Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Kheri na Baraka. Show all posts
Showing posts with label Kheri na Baraka. Show all posts

Sunday 12 June 2016

Nawatakia Jumapili iliyo njema;Burudani-William Yilima-Yesu Nitie NguvuNimalize Salama,Ee MUNGU,Uko Wapi,Subiri Muujiza Wako,UmulunguMwinza....



Habari za Jumapili wapendwa/wangwana..
nawatakia jumapili yenye baraka tele...




Neno La Leo;Ufunuo 2:1-29
Ujumbe kwa Efeso







Ujumbe kwa Smurna






Ujumbe kwa Pergamumu








Ujumbe kwa Thuatira





































"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Sunday 29 May 2016

Natumaini Jumapili ilikuwa/inaendelea vyema;Burudani-Ephraim Sekelet Uniongoze,Majaribu Ni Mtaji By Ambwene Mwasongwe,Yesu Ni Bwana by E R Mwansasu Chidumule

Wapendwa habari za Jumapili,Natumai ni njema/inaendelea vyema..
kwetu ni salama kabisa na tunaendelea vyema na leo kulikuw na jua
jumapili inaishia vizuri..

Basi tuendelee kuombeana katika yote,Uwepo wa Mungu utawale pale ulipo,
Watoto wanaondelea na shule Mungu akawaongoze vyema,wale walio kwenye mapumziko kama hapa
kwetu wakawe na wakati mzuri,
Mungu awabariki na kuwaongoza..

          

Neno La Leo;3 Yahane 1-15
Mimi mzee, nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
2Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni. 3Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakashuhudia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli. 4Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.

                       Uaminifu wa Gayo
5Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni. 6Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu. 7Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.8Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.



Diotrefe na Demetrio
9Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza. 10Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuza nje ya kanisa.
11Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
12Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.


 
                                 
 

Salamu za mwisho
13Ninayo bado mengi ya kukuambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino. 14Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana.
15Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.







"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Sunday 22 May 2016

Natumaini Jumapili ilikuwa njema/inaendelea vyema;Burudani-Natembea kidogo kidogo nikinyatanyata......Happy Birthday da'Tracey-Sarah

Wapendwa natumai Jumapili ilikuwa/inaendelea vyema..
Mungu azidi kuwabariki katika yote..


Hapa kwetu Jumapili ni njema kabisaa
Leo tunaungana na binti yetu mpendwa kwa kumbukumbu yake ya siku ya kuzaliwa
Siku kama ya leo Mungu alitubariki na kutujaalia mtoto wa kike da'Trace-Sarah
Mungu anaendelea kumtunza vyema katika yote..
Mungu yu mwema sana tunamrudishia sifa na utukufu kwakwe
Tunamwachilia binti huyu mikononi mwake Baba wa Mbinguni katika yote
Aendelee kuwa Baraka kwetu kama wazazi,walezi, Ndugu,Jammaa,Marafiki na Jamii yote
Mungu yu Mwema mnoooo
Happy Birthday da'Tracey-Sarah.

 8Mungu asema: “Nitakufunza
na kukuonesha njia unayopaswa kufuata.
Nitakushauri kwa uangalifu mkubwa.

Neno La Leo;Zaburi:32:8-11

9Usiwe mpumbavu kama farasi au nyumbu,
ambao lazima wafungwe lijamu na hatamu,
la sivyo hawatakukaribia.”
10Watu waovu watapata mateso mengi,
bali wanaomtumainia Mwenyezi-Mungu wazungukwa na fadhili zake.
11Furahini na kushangilia kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu enyi waadilifu;
pigeni vigelegele vya shangwe enyi wanyofu wa moyo.

Bible Society of Tanzania


"Swahili Na Waswahili"Muwe na wakati mwema.

Sunday 15 May 2016

Nawatakia Jumapili njema:Burudani/Mahubiri na Mwl.Christopher Mwakasege...


wapendwa nimatumaini yangu jumapili ni njema na inaendelea vyema
Nawatakia Amani kutoka Moyoni,Imani,Baraka na Mkono wa Mungu ukawaguse
wote wenye kukata tamaa,wagonjwa,misiba,woga,kuonewa,kukataliwa/kutengwa
wagonjwa na wenye shida/tabu..
Amini Mungu yupo na ukimuita ataitika,Mungu wetu si kiziwi,kipofu...Anaweza na alitenda anatenda anaendelea kutenda....














