Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 14 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 12...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu na kumsifu Daima..

Mshangilieni Mwenyezi-Mungu, enyi nchi zote! Mwabuduni Mwenyezi-Mungu kwa furaha, nendeni kwake mkiimba kwa shangwe! Jueni kwamba Mwenyezi-Mungu ni Mungu. Yeye ndiye aliyetuumba, nasi ni mali yake; sisi ni watu wake, ni kondoo wa malisho yake. Pitieni milango ya hekalu lake kwa shukrani, ingieni katika nyua zake kwa sifa. Mshukuruni na kulisifu jina lake. Mwenyezi-Mungu ni mwema; fadhili zake zadumu milele, na uaminifu wake katika vizazi vyote.

Tunakushuru eeh Mungu wetu,Baba yetu,Mwamba wetu,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi..Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..
Asante kwa yote uliyotutendea/unayoendelea kututendea,Imani na Tumaini tunaweka kwako..

Asante kwa kutuchagua tena kuendelea  na kutupa kibali cha kuiona siku hii Baba wa Mbingu..Neema/Rehema zako zatutosha Mwenyezi-Mungu,Faraja yako inatutosha Baba,Upendo wako wadumu milele,Hakuna wa kufanana nawe Jehovah..!! Hakuna na hatokuwepo Yahweh..!!
Mungu usiye sinzia wala kulala..Mungu unayejibu na kutenda,Mungu unayebariki,Mungu uponyae..wewe watosha Baba wa Mbinguni...wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho Yahweh..!!
Mfalme wa Amani tuyaweka maisha yetu mikononi mwako..Baba ukatubariki tuingiapo/tutokapo,vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Jehovah..!
Mfalme wa Amani ukabariki Kazi zetu,Bishara zetu,Masomo na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana wetu Yesu Kristo..

Baba ukatutakase Miili yetu na Akili zetu..Ukatuokoe na yule Mwovu na kazi zake zote..Ukatufunike na Damu ya mwanao Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..Yeye aliteseka pale msalabani ili sisi tupate kupona..
Yahweh..!! Tazama wenye Shida/Tabu, wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali,waliokuwa vifungoni,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao..
Baba tunaomba kwa mkono wako ukawaguse na kuwaponya..wapate kupona kimwili na kiroho,,Baba ukaonekane kwenye  shida zao..
Baba tunakuja mbele zako kwa kujinyenyekeza na tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Jehovah..! kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutokujua..
Baba tunaomba nasi utupe Neema yakuweza kuwasamehe wale waliotukosea..

Ee Mwenyezi-Mungu, utusikie; utusamehe ee Mwenyezi-Mungu. Ee Mwenyezi-Mungu, kwa hisani yako utusikie na kuchukua hatua, wala usikawie, ee Mungu wangu, kwa ajili ya mji huu na watu hawa wanaoitwa kwa jina lako!

Asante Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako,Tunakusifu na kukushukuru katika yote..Tukiamini ya kwamba wewe ni Mungu wetu na Mwokozi wetu..
Amina..!!

Muwe na wakati mwema  wote 

mliopita hapa na Mungu aendelee kuonekana Maishani mwenu.





Pasaka
(Kumb 16:1-8)

1 Taz Lawi 23:5; Hes 9:1-5; Kumb 16:1-2 Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose na Aroni, walipokuwa bado nchini Misri, 2“Mwezi huu utakuwa kwenu mwezi wa kwanza wa mwaka. 3Iambieni jumuiya yote ya Waisraeli kwamba mnamo siku ya kumi ya mwezi huu, mtachukua mwanakondoo mmoja kwa kila jamaa moja. 4Kama jamaa moja ni ndogo mno hata isiweze kumaliza kondoo mmoja, itashirikiana na jamaa jirani kadiri ya idadi ya watu wake; kisha watachagua mnyama ambaye kila mtu ataweza kula. 5Mwanakondoo huyo asiwe na kilema chochote, awe wa kiume na wa mwaka mmoja. Anaweza kuwa mwanakondoo au mwanambuzi. 6Mtamweka mnyama huyo mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi huu. Siku hiyo, jumuiya yote ya Waisraeli watawachinja wanyama hao wakati wa jioni. 7Kisha, watachukua damu ya hao wanyama na kupaka kwenye miimo na vizingiti vya kila nyumba watakamolia wanyama hao. 8Wataila nyama hiyo usiku huohuo baada ya kuichoma; wataila pamoja na mkate usiotiwa chachu na mboga chungu za majani. 9Imekatazwa kuila ikiwa mbichi au imechemshwa kwa maji, bali lazima ichomwe yote, pamoja na kichwa, miguu na nyama zake za ndani. 10Hali kadhalika msibakize nyama yoyote mpaka asubuhi. Nyama yoyote itakayobaki hadi asubuhi mtaiteketeza motoni. 11Na hivi ndivyo mtakavyomla mnyama huyo: Mtakuwa mmejifunga mikanda viunoni mwenu, mmevaa viatu na fimbo zenu mikononi. Tena mtamla kwa haraka. Hiyo ni Pasaka ya Mwenyezi-Mungu.
12“Usiku huo, nitapita katika nchi ya Misri na kuwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri, watu kwa wanyama. Nitaiadhibu miungu yote ya Misri. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu. 13Basi, ile damu itakuwa ishara yenu ya kuonesha nyumba mtakamokuwa. Nami nitakapoiona hiyo damu, nitawapita nyinyi, na hamtapatwa na dhara lolote wakati nitakapoipiga nchi ya Misri. 14Taz Kut 23:15; 34:18; Lawi 23:6-8; Hos 28:17-25; Kumb 16:3-8 Vizazi hata vizazi mtaadhimisha tukio hilo kwa sikukuu kubwa kwa heshima yangu mimi Mwenyezi-Mungu. Hilo litakuwa agizo la milele kwenu.”

Sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu

15Mwenyezi-Mungu akasema, “Kwa muda wa siku saba, mtakula mikate isiyotiwa chachu. Siku ya kwanza ya siku hizo saba, mtaondoa chachu katika nyumba zenu. Mtu yeyote akila kitu kilichotiwa chachu katika muda huo wa siku saba, ni lazima aondolewe miongoni mwa Waisraeli. 16Siku ya kwanza na siku ya saba mtakuwa na mkutano mtakatifu. Katika siku hizo mbili hamtaruhusiwa kufanya kazi yoyote isipokuwa kazi ya lazima ya kutayarisha chakula. 17Mtaadhimisha sikukuu hii ya mikate isiyotiwa chachu kama ukumbusho wa siku nilipowatoa nyinyi, vikundi vya Israeli, kutoka Misri. Sikukuu hiyo itaadhimishwa na vizazi vyenu vyote vijavyo, kama agizo la milele. 18Basi, mtakula mikate isiyotiwa chachu kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, mpaka jioni ya siku ya ishirini na moja ya mwezi huohuo wa kwanza. 19Katika siku hizo saba, msiwe na chachu yoyote katika nyumba zenu. Mtu yeyote, awe mgeni au mwenyeji, akila kitu kilichotiwa chachu, ataondolewa miongoni mwa jumuiya ya Waisraeli. 20Popote pale mnapoishi, ni mwiko kabisa kula chochote kilichotiwa chachu. Mnapaswa kula mikate isiyotiwa chachu.”

