Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label jikoni leo. Show all posts
Showing posts with label jikoni leo. Show all posts

Thursday 6 December 2012

Jikoni Leo;Tupike Pamoja-Mapishi ya Meat Roll - Recipe of (in Swahili subtitled in english)!!!!!



Waungwana;"Jikoni Leo" ni Tupike Pamoja wametuletea............

Mapishi ya Meat Roll.....


Hakuna kinachoshindikana Kujaribu ndiyo kujifunzaaa...pia usisite kuuliza.

Kujua Meengi ungana na da'Sophi kupitia;
www.tupikepamoja.com/Tupike Pamoja


Mhhhhh Tamu saaaaaana!!!!!!!!!
             
"Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana. 

Thursday 22 November 2012

jikoni Leo;Tupike Pamoja-Mapishi ya Puréed Vegetables - Recipe of (In Swahili)!!!!!



Waungwana; "Jikoni Leo" ni  Puréed vegetables (a special meal for children from 18 months to 4 years old)

 Mpishi si Wengine ni da'Sophi wa "Tupike Pamoja". Mmmhhh Tamu Saaaana!!!!! 

Kwa kujua zaidi ingia;Tupike Pamoja  au www.tupikepamoja.com

"Swahili NA Waswahi" Pamoja Daima.

Friday 16 November 2012

Jikoni Leo;Tupike Pamoja-Mapishi ya Country salad - Recipe of (Swahili)!!!!!!

Waungwana;"Jikoni leo" si wengine ni "Tupike Pamoja," Walipotea kidogo lakini waswahili wanasema kinya kingi kina.............basi wamerudi tena kwa kishindo.

Nisiwachoshe kwa maneno meeengi.Fuatana nasi katika Pishi la Leo ni "Country Salad" ...

Haya mambo hayo...ukitaka kujua zaidi usisite ingiaTupike Pamoja au www.tupikepamoja.com            

"Swahili NA Waswahili"Karibuni Woote!!!
 

Friday 5 October 2012

Jikoni Leo-Mitaani-Hot Dog...!!!

Waungwana; "Jikoni Leo" lilikuwa Mtaani, haya jiko hilo moto ukiwa mwingi unapandisha juu kama bembeaaaa..
Vipi Jiko hili kwa Kuchomea Mahindi,Mihogo,Mishikaki/Nyama Choma  na ............
 Mambo ya Hot Dog hayooo mitaani...Vipi wewe kilaji hiki kinapanda/unakipenda?

 Ahh Wadhungu kwa mikate wanaibadili Jina tuu na kuweka vitu tofauti lakini ni Mkate tuu.
 Hahhaha tena Nyumbani wanywaji Bia kwenye Bar wanakula Nyama choma au Michemsho..Wao Ngano kwa Ngano, Bia kwa Mkate.....

Jee Wanywaji mliokuwa Nje ya Bongo/Tanzania Nanyi mnaweza kunywa Bia kwa Mkate?....

Tunasubiri Maoni,Ushauri na Kuelimisha kwa Upendo..!!  

"Swahili na Waswahili" Pamoja Daima.

Wednesday 15 August 2012

Jikoni Leo; Mswahili alilifuata Mtaani;Burudani-MIRIAM MAKEBA - Pata, Pata!!!

  Huu ulikuwa Mchanganyiko[Msetoo], Mchele,spaghetti,Karoti naaaNjegere yaani kama Biliyani,Pilau. haa hhaaaaaa [Mchanyatooo]

 Huyu alipika Nyama iliyochanganywa na Majani siyajui, Ndizi na vingine vingi kama Tulavyo Waswahili lakini Michanganyo yake tofauti kidogo.[Jamaica]


 Hawa waliandaa OLIVE Kwa radha Tofauti, hii mimi nilitaka kurudisha Chenji[sikuweza kumeza]

 Hii ni Nazi, hiyo Nyeupe kabla haija Okwa, hii ya chini imeOkwa nilipenda sana.

 Hawa walitengeneza/kupika kutumia Tambi[Noodles]Ngano na Viungo vya kwao....


 Hawa walitumia Ngano zaidi.Mmmhhh Ngano ina mambo meeengi sana!!

