Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 28 April 2014

Mhe Mwigulu Nchemba akizungumzia suala la uraia pacha Washington DC‏

Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba akihojiana na Mubelwa Bandio wa Kwanza Production Washington DC.

Photo Credits: Habari Kwanza blog
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba, amesema kuwa anajivunia kiasi cha UZALENDO walichonacho waTanzania hapa nchini, jambo linalompa moyo kuendeleza harakati zake za kusaidia kupatikana kwa uraia pacha, ombi lililo kuu kwa waTanzania waishio nje ya nchi katika mabadiliko ya katiba mpya.

Mhe Nchemba, ambaye alikuwa mmoja wa wageni waalikwa kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanzania yaliyofanyika jijini Washington DC nchini Marekani, amesema kuwa ushiriki wa waTanzania na rafiki zao katika maadhimisho haya, umemdhihirishia nia na mapenzi yao kwa nchi yao, na hilo limemsukuma zaidi kusaidia kupitishwa kwa suala la uraia pacha kwenye katiba mpya.

Hii ni ripoti katika kipindi cha Morning Jam

Hotuba Ya Mhe. Mwigulu Nchemba katika sherehe za Muungano Washington DC‏


Mhe. Mwigulu Nchemba akizungumza katika moja ya hafla hapa Washington DC
Picha kwa hisani ya Vijimambo Blog
Ifuatayo ni hotuba ya Mhe Mwigulu Nchemba.

Naibu Waziri wa Fedha na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (Tanzania Bara) aliyoitoa katika maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano hapa Washington DC.

Audio hii ni kwa hisani ya Vijimambo Blog


Sunday 27 April 2014

Muendelee Vyema na Jumapili Hii Iwe Yenye Maono Na Imani;Burudani-Upendo Group Kijitonyama - Mungu Anakupenda,Sifa na Zivume!!!!

Wapendwa,Natumaini J'Pili hii inaendelea vyema,Na iwe Yenye Imani,Maono/Ndoto,Shukrani na Hekima.
Mithali:29:18;Pasipo Maono,watu huacha kujizuia;Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.


Neno La Leo;Waebrania:11:1-40.[Maana Ya Imani]
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo,ni bayana ya mambo yasiyoonekana.






"Swahili Na Waswahili"MUNGU Atubariki Sote.

Friday 25 April 2014

Maandalizi ya sherehe za Muungano Washington DC‏





Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Liberata Mulamula akizungumzia maandalizi ya sherehe za miaka 50 ya muungano ofisini kwake Washington Dc Jumatano, Aprili 23, 2014.
Photo: Sunday Shomari

Thursday 24 April 2014

Mswahili wetu Leo;Da'Faiza wa Fabuloustaa!!!!!!!

Mswahili wetu Leo ni  da'Faiza Omar.
Binti huyu ni Blogger na ana mambo meengi mazuri
Kumjua zaidi Karibu sana kwenye Blog yake.

Mtembelee hapa;http://fabulousfaa.blogspot.co.uk

Tuesday 22 April 2014

Mazungumzo na Dr Patrick Nhigula kuhusu Bunge maalum la Katiba‏





Karibu katika mazungumzo na Dr Patrick Nhigula kuhusu mwenendo wa Bunge Maalum la Katiba na mwenendo mzima wa nchi ya Tanzania.
Huu ni mfululizo wa mazungumzo na watu mbalimbali kuhusu suala hili muhimu kwa mustakabali wa nchi ya Tanzania.
Karibu

Kwa maoni, tafadhali wasiliana nasi kwa barua pepe kwanzaproduction at gmail dot com