Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Watoto na Malezi. Show all posts
Showing posts with label Watoto na Malezi. Show all posts

Tuesday 5 July 2011

Mama Lwanji Asema, Shikamoo zikizidi ni ukosefu wa Akili!!!

                                 Mwalimu Lilian Lwanji [mke wa muheshimiwa Lwanji].
                                 Muheshimiwa Lwanji akitoa machache na mama pembeni.
                              Mama Lwanji akiwa na binti yake.
Nanukuu;  Hivi mtoto wako ukikutana nae Sebuleni akakuamkia Shikamoo,Muda mfupi baadae unakutana nae chumba cha stoo akakupa Shikamoo, Tena unakukutana nae chumba cha Kulia chakula anakuamkia Shikamoo,Je hiyo itakuwa ni Heshima au ni ukosefu wa Akili?

Maneno hayo  ya Mwalimu Liliana Lwanji, Jee wazazi/walezi manasemaje kuhusu hizo Shikamoo?

Karibuni sana Waungwana!!!!!!

Habari na Picha,zaidi  zinapatikana;kwa, Mohammed Dewji blog!!!!!!



Wednesday 25 May 2011

Je Utoto wako Ulipitia huku???.

Kunamambo mengi sana  watu hupitia katika safari ya Maisha ya Utoto mpaka Ukubwani.Kama Udokozi wa mboga,pesa,Sukari.Pia Kujaribu kuvuta Sigara,Bangi.Utoro shuleni,Ugomvi/Ubabe,Matusi na mengi mabaya ambayo hayapendeezi katika jamii.Je wewe ulikuwa katika kundi lipi katika haya na je ulibadilika mwenyewe au kwa msaada wa Wazazi/walezi?. Karibuni sana kwa Maoni,Ushauri na Kuelimishana.

Saturday 7 May 2011

Watoto na Urembo!!!!!!

Mzazi/Mlezi na Mwana familia.Unamawazogani kwa watoto wadogo na  kujiremba?.
Hasa kwa mtoto wakike wa Leo/Sasa, Unafikiri ni umri gani kwake unafaa kwa kuanza kupaka,Shedo,Wanja,Rangi za mdomo,Kunyoa nyusi, kupaka Poda na mapambo mengine yanauotumiwa na Wanawake /kina Mama.Na si kila Mama/Mwanamke anayependa kujiremba pia.
Karibuni sana kwa Kuelimishana na Kusaidiana katika Malezi ya Watoto wetu.

Monday 25 April 2011

Wazazi wa sasa na Malezi!!!!!!!


Katika pitapita zangu nimekutana na malezi tofauti ya Watoto.Hasa ya kule Nyumbani Afrika/Tanzania na Wanaoishi nje ya Nchi.Watoto wa Nyumbani wengi wao bado wanaheshima kwa wakubwa wote awe mzazi au jilani,kwa Mgeni au Mwenyeji,Akufahamu/kukujua au Asikufahamu/Kukujua.Unyenyekevu na Usikivu. na mengine mengi.
Watoto wa waishio nje ya Afrika/Ng'ambo Wengi wao ni wabinafsi, wanauthubutu wa kukujibu lolote analoweza,anaweza asikusalimie,hawana karibu wala heshima kwa wakubwa,wanamaamuzi zaidi na matakwa yao,Akisema sitaki na hataki,Na  baadhi ya wazazi wao wanawasilkiliza zaidi, Hata  hawana Aibu kwa matendo ya watoto wala Hofu.
Je Msomaji wewe unamawazo gani katika haya,je ni Mazingira,Maendeleo,Malezi ya kisomi au ni nini kwa hawa wa Nje?.
Na jee hawa wa Nyumbani ni Waoga,Hofu,Kutojiamini au Washamba na wanapitwa na wakati?
Karibuni sana  kwa Kuelimishana na Kufundishana .

Wednesday 13 April 2011

Watoto naTV!!!!!!!!

Wapendwa vipi watoto  na kusogelea TV.Kumekuwa na dhana kwamba watoto hasa wa Afrika wakikaa karibu sana na TV wanaonekana/kuwaita Washamba.Hivi unafikiri kwa nini wanapenda kusogelea TV?.Ili waone vizuri au ndiyo Ushamba? Hata hapa mtoto wangu mmoja tunakosana mara nyingi kwa tabia hiyo!!!!Wewe unamaoni/mawazo gani kuhusiana na hili? Karibu sana tuelimishane.

Thursday 3 March 2011

Mtoto wetu leo ni Naomi Nyembo!!!!!Mswahili anayeishi Holland!!!!!!!!


Naomi ni mtoto mcheshi na mdadisi mwenye vituko vingi sana , Anayependa shule, picha,kula,kupendeza wakati  wowote na  kupati!!.Je wapendwa matendo ya watoto wetu ni urithi kutoka kwetu,Au ni matokeo ya utandawazi? Nasubiri  maoni yako/yenu ili tuelimishane zaidi,Karibuni  wapendwa!!!!!!!!.

Monday 14 February 2011

Watoto na Uhuru!!!!!!!!

Wazazi /Walezi wenzangu.Wewe una  mawazo  gani  kwa watoto chini ya miaka 15,kupewa uhuru wa kusheherekea  siku zao za kuzaliwa na rafiki zao nje ya nyumbani,tena bila ya usimamizi wetu?.Je ndiyo maendeleo,kuwapatia nafasi wajimwage au?Nasubiri mawazo yako ili tujifunze na kuelimishana katika malezi ya watoto wetu, karibuni sana!!!!!!!!!!!!!

Tuesday 11 January 2011

Je matendo yako ya utotoni yanafanana na watoto waleo?

kuvaa nguo za kufanana,,kunywa maji kwa kikombe kimoja, kugombea kitu kama mimi nimekiwahi hiki na vingine vingi!!!!!!!!!!!