Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label urembo/utanashati. Show all posts
Showing posts with label urembo/utanashati. Show all posts

Saturday 14 April 2018

Wanawake na Urembo,Kucha..

Habari za Jumamosi wapendwa//waungwana..?
weekend yako inakwendaje ?
Jumamosi hii umeamua kufanya nini tofauti?
Na kila jumamosi utaratibu wako ukoje?
Ni kufanya usafi mkubwa wa nyumba?
Kufanya usafi wa nywele,kucha,nyusi au?
najua usafi wa mwili na hivyo vyote ni vya kawaida lakini kuna
vile vya kuongezea na si lazima....

Mimi leo nimekuletea usafi na urembo wa kucha
Jee wewe ni mpenzi wa kuweka kucha bandia?
Jee kama ndiyo huwa unaziacha/kubadili baada ya muda gani?
usipo fanya hivyo unajisikiaje ?
kazi yako inaruhusu uwe na kucha ndefu au kucha za bandia?
jee kama ndiyo vipi ukipata kazi isiyoruhusu urembo huu?
Asanteni karibuni tena.....

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.

Tuesday 9 January 2018

Urembo/Utanashati;Matumizi ya Perfume/Manukato/Mafuta mazuri..

Habari zenu wapendwa/waungwana,Nimatuini yangu mpo vyema..
Leo tuongelee matumizi ya Perfume/manukato/Mafuta mazuri vile wewe unavyoita..
Wewe mpendwa unapenda manukato? jee ipi Perfume unayoipenda sana
au aina gani ya perfume unatumia?
Lini ulianza kutumia haya mafuta mazuri/manukato?
Unasababu za msingi za kutumia au mapenzi  tuu?
Unatumiaje manukato haya? 
unapulizia kwenye mwili,Nguo na kama mwilini ni sehemu zipi?
Wakati gani unatumia?wakati wote au unapotoka tuu
Unajisikiaje ukitumia manukato na usipotumia jee?
Matumizi ya manukato yanaweza kuwa  ulevi kwa mtu/mtejaa?
Umri gani unafaa mtu kuanza kutumia manukato?
Nitatoa zawadi kwa akataye elezea/jibu vizuri


"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.