Showing posts with label Kheri na Baraka. Show all posts
Showing posts with label Kheri na Baraka. Show all posts
Sunday 12 June 2016
Sunday 29 May 2016
Natumaini Jumapili ilikuwa/inaendelea vyema;Burudani-Ephraim Sekelet Uniongoze,Majaribu Ni Mtaji By Ambwene Mwasongwe,Yesu Ni Bwana by E R Mwansasu Chidumule
Mimi mzee, nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
Uaminifu wa Gayo
2Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni. 3Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakashuhudia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli. 4Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.
Uaminifu wa Gayo
5Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni. 6Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu. 7Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.8Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.
Diotrefe na Demetrio
9Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza. 10Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuza nje ya kanisa.
11Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
12Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.
Salamu za mwisho
13Ninayo bado mengi ya kukuambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino. 14Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana.
15Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.
Bible Society of Tanzania
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.
Sunday 22 May 2016
Natumaini Jumapili ilikuwa njema/inaendelea vyema;Burudani-Natembea kidogo kidogo nikinyatanyata......Happy Birthday da'Tracey-Sarah
8Mungu asema: “Nitakufunza
na kukuonesha njia unayopaswa kufuata.
Nitakushauri kwa uangalifu mkubwa.
Neno La Leo;Zaburi:32:8-11
9Usiwe mpumbavu kama farasi au nyumbu,
ambao lazima wafungwe lijamu na hatamu,
la sivyo hawatakukaribia.”
10Watu waovu watapata mateso mengi,
bali wanaomtumainia Mwenyezi-Mungu wazungukwa na fadhili zake.
11Furahini na kushangilia kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu enyi waadilifu;
pigeni vigelegele vya shangwe enyi wanyofu wa moyo.
Bible Society of Tanzania
Bible Society of Tanzania
"Swahili Na Waswahili"Muwe na wakati mwema.
Sunday 15 May 2016
Nawatakia Jumapili njema:Burudani/Mahubiri na Mwl.Christopher Mwakasege...
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.
Sunday 8 May 2016
Jumapili iendelee kuwa Njema;Burudani-Christopher Mwahangila-Mungu Ni Mungu Tu na Edson Mwasabwite - Ni Kwa Neema Na Rehema
Natuini Jumapili ilikuwa/inaendelea vyema.. Mungu azidi kuwabariki kwa kila jambo.. wanaopitia magumu..Mungu akawaguse.. Mungu yu mwema sana... Nawapenda wote na muwe na wakati mwema... |
Umuhimu wa methali
1 Hizi ni methali za Solomoni mfalme wa Israeli, mwana wa Daudi.2Methali hizi zawapatia watu hekima na nidhamu; zawafanya waelewe maneno ya busara, 3zawafanya kuwa na nidhamu, utaratibu, uadilifu, haki na kutenda kwa usawa. 4Huwapatia wajinga werevu na vijana maarifa na hadhari. 5Mwenye hekima azisikie na kuongeza elimu yake, naye mwenye busara apate mwongozo. 6Mtu aelewe methali na mifano, maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.
lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.
Bible Society of Tanzania"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.
Sunday 13 March 2016
Wapendwa Natumaini Jumapili ni Njema;Burudani-Anchor - Hillsong Live,My God is Awesome - Charles Jenkins,Break Every Chain (Live) - Tasha Cobbs,
Neno La Leo;Wagatia:6:1-18
Tuvumiliane na kusaidiana
1Ndugu, kama mkimwona mtu fulani amekosea, basi, nyinyi mnaoongozwa na Roho mwonyeni mtu huyo ajirekebishe; lakini fanyeni hivyo kwa upole, mkiwa na tahadhari msije nanyi wenyewe mkajaribiwa. 2Saidianeni kubeba mizigo yenu na hivyo mtatimiza sheria ya Kristo.3
7Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna. 8Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu; lakini akipanda katika Roho, atavuna kutoka kwa Roho uhai wa milele. 9Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake. 10Kwa hiyo, tukiwa bado na wakati, tuwatendee watu wote mema, na hasa ndugu wa imani yetu.
Mawaidha ya mwisho na salamu
11Tazameni jinsi nilivyoandika kwa herufi kubwa, kwa mkono wangu mwenyewe. 12Wale wanaotaka kuonekana wazuri kwa mambo ya mwili ndio wanaotaka kuwalazimisha nyinyi mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu moja tu: Kusudi wao wenyewe wasije wakadhulumiwa kwa sababu ya msalaba wa Kristo.13Maana, hao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki sheria; huwataka nyinyi mtahiriwe wapate kujivunia alama hiyo mwilini mwenu. 14Lakini mimi sitajivunia kamwe chochote isipokuwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo; maana kwa njia ya msalaba huo ulimwengu umesulubiwa kwangu, nami nimesulubiwa kwa ulimwengu
17Basi, sasa mtu yeyote asinisumbue tena, maana alama nilizo nazo mwilini mwangu ni zile za Yesu.
18Ndugu, neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amina.
"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.
Subscribe to:
Posts (Atom)