 Waungwana;"JIKONI  LEO"Lilikuwa Mitaani kuona,kujifunza,kuonja tusivyovijua/Mapishi ya watu wa Nchi Mbalimbali.
Kulikuwa na mambo meengi, Leo tuanze na Jikoni.Kuonja ilikuwa Bureeeee ,Duhh nilionja mpaka nilichoka Mmmmhh vingine havionjeki. Nafikiri ni Mazoea ya Vyakula.
Nazi ilitengenezwa kivingine,Ngano ambayo mimi nimezoea kwa Maandazi,Chapati na vitu vichache vya Kiswahili, nayo ilipikwa kivingine.
Duuhh sijui nianzie wapi niishie wapi,wewe kula kwa picha tuu.MCHELE MMOJA Mapishi Mbali mbali..........

Yote tisa Chakula cha Waswahili Hakikuwepo,Sikujua kwa nini labda hawakuwa na Taarifa au Mwezi Mtukufu waliona walaji Wachacheeeee!!
Katika Kutembea watoto wakaniita Mama tumeona Banda la ZANZIBAR!!!!!!Lakini Tumemsalimia kwa KISWAHILI Amecheka tuu,Tukamsalimia kwa Kiinglishi[ENGLISH] Ametujibu.Nilipofika hapo nikakutana na Muhindi Amezaliwa KENYA naye anamuuliza kama ametokea TANZANIA?Kwa KISWAHILI,Duhhh kaka Muuzaji alichekaaaaa.Akasema hajui hiyo Lugha yeye anajua hiyo kitu ZANZIBAR na MASAI Tuu.Baada ya kuongea Nae Akasema yeye ni MJAMAIKA[JAMAICAN] Hupenda kujifunza Mapishi na Mambo ya Nchi Tofauti.

Mimi nikamsalimia MUHINDI Tuka chapa SWAHILI YETU  na TUKAFURAHI.

Jee Unalolote la Kuongezea kuhusu kwanini WASWAHILI Kutokuwepo/Kutokuwa na Banda hapo?
Uoga,Kutojiamini,Hatupendi kujitangaza,Hatuna Muda/Nafasi ,Mwezi Mtukufu,Hatufuatilii nini kinaendelea Sehemu Tunayo Ishi ...AU?
Karibuni sana kwa Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

 Hii ilikuwa; COVENTRY.U.K.
 "Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.


Monday 6 August 2012

Jikoni leo;Somali Rice Cake (Mkate wa Maashara)na Cilantro Rice!!!!!

Waungwana "JIKONI LEO"Ngoja niwapeleke kwa jarani zetu Wasoli.
Vyakula vyao si vigeni saaana naona tunatofautiana majina na uandaaji labda.Waswahili wanasema MCHELE MMOJA..........."

Kujua Zaidi ingia.SomaliFoodBlog
Shukrani saana.
Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Monday 23 July 2012

Jikoni Leo;Maidana-na JIKO LANGU,Mapishi-Maandazi ya Yogurt!!!!!!!!!

MAHITAJI
yogurt vijiko 2vya chakula
sukari 1/4 mug
hamira kijiko kimoja cha chai
iliki kijiko kimoja cha chai
samli kijiko kimoja cha chakula
unaweza tumia,maji/maziwa/nazi yapime katika mug uliyopimia sukari
ponda hadi unga wako uwe mlaini kiasi,katakata matonge,sukuma kata maandazi yako
yaache yaumuke yachome.
unaweza kutumia maharage,mchuzi wa nyama,maini,samaki kama kitoeo.





Waungwana Mapishi yapo Mengi haya "JIKONI LEO" ni Maandazi ya Yogurt ,Siyo Nazi kaazi kwako kama wewe Mpishi au Muonjaji!!!!


 Mpishi si Mwingine ni da'MAIDANA na "JIKO LANGU"  [LAKE].
kwa Maelezo Zaidi ingiahttp://jiko-langu.blogspot.co.uk/




"Swahili NA Waswahili" inawatakia Ramadhani Njema Waislam woote Dunia.

Tuesday 17 July 2012

How to make fresh coconut-milk (Tui la Nazi) - By Miriam Rose Kinunda!!!!!


Waungwana "JIKONI LEO"Si mwingine ni da'Miriam Rose  Kinunda wa "TASTE OF TANZANIA"
Leo anatuletea jinsi ya kuandaa Tui la Nazi.
Pia kaa Tayari kwa Video mpya zinakuja,Kitabu pia Kipo Njiani.
Kipende chako au........Kujua Zaidi Ingi http://tasteoftanzania.com/blog

Jamani eehh Nazi za Kopo,Box,Unga mzipumzishe haswa mliokuwa Nje ya Nyumbani.
Tena Mwezi wa Ramadhani unakuja kwa Wenzetu Wanaofunga Nazi ndiyo yenyewe au vipi?

