Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 8 November 2013

Mapenzi Na Wapenzi; [Love Story]Jee Ulimpata wapi huyo Mwenza wako?


Waungwana;Safari ya maisha huanzia mbali sana mpaka watu Kuchumbiana na  wakaamua Kufunga Ndoa/kuishi Pamoja kama Mke na Mume..Pia kila mtu/watu wanapo walipoanzia.
 Jee wewe ulianzia wapi?
 Hahahah..huyo Mchumba wako,Mkeo/Mumeo ulimtoa/Muona/kutana naye wapi?...
Ulitafutiwa,Mlikutana Njiani,kwenye basi,kazini,Chuoni au....?
Jee Unaushauri gani kwa wanaotafuta Wenza/Wachumba/Mke-Mume?






"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.

Tuesday 5 November 2013

Mahojiano ya Jamii Production na Dj Luke Joe‏


Dj Luke akiwa studio na Mubelwa Bandio wa Jamii Production
Karibu katika mahojiano na Dj mkongwe kutoka Tanzania na
mmiliki wa blog ya Vijimambo Lucas Mkami a.k.a Dj Luke Joe


Dj Luke ambaye makazi yake kwa sasa ni Maryland nchini Marekani ameeleza mengi kuhusu kazi zake hizi.

Katika mahojiano haya, ameeleza historia yake katika kuchezesha muziki, aliyemvutia kuingia katika kazi ya uDj, mafanikio ya Dj, changamoto zake, ku-blogu na mengine mengi.


Karibu Uuungane nasi



--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Monday 4 November 2013

Kipindi cha FAMILIA kutoka Jamii Production......FAMILIA ZA KAMBO (sehemu ya mwisho)‏





Mtayarishaji na mtangazaji wa kipindi cha FAMILIA, Georgina Lema
Moja ya sababu zilizotusukuma kujadili masuala kuhusu FAMILIA ZA KAMBO ni takwimu zilizopo hivi sasa kuhusu familia hizi.
Kwa mujibu wa mtandao wa www.blendedandbonded.com, hapa Marekani
• 41% ya ndoa za kwanza huishia kwenye talaka
• 60% ya ndoa za pili huishia kwenye talaka
• 73% ya ndoa za tatu huishia kwenye talaka
• 45% ya wanawake na 50% ya wanaume wataoa tena ndani ya miaka mitano ijayo
• 50% ya ndoa za marudio huhusisha watoto wa mahusiano yaliyopita walio chini ya miaka 18
•Ndoa 2100 huanzishwa kila siku nchini Marekani
• 42% ya watu wazima wana uhusiano wa kambo. Hii inajumuisha mzazi wa kambo / mtoto wa kambo ama ndugu wa kambo
Kwa idadi ya Marekani, takwimu hizi zinamaanisha kuwa familia za kufikia zinahusisha watu wazima wapatao milioni 95.5
•Kuna baba wa kambo milioni 16.5
•Kuna Mama wa kambo milioni 14.
•Wataalamu
wa mahusiano wanasema kuwa ndoa za kufikia ndio zitakuwa ndoa zenye
umaarufu na nyingi zaidi nchini Marekani na kuwa, kutokana na kukosekana
kwa taarifa sahihi kuhusu familia za kufikia, familia hizi mara nyingi
zimejikuta kwenye migogoro na mafarakano.
Nasi tuko hapa kujaribu kuepusha hilo kwa kushirikiana nanyi katika kile tunachoweza kuelimisha kudumisha ndoa hizo.
Ungana nasi katika sehemu hii ya mwisho ya MADA hii.




--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Sunday 3 November 2013

Nawatakia J'Pili Njema yenye Amani;Burudani-bado tupo ,Kijitonyama Choir,Ee Baba,Jehova Baba wa Upendo na...!!!!

Wapendwa Nawatakia J'Pili hii iwe njema..Na usikate tamaa MUNGU yupo na Anatenda/Ametenda/Atatendaaa.. Jehova Baba wa Upendo..Eeee Baba kama si wewe Ningekuwa/Tungekuwa/Ungekuwa Wapi?...Mhhh Acheni MUNGU aitwe MUNGU Bwaana!!!!!

Watulizeni mioyo,Watulizeni mioyo,Watu wangu asema MUNGU wetu....
Neno La Leo;Isaya:40:1-31;

Bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai;watapiga mbio,wala hawata choka;watakwenda kwa miguu,wala hawatazimia.






"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Saaana.

Saturday 2 November 2013

Chaguo La Mswahili Leo;Oliver N'goma-Bane na Nyimgine..!!!






Waungwana "Chaguo La Mswahili Leo" Ni Oliver N'goma...
Mhh..wewe unakumbuka wapi na ilikuwaje/ulikuwa wapi wakati huo?
Maneno Meengi sina nasikiliza kutoka kwako..

Twende Sote sasaaa......





Swahili Na Waswahili Pamoja Sana.