Pasaka ya kwanza

21Basi, Mose akawaita wazee wote wa Waisraeli, akawaambia, “Chagueni kila mmoja wenu, kulingana na jamaa yake, mwanakondoo na kumchinja kwa sikukuu ya Pasaka. 22Mtachukua majani ya husopo na kuyachovya katika damu ndani ya birika12:22 na kuyachovya … birika: Au na kuyaweka juu ya kizingiti. na kupaka kwenye vizingiti na miimo yote miwili ya milango ya nyumba zenu. Mtu yeyote asitoke nje ya nyumba usiku huo hadi asubuhi. 23Taz Ebr 11:28 Maana mimi Mwenyezi-Mungu nitapita kuwaua Wamisri. Lakini nitakapoiona damu iliyopakwa kwenye vizingiti na miimo ya nyumba zenu, nitazipita na wala sitamruhusu mwangamizi12:23 Mwangamizi: Au Malaika wa kifo. kuingia katika nyumba zenu na kuwaua. 24Shikeni jambo hilo nyinyi na wazawa wenu kama agizo la milele. 25Mtakapoingia katika nchi ile ambayo mimi Mwenyezi-Mungu nitawapa, kama nilivyoahidi, ni lazima kulitekeleza. 26Kila wakati watoto wenu watakapowauliza, ‘Jambo hili lina maana gani?’ 27Nyinyi mtawajibu, ‘Hii ni tambiko ya Pasaka kwa heshima ya Mwenyezi-Mungu, kwa sababu alizipita nyumba za Waisraeli nchini Misri alipowaua Wamisri, lakini sisi hakutuua.’” Waisraeli wakainamisha vichwa na kumwabudu Mwenyezi-Mungu.
28Kisha Waisraeli wakaenda, wakafanya kama walivyoambiwa na Mose na Aroni kulingana na amri ya Mwenyezi-Mungu.

Pigo la kumi: Kuuawa kwa wazaliwa wa kwanza wa Wamisri

29 Taz Kut 4:22-32 Mnamo usiku wa manane, Mwenyezi-Mungu aliwaua wazaliwa wa kwanza wote wa Misri. Wote walikufa, tangu mzaliwa wa kwanza wa Farao, mrithi wa ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa mfungwa gerezani. Hata wazaliwa wa kwanza wa wanyama nao walikufa. 30Basi Farao, watumishi wake na wakazi wote wa Misri wakaamka usiku. Kukawa na kilio kikubwa nchini kote Misri kwa maana hapakuwa hata nyumba moja ambamo hakufa mtu. 31Hapo Farao akawaita Mose na Aroni, usiku huohuo, akamwambia, “Amkeni! Ondokeni miongoni mwa watu wangu. Nendeni, nyinyi pamoja na hao Waisraeli, mkamtumikie Mwenyezi-Mungu kama mlivyosema. 32Chukueni makundi yenu ya kondoo na ng'ombe, mwondoke; niombeeni na mimi baraka.”
33Wamisri wakawahimiza Waisraeli waondoke haraka, wakisema, “Hakika tutakufa sote!” 34Basi, Waisraeli wakauchukua unga wao uliokandwa kabla haujatiwa chachu, na mabakuli yao ya kukandia wakiwa wamezifunga kwa nguo na kubeba mabegani. 35Taz Kut 3:21-22 Waisraeli walikuwa wamekwisha fanya kama Mose alivyowaagiza hapo awali: Waliwaomba Wamisri wawapatie vito vya fedha, dhahabu na mavazi. 36Naye Mwenyezi-Mungu alikwisha wafanya Waisraeli wapendwe na Wamisri, nao Wamisri wakawapa kila kitu walichoomba. Ndivyo Waisraeli walivyowapokonya Wamisri mali yao.

Waisraeli wanaondoka Misri

37Waisraeli waliondoka mjini Ramesesi, wakasafiri kwa miguu kuelekea Sukothi. Walikuwa wanaume wapatao 600,000, licha ya wanawake na watoto. 38Kulikuwa pia na kundi la watu wengine walioandamana nao pamoja na mifugo mingi, kondoo na ng'ombe. 39Kwa kuwa walikuwa wameondoka Misri kwa haraka, hawakuweza kutayarisha chakula cha safarini, ila tu ule unga uliokandwa bila kutiwa chachu. Basi, wakaoka mikate isiyotiwa chachu.
40 Taz Mwa 15:13; Gal 3:17 Waisraeli walikuwa wameishi nchini Misri kwa muda wa miaka 430. 41Katika siku ya mwisho ya mwaka wa 430, siku hiyohiyo maalumu ndipo makabila yote ya Mwenyezi-Mungu yaliondoka nchini Misri. 42Usiku huo ambao Mwenyezi-Mungu alikesha ili kuwatoa Waisraeli nchini Misri, unapaswa kuadhimishwa na Waisraeli wote na vizazi vyao vyote, kama usiku wa kukesha kwa heshima ya Mwenyezi-Mungu.

Taratibu za Pasaka

43Mwenyezi-Mungu aliwaambia Mose na Aroni, “Yafuatayo ni maagizo juu ya adhimisho la Pasaka. Mgeni yeyote hatashiriki chakula cha Pasaka. 44Lakini mtumwa yeyote aliyenunuliwa kwa fedha, baada ya kumtahiri, ataruhusiwa kushiriki. 45Msafiri yeyote, wala kibarua yeyote, hatashiriki chakula hicho. 46Taz Hos 9:12; Yoh 19:36 Mwanakondoo wa Pasaka ataliwa katika nyumba moja. Hamtatoa nyama yoyote nje ya nyumba alimochinjiwa, wala hamtavunja hata mfupa mmoja wa mnyama wa Pasaka. 47Jumuiya yote ya watu wa Israeli itaadhimisha sikukuu hiyo. 48Mgeni yeyote anayeishi miongoni mwenu akipenda kuadhimisha sikukuu ya Pasaka, ni lazima kwanza wanaume wote wa nyumba yake watahiriwe; hapo atahesabiwa kuwa kama mwenyeji na kuruhusiwa kushiriki. Mwanamume yeyote asiyetahiriwa asishiriki kamwe. 49Sheria zilezile zitamhusu mzalendo Mwisraeli na wageni watakaoishi miongoni mwenu”. 50Waisraeli wote walitii sheria hiyo na kufanya kama Mwenyezi-Mungu alivyowaagiza Mose na Aroni. 51Siku hiyohiyo Mwenyezi-Mungu aliwatoa Waisraeli nchini Misri kwa makundi.

