Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label WaTanzania/Waswahili. Show all posts
Showing posts with label WaTanzania/Waswahili. Show all posts

Tuesday 26 February 2013

Watanzania wa Ujerumani kusherekea miaka 49 ya Muungano ,jumamosi 27-04-2013 Mjini Koln ! Ujerumani.!!!!!



Umoja wa watanzania Ujerumani (U.T.U) Unapenda kuwajulisha kwamba  Sherehe za miaka ya Muungano Wa Tanzania Bara na Visiwani zitafanyika mjini Koloni, ujerumani siku ya jumamosi Tarehe 27.04.2013 Kuanzia saa 8 za Mchana
katika ukumbi wa Circus Fabric uliopo katika anuani hii::- 
Bergisch Gladbacher Strasse 1007a
51069 Kцln

Vikundi mbali mbali vinatarajiwa kutumbuiza
Ufunguzi saa 8 mchana
Maigizo ya watoto  
Sarakasi ya watoto
Sarakasi ya wakubwa
Ngoma za kiasili kutoka Tanzania 
Break Dance 
Live Bands
Maonyesho ya mavazi ya kisili ya kitanzania
Pia kutakuwa na chakula (a.k.a mnuso)

Kila mtanzania anaweza kushiriki kuuza bidhaa zake binafsi za sanaa kama Vinyago, picha,michoro, ususi NK. kuchukua nafasi katika ratiba ya maonyesho, wasanii wanaotaka kushiriki katika maonyesho wanatakiwa kujiandikisha moja kwa moja kwa Mwenyekiti wa UTU kupitia barua pepei ifuatayo-:


Cell:   +491733 779720 
Cell    +491734297997
Umoja ni Nguvu! Utengano ni Udhaifu !


Wednesday 28 November 2012

Watanzania waishio Ujerumani kufanya hafla ya kumuaga Mhe,Balozi Bw.Ahmada Ngemera !!!








Watanzania waishio Ujerumani kufanya hafla ya kumuaga Mhe,Balozi Bw.Ahmada Ngemera !
Jumamosi 08-December 2012 mjini Berlin,Ujerumani



Umoja wa Tanzania Ujerumani (UTU) unaheshima kubwa kutarifu na kuwaomba watanzania wote
wanaoishi ujerumani na jirani ya Ujerumani kuwa umoja wetu tunatarajia kufanya afla ya kumuaga
Mheshimiwa balozi  Bw. Ahmada Ngemera ambaye anamaliza mda wake wa kufanya kazi,
Afla hiyo itafanyika mjini Berlin siku ya Jumamosi tarehe 8.12.2012 .
Mhe.Balozi bwana Ahmada Ngemera amekua balozi wa Tanzania nchini Ujerumani na watanzania
wanaoishi ujerumani watamkumbuka daima Mheshimiwa Balozi Bw.Ahmada Ngemera kwa kuwa
karibu sana na jamii ya watanzania,pia atakumbukwa kwa jitihada zake au kile ambacho watanzania
 wa ujerumani wanachokiita kuasisi Umoja na mshikamano wa watanzania nchi ujerumani,ambapo
 Mhe.Balozi Bw.Ngemera na msaidizi wake Mhe.Bw.Ali Siwa wahamua kuhamasisha watanzania 
waishio Ujerumani kuungana katika kila hali kuanzisha umoja wa mshikamano wa watanzania,kitu 
ambacho mabalozi wengi walishindwa kufanikiwa kufanya labda kwa sababu ya ukubwa wa nchi ya
 ujerumani wa watanzania wanaishi katika miji mbali mbali,lakini kazi hiyo ya kuwaungunganisha 
watanzania, Balozi Bw.Ahmada Ngemera na Msaidizi wake Bw.Ali Siwa walifanikiwa kuwafikia
 watanzania wote waishio Ujerumani na kuwashauri waanzishe umoja wa mshikimano,na matunda
ya juhudi zao ndipo kukazaliwa Umoja wa waTanzania Ujerumani.(UTU)  Umoja ambao ni chombo
 cha watanzania wote ! chombo ambacho watanzania waishio ujerumani wanajivunia !
UMOJA NA MSHIKAMANO NDIO MSINGI WETU IMARA!
OMBI:
TUNAWAOMBA WATANZANIA WOTE ! NA MARAFIKI WOTE WA TANZANIA
AMBAO WANATAKA KUSHIRIKI KATIKA AFLA HII,
TUNAOMBA MTOE MCHANGO WA EURO 20.00 NA KWA WANAFUNZI EURO 10.00 TU
 kwa kupitia Account : Union of Tanzania in German e.V.
VR Bank Rosenheim-Chiemsee AG
Konto-No.: 59641   BLZ: 71160161
Verwendungszweck: „Kumuaga Mhe. Balozi Ngemera


Pia unaweza kuwasiliana na kamati.utu@googlemail.com
simu namba +491734297997 au Katibu simu namba 01734744265 .