Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 22 November 2011

Siku kama ya Leo dada Akhram wa Billy Alizaliwa!!!!

Siku kama ya leo Familia ya Bibi na Bwana Billy, Walipata mtoto wa kike na wakamwita Akhram!!
dada huyu ni mtu wakucheka wakati wote mpole na mwenye heshima,Si muoengeaji sana mpaka akuzoee sana,Nakuongea kwake uwe na muda ili mmalize hayo maongezi kwani ni taratibu mnoo,Ukiona kafunga mdomo bila tabasamu ujue NJAAA Kwenye sekta ya msosi ahaaa hana Tabu kabisa!!!Usikivu,samahani na kufanya vyema darasani kwake ni maisha  ya kawaida.
Mungu awabari wazazi na awape hekima katika Malezi yenu.


Swahili na Waswahili tunakutakia kila lililo jema mwanakwetu!!!!

Thursday 17 November 2011

SHUKRANI KUTOKA KWA FAMILIA YA JUMA PENZA[JP]!!!


Marehemu JUMA PENZA enzi za uhai wake.
Familia ya Juma Penza ya Gongo la Mboto Dar es Salaam inapenda kutoa shukrani za dhati kwa ndugu, jamaa na marafiki walioshirikiana  nasi katika kufanikisha shughuli za msiba wa baba yetu mpendwa, aliyefariki dunia tarehe 12/10/2011 katika hospitali ya Hindu Mandal na kuzikwa tarehe 13/11/2011 katika makaburi ya Kisutu. 



Tunatoa shukrani za pekee kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. J.M. Kikwete, CCM Makao Makuu, ndugu, jamaa, majirani na marafiki kwa misaada yenu ya hali na mali na kwa namna mlivyoshiriki katika shughuli zote za mazishi.  Shukrani za pekee ziwaendee Dr. Macha Ocean Road, wauguzi na madaktari  wa Hindu Mandal.


Kwa kuwa ni vigumu kumshukuru  kila mtu kipekee, tunaomba shukrani hizi  mzipokee  wote kwa mikono miwili  kutokana na jinsi mlivyohusika kwa njia moja ama nyingine katika kufanikisha  shughuli nzima ya msiba wa baba yetu mpendwa Mzee JP.


Tunawashukuru kwa jinsi mlivyokuwa karibu  nasi  kwa dua  na maombi wakati wote  hadi tulipompumzisha baba yetu kipenzi .


Vilevile  tunapenda  kuwakaribisha  katika  mkesha  wa dua  itakayofanyika  Ijumaa usiku  Novemba 18 kuamkia siku ya Jumamosi Novemba 19 ambapo khitma  itasomwa  nyumbani kwa marehemu  Gongo la Mboto Dar es es Salaam wote mnakaribishwa .


Tunawakaribisha wote kwenye Arobaini ya marehemu. Mkesha na kisomo utafanyika siku ya Ijumaa tarehe 18/11/2011 na kufuatiwa na  Khitma itakayosomwa Jumamosi tarehe 19/11/2011 kuanzia saa 5:00 asubuhi nyumbani kwa marehemu Gongo la Mboto Jijini Dar es Salaam.Inna lilah Wainna Ilaih Rajiun

Wednesday 16 November 2011

Kuna Siku za Furaha na Siku za Vilio,Yote ni MaishaTusikate Tamaa!!!

                 Siku Ndugu zangu walipokuwa na Furaha.
                                        Mshumaa ulio Zimika.
                                            Mshumaa ulioZimika

Mungu awatie Nguvu katika wakati huu Mgumu na Sikuzote,Zaidi tudumishe Upendo,Umoja,Ushirikiano na Tusikate Tamaa,Wakati kama huu ndiyo utamjua Rafiki,Ndugu wa Kweli na Mengi Mema kwa Mabaya unaweza kuyasikia.Na niwakati kwa Waliopoteza Wazazi/Wapendwa wao Kuwakumbuka na Kulia tena,Nimeamini wanaosema Kilio hakiishi Utalia kila unapokumbuka.Nilitamani niwe nanyi lakini Mungu aliye nanyi ni Zaidi yetu sisi Tuliyo mbali.Mungu awalaze Mahali Pema Peponi Nduguzangu na Rafiki zangu,Jirani zangu na Wote waliotangulia.Sina Mengi ya Kusema bali nasema Asante Mungu.Wenu MWANAPENZA.

Monday 14 November 2011

Wanawake Waswahili wa Coventry wanakutakia,Kila la kheri da'May!!!!!!!!

                                        Mwenyewe da'May.
                                           Kekiiiii
                                               Kata mwanangu kataaa Keki
             May akilishwa na dada yake Esther,dada huyu ndiyo chanzo cha shughuli hii
                       May akimlisha dada yake kwa Furaha
             Da'May baada ya kumlisha dada yake wakaangaliana,May akasema Asante dada yangu
                   May na Mswahili wa Congo
                Mama mwenye nyumbaaa alilishwa pia
                    dada akisogea kutoa Nasaha zake mambo ya Tanga hayo
                           Heheheheee da'Stellah Akitoa Nasaha zake
                   Weshuuu!! da'Tina akitoa Nasaha zake
                           Wamama wakifuatilia Nasaha mbalimbali
                        Waswahili kutoka Milton nao walikuwepo
                          Da'Edna alikuwa MC siku hiyo, Yupo sambamba na mwali
                           Da'Asha mwenye furaha akifuatilia mapango mzima wa Nasaha
                              Wamama hawa wameguswa na Nasaha
                          Da'Bai yupo makini na kamera yake,lakini sikio lipowazi Kusikiliza Nasaha
                     Da'Sarah,Mamie na Stellah,Shughuli ilikamalika
                                 Da'Tinna alikuwepo
                        Dadazzzz walikuwepo,Neema,Maggie na Vick
                           Penye Wanawake Waswahili hakukosi Mila babuu Mtu kwako yakheeee
                         Haya funga Vibwebwe jamaniiiii!!!!Twende sasa!!
                                Hahhahahha Mwali kakuaaaaaaaaaaa,Swahili na Waswahili Wapendwaaaa


                         Nyanyuka sasa Mdogo wangu ya Coventry yameisha Subiri ya Dar na  Tangaaa

                    Mpango mzima wa muziki na Ngoma ulisababishwa na da'Chikuuuu huyo wa Mwisho


Shughuli hii ndogo ya Kumtakia Ndoa Njema dada May,Iliandaliwa na da'Esther,yeye ni dada wa bi Arusi mtarajiwa, Wanawake Waswahili wa Coventry U.K,[WWCU]Walikuwa bega kwa bega na da'Esther kufanikisha jambo hili.
Wanawake Coventry mpo juu na Mungu awabariki sana!!!


Dada May anatarajia kufunga Ndoa hivi karibuni,Ndoa hiyo itakuwa Nyumbani Tanzania[Bongo].
Kwaniaba ya Wanawake wenzangu;Da'May Tunakutakia Safari njema,Ndoa njema yenye baraka na Mungu akutangulie kwa kila jambo wewe na Mume wako Mtarajiwa pamoja na Familia na Wote watakaofanikisha.
Mengi yalishasemwa  pale kwenye sherehe,Hatuna la zaidi sisi TUNAKUPENDA SANA!!!!!!!