Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 27 August 2014

Wanawake Na Mitindo;[Natural Hair]Nywele zisisowekwa dawa[Chukuchuku]

Waungwa;Wanawake na Urembo,Mitindo..Sikuhizi Wanawake/Kinadada wengi wameamua kurudi/kubaki kwenye Nywele zao za Asili... [Chukuchuku]Wengine hawaweki Dawa wala kusukia Nywele Bandia.Na wengine wanaongezea "Madoido"   kidogo ili kupendezesha Nywele hizo, Wengine wanasuka na kuongezea nywele bandia kidogo lakini hawaendi mbali saana na mitindo ya Kizamani/yakina Mama..Lakini wote wanapendeza tuu..

Jee wewe ni mpenzi wa mitindo hii?
Jee ni kuishiwa/kukosa ubunifu wa mitindo mipya?

Jee kuchoshwa na Mitindo hiyo au kuna/ina  Madhara kiafya?







kwa mitindo na Urembo zaidi tufuate huku;http://mitindoafrica-abroad.blogspot.co.uk/
 "Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima

Sunday 24 August 2014

Tumalizie JumaPili hii Kwa Amani na Baraka;Burudani-Angalia baba,Pamoja na Wewe-Elisha Muliri!!!!!!!

Natumaini Jumjapili hii ilikuwa Njema,Mungu azidi Kuwabariki,Kuwa na Imani,Kusifu,Kuabudu,Kushukuru na Kutukuza...
Akaanza kufundisha tena kando ya bahari.Wakamkusanyikia mkutano mkubwa mno,hata yeye akapanda chomboni, akakaa baharini,mkutano wote ulikuwako juu ya nchi kavu kando ya bahari.2;Akawafundisha mambo mengi kwa mifano,akawaambia katika mafundisho yake.
Neno La Leo;Marko Mtakatifu4:1-40
3;Sikilizeni;Tazama mpanzi alitoka kwenda kupanda;4;Ikawa alipokuwa akipanda, Mbegu nyingine  ilianguka kando ya njia, wakaja ndege wakaila.5;Nyingine ikaanguka penye mwamba,Pasipokuwa na udongo mwingi,;Mara ikaota kwakuwa na udongo hapa;6;Hata jua lilipozuka iliungua, na kwa kuwa haina mizizi ikanyauka.7;Nyingine ikaanguka penye miiba;Ile miiba ikamea ikaisonga, isizae matunda.8;Nyingine zikaanguka penye udongo ulio  mzuri,zikazaa matunda,Zikimea na kukua, na  kuzaa, moja thelathini, moja sitini, na moja mia.9;Akasema, Aliye na masikio ya kusikilia, na asikie.


Mfano Wa Mpanzi:1-9


Shabaha Ya Mifano:10-13[Mat13:10-17[Luka:8:9-10]


Yesu anafafanua mfano wa Mpanzi:13-20[Mat 13:18-23][Luka 8:11-15]

Taa iliyofunikwa:21-25[Luka 8:16-18]

Mfano wa Mbegu inayoota:26-29

Mfano wa Mbegu ya Haradali:30-34[Mat 13:31-32,34][Luka 13:18-19]


Yesu anaamuru dhoruba itulie:35-40[Mat 8:23-27][Luka 8:22-25]




"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Tuesday 19 August 2014

[VIDEO]: Mazungumzo na Liberatus Mwang'ombe na Solomon Chris baada ya Uchaguzi DMV‏


Mubelwa Bandio kati akiwa na aliyekuwa mgombea wa nafasi za Mwenyekiti wa Jumuiya DMV Liberatus Mwang'ombe (L) na mgombea nafasi ya Katibu Msaidizi Solomon Chris (R0 wakati wa mahojiano

Agosti 9, 2014, Jumuiya waTanzania waishio Washington DC, Maryland na Virginia nchini Marekani ilifanya uchaguzi wake mkuu.

Matokeo yake yamekuwa yakipingwa na waliokuwa wagombea wa uchaguzi huo kutokana na sababu mbalimbali.

Wamaketi na Vijimambo Blog na Kwanza Production kueleza sababu hasa za kupinga matokeo hayo siku ya Jumatano ya Agosti 13, 2014.

Karibu uungane nasi kusikia wanachopinga

Mazungumzo na Salma Moshi kuhusu uchaguzi DMV‏




 Salma Moshi akizungumza na Mubelwa Bandio kwenye mahojiano haya


Agosti 9, 2014, Jumuiya waTanzania waishio Washington DC, Maryland na Virginia nchini Marekani ilifanya uchaguzi wake mkuu.

Matokeo yake yamekuwa yakipingwa na waliokuwa wagombea wa uchaguzi huo kutokana na sababu mbalimbali.

Mmoja wa wagombea hao, Salma Moshi amaketi nasi kueleza sababu hasa za kupinga matokeo hayo siku ya Jumatano ya Agosti 13, 2014 chini ya utayarishaji wa Vijimambo Blog


Karibu uungane nasi kusikia anachopinga

 
 

Wednesday 13 August 2014

Mahojiano ya Kwanza Production na Jhiko Manyika a.k.a JhikoMan‏



JhikoMan akitumbuiza kwenye Tamasha la Majahazi 2013
Karibu katika mahojiano kati ya Kwanza Production na Jhiko Manyika a.k.a
JhikoMan aliyejiunga nasi moja kwa moja kutoka Helsinki Finland mwishoni mwa mwezi Julai

Amezungumza
mengi kuhusu ziara yake ya Ulaya iliyoanza mwezi wa nne, maonyesho
aliyofanya, kazi alizorekodi na pia watu aliowashirikisha kwenye albamu
yake mpya ijayo.

Amezungumzia IMANI ya RASTA na pia MUZIKI WA TANZANIA kwa ujumla

Ameongea mengi mema

KARIBU UJIUNGE NASI


Tuesday 12 August 2014

Pitapita ya Mswahili mitaani;Mtu Kwao.!!!!!!!



Tulikutana na hili bango mitaani hapa UK,kuona Bendera ya Kwetu,"Tanzania" Tukavutiwa..
Nyumbani Kwetu ni Kuzuri,Watu wa Kwetu ni Wakarimu..Karibuni Tanzania Karibuni Mtwara. Mambo Ipo Huko!!!!!!!
"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima

Hotuba fupi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Azania Bank kwa DIASPORA‏


Mkurugenzi Mtendaji wa Azania Bank Charles Singili alipokuwa akizungumzia huduma za benki yake kwa waTanzania jijini Washington DC
PICHA ZOTE KWA HISANI YA IKULU
Hotuba fupi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Azania Bank Charles Singili alipokutana na waTanzania waishio nchini Marekani usiku wa Agosti 2, 2014.

Hotuba hii ilitolewa kwenye mkutano kati ya waTanzania wa Marekani na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk Jakaya Kikwete

Karibu umsikilize