Mimi hicho Kibao  cha Mbuzi hapa ninapoishi sijakiona,Lakini sina Hofu Jirani  yangu anaweza kuwa nacho si wanasema mpende Jirani yako? hahahhaa..
Na jee kwanini kiliitwa Kibao cha Mbuzi?

Jee wewe Unapenda Nazi? na Unapenda kuunga/kuweka kwenye Chakula Gani?

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Saaana!!!

Monday 16 July 2012

Jikoni Leo-Mapishi ya coated chicken with chutney - Recipe of (Swahili)!!!!

Waungwana "JIKONI LEO"Si wengine ni "TUPIKE PAMOJA"
Leo wametuletea Mapishi ya Coated Chicken With Chutney.Mmmmhhhh Tamu Sanaaa!!
Hii ni Video Mpya Waungwana Usikose kupitia www.tupikepamoja.com kwa vipimo na kujua zaidi.

"Swahili NA Waswahili" Pamoja saaaana!!!

Monday 2 July 2012

Jikoni Leo;Tupike Pamoja-Mapishi ya Cold Vegetable Soup - Recipe of (Swahili)!!!!!!


Waungwana "JIKONI LEO" Pata video mpya kutoka "TUPIKE PAMOJA" Wanakuletea mambo ya Supu!!
Supu si Nyama tuu, Ungana nao kupitia www.tupikepamoja.com pia unaweza kuungana nao You tube.
Mhhh Tamu sana!!!!!!!!
 Unaswali au Maoni? Usisite kuongea nao ,Usife nalo....hahahaaha "Pamoja sana Swahili NA Waswahili"

Saturday 23 June 2012

Jikoni Leo;Tupike Pamoja, Video Mpya-How to cook Donuts [in Swahili]!!!!!!!

Waungwana "JIKONI LEO"
Ni "TUPIKE PAMOJA" Wametoa Video mpya Jinsi ya Kupika Donuts.kama una Swali,Ushauri Usisite kuwasiliana nao kupitia.www.tupikepamoja.com.

"SWAHILI na WASWAHILI"
Pamoja Sana!!!!!

Friday 15 June 2012

Jikoni Leo;Tupike Pamoja-How to cook Russian salad (In Swahili)!!!!!!!

Waungwana; "JIKONI LEO;"Ni Tupike Pamoja wametoa Mapishi mapya ya Russian Salad,kwa njia ya Video.Lugha ni Kiswahili.
 Usikose kujifunza kupitia "TUPIKE PAMOJA" Mmmmmhh Tamu Saaaana.
Kuona mengi zaidi ingia;www.tupikepamoja.com au hapo pembeni kuna nembo yao bonyeza tuu.

 Pamoja sana Waungwana. "SWAHILI na WASWAHILI"

Wednesday 6 June 2012

Jikoni Leo; ni da'Maidana wa Tmark!!!!!!!!!

Mwenyewe da'Maidana,mamake na Taqqiyyah
Samaki na Mazagazaga na ameungwa/tiwa Nazi
Kitu Samaki kimepakuliwa
Samaki wa Kubanikwa
Visheti,Kashata,Keki, hivyo vyenye kidoti mie naviitaga vibata, sijui vyaitwaje?Hapa bado Ufuta jamani duuhh
Mikate,sijui wewe utaitaje kwani hapa kwangu kila mtu anajina lake!
                                           Ipo kwa umbo tofauti

Waungwana karibuni tena  "JIKONI LEO".Leo Mpishi wetu si Mwingine ni da'Maidana,Ni blogger Mwenza,Pia ni MjasiriaMali,Ukitaka kujua zaidi. Anapatikana.http://tmark-turn.blogspot.co.uk

Nimegundua Waswahili Wengi Wanapenda kupika na kujifunza Mapishi Mbalimbali.
Vipi wewe mwenzangu unapenda kupika?jee mbali na kupika Unapenda/Unaweza Kufanya  nini kwa Mikono yako?



Karibuni sana Waungwana katika yoote!!!!!!
"Swahili na Waswahili" pamoja sana!!!!

Monday 21 May 2012

Jikoni Leo. Mswahili; da'Sophi na Tupike Pamoja!!! Angalia Video!!!!