Kutoka12;1-51

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 13 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 11...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa Matendo yake makuu kwetu..
Yeye anatujua kuliko tunavyojijua,Yeye ni Mungu wetu na Kimbilio letu,Yeye aliyetupa Kibali cha kuendelea kuiona Leo hii..Yeye ni Muumba wetu na Muumba wa Mbingu na Nchi..Yeye ni mwanzo na yeye ni mwisho,Yeye ni Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo, Yeye ni Alfa na Omega..Yeye ni Mlinzi mkuu na Mtawala,Amani,Furaha,Upendo na Fadhili zipo kwake..Yeye akisema ndiyo hakuna wakusema siyo..Yeye atosha Maishani kwetu.ukimuita aitika,ukimuomba anakupa,ukifuata njia zake na kumuabudu yeye hutojuta..



Mungu si mtu, aseme uongo, wala si binadamu, abadili nia yake! Je, ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?[Hesabu 23:19]
Asante Baba wa mbinguni kwa Neema/Rehema yako uliyotupa..Tazama Jana imepita Baba Leo ni Siku mpya na Kesho ni siku nyingine..
Jehovah..!! tunaomba uibariki siku hii ikawe njema , yenye Amani na kukupendeza wewe..Ukabariki kuingia kwetu na kutoka kwetu,Vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Baba..
Tunaomba ukabariki Vilaji/Vinywaji, Kazi zetu,Biashara,Masomo na Vyote tunavyoenda kugusa/kutumia ukavitakasase kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..

Baba tunakwenda kinyume na adui mwovu na kazi zake zote..Tunaomba ukatuokoe,kutulinda na kutufunika na Damu ya Mwokozi wetu Bwana Yesu Kristo..
Baba tukuja mbele zako na kujinyeyekeza tunaomba utusamehe pale tulikwenda kinyume nawe..kwakuwaza,kwakunena,kwakujua/kutojua..Mfalme wa Amani tunaomba utupe nasi Neema ya kuweza kuwasamehe wote waliotukosea..
Roho mtakatifu akatuongoze vyema katika yote..
Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..

Jehovaha..!!!Ukawaguse na kuwaokoa wote wanaopitia magumu/mapito,shida/tabu,Wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao,waliokata tamaa,waliokataliwa na wakapate tumaini lako..
ukawaponye kimwili na kiroho pia..

Tunayaweka haya mikononi mwako Yahweh..Sifa na Utukufu ni wako Daima.
Tunashukuru na kuamini wewe ni Mungu wetu leo na hata milele.


11Maandiko Matakatifu yasema: “Kila anayemwamini hataaibishwa.[Waroma10;11]
Amina..!!
Muwe na wakati mwema..nawapenda.


Tangazo la kuuawa wazaliwa wa kwanza wa Wamisri

1Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Bado kuna pigo moja nitakalomletea Farao na nchi ya Misri. Baadaye atawaacheni mwondoke hapa. Tena atakapowaacheni mwondoke, yeye mwenyewe atawafukuza mwondoke kabisa. 2Waambie Waisraeli sasa wasikie vizuri kwamba kila mmoja wao, mwanamume kwa mwanamke, ni lazima amwombe jirani yake vito vya fedha na dhahabu.” 3Mwenyezi-Mungu akawafanya Waisraeli wapendeke mbele ya Wamisri. Tena, Mose mwenyewe akawa mtu mashuhuri sana nchini Misri, na mbele ya maofisa wa Farao na watu wote.
4Mose akamwambia Farao, “Mwenyezi-Mungu asema hivi: ‘Panapo usiku wa manane leo, nitapitia katikati ya nchi ya Misri. 5Nitakapopita, kila mzaliwa wa kwanza nchini Misri atakufa: Kuanzia mzaliwa wa kwanza wako wewe Farao ambaye ni mrithi wako, hadi mzaliwa wa kwanza wa mjakazi anayesaga nafaka kwa jiwe. Hata wazaliwa wa kwanza wa mifugo nao wote watakufa. 6Kutakuwa na kilio kikubwa kote nchini Misri, kilio ambacho hakijapata kutokea, wala hakitatokea tena. 7Lakini miongoni mwa Waisraeli hakuna mtu, mnyama au mbwa wao atakayepatwa na madhara yoyote, ili upate kutambua kwamba mimi Mwenyezi-Mungu hutofautisha kati ya Waisraeli na Wamisri.’” 8Mose akamalizia kwa kumwambia Farao, “Watumishi wako hawa watanijia na kuinama mbele yangu kwa heshima, wakinisihi niondoke nchini Misri, mimi pamoja na watu wote wanaonifuata. Baada ya hayo, nitaondoka.” Kisha Mose, huku akiwa ameghadhabika, akaondoka kwa Farao.
9Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Farao hatakusikiliza, ili maajabu yangu yapate kuongezeka nchini Misri.” 10Basi, Mose na Aroni walifanya maajabu hayo yote mbele ya Farao. Lakini Mwenyezi-Mungu alimfanya Farao kuwa mkaidi, akakataa kuwaruhusu Waisraeli waondoke nchini mwake.

Kutoka11;1-10

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 12 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 10...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Mungu wetu yu mwema sana...

Asante Baba wa Mbinguni kwa Neema/Rehema hii uliyotupa Umetupa Kibali cha kuendelea kuiona siku hii Baba...
Sifa na Utukufu ni kwako daima..
Tunajiachilia mikononi mwako na kujinyeyekeza mbele zako Yahweh..!!
Tunaomba Utubariki katika maisha yetu na ukatuongoze katika yote..
Jehovah..!!Ukatuokoe na Mwovu pamoja na kazi zake zikashindwe katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Tukawe barua njema na tukasomeke vyema..

