaa wa kwanza duniani.
11Wazawa wa Misri ni Waludi, Waanamu, Walehabi, Wanaftuhi, 12Wapathrusi Wakaftori na Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti). 13Wana wa Kanaani walikuwa Sidoni, mzaliwa wake wa kwanza, na Hethi. 14Kanaani pia ndiye babu yao Wayebusi, Waamori, Wagirgashi, 15Wahivi, Waarki, Wasini, 16Waarvadi, Wasemari na Wahamathi.
17Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuri, Arpaksadi, Ludi, Aramu, Usi, Huli, Getheri na Mesheki. 18Arpaksadi alimzaa Shela, Shela akamzaa Eberi. 19Eberi alikuwa na wana wawili; mmoja wao aliitwa Pelegi, (kwa maana wakati wake watu walikuwa wametawanyika duniani), na ndugu yake aliitwa Yoktani. 20Wana wa Yoktani walikuwa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera, 21Hadoramu, Uzali, Dikla, 22Obali, Abimaeli, Sheba, 23Ofiri, Havila na Yobabu. Hao watu ni wana wa Yoktani.
24Ukoo wa Abrahamu kutokea Shemu ni kama ifuatavyo: Shemu alimzaa Arpaksadi, naye Arpaksadi akamzaa Shela. 25Shela akamzaa Eberi, Eberi akamzaa Pelegi, Pelegi akamzaa Reu; 26Reu akamzaa Serugi, Serugi akamzaa Nahori, Nahori akamzaa Tera, 27na Tera akamzaa Abramu, ambaye ndiye Abrahamu.

Wazawa wa Ishmaeli

(Mwa 25:12-16)

28Abrahamu alikuwa na watoto wawili wa kiume: Isaka na Ishmaeli. 29Hivi ndivyo vizazi vyao: Mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli alikuwa Nebayothi na wengine ni Kedari, Adbeeli, Mibsamu, 30Mishma, Duma, Masa, Hadadi, Tema, 31Yeturi, Nafishi na Kedema. Hao ndio wana wa Ishmaeli.
32Abrahamu alikuwa na suria aliyeitwa Ketura. Ketura alimzalia Abrahamu: Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua. Wana wa Yokshani walikuwa Sheba na Dedani. 33Wana wa Midiani walikuwa: Efa, Eferi, Henoki, Abida na Eldaa. Wote hao walikuwa wazawa wa Ketura.

Wazawa wa Esau

(Mwa 25:12-16)

34Isaka, mwana wa Abrahamu, alikuwa na wana wawili: Esau na Israeli. 35Wana wa Esau walikuwa Elifazi, Reueli, Yeushi, Yalamu na Kora. 36Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Sefo, Gatamu, Kenazi, Timna na Amaleki. 37Wana wa Reueli walikuwa Nahathi, Zera, Shama na Miza.

Wazawa wa asili wa Edomu

(Mwa 36:20-30)

38Wana wa Seiri walikuwa Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, Dishoni, Eseri na Dishani. 39Wana wa Lotani walikuwa wawili: Hori na Homamu. Lotani alikuwa na dada yake aliyeitwa Timna. 40Wana wa Shobali walikuwa Alvani, Manahathi, Ebali, Shefi1:40 Shefi: Mwa 36:23: Shefo. na Onamu. Wana wa Sibeoni walikuwa Aya na Ana. 41Mwana wa Ana alikuwa Dishoni; na wana wa Dishoni walikuwa Hamrani,1:41 Hamrani: Mwa 36:26: Hemdani. Eshbani, Ithrani na Kerani. 42Wana wa Eseri walikuwa Bilhani, Zaawani na Akani; na wana wa Dishoni1:42 Dishoni: Mwa 36:26: Dishani. walikuwa Usi na Arani.