Karibuni "tupikepamoja.com"


Habari utakazo zipata katika tovuti hii ni picha za video na maelezo ya kina kuhusu namna ya kupika mapishi na vyakula vizuri vya kimataifa muhimu zaidi ni rahisi kupika.
Tovuti hii ni kwa ajili ya watu wanaopenda kupika, kujaribu vyakula vipya na ladha mpya ili kuwashangaza rafiki na familia zao kwa ladha hizo. Maelekezo ya mapishi utakayopata hapa ni kwa ajili ya meza kuu ingawa wakati mwingine tunashirikiana nawe katika vinywaji na viburudisho (deserts & sweets).
kwa kuanzia ni matumaini yetu utafurahia kupika kama sisi.
Pia usisahau kututumia maoni yako, maswali na ujumbe tuweze kuboresha na kutimiza mahitaji yako, Asante kwa ushirikiano wako
Furahia chakula chako!

Kujua zaidi Mtembelee.www.tupikepamoja.com
Haya Waungwana Mambo hayo kazi kwenu na "Tupike Pamoja"

Hongera da'Sophi kazi nzuri.

Wednesday 9 May 2012

Jikoni Leo;Kitabu cha Mapishi cha da'Miriam Rose.Mapishi ya vitumbua kutoka kwa da'Cecy!!!

Cookbook Sneak Peek – Kitabu cha mapishi

Muonekano wa kitabu cha mapishi cha"A Taste of Tanzania".

Cover ame-Design Mwenyewe na Picha amepiga mwenye.Kitabu kitatoka hivi karibuni.

Utakipataje;Ataweka wazi jinsi gani unaweza kupata Kitabu.Ukiingia pale kwake kunasehemu ya mawasiliano,Unaweza kuwasiliana nae Zaidi kupitia http://www.tasteoftanzania.com

Jee da'Miriam anajua KISWAHILI?JIBU;Ndiyo,anakichapa haswa, kama ulivyoona kwenye ile post iliyopita niliandika ni Mswahili.

Nafikiri nimewajibu nijuavyo Waungwana mlionitumia Email na mlionitumia Messages kwenye sim.Na nimeweka hapa kama kuna wengine waliokuwa na maswali kama haya nao Wamepata Jibu.

Haya Waungwana pata mapishi ya UJI na FUTARI kutoka kwa da'Miriam Rose.Hapo juu.

Hapo chini;Mapishi ya "VITUMBUA"Kutoka kwa da'Cecy anapatikana http://mapishinacecy.blogspot.co.uk.

Mswahili mimi kupika vikorombwezo saaaana siweziiiiii,Najua kupika kiasi cha Kula  MUBENA yangu na Watoto yangu na Wageni kidogo tuu,Si kila mtu anaweza kila kitu jamani, Watu na VIPAJI Vyao.MIMI nitakuwa nakurushia Matukio tuu hapa.Na nikipata Muda nitaweza Kuwatembelea Wapishi Nyumbani kwao na Kuwawekea MAZUNGUMZO na MAPISHI HAPA!!AU VIPI WAUNGWANA.SWAHILI NA WASWAHILI!!!PAMOJA SANA TUU.

Monday 7 May 2012

Jikoni Leo;Mswahili,da'Miriam Rose Kinunda,Pishi-Green Bananas na Mengine meengi ya kujifunza!!!


Da'Miriam Rose
imi huwa navutiwa mnoo na kazi zake dada huyu.Huwa sisiti kumuuliza pale nitakapo kujua zaidi.Sijapata nafasi ya k
HayaWaungwana leo nimewaletea da'Mriam Rose wa Kinunda.


Mukutana nae,Lakini kwa mawasiliano tuu kwangu ni mtu asiye na Majivuno,dharau,Umimi/Ubinafsi.Ni dada Mcheshi na mwenye Upendo, na meeengi.


Hongera sana na Ahsante sana da'Miriam Rose kwa yooote,Mungu azidi kukubariki.


Kufahamu zaidi kazi zake na yeye ni nani ingia "Taste of Tanzania"   http://www.tasteoftanzania.com

Wednesday 25 April 2012

Swali kutoka kwa Mwanamke wa Shoka[da'Mija] na Blogger wa Kwanza Mwanamke Mswahili!!!