Je, tunaanza tena kujipendekeza? Je, tunahitaji barua ya utambulisho kwenu, au kutoka kwenu, kama watu wengine? Nyinyi wenyewe ni barua yetu; barua iliyoandikwa mioyoni mwetu kila mtu aione na kuisoma. Ni dhahiri kwamba nyinyi ni barua ya Kristo aliyoipeleka kwa mikono yetu. Barua yenyewe imeandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu aliye hai; imeandikwa si juu ya kipande cha jiwe, bali juu ya mioyo ya watu. Tunaweza kusema hayo kwa sababu ya tumaini letu tulilo nalo kwa Mungu kwa njia ya Kristo. Si kwamba sisi tunaweza kufanya chochote kwa nguvu zetu wenyewe, ila uwezo wetu wote hutoka kwa Mungu: Maana yeye ndiye aliyetuwezesha kulihudumia Agano Jipya ambalo si agano la sheria iliyoandikwa, bali agano la Roho. Maana sheria iliyoandikwa huleta kifo, lakini Roho huleta uhai.

Ukabariki familia zetu Jehovah..!!!Amani ikawe nasi daima..
Mfalme wa Amani ukatawale, Ukatamalaki na kutuatamia.Ukawe mlinzi mkuu na ukawaguse na kuwaponya wote waliofungwa kimwili na kiroho,Wagonjwa,wenye shida/tabu,wafiwa ukawe mfariji wao..
Mungu wetu, Baba yetu,Muumba wetu,Muumba wa vyote na vyote ni mali yako Baba..
Tunaomba ukabariki Ridhiki zetu ziingiazo na zitokazo..


Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Yahwehh..kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua...
Nasi ukatupe neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika safari yetu ya maisha..

6Mtafuteni Mwenyezi-Mungu wakati bado anapatikana,
mwombeni msaada wakati yupo bado karibu.[Isaya55:6]

Tunayaweka haya mikononi mwako,Tukishukuru na kuamini wewe ndiye Mungu wetu na Muumba wetu..Hakuna linaloshindikana kwako Baba..

Naye Mungu aliye chanzo cha amani hatakawia kumponda Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.[waroma16:20]


Amina..!!!


Pigo la nane: Nzige

1Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao. Mimi nimemfanya kuwa mkaidi na maofisa wake ili nipate kutenda ishara hizi miongoni mwao, 2ili nyinyi mpate kuwasimulia watoto wenu na wajukuu wenu, jinsi nilivyowadhihaki Wamisri kwa kuzifanya ishara hizo miongoni mwao. Hivyo mtatambua kuwa mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.”
3Basi, Mose na Aroni wakamwendea Farao na kumwambia, “Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Waebrania, anasema hivi, ‘Mpaka lini utakataa kujinyenyekesha mbele yangu? Waache watu wangu waondoke ili wapate kunitumikia. 4Ukikataa kuwaacha watu wangu waondoke, basi, kesho nitaleta nzige waivamie nchi yako. 5Nchi yote ya Misri itakuwa giza kwa sababu ya nzige hao. Watakula kila kitu kilichosalimika baada ya ile mvua ya mawe; pia hawataacha chochote juu ya miti inayoota mashambani. 6Nzige hao watajaa katika nyumba zako, nyumba za maofisa wako na za Wamisri wote; watakuwa wengi kiasi ambacho hata wazee wenu hawajapata kuona tangu walipozaliwa, hadi leo.’” Basi, Mose akatoka kwa Farao.
7Viongozi wa Farao wakamwuliza, “Je, mtu huyu atatusumbua mpaka lini? Waache watu hawa waende zao wakamtumikie Mwenyezi-Mungu, Mungu wao. Je, hujali kwamba nchi ya Misri inaangamia?”
8Hapo, Mose na Aroni wakaitwa warudi kwa Farao, naye akawaambia, “Nendeni mkamtumikie Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu. Lakini, nauliza: Ni kina nani watakaokwenda pamoja nanyi?” 9Mose akamjibu, “Kila mtu: Vijana na wazee, tutaondoka na watoto wetu wa kiume na wa kike, kondoo na mbuzi wetu na ng'ombe; kwa maana ni lazima tumfanyie sikukuu Mwenyezi-Mungu.”
10Kwa kuwapuuza, Farao akawaambia, “Ehe! Mwenyezi-Mungu awe nanyi kama nitawaruhusu kamwe mwende zenu na watoto wenu. Ni dhahiri kwamba mnayo nia mbaya moyoni mwenu. 11La hasha! Ni wanaume tu watakaokwenda kumtumikia Mwenyezi-Mungu, maana hilo ndilo mnalotaka.” Hapo Mose na Aroni wakafukuzwa mbele ya Farao.
12Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Nyosha mkono wako juu ya nchi ya Misri, nzige watokee ili waingie na kula mimea yote nchini na vyote vilivyosazwa na ile mvua ya mawe.” 13Basi, Mose akainyosha fimbo yake juu ya nchi ya Misri. Mwenyezi-Mungu akaleta upepo toka mashariki, ukavuma juu ya nchi mchana kutwa na usiku kucha. Kulipokucha, ule upepo ukawa umeleta nzige. 14Taz Ufu 9:2-3 Hao nzige wakaenea kila mahali nchini Misri, wakatua juu ya ardhi yote. Nzige hao walikuwa kundi kubwa kupindukia, kiasi ambacho hakijapata kutokea wala hakitatokea tena. 15Waliifunika nchi yote ya Misri, hata ardhi ikaonekana kuwa giza. Walikula mimea yote na matunda yote yaliyosalia wakati wa ile mvua ya mawe. Hakuna hata jani moja lililosalia nchini. Hakuna jani lolote lililosalia juu ya miti wala mimea popote katika nchi yote ya Misri.
16Hapo Farao akawaita Mose na Aroni kwa haraka, akawaambia, “Nimetenda dhambi dhidi ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, na dhidi yenu. 17Kwa hiyo sasa ninawasihi mnisamehe dhambi yangu, mara hii moja tu, mkaniombee kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, aniondolee kifo hiki.”
18Basi, Mose akaondoka kwa Farao, akaenda kumwomba Mwenyezi-Mungu. 19Naye Mwenyezi-Mungu akaleta upepo mkali toka magharibi, ukawainua wale nzige na kuwasukumia kwenye bahari ya Shamu. Hakuna hata nzige mmoja aliyebaki katika nchi nzima ya Misri. 20Lakini Mwenyezi-Mungu akamfanya Farao kuwa mkaidi, naye hakuwaachia Waisraeli waondoke.

