Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 19 April 2012

MWAKILISHI MKAAZI WA UNOPS NDUGU OMARY MJENGA AKIBADILISHANA MIKATABA YA UJENZI WA HOSPITALI YA WATOTO NCHINI SIERA LEONE




Ndugu Mjenga wakijadiliana jambo na Naibu Mwakilishi wa UNICEF Bw Gopal Sharma wa nchini Siera Leone

Kutoka kulia ni Bwana Omar Mjenga, Mwakilishi Mkazi wa UNOPS Nchini Sierra Leone, akibadilisha mikataba ya ujenzi wa hospitali tatu za kisasa za watoto na Naibu Mwakilishi wa UNICEF Bw Gopal Sharma aliyemwakilisha Bw Mahimbo Mdoe ambaye ni Mwakilishi Mkazi wa UNICEF Nchini Sierra Leone na Kushoto, ni mwakilishi wa Waziri wa Afya wa Siera Leone.


Bw Mahimbo ni Mtanzania mwingine mwenye cheo cha uwakilishi. Mtanzania mwingine mwenye cheo cha uwakilishi ni Bw Gabriel Rugalema, ambaye ni Mwakilishi Mkazi wa FAO Nchini Sierra Leone. Tanzania inazidi kutamba katika nyanja za kimataifa


Habari hii nimetumiwa na KapingaZ Blog. http://kapingaz.blogspot.co.uk
Ahsanteni sana.

Wednesday 18 April 2012

Jikoni Leo ni Kakazzz,Burudani-Tmk wanaume family - Dar mpaka moro!!!!!!

Kina kaka walioandaa huu msosi.
Kachumbari

Samaki au dagaa?
vipi hapo ugali utaisha?
Mimi nafikiri mboga za leo mwenzake Nguna/Ugali,Jee mwenzangu?
Mboga ya Majani. Jee ukishiba utashushia na nini?

Waungwana Wanaume Leo ndiyo waliotuandalia Chakula,
Kumbe wakiamua wanaweza,Huko nyuma tulijadili kuhusu ''WANAUME NA JIKO'',Kaka S. [Sam mwana wa  Mbogo]Alielezea vyema sana, Hasa yeye anavyohusika Jikoni.Pia akasema Wanawake wengi wakisaidiwa huwa Wanatabia ya Kujisahau.


Kaka zangu hawa nao wanasema wao hupenda kujipikia zaidi kuliko kupikiwa.


Swali;Eti Wanaume wengi wanaopenda Kupika na Kujifanyia kazi za ndani wenyewe Huchagua sana Wanawake wa Ku OA,Huchelewa KUOA au Kuto OA Kabisa?.


Jee wewe Mwenzangu una Maoni,Ushauri Gani? Pamoja sana!!!

Sunday 15 April 2012

Nawatakia J'Pili njema,Burudani-ni wewe baba unaweza na Sifa ni kwako- living water choir!!!!!!!

Muwe na J'Pili Njema woote, Yenye Amani,Furaha, Upendo na Umoja.
Mungu akasema Iwe nuru;Ikawa nuru. Mungu akaiona Nuru,ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza.
Neno la Leo.Mwanzo1:1-8.
Mbarikiwe sana,Upendo Daima.

Friday 13 April 2012

Chaguo la Mswahili Leo;Swahili Taarab Bi Malika - Sitaki sitaki na Vidonge,Isaa Matona-Msumeno!!

Waungwana Mwajionaje na Khariiii?Teheheheeheh .Nimatumaini yangu woote wazima,Leo nimewaletea Taarab za Zamani kidogo,Hizi Taarab hasa hizi za Zamani zinamafumbo sana, yaani kunamaneno mengine unaweza usiyaelewe anamaanisha nini.
Jee wewe ni mpenzi wa Taarab au huwa unasikiliza/kuangalia au kucheza?
Unaona tofauti gani kati ya Taarab za Zamani na sasa na jee Unafikiri Taarab za Zamani Zinamvuto zaidi ya sasa au Za Sasa Zinamvuto kuliko za Zamani?
Karibuni sana kama hujahi kuzisikia Leo jaribu, na Wapenzi wa Taarab Jimwageni Uwanjani au...Swahili na Waswahili.Pamoja sana tuu!!!!!

Thursday 12 April 2012

Siku kama ya leo da'Victoria-Ruth Alizaliwa!!!!!!

Siku kama ya leo Bibi na Bwana Malonga wa Tanga,Walipata mtoto wa kike na wakamwita Victoria-Ruth.
Hongereni sana wazazi/Walezi na Mungu awabariki sana.


Hongera sana da'Vick-Ruth kwa kuongezeka,Mungu azidi kukubariki na kukulinda siku zote za maisha yako.
Uwe baraka kwa wazazi/walezi ndugu,jamaa ,marafiki  na watu wote wadogo kwa wakubwa.
Uwe na Wakati mzuri leo na siku zote.MUNGU NI PENDO.


Swali la Kizushi:Wapendwa eti watu wenye kutumia the,thatha badala se au sasa,Athante,ASante,walipokuwa watoto walinyonya vidole sana,walideka,walichelewa kuongea au.......


Karibuni Waungwana!!!!!!

Tuesday 10 April 2012

Maelfu ya watanzania wajitokeza kumzika Kanumba Jijini Dar !!..pata na [Video]


Safari ya Mwisho ya Mpendwa wetu Kanumba.Sisi Tulikupenda Lakini Mungu amekupenda zaidi.Ulale kwa Amani.
Picha kwa Masaada wa kaka LUKAZA wa http://josephatlukaza.blogspot.co.uk,Ubarikiwe.
Video kwa msaada wa[ Michuzi blog]http://issamichuzi.blogspot.co.uk.Ahsanteni Sana na   Tulie kwa Amani yeye Amekwenda..

Steven Kanumba (kauli yake ya mwisho) [HD]