"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.

Sunday 8 May 2016

Jumapili iendelee kuwa Njema;Burudani-Christopher Mwahangila-Mungu Ni Mungu Tu na Edson Mwasabwite - Ni Kwa Neema Na Rehema





Natuini Jumapili ilikuwa/inaendelea vyema..
Mungu azidi kuwabariki kwa kila jambo..
wanaopitia magumu..Mungu akawaguse..
Mungu yu mwema sana...
Nawapenda wote na muwe na wakati mwema...


Umuhimu wa methali
1  Hizi ni methali za Solomoni mfalme wa Israeli, mwana wa Daudi.2Methali hizi zawapatia watu hekima na nidhamu; zawafanya waelewe maneno ya busara, 3zawafanya kuwa na nidhamu, utaratibu, uadilifu, haki na kutenda kwa usawa. 4Huwapatia wajinga werevu na vijana maarifa na hadhari. 5Mwenye hekima azisikie na kuongeza elimu yake, naye mwenye busara apate mwongozo. 6Mtu aelewe methali na mifano, maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.
7  Kumcha Mwenyezi-Mungu ni msingi wa maarifa,
lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.
Bible Society of Tanzania





"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Sunday 13 March 2016

Wapendwa Natumaini Jumapili ni Njema;Burudani-Anchor - Hillsong Live,My God is Awesome - Charles Jenkins,Break Every Chain (Live) - Tasha Cobbs,


Wapendwa;Ni Jumapili nyingine tena Mungu ametupa kibali cha kuwa pamoja tena....
Natumai wote wazima na jumapili ilikuwa/inaendelea vyema..
Tumshukuru Mungu kwa kila jambo,Hakuna na hatokuwepo kama yeye..

 "Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake."
Neno La Leo;Wagatia:6:1-18
Tuvumiliane na kusaidiana
1Ndugu, kama mkimwona mtu fulani amekosea, basi, nyinyi mnaoongozwa na Roho mwonyeni mtu huyo ajirekebishe; lakini fanyeni hivyo kwa upole, mkiwa na tahadhari msije nanyi wenyewe mkajaribiwa. 2Saidianeni kubeba mizigo yenu na hivyo mtatimiza sheria ya Kristo.3
                      3Mtu akijiona kuwa ni kitu, na kumbe si kitu, huyo anajidanganya mwenyewe. 4Lakini kila mmoja na aupime vizuri mwenendo wake mwenyewe. Ukiwa mwema, basi, anaweza kuona fahari juu ya alichofanya bila kuwa na sababu ya kujilinganisha na mtu mwingine. 5Maana kila mmoja anapaswa kuubeba mzigo wake mwenyewe.
                        Mwenye kufundishwa neno la Mungu na amshirikishe mwalimu wake riziki zake.
7Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna. 8Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu; lakini akipanda katika Roho, atavuna kutoka kwa Roho uhai wa milele. 9Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake. 10Kwa hiyo, tukiwa bado na wakati, tuwatendee watu wote mema, na hasa ndugu wa imani yetu.
                           Mawaidha ya mwisho na salamu
11Tazameni jinsi nilivyoandika kwa herufi kubwa, kwa mkono wangu mwenyewe. 12Wale wanaotaka kuonekana wazuri kwa mambo ya mwili ndio wanaotaka kuwalazimisha nyinyi mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu moja tu: Kusudi wao wenyewe wasije wakadhulumiwa kwa sababu ya msalaba wa Kristo.13Maana, hao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki sheria; huwataka nyinyi mtahiriwe wapate kujivunia alama hiyo mwilini mwenu. 14Lakini mimi sitajivunia kamwe chochote isipokuwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo; maana kwa njia ya msalaba huo ulimwengu umesulubiwa kwangu, nami nimesulubiwa kwa ulimwengu

        15Kutahiriwa au kutotahiriwa si kitu; cha maana ni kuwa kiumbe kipya.16Wanaoufuata mwongozo huo nawatakia amani na huruma; amani na huruma kwa Israeli – watu wa Mungu.
17Basi, sasa mtu yeyote asinisumbue tena, maana alama nilizo nazo mwilini mwangu ni zile za Yesu.
18Ndugu, neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amina.










"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.