Pigo la tisa: Giza

21 Taz Hek 17:1-21 Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Nyosha mkono wako juu mbinguni ili giza nene litokee nchini Misri, giza nene ambalo mtu ataweza kulipapasa.” 22Taz Zab 105:28; Ufu 16:10 Basi, Mose akanyosha mkono wake juu mbinguni, kukawa na giza nene kote nchini Misri kwa muda wa siku tatu. 23Watu hawakuweza kuonana wala kuondoka mahali walipokuwa kwa muda huo wa siku tatu. Lakini Waisraeli wote walikuwa na mwanga huko Gosheni walimokuwa wanakaa.
24Kisha, Farao akamwita Mose, akamwambia, “Nendeni mkamtumikie Mwenyezi-Mungu. Watoto wenu pia wanaweza kwenda pamoja nanyi. Lakini kondoo na mbuzi, na ng'ombe wenu wabaki.” 25Lakini Mose akamwambia, “Ni lazima uturuhusu kuchukua wanyama wa tambiko na sadaka za kuteketezwa ili tukamtambikie Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu. 26Ngombe wetu ni lazima pia tuwachukue wala hakuna hata ukwato mmoja utakaobaki nyuma, kwa sababu kutoka katika mifugo yetu wenyewe, tutamtumikia Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, wala sisi hatujui ni mnyama yupi tutakayemtolea Mwenyezi-Mungu tambiko mpaka tutakapofika huko.”
27Lakini Mwenyezi-Mungu akamfanya Farao kuwa mkaidi, akakataa kuwaachia Waisraeli waondoke. 28Farao akamwambia Mose, “Toka mbele yangu. Jihadhari sana. Usije kuniona tena, maana siku utakapokuja tena mbele yangu, utakufa!” 29Mose naye akamwambia, “Sawa! Kama ulivyosema sitakuja kukuona tena.”

Kutoka10;1-29


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 11 April 2017

Jikoni Leo;MKATE WA AJEMI/BWANA - KISWAHILI,Mpishi da'Fathiya..




Mahitaji:
Mahitaji
Unga wa ngano vicombe 4 - 520 gms
Hamira kijiko 1 kikubwa - 17 gms
Baking soda kijiko cha chai 1 & 1/2 - 10.5 gms
Chumvi kijiko cha chai 1 & 1/2 - 9 gms 
Maziwa ya mtindi kikombe 1 
Maji nusu kikombe ( kwa kuzimua mtindi)
Mafuta vijiko 2 vikubwa 
Yai 1

Shukrani;Aroma of Zanzibar

"Swahili na Waswahili"Pamoja Daima.

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 9...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Mungu kwetu ni Kimbilio na yeye atosha..


Mungu ni kimbilio letu na nguvu yetu; yeye ni msaada wetu daima wakati wa taabu. Kwa hiyo hatutaogopa chochote, dunia ijapoyeyuka na milima kutikisika kutoka baharini; hata kama bahari ikichafuka na kutisha, na milima ikatetemeka kwa machafuko yake. Kuna mto ambao maji yake hufurahisha mji wa Mungu, makao matakatifu ya Mungu Mkuu. Mungu yumo mjini humo, nao hauwezi kutikiswa; Mungu ataupa msaada alfajiri na mapema. Mataifa yaghadhibika na tawala zatikisika; Mungu anguruma nayo dunia yayeyuka. Mwenyezi-Mungu wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu. Njoni mwone matendo ya Mwenyezi-Mungu; oneni maajabu aliyoyafanya duniani. Hukomesha vita popote duniani, huvunjavunja pinde na mikuki, nazo ngao huziteketeza. Asema: “Nyamazeni na kujua kuwa mimi ni Mungu! Mimi natukuka katika mataifa yote; mimi natukuzwa ulimwenguni kote!” Mwenyezi-Mungu wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu.
Asante Baba wa Mbinguni kwa kutuchagua tena na Kutupa Kibali cha kuendelea kuiona tena Leo hii..si kwa uwezo wetu wala si kwakuwa sisi ni wema sana na wala si kwamba sisi niwazuri mno zaidi ya wengine leo hii wapo kitandani hawajiwezi, wengine hawana kauli hata ya kukuita wala kutubu..wengine wameshatangulia Baba..Sisi ni nani? Tunajua ni kwa Neema/Rehema yako tuu umetupa tena nafasi hii...
Tazama Jana imepita Baba Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine Jehovah..!! Mungu wetu,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi,Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo....Baba wa Yatima,Mume wa Wajane..Mfalme wa Amani..Tunakuja mbele zako na kujinyenyekeza..Tunajiachilia mikononi mwako Bwana wa Majeshi..
Tunaiweka siku hii na Maisha yetu mikononi mwako Baba..

Tunaomba ukaibariki na kutuongoza Mfalme wa Amani..
Ikawe yenye faida, Furaha, Upendo,Amani, Uponyaji na tukawe na kiu zaidi ya kukutafuta na kufuata nja zako Yahweh..!
Utubariki Tuingiapo/tutokapo,Vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!!
Ukabriki Vilaji/Vivywaji,Kazi zetu,Biashara,Masomo na ukavitakase vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba na Damu ya Mwanao Bwana wetu na Mwokozi wetu Bwana Yesu wa Nazareti..Aliteseka na kumwaga Damu ili sisi tupate kupona..Baba ukatutakase Miili yetu na Akili zetu..Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye Kunena/Kutenda,Kutambua/Kujitambua..
Baba wa Mbinguni Tunakwenda Kinyume Na Nguvu za Giza,Nguvu za mapepo,Nguvu za mpinga Kristo..Zishindwe katika Jina kuu yashindayo majina yote la Bwana wetu Yesu Kristo..
Ukatamalaki na kutuatamia,Ukatuponye na kutuokoa,Ulinzi upo mikononi mwako..Utufunike kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..!!!
Yahweh..!! Jehovah..!!Baba wa Mbinguni Tunawaweka wote waliovifungoni mwa Mwovu,Walio magerezani pasipo na hatia,Wagonjwa,Wafiwa ukawe mfariji wao, wenye Shida/Tabu na wote wanaopitia Magumu/Majaribu yoyote Baba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu,Ukawaponye na kuwaokoa..wapate kupona kimwili na kiroho..
Baba wa Mbinguni tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe, kwakuwaza/kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Tunaomba pia tupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea Yahweh..
Ukatufinyange na kutufanya chombo chema..Tukapate kutumika sawasawa na mapenzi yako Yahweh..!!
Tunayaweka haya yote mikononi mwako..Tukisifu, Tunashukuru na kuamini wewe ni Mungu wetu na kimbilio letu..Hakuna silowezekana kwako wewe Muumba wetu..

Kwakuwa Ufalme ni wako, na Nguvu, na Utukufu, Hata milele..
Amina...!!!


Nawapenda wote miliopita hapa na Mungu aendelee kuwabariki.