Wafalme wa Edomu

(Mwa 36:31-39)

43Wafuatao ndio wafalme waliotawala nchi ya Edomu kabla mfalme yeyote hajatawala Waisraeli: Bela mwana wa Beori alitawala nchi ya Edomu, akiwa na makao yake makuu katika mji wa Dinhaba. 44Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra alitawala badala yake. 45Yobabu alipofariki, Hushamu wa nchi ya Watemi alitawala badala yake. 46Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi alitawala badala yake, makao yake makuu yakiwa katika mji wa Avithi. Huyu ndiye aliyewapiga na kuwashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu. 47Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka alitawala badala yake. 48Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ulio karibu na mto Eufrate, alitawala badala yake. 49Shauli alipofariki, Baal-hanani mwana wa Akbori alitawala badala yake. 50Baal-hanani alipofariki, Hadadi kutoka Pai alitawala badala yake na jina la mkewe Akbori lilikuwa Mehetabeli, binti Matredi, binti Mezahabu. 51Naye Hadadi akafariki.
Wakuu wa makabila ya Edomu walikuwa Timna, Alva, Yethethi, 52Oholibama, Ela, Pinoni, 53Kenazi, Temani, Mibsari, 54Magdieli na Iramu. Hao ndio wakuu wa makabila ya Edomu.





1Mambo ya Nyakati1;1-54


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 9 May 2018

PICHA NA HABARI ZA USIKU WA WASATU, BIRMINGHAM, UINGEREZA, APRILI 28



Na Freddy Macha


Jumuiya ya wasanii Watanzania Uingereza (WASATU) ilichemsha supu, ukumbi wa Heartlands , Birmigham, Uingereza Jumamosi iliyopita. Makutano haya yalikuwa pia sehemu ya mchango mahususi kusaidia wasichana wanaopewa mimba kabla ya kuwa watu wazima, kitongoji cha Tengeru, Arusha. Fedha zilikusanywa na mjasiria mali mkazi wa Birmingham, Mtanzania Sia Travel. Sia alijaa mlangoni akihakikisha kila senti iiliyolipwa na wahudhuriaji watashiba chakula , sanaa usiku kucha na kuwafariji vigoli wetu.
WASATU iliyoundwa mwaka 2016 chini ya udhamini wa Balozi wetu Uingereza, Mhe Asha Rose Migiro, inakutanisha wasanii wa ala mbalimbali chini ya viongozi- mwanamuziki na mcheza sarakasi mwenye nidhamu ya hali yajuu, Fab Moses na mtangaza mapishi ya Kitanzania, Uingereza, Bi Neema Kitilya, aliyetulizana kama shingo ya twiga.
Mwaka jana, 2017, shughuli hii ilifanywa Northampton na asilimia 20 ya kipato iliwafikia Watanzania waliofikwa na maafa ya mafuriko ya maji.







Warembo wa kujitolea, walioonesha mavazi yaliyoandaliwa na kampuni ya “All Things African” (inayoendeshwa na Mtanzania, mchapa kazi, asiyejua uvivu kabila gani, Hamida Mbaga). Toka kushoto, Yvonne Waweru, Georgeous Katega, Victoire Koleilas, Maureen Tibenda

Viongozi wa WASATU – Neema Kitilya na Fab Moses wakijadiliana huku shughuli zikikwea minazi na kuta

Fahari ya Tanzania – imesambazwa meza ya bidhaa mseto na “All Things African”

Mcheza ngoma aliyepitia mitihani mikali na vikundi maarufu vya mila zetu- Kibisa na Muungano - Likiwa Ismail- akionesha SINDIMBA – bila aibu, staha wala wasiwasi.


Rama Sax akipuliza vitu. Zamani alipiga na Simba Wanyika akashiriki kurekodi wimbo wa “Sina Makosa”. Rama Sax ni pia mwimbaji mahiri

Baadhi ya vyakula vya Kitanzania

Msanii wa mapishi Neema John aliyechangia kazi njema na Neema Kitilya.

Wageni toka Tanzania na Uganda. Huyo Mganda (kushoto) ni mwanafunzi wa lugha ya Kiswahili

Mpiga Gitaa mkuu wetu, Jioni Ticha na kipande cha kuku baada ya kazi jukwaani. Alisafiri toka Leeds. Mbali sana na hapa

Watanzania wakichangamkia shughuli
Sia Travel akihamasika. Hakupitwa

Mwanamuziki Saidi Kanda,(aliyesimama) mbabe na mtukuzaji wa vyombo asilia vya muziki wa Kitanzania, akijumuika na Wabongo nadhif, waliokuwemo

Mwandishi na mwanamuziki, F Macha pamoja na wasanii Likiwa Ismail (ngoma) na Rama Sax.



Shukrani...
kwa habari na Matukio nitumie kupitia Email;rasca@hotmail.co.uk

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.