Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Marekani.. Show all posts
Showing posts with label Marekani.. Show all posts

Sunday 8 November 2015

EXIM BANK YAFANYA USAILI KWA WANA-DIASPORA NEW YORK


Exim Bank ya Tanzania siku ya Jumamosi ilifanya usaili kwa Diaspora
Watanzania wanaoishi nchini Marekani jijini New York kwa ajili ya
kuwapa kipaumbele Diaspora na hatimaye kuwapatia kazi kwenye Benki
 hiyo yenye makao makuu yake Dar es Salaam, Tanzania.

Akiongea na Vijimambo/Kwanza Production mkuu wa human resources Bwn.
Fredirick Kanga alisema sababu kubwa ya Benki hiyo kuwafanyia usaili
Diaspora ni kutambua mchango wao na mfumo wa uchapa kazi waliouzoea
ili waweze kuutumia nyumbani katika kuleta maendeleo yenye ufanisi
katika sekta mbalimbali kwenye Benki hiyo ambayo kazi kubwa ni kutoa
huduma bora kwa wateja wake.

Bwn. Fredirick Kanga akijibu swali ni kwanini wasitafute wafanyakazi
waliopo Tanzania ambao wengi wao wamemaliza masomo ya juu na hawana
kazi. Bwn. Kanga alisema sababu kubwa ya kuja Diaspora nikutokana na
kutambua mchango mkubwa wa Diaspora na ufanisi wao katika kazi na sio
kweli kwamba hatuajili Watanzania waliopo nyumbani, tunachojaribu ni
kuchanganya ujuzi wa Diaspora na nyumbani ili kufanikisha na hatimae
kutoa  huduma bora na zenye ufanisi mkubwa, huku akisema Benki ya
Exim ndio Benki yenye asilimia ndogo ya makato kwenye akaunti za
wateja wao nchini Tanzania.

Bwn. Kanga alisema tangia tuanze kuasaili Diaspora tumeisha wapatia
kazi wapatao 25 na mwaka jana pekee tuliwapatia nafasi Diapora 6 toka
Uingereza na 3 kutoka nchini Marekani. Baadhi ya Diaspora wanapenda
kurudi nyumbani lakini wanahofia jinsi gani ya kuanza maisha yao mapya
baada ya kukaa ughaibuni kwa muda mrefu. Exim Benki imeliangalia hilo
na ndio sababu kubwa inayowafanya kufanya usaili kwa WanaDiaspora
anaporudi nyumbani anauhakika na kazi yake.
 Kulia ni Paul Rupia kutoka Massachusetts akifanyiwa usaili na
Bwn. Frederick Kanga na  Dinesh Arora (kulia) ambaye ni Chief
Executive Officer wa Exim Bank siku ya Jumamosi Novemba 7,
2015 katika hotel ya Hilton
katikati ya jiji la New York
 Kulia ni Ability Kakama kutoka New York akifanyiwa usaili na
Bwn. Frederick Kanga na  Dinesh Arora (kulia) ambaye ni Chief
Executive Officer wa Exam Bank siku ya Jumamosi Novemba 7,
2015 katika hotel ya Hilton
katikati ya jiji la New York
 Kulia ni Pamela Mgema kutoka Texas akifanyiwa usaili na Bwn.
Frederick Kanga na  Dinesh Arora (kulia) ambaye ni Chief
Executive Officer wa Exim Bank siku ya Jumamosi Novemba 7,
2015 katika hotel ya Hilton
katikati ya jiji la New York
 Kulia ni Peter Mgema kutoka Texas akifanyiwa usaili na Bwn.
Frederick Kanga na  Dinesh Arora (kulia) ambaye ni Chief
Executive Officer wa Exim Bank siku ya Jumamosi Novemba 7,
2015 katika hotel ya Hilton
katikati ya jiji la New York
 Kulia ni Mariam kutoka Columbus, Ohio akifanyiwa usaili na
Bwn. Frederick Kanga na  Dinesh Arora (kulia) ambaye ni Chief
Executive Officer wa Exim Bank siku ya Jumamosi Novemba 7,
2015 katika hotel ya Hilton
katikati ya jiji la New York
Kie Mlay (kulia) kutoka Maryland akiongea jambo na Bwn, Frederick
Kanga wakati wa usaili wa kujaribu kuwaoatia Diapora nafasi za kazi
kwenye Benki ya Exim yenye makao makuu yake jijini Da es Salaam siku
ya Jumamosi Novemba 7, 2015 katika hotel ya Hilton katikati ya jiji la
New York..





Monday 21 September 2015

SWAHILI FEST COMMUNITY PICNIC YAFANA DMV


Mshereheshaji Tuma akielekeza jambo kwenye tamasha la Swhili Fest lililofanyika siku ya Jumapili Septemba 20, 2015 Bladensburg, Water Front iliyopo jimbo la Maryland nchini Marekani. Picha na Vijimambo Blog/ Kwanza Production.
Patrick Kajale mmoja ya waratibu wa swahili fest akipata picha ya pamoja na mmoja ya watoto walioshinda kucheza wimbo wa Bongo Flava. Waratibu wengine ni Amri Maliyatabu, Seif Ndossa na Frank Kajale.
Patrick Kajale mmoja ya waratibu wa swahili fest akipata picha ya pamoja na mmoja ya watoto walioshinda kucheza wimbo wa Bongo Flava.
Patrick Kajale mmoja ya waratibu wa swahili fest akipata picha ya pamoja na mmoja ya watoto walioshinda kucheza wimbo wa Bongo Flava.
Rais wa Jumuiya ya Watanzania DMV bwn. Iddi Sandaly akiongea machache kwa wageni waliohudhuria tamasha la Swahili Fest.
Mwalimu wa darasa la Kiswahili DMV na mdau wa CHAUKIDU Bi. Asha Nyang'anyi akiongea machache.
Mdau wa CHAUKIDU Bwn. Elius Magembe akilonga machache.
Wageni waliohudhuria tamasha hilo katika picha