Pigo la tano: Vifo vya mifugo

1Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie kwamba mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Waebrania, nasema, ‘Waache watu wangu waondoke ili wakanitumikie. 2Kama ukikataa kuwaacha waondoke na ukiendelea kuwashikilia, 3nitaunyosha mkono wangu na kuleta maradhi mabaya sana juu ya mifugo yenu yote: Ng'ombe, farasi, punda, ngamia, mbuzi na kondoo. 4Na, nitaitenganisha mifugo ya Waisraeli na mifugo ya Wamisri ili mnyama hata mmoja wa Waisraeli asife.’” 5Tena, Mwenyezi-Mungu akaweka wakati maalumu akisema, “Kesho mimi Mwenyezi-Mungu nitatekeleza jambo hilo nchini Misri.”
6Kesho yake Mwenyezi-Mungu akafanya alichosema. Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna mnyama hata mmoja wa Waisraeli aliyekufa. 7Farao akauliza habari juu ya wanyama wa Waisraeli, akaambiwa kuwa hakuna mnyama wao hata mmoja aliyekufa. Hata hivyo, Farao akabaki mkaidi, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.
Pigo la sita: Majipu

8Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni kila mmoja wenu magao ya majivu ya tanuri, kisha Mose ayarushe juu hewani mbele ya Farao. 9Majivu hayo yatakuwa vumbi nyembamba itakayoenea juu ya nchi yote ya Misri. Yatasababisha majipu yatakayotumbuka na kuwa vidonda kwa watu na wanyama kila mahali nchini Misri.” 10Taz Ufu 16:2 Basi, wakachukua majivu kutoka kwenye tanuri, wakamwendea Farao, naye Mose akayarusha juu hewani. 11Watu na wanyama wakavamiwa na majipu hata wale wachawi hawakuweza kujitokeza maana wao pamoja na Wamisri wote pia walivamiwa na majipu hayo. 12Lakini Mwenyezi-Mungu akamfanya Farao kuwa mkaidi, naye hakuwasikiliza kama vile Mwenyezi-Mungu alivyomwambia Mose.

Pigo la saba: Mvua ya mawe

13Kisha, Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Kesho, amka alfajiri na mapema umwendee Farao, umwambie kwamba mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Waebrania, nasema hivi, ‘Waache watu wangu waondoke ili wakanitumikie. 14Maana safari hii, wewe mwenyewe, maofisa wako na watu wako mtakumbana na mapigo yangu makali. Nawe utatambua kwamba hakuna yeyote duniani aliye kama mimi. 15Ningalikwisha kukuangamiza tayari wewe na watu wako kwa maradhi mabaya, nanyi mngalikuwa mmekwisha angamia. 16Taz Rom 9:17 Lakini nimewaacheni muishi ili kudhihirisha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kuwa mimi ni nani. 17Lakini bado unaonesha kiburi dhidi ya watu wangu, wala huwaachi waondoke. 18Kwa hiyo kesho, wakati kama huu, nitaleta mvua kubwa ya mawe ambayo haijawahi kutokea nchini Misri, tangu mwanzo wake hadi leo. 19Kwa hiyo agiza mifugo yako na chochote kilicho huko mashambani viwekwe mahali salama; kwa maana mvua ya mawe itamnyeshea kila mtu na mnyama aliye shambani na ambaye hayuko nyumbani; wote watakufa.’”
20Baadhi ya maofisa wa Farao waliyatia maanani maneno hayo ya Mwenyezi-Mungu, wakawapeleka watumwa na wanyama wao nyumbani mahali pa usalama. 21Lakini yule ambaye hakulijali neno la Mwenyezi-Mungu aliwaacha watumwa wake na wanyama wake mashambani.
22Kisha, Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Nyosha mkono wako juu mbinguni, ili mvua ya mawe inyeshe kila mahali nchini Misri. Imnyeshee mtu, mnyama na kila mmea shambani.” 23Basi, Mose alinyosha fimbo yake kuelekea mbinguni. Naye Mwenyezi-Mungu akaleta mvua ya mawe na ngurumo; umeme ukaipiga nchi. Mwenyezi-Mungu alinyesha mvua ya mawe nchini Misri, 24Taz Ufu 8:7; 16:21 mvua kubwa ya mawe iliyoandamana na mfululizo wa umeme, ambayo hakuna mwananchi yeyote wa Misri aliyepata kamwe kushuhudia kabla. 25Mvua hiyo ya mawe ilivunjavunja kila kitu katika mashamba na kila mahali nchini Misri: Wanyama na watu. Mawe ya mvua yakavunjavunja mimea yote na miti mashambani. 26Jambo hilo lilifanyika kote nchini Misri isipokuwa tu sehemu ya Gosheni walimokaa Waisraeli; humo haikuwako mvua ya mawe.
27Basi, Farao akaagiza Mose na Aroni waitwe, akawaambia, “Safari hii nimetenda dhambi. Mwenyezi-Mungu ana haki; mimi na watu wangu tumekosa. 28Mwombeni Mwenyezi-Mungu kwani ngurumo hii na mvua ya mawe vimezidi. Mimi nitawaacheni mwondoke na wala hamtakaa tena zaidi.” 29Mose akamwambia, “Mara tu nitakapotoka nje ya mji nitainua mikono na kumwomba Mwenyezi-Mungu. Ngurumo itakoma na hakutakuwa na mvua ya mawe tena ili utambue kwamba dunia ni yake Mwenyezi-Mungu. 30Lakini najua kwamba wewe na maofisa wako bado hammwogopi Mwenyezi-Mungu.”
31(Kitani na mimea ya shayiri vyote vilikuwa vimeharibiwa, kwa sababu shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa imechanua maua. 32Lakini ngano na jamii nyingine ya ngano havikuharibiwa kwa kuwa hiyo huchelewa kukomaa).
33Basi, Mose akaondoka nyumbani kwa Farao, akatoka nje ya mji. Kisha akainua mikono yake kumwomba Mwenyezi-Mungu. Ngurumo na mvua ya mawe vikakoma; mvua ikaacha kunyesha duniani. 34Lakini Farao alipoona kuwa mvua ya mawe na ngurumo vimekoma, aliirudia dhambi yake tena, akawa mkaidi, yeye pamoja na maofisa wake. 35Basi, kama Mwenyezi-Mungu alivyombashiria Mose, Farao alikaidi akakataa kuwaruhusu Waisraeli waondoke.Kutoka9;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 10 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 8...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu katika roho na kweli..
Mtakatifu , Mtakatifu, Mtakatifu...!! Baba wa mbinguni, Baba yetu Mungu wetu, Muumba wetu,Muumba Mbingu na nchi na Vyote vilivyomo ni mali yako, Hata sisi Baba ni mali yako..Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo, Muweza wa yote,wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho...Alfa na Omega...
Yahweh..!!!!!Jehovah..!!
Tunashukuru Baba kwa kutupa Kibali hiki cha kutuchagua na kuendelea kuiona Leo..Baba si kwamba wajuzi sana, wenye nguvu sana, wema na wazuri mno.. Hapa ni kwa Neema/Rehema yako tuu Mfalme wa Amani...
Baba tunaomba ukaibariki siku hii ikawe njema na yenye Amani, Furaha, wema na Fadhili,Ukatubariki tuingiapo/tutokapo,vyombo vya usafiri, tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Baba...
Baba ukabariki  kazi zetu,Biashara,Masomo na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..Yeye aliteseka pale Msalabani ili sisi tupate kupona..Ukatutakase Akili na miili yetu..Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda, kutambua/kujitambua..
Baba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwa kuwaza,kutenda, kwakujua/kutojua..Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Mfalme wa Amani ukawaguse na kuwaponya wote wanaopitia magumu/majaribu,shida/tabu,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao,waliovivfungoni baba ukawafungue na kuwaponya kimwili na kiroho pia..
Baba ukatamalaki katika nchi hii tunayoishi.. Ukaibariki na kutubariki wote tunaoishi hapa..ukatulinde na adui yeyote anayepanga kwenda kinyume nawe..Ukatuatamie Jehovah..!!

