Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 15 December 2014

Jikoni Leo;[Mkate wa Mchele]Makate or Rice Cake na Raihana Mulla...

Waungwana "Jikoni Leo" na bi'Rahiana Mulla..Mapishi ni Mkate wa Mchele[Mkate wa kumimina].
Waswahili wanasema Mchele mmoja Mapishi mbalimbali..

Haya tuendelee kujifunza......

Thanks/Shukrani;Zaidi-Raihana Mulla
"Swahili Na Waswahili"Pamoja daima.

Friday 12 December 2014

Swahili/Kiswahili Na Waswahili;ULIMI, MATAMSHI, NA KUKAA UGENINI

Watangazaji wa DW wakijadili na kujadiliana masuala kadhaa ya kilugha likiwemo lugha asilia ya mtu huathirika vipi akikaa ugenini kwa muda mrefu, yaani kwenye mazingira ambako lugha yake ya kuzawa nayo haitumiki? Jee, matamshi yake yatapotoshwa mpaka aonekane msemaji mgeni kila azungumzapo kwa lugha yake asilia? Na vipi msamiati wake, utapigwa na wakati au la?







Shukrani;John Mtembezi Inniss

Monday 8 December 2014

Tunaweza Badilika - Mzee Yusuf & Khadija Kopa


Collabo ya kihistoria kati ya Mfalme Mzee Yusuf na Malkia Khadija Kopa katika wimbo na video ya pamoja yenye malengo ya kuhamasisha jamii kupinga ukatili dhidi ya wanawake.

Video hii iliyorekodiwa mkoani Morogoro inamuonyesha Mzee Yusuf na Khadija Kopa kama mume na mke ambao wamebahatika kupata watoto wawili 'Kulwa' na 'Doto' ambao ni mapacha. Mzee Yusuf ni dereva wa daladala wakati Khadija ni mama wa nyumbani lakini pia mjasiriamali.

Pamoja na kwamba watoto wao ni mapacha ambao wanafanana na kulingana kwa karibu kila kitu ikiwemo umri lakini tofauti ya jinsi yao inaonekana kumpa haki zaidi mtoto wa kiume ambaye anaonekana kuelekea shuleni wakati pacha mwenzie anaonekana kuhangaika na shughuli za nyumbani ikiwemo kutafuta maji, kufanya usafi n.k.

Kwa upande mwingine, Mzee anaonekana kutokuijali familia yake haachi pesa ya matumizi nyumbani na hata anapoulizwa anakuwa mkali sana wakati huo huo anaonekana kuchezea mabinti wengine akiwa kazini.

Stori inabadilika kabisa pale mzee anapokutana na Mwanamabadiliko ambaye anafanikiwa kumshawishi kubadili tabia hizo kwa ajili ya manufaa ya familia yake. Kuanzia hapo Mzee anaonekana akinunua nguo za shule za mwanae wa kike na kubandika ujumbe wa mabadiliko katika gari na nyumba yake.

Baada ya hapo maisha yanaonekana kuwa ya raha mustarehe.

"Tukae na tu-starehe tule raha na maisha." Kinasema kibwagizo katika wimbo huo.



Shukrani,zaidi ingia;Tunaweza

Sunday 7 December 2014

Muendelee na Jumapili Hii Vyema;Burudani- Mchanganyiko Tusifu na Kuabudu...!!!

Wapendwa nawatakia/Muendelee na Jumapili hii Njema...
Leo sina mengi..Tusifu na Kuabu..MUNGU wetu ni mwema sana sana...
Tuwaweke kwenye maombi/sala watu wote wenye Shida/Tabu,Wanaopitia Majaribu,kukata tamaa,Wenye kuhitaji.....2Ndugu zangu, muwe na furaha mnapopatwa na majaribu mbalimbali, 


Neno la Leo;Yakobo1:1-27
Salamu;1
Imani na hekima;2-8

Umaskini na utajiri;9-11
Majaribio;12-18
Kusikia na kutenda;19-27

Bible Society of Tanzania









"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Monday 1 December 2014

Mswahili Wetu Leo;da'Louise UWACU-U&I TALK [ NUBI-KMT ] Episode 3 in Ki SWAHILI

Mswahili wetu Leo ni "da'Louise"..yeye ni mzaliwa wa Rwanda[Mnyarwanda].
da'Louise yeye anapenda kujifunza zaidi kiswahili...

Basi nisikuchoshe ungana na dada huyu wa Kinyarwanda...Hongera da'Louise.



Thanks/Shukrani;uwacuvideo

"Swahili Na Waswahili"Pamoja sana.

Sunday 30 November 2014

Nawatakia Jumapili Njema;Burudani-Angela Chibalonza- Uliniumba nikuabudu na Nyingine....

Wapendwa;Natumaini jumapili ilikuwa/ inaendelea Vyema,
1Njoni tumwimbie Mwenyezi-Mungu,
tumshangilie mwamba wa wokovu wetu!

Neno La Leo;Zaburi:95;1-11
Utenzi wa kumsifu Mungu
1Njoni tumwimbie Mwenyezi-Mungu,
tumshangilie mwamba wa wokovu wetu!
2Twende mbele zake na shukrani;
tumshangilie kwa nyimbo za sifa.
3Maana Mwenyezi-Mungu, ni Mungu mkuu;
yeye ni Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
4Vilindi vyote vya dunia vimo mikononi mwake,
vilele vya milima ni vyake.
5Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya;
kwa mikono yake aliiumba nchi kavu.
6Njoni tusujudu na kumwabudu;
tumpigie magoti Mwenyezi-Mungu, Muumba wetu!
7 Maana yeye ni Mungu wetu,
nasi ni watu wa kundi lake,
ni kondoo wake anaowachunga.
Laiti leo mngesikiliza sauti yake:
8“Msiwe wakaidi kama kule Meriba,
kama walivyokuwa kule Masa jangwani,
9wazee wenu waliponijaribu na kunipima,
ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea.
10Kwa miaka arubaini nilichukizwa nao,
nikasema: ‘Kweli, hawa ni watu waliopotoka!
Hawajali kabisa njia zangu!’
11 Basi, nilikasirika, nikaapa:
‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko!’”
Bible Society of Tanzania



"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.