Kwangu mimi ni Mwanamke wa Shoka huyu dada,Kichwa,mama Vipaji.
Ni Mwanamke wa Kwanza Blogger Mswahili mimi kumfahamu.blog yake http://damija.blogspot.co.uk
Da'Mija na Wanawake wa Shoka.
Swali;wewe Unafikiri Wanawake wa Shoka Wakoje?.

Haya tukiachana na hayo, Shuka Chini uone Swali lake analotaka KuJibiwa,Linatokana na  Mada ya Jikoni leo ni Kakazz.
Mama MM[Jina lake linaanzia na M,Mume wake M, watoto wao M.M]
Kidada zaidi au vipi!!Una mbwembwe wewe dadake.
Nanukuu..
"Swali;Eti Wanaume wengi wanaopenda Kupika na Kujifanyia kazi za ndani wenyewe Huchagua sana Wanawake wa Ku OA,Huchelewa KUOA au Kuto OA Kabisa?."


Nami ngoja niulize kulingana na swali.."Kwani nafasi ya mwanamke ni ipi katika ndoa..Je ni kupika na kufanya kazi za ndani? au kwa maana nyingine ni kwa nini hasa mwanaume huamua kuoa?


Wanaume tungependa majibu yenu zaidi hapa...

        

Wednesday 18 April 2012

Jikoni Leo ni Kakazzz,Burudani-Tmk wanaume family - Dar mpaka moro!!!!!!

Kina kaka walioandaa huu msosi.
Kachumbari

Samaki au dagaa?
vipi hapo ugali utaisha?
Mimi nafikiri mboga za leo mwenzake Nguna/Ugali,Jee mwenzangu?
Mboga ya Majani. Jee ukishiba utashushia na nini?

Waungwana Wanaume Leo ndiyo waliotuandalia Chakula,
Kumbe wakiamua wanaweza,Huko nyuma tulijadili kuhusu ''WANAUME NA JIKO'',Kaka S. [Sam mwana wa  Mbogo]Alielezea vyema sana, Hasa yeye anavyohusika Jikoni.Pia akasema Wanawake wengi wakisaidiwa huwa Wanatabia ya Kujisahau.


Kaka zangu hawa nao wanasema wao hupenda kujipikia zaidi kuliko kupikiwa.


Swali;Eti Wanaume wengi wanaopenda Kupika na Kujifanyia kazi za ndani wenyewe Huchagua sana Wanawake wa Ku OA,Huchelewa KUOA au Kuto OA Kabisa?.


Jee wewe Mwenzangu una Maoni,Ushauri Gani? Pamoja sana!!!

Tuesday 27 March 2012

Jikoni Leo-Ni kwa Mama Mwakitalu!!!Pata na Burudani ya Ngoma!!!!![Mwanamke jiko au Mwaume Jiko?]



Da'Masika/mama Mwakitalu
Mboga za Majani Mchanganyiko,Majani ya Kunde na Majani ya Maboga
Mchuzi wa Samaki Umeungwa/wekwa Nazi na nyanyachungu

Maandaziiiiii na hapo chini ni Mahindi ya Kuchemsha.

Haya Waungwa,vipi wewe unapenda kupika?au Unapika kwasababu ni lazima upike na ule?Kwenye kazi za Nyumbani kila mmoja kuna kazi anapenda kuifanya, Na kuna baadhi ya Kazi hatuzipendi,Lakini tunafanya kwa sababu ni lazima zifanywe,Na utasikia duuh yule kaka/dada au Mama/Baba anajua Kupika sana,Hivi kujua kupika ni Chakula kiive au?
Kwani Utamu/Radha ya chakula wewe unaweza kupendezwa nacho na mwingine asipendezwe nacho.
Jee Kazi/Ujuzi wa Kupika ni kwa Wanawake tuu?Kwani mara nyingi utasikia Mwanamke jiko na si Mwanaume Jiko,Hasa kwa Maisha ya Leo,
 kwa Maisha ya Zamani wengi wao Mama/Dada kazi yao kubwa ni Upishi na Baba wengi ndiyo walikuwa wanafanya Kazi hasa Mijini, Kwa Vijijini Woote BABA na MAMA Wanaenda shambani lakini Kupika ni MAMA.Jee Leo Tunaweza Thubutu kusema MWANAUME JIKO? AU TUTAKUA TUMEWADHALILISHA?Kwani wapo Wanakarangiza haswaaaa kutushinda au Hamjakutana nao?.


Karibuni Waumgwana kwa Mawazo na Kuelimisha na Kwa upendo.