Mfalme wa Amani Tanzania tunaiweka mikononi mwako na watanzania wote popote walipo,Ukaibariki na kutubariki katika kila lililojema na ukatulinde na uovu wowote unaondelea na kunaopangwa kufanyika..mikononi mwako yote yanawezekena..
Afrika ikawe nawe Baba wa mbinguni ..Dunia yote ukawe mtawala na Amani iliyo juu yako ikatawale..
Ukawabariki na kuwaongoza wote wanaotuongoza wakatuongoze katika haki na kweli..


2“Hakuna aliye mtakatifu kama Mwenyezi-Mungu;
hakuna yeyote aliye kama yeye;

hakuna aliye mwamba kama Mungu wetu.[1 Samueli 2:2]
 20Hakuna mwingine kama wewe, ee Mwenyezi-Mungu, na yote tunayoyasikia yanathibitisha kwamba hakuna Mungu mwingine ila wewe.[1 Mambo ya Nyakati 17:20]
Tunayaweka haya yote mikononi mwako, Tukijinyeyekeza, kukusifu,Tunashukuru na kuamini wewe ni Mungu wetu na hakuna mwingine kama wewe na hatokuwepo..Milele na Milele..
Amina..!!!!! 





Pigo la pili: Vyura

1Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie Mwenyezi-Mungu asema hivi: Waache watu wangu waondoke ili wanitumikie. 2Lakini ukikataa kuwaacha waondoke, basi, nitaipiga nchi yako yote kwa kuiletea vyura. 3Mto Nili utafurika vyura, nao wataingia mpaka ndani ya nyumba yako, chumba chako cha kulala, kitandani mwako, na katika nyumba za watumishi wako na watu wako. Vyura hao wataingia katika majiko yenu na vyombo vyenu vya kukandia unga. 4Vyura watapanda juu ya mwili wako, miili ya watu wako na watumishi wenu!”
5Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Mwambie Aroni anyoshe mkono wake na fimbo yake juu ya mito, juu ya mifereji na madimbwi, nao vyura watatokea na kuenea kila mahali nchini Misri.”8:5 katika makala ya Kiebrania ni 8:1. 6Basi, Aroni akanyosha fimbo yake juu ya maji yote, vyura wakatokea na kuifunika nchi nzima ya Misri. 7Lakini wachawi wa Misri kwa uchawi wao pia wakaleta vyura nchini Misri.
8Kisha Farao akamwita Mose na Aroni, akamwambia, “Msihi Mwenyezi-Mungu, ili aniondolee mimi na watu wangu vyura hawa, nami nitawaacha Waisraeli waende zao na kumtambikia Mwenyezi-Mungu.” 9Mose akamjibu Farao, “Haya! Waweza kutaja wakati unaotaka nikuombee kwa Mungu, niwaombee maofisa wako na watu wako; nitamwomba awaangamize vyura hawa waliomo katika nyumba zenu; watabaki tu mtoni Nili!”
10Farao akamwambia, “Kesho.” Mose akasema, “Nitafanya kama unavyosema, ili ujue kwamba hakuna yeyote anayelingana na Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu. 11Vyura wataondoka kwako, na kwenye nyumba zenu, kwa maofisa wako na kwa watu wako; watabaki tu katika mto Nili.”
12Basi, Mose na Aroni wakaondoka nyumbani kwa Farao, na Mose akamlilia Mwenyezi-Mungu amwondolee Farao uvamizi wa vyura hao aliomletea. 13Mwenyezi-Mungu akafanya kama Mose alivyomwomba: Vyura wakafa majumbani, viwanjani na kwenye kumbi za nyumba na katika mashamba. 14Watu wakawakusanya vyura hao marundo marundo; nchi nzima ikanuka. 15Lakini Farao alipoona kwamba nchi imepata nafuu, akawa mkaidi tena, wala hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama Mwenyezi-Mungu alivyokuwa amesema.

Pigo la tatu: Viroboto

16Kisha, Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Mwambie Aroni anyoshe fimbo yake na kuyapiga mavumbi, nayo yatageuka kuwa viroboto kote nchini Misri.” 17Mose na Aroni wakafanya hivyo. Aroni alinyosha fimbo yake na kuyapiga mavumbi, nayo yakageuka kuwa viroboto na kuwaparamia watu na wanyama. Mavumbi yote nchini kote Misri yakageuka kuwa viroboto. 18Wachawi wa Misri, kwa uchawi wao, wakajaribu kuyageuza mavumbi yawe viroboto, lakini hawakufaulu. Viroboto hao wakaenea juu ya watu na wanyama. 19Taz Luka 11:20 Wale wachawi wakamwambia Farao, “Hii ni kazi ya mkono wa Mungu.”8:19 au Hii ni nguvu ya kimungu Kiebrania, neno kwa neno: “Ni kidole cha Mungu”. Lakini moyo wa Farao ukaendelea kuwa mgumu; wala hakuwasikiliza Mose na Aroni. Ikawa kama Mwenyezi-Mungu alivyokuwa amesema.