Wednesday 30 October 2013

Tanzania: Tunaweza kujitoa A. Mashariki

Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete

Serikali ya Tanzania imesema inatafakari ushiriki wake ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na inaweza kujitoa ndani ya Jumuiya hiyo iwapo itaendelea kutengwa katika baadhi ya vikao.
Aidha imesema Tanzania haitambui vikao vinavyofanywa na nchi tatu zilizopo ndani ya Jumuiya hiyo ambazo zimekuwa zikizitenga Tanzania na Burundi.
Taarifa zinazohusiana
Tanzania, Afrika Mashariki, Afrika
Waziri anayehusika na masuala ya Afrika Mashariki wa Tanzania Samwel Sitta ameliambia Bunge la Tanzania kuwa makubaliano ya vikao hivyo vinavyofanywa na nchi za Kenya, Rwanda na Uganda yatatekelezwa na nchi hizo zinazofanya vikao hivyo kwa sababu vinafanyika nje ya utaratibu wa mkataba wa jumuiya hiyo.
Katika mikutano iliyofanyika hivi karibuni Tanzania na Burundi hazikualikwa kwenye vikao hivyo.
Kwa mujibu wa Waziri Sitta mikutano ya wakuu wa nchi za Rwanda, Kenya na Uganda ambayo ilianza kwa kuitenga Tanzania ilifanyika Entebbe nchini Uganda mwezi Juni mwaka huu na kufuatiwa na mkutano wa pili uliofanyika Agosti mwaka huu huko Mombasa nchini Kenya ambapo nchi hizo tatu bila kuishirikisha Tanzania walizungumzia uanzishaji wa himaya moja ya forodha.
Mambo mengine waliyozungumza wakuu hao ilikuwa uanzishaji wa visa moja ya utalii kwa nchi zao na matumizi ya vitambulisho vya uraia ambavyo vitatumika kama hati za kusafiria miongoni mwa nchi hizo.
Aidha Waziri Sitta amesema ndani ya mikutano hiyo pia walizungumzia kuanzisha mchakato wa kuanzisha shirikisho la nchi hizo.
Tayari Tanzania imeanza mazungumzo na nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kuangalia ni kwa namna gani zitaanzisha ushirikiano nje ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kama zinavyofanya nchi za Rwanda, Uganda na Kenya.
Habari kutoka;http://www.bbc.co.uk/swahili/habari

Tuesday 29 October 2013

JAMII PRODUCTION YAZINDULIWA RASMI‏ !!




Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara alipokuwa akisisitiza jambo wakati wa mahojiano mafupi aliyofanya na Jamii Production kabla ya KUZINDUA RASMI shughuli za kutayarisha na kusambaza matangazo ya Radio na Video.



Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akiwa na waanzilishi wa Jamii Production, Mubelwa Bandio (kulia) na Abou Shatry (kushoto)

Naam....
Kwa baraka za Mhe. Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt
Fenella Mukangara, JAMII RASMI IMEZINDULIWA RASMI Oktoba 26, 2013,
alipotutembelea kuangalia utendaji wetu na kuizindua rasmi hapa ofisini
kwetu Washington DC.
Hii ilikuwa ni ZAIDI YA TUKIO.
Ilikuwa ni BARAKA KWETU na tunamshukuru kila aliyewezesha hili.
NA SASA.....
Kazi ya kutekeleza yale yaliyousiwa na Mhe Waziri, yaliyo yaliyo msingi
wa kituo chetu, yale yaliyo MAHITAJI ya walaji (hadhira yetu) NA WAJIBU
WA FANI YETU ndio imeanza.
Na......
Hakuna litajalokuwa na maana kama hatutajua namna ambavyo utendaji wetu unaathiri maisha yako kwa namna CHANYA na HASI
Wewe (msikilizaji, mtazamaji na msomaji wetu) ni mdau mkubwa wa kufanikisha hili.
Tuzidi kushirikiana
TWAWAPENDA



Msimamizi wa vipindi na mpigapicha mkuu wa Jamii Production Abou Shatry akisisitiza jambo kabla ya kuwasili kwa mgeni rasmi


Mtayarishaji na Mtangazaji wa kipindi cha FAMILIA Georgina Lema akiwa "kitini"


Mmoja wa wawezeshaji wakuu wa Jamii Production Bwn Isidory Lyamuya wa Prestige Health Services akijaribu vitendea kazi vya kituo


Mhe. Waziri Mukangara akipokea maelezo ya utendaji wa kituo. Kushoto ni Afisa Ubalozi Mindi Kasiga

 
Mhe. Waziri akisikiliza RISALA ya Jamii Production 



 Mhe. Waziri Mukangara akijibu risala ya Jamii Production


Bwn Isidory Lyamuya akipata akipata picha ya pamoja na Mhe. Waziri kwa msaada anaotoa kufanikisha kazi za Jamii Production



Bwn Isidory Lyamuya akipata mkono wa pongezi toka kwa Mhe. Waziri kwa msaada anaotoa kufanikisha kazi za Jamii Production

Abou Shatry akipongezwa na Mhe Waziri Mukangara


"Mwanamama" Georgina Lema wa kipindi cha FAMILIA akipata kumbukumbu na Mhe. Waziri


 Mkurugenzi wa Mambo Jambo Radio Bwn Julius Makiri ambaye aliungana nasi katika uzinduzi huu rasmi akipata kumbukumbu na Mhe. Waziri



 Mhe. Waziri Dkt Fenella Mukangara na Afisa Habari katika Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani Mindi Kasiga pamoja na wanaJAMII

 


Hakuna ZAWADI kubwa sawa na kilichofanyika. Na zawadi pekee tuliyonayo ni UPENDO. Ambao hauonyesheki wala haupimiki.

Lakini....tunapenda POPOTE UWAPO, UKUMBUKE SIKU YA LEO.
Na hivyo..twaomba KIKOMBE hiki kiwe kumbukumbu ya tukio hili kubwa kwetu

Abou Shatry akiwa mahala anapopatawala zaidi...


--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"