Pigo la nne: Nzi

20Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Kesho amka asubuhi mapema umwendee Farao wakati anapokwenda mtoni umwambie, ‘Mwenyezi-Mungu asema hivi: Waache watu wangu waondoke ili wanitumikie. 21Kama ukikataa kuwaacha waondoke, basi, nitakuletea makundi ya nzi, wewe, maofisa wako na watu wako wote. Wataingia kwenye nyumba zenu na nyumba zote za Wamisri zitajaa makundi ya nzi, kadhalika na ardhi yote ya Misri. 22Lakini siku hiyo sehemu ya Gosheni wanakoishi watu wangu nitaikinga: Humo nzi hao hawatakuwamo. Hapo ndipo utakapotambua kwamba mimi Mwenyezi-Mungu natenda mambo nchini mwako. 23Nitawakinga watu wangu na mambo yatakayowapata watu wako. Mambo hayo yatafanyika kesho.’” 24Mwenyezi-Mungu akafanya kama alivyosema: Makundi makubwa ya nzi yakaivamia nyumba ya Farao, nyumba za maofisa wake na nchi nzima ya Misri. Nchi nzima ya Misri ikaharibiwa na nzi hao.
25Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni, akasema, “Mnaweza kwenda kumtambikia Mungu wenu, lakini iwe humuhumu nchini Misri.” 26Lakini Mose akamjibu, “La! Haifai kufanya hivyo, maana tambiko tutakazomtolea Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, zitawachukiza Wamisri. Je, Wamisri wakituona tukitoa tambiko ambazo ni chukizo kwao, si watatupiga mawe? 27Ni lazima tusafiri mwendo wa siku tatu jangwani tukamtambikie Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, kama atakavyotuamuru.”
28Basi, Farao akasema, “Nitawaacha mwende zenu kumtambikia Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, jangwani. Walakini msiende mbali mno. Niombeeni na mimi.” 29Mose akamjibu, “Mara tu nitakapokuacha, nitamwomba Mwenyezi-Mungu makundi haya ya nzi yatoweke kwako wewe Farao, maofisa wako na watu wako, kesho. Lakini wewe usitudanganye tena kwa kukataa kuwaacha watu kwenda kumtambikia Mwenyezi-Mungu.”
30Basi, Mose akaondoka nyumbani kwa Farao, akamwomba Mwenyezi-Mungu. 31Mwenyezi-Mungu akafanya kama Mose alivyomwomba, wale nzi wakatoweka kutoka kwa Farao, maofisa wake na watu wake, wala hakusalia hata mmoja. 32Lakini hata safari hii Farao alikuwa mkaidi, wala hakuwaruhusu Waisraeli kuondoka.Kutoka8;1-32

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Sunday 9 April 2017

Nimatumaini Yangu Jumapili ilikuwa/inaendelea nyema;Burudani-UPENDO CHOIR. AZANIA FRONT KKKT CATHEDRAL CHURCH (TUKITEMBEA NURUNI ALBUM)

Wapendwa/Waungwana nimatumaini yangu mmekuwa na mnaendelea na Jumapili hii vizuri..hapa kwetu ni salama kabisa na leo kijua kimeonekana..
Mungu yu mwema na aendelee kuwabariki katika yote..Mkawe na wakati mwema..
Watoto hapa kwetu wapo likizo pia baadhi ya wazazi waliowahi kuomba likizo muwe na wakati mwema natumai mtakuwa na wakati mwema na watoto/familia..
Wanaondelea na kazi Mungu aendelee kuwaongoza katika kazi zenu...
Basi tukatumie Ulimi wetu vyema..Roho mtakatifu akatuongoze katika yote na tuwe na kiasi..

Nawapenda...
 Neno La Leo;Yakobo3:1-18

Ulimi
1Ndugu zangu, wengi wenu msiwe waalimu. Kama mjuavyo, sisi waalimu tutapata hukumu kubwa zaidi kuliko wengine. 2Lakini kama mtu hakosi katika usemi wake, basi, huyo ni mkamilifu, na anaweza kutawala nafsi yake yote. 3Sisi huwatia farasi lijamu kinywani mwao ili watutii; na kwa njia hiyo twaweza kuwaongoza kokote tunakotaka. 4Meli nazo pia, ingawa ni kubwa sana, na husukumwa na upepo mkali, huweza kugeuzwa kwa usukani mdogo sana, zikaelekea kokote nahodha anakotaka. 5Vivyo hivyo, ulimi, ingawa ni kiungo kidogo cha mwili, hujisifia makuu sana.
Moto mdogo waweza kuteketeza msitu mkubwa. 6Hali kadhalika ulimi ni kama moto. Umejaa maovu chungu nzima, unayo nafasi yake katika miili yetu na hueneza ubaya katika nafsi zetu zote. Huteketeza maisha yetu yote kwa moto utokao Jehanamu kwenyewe

7Binadamu anaweza kuwafuga wanyama, na amefaulu kufuga viumbe vyote – wanyama wa mwituni, ndege, nyoka na viumbe vya baharini. 8Lakini hakuna mtu aliyefaulu kuufuga ulimi. Ulimi ni kitu kiovu, hakitawaliki, na kimejaa sumu inayoua. 9Kwa ulimi sisi twamshukuru Bwana na Baba yetu. Kwa ulimi huhuo twawalaani watu, watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu. 10Maneno ya kubariki na ya kulaani hutoka katika kinywa kimoja. Ndugu zangu, mambo haya hayapaswi kuwa hivyo. 11Je, chemchemi moja yaweza kutoa maji matamu na maji machungu pamoja? 12Ndugu zangu, je, mtini waweza kuzaa zeituni? Au, mzabibu waweza kuzaa tini? Chemchemi ya maji ya chumvi haiwezi kutoa maji matamu.

Hekima itokayo juu mbinguni
13Je, ni nani mwenye hekima na akili miongoni mwenu? Basi, aoneshe jambo hilo kwa mwenendo wake mzuri na kwa matendo yake mema yanayofanyika kwa unyenyekevu na hekima. 14Lakini ikiwa mioyo yenu imejaa wivu, chuki na ubinafsi, basi, msijisifu na kusema uongo dhidi ya ukweli. 15Hekima ya namna hiyo haitoki juu mbinguni; hekima hiyo ni ya ulimwengu, na ya kidunia, tena ni ya kishetani. 16Maana popote palipo na wivu na ubinafsi, hapo pana fujo na kila aina ya uovu. 17Lakini hekima itokayo juu mbinguni, kwanza ni safi; inapenda amani, upole na huwajali watu; imejaa huruma na huzaa matunda ya matendo mema; haina ubaguzi wala unafiki. 18Uadilifu ni mazao ya mbegu ambazo wapenda amani hupanda katika amani.




Shukrani;Daniel Christopher

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.