Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Hongera. Show all posts
Showing posts with label Hongera. Show all posts

Thursday 3 May 2012

Siku ya "Uhuru wa Habari" Duniani


        Ngoma Africa band yatoa salam za hongera kwa wanahabari


Bendi ya maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya "Ngoma Africa band" aka FFU
yenye maskani yake nchini Ujerumani ,inatoa salam za hongera na pongezi nyingi
kwa wanahabari na vyombo vya habari vyote duniani,katika sherehe ya siku ya 
"uhuru wa vyombo vya habari" 3 Mai 2012,bendi hiyo inawapongeza wanahabari
na vyombo vyao,kwa kazi muhimu wanazofanya za kuwapasha habari walimwengu,
kwani mchango wa wanahabari katika kila jamii duniani,ni sawa na mbolea katka maisha 
ya kila siku,kwani maisha bila ya habari ,ni sawa miti bila mizizi,
Hongereni sana wanahabari na Wanalibeneke wote duniani.
FFU wa Ngoma Africa band sasa wanatamba song lao jipya
"Uhuru wa habari" wimbo ambao unasikika at www.ngoma-africa.com
au http://www.ngoma-Africa.com






Tuesday 6 March 2012

Kaka Farid atimiza miaka 14-Ona mambo yake!!!

                                               Poziii
                                     Mpirani
                          Shughulika baba!!!!
                                             Vituko
                                           Mapenzi kwa mama.
Hongera sana kaka Faridi kwa kutimiza miaka 14,Mungu akubariki na kukulinda wakati wote.
Uwe baraka kwa wazazi na watu wote.
Hongera pia Wazazi na Mungu awape Maarifa, Usimamizi na Mema  Yote kwenye Malezi.


Waungwana; Eti watoto Wengi  wa  Kiume ni rafiki/wapo karibu  sana na MAMA kuliko BABA?
Pamoja Wapendwa!!

Saturday 14 January 2012

Siku kama ya leo kaka Isaac Alizaliwa!!!!!!

Siku kama ya Leo miaka kadhaa iliyopita, Kaka Isaac, babake  Sandra na Tracey,Mume ya MadameRachel-siwa,Alizaliwaaa!!!
Tunamshukuru sana Mungu kwa yote juu yako,Mungu akubariki na kukulinda kila inapoitwa Leo.
Akuongezee Miaka Mingi na Ufanikishe malengo yako.Uzidi kuwa Baraka kwetu na Kwa Watu wote.
 Tunakupenda saaana,Wako Rachel,Sandra,Tracey[ Rasca].


Friday 9 December 2011

Kheri ya Miaka 50 yaUhuru,Na Siku kama ya Leo da'Halima Kiwinga Alizaliwa!!!

Nawatakia Kheri ya  Miaka 50 ya Uhuru!Pia Siku kama ya Leo Familia ya M.S.Kiwinga wa Ilala,Sharifu/Shamba,  Ilipata Mtoto wa kike na Wakamwita HALIMA!!!Leo ametimiza miaka 50!!!!!Hongera sana dada yetu mpendwa,Mungu akubariki sana katika yote,Sisi wadogo zako Tunakupenda,kukujali,kukuthamini na Tunajidai kuwa na dada kama wewe .Da'HALIMA Uwe na Wakati mzuri  Leo na siku zote za Maisha yako.MUNGU NI PENDO.Kwaniaba ya Familia ya Marehemu Mzee Kiwinga ni mimi Rachel-Siwa.

Thursday 8 December 2011

Siku kama ya leo kaka Henry Mwana wa Kapinga Alizaliwa!!!!!!



MPIGANAJI SASA ATIMIZA MIAKA KADHAA!!!

Mpiganaji wenu Henry Kapinga wa Blog yenu ya KAPINGAZ Blog leo Tarehe 8/12 ndio siku aliyozaliwa.
Nawashukuru wale wote walionipa Hongera kwa kuukaribia uzee, sasa sijui kama ni wote mnaupenda uzee, manake fainali yake ni shughuli.
ASANTENI SANA!
Nasi Swahili na Waswahili tunakutakia kila lililojema katika maisha yako.

Tuesday 22 November 2011

Siku kama ya Leo dada Akhram wa Billy Alizaliwa!!!!

Siku kama ya leo Familia ya Bibi na Bwana Billy, Walipata mtoto wa kike na wakamwita Akhram!!
dada huyu ni mtu wakucheka wakati wote mpole na mwenye heshima,Si muoengeaji sana mpaka akuzoee sana,Nakuongea kwake uwe na muda ili mmalize hayo maongezi kwani ni taratibu mnoo,Ukiona kafunga mdomo bila tabasamu ujue NJAAA Kwenye sekta ya msosi ahaaa hana Tabu kabisa!!!Usikivu,samahani na kufanya vyema darasani kwake ni maisha  ya kawaida.
Mungu awabari wazazi na awape hekima katika Malezi yenu.


Swahili na Waswahili tunakutakia kila lililo jema mwanakwetu!!!!

Wednesday 9 November 2011

DR. REGINA KAPINGA AIPEPERUSHA VEMA BENDERA YA TANZANIA NDANI YA BILL AND MELINDA GATE FOUNDATION.



DR. Regina Kapinga

Mama Regina (Program Officer of Bill & Melinda Gate Foundation) ni Mtanzania wa kwanza kuchaguliwa kuwa Staff wa Bill and Melinda Gate Foundation.

kutokana na Elimu na uzoefu aliokuwa nao katika kufanya kazi kwenye Taasisi za kimataifa, Taasisi ya kimataifa inayomilikiwa na Tajiri mkubwa Duniani Bill Gate ambaye ni mmiliki wa kampuni kubwa ya technolojia ya Microsoft ikaona imtumie katika kuweza kusimamia shughuli zote zinazohusu misaada mbali mbali katika mabara maskini Duniani, yaani Afrika na Asia.

Watanzania tunakutakia afya njema ili uweze kuitangaza zaidi Nchi yetu, tunaamini kupitia wewe Taifa letu litafaidika na misaada mbali mbali kutoka kwenye Foundation hiyo.
        
Habari hii nimetumiwa na KapingaZ Blog
Asante sana.

Monday 7 November 2011

Da'Arianna Atimiza Miaka 3!!!!!!!

                     da'Arianna  kasimama tayari.
                           Kitu  cha kekiii.
              Mwenyekiti da'Mija akiandaa kekii.
                                 Arianna na mama'ke wakifurahia.
                          Mama Arianna akimsaidia kukata keki.
                              Kula mwanangu weee.
                                Dadazzzzz wakitabasamu.
               watoto wakibadilishana mawazo.
                  dada unajua mchezo huu?
                 Watoto wa Swahili Fellowship, wakisubiri kekii.
                  wametulia wenyewe.
                                    Watoto wanatabasamu naona mambo yalianza kusogea.
                       Watoto waliitikia mwaliko.
                        Mama kula eehhh,mama alikula mwishoni baada ya kuhakikisha watoto wote wamepata keki.

Familia ya bibi na bwana  Jonathan Mbwambo wa Coventry U.K.
Wanamshukuru sana Mungu kwa Mema mengi aliyo watendea, Moja  kati ya hayo ni kumlinda mtoto wao mpendwa da'Ariann mpaka leo Ametimiza miaka 3, Mungu ni Mwema sana.
Pia wanapenda kutoa Shukrani kwa Wazazi  na Watoto wa Coventry Christian Swahili Fellowship,na Wote waliojumuika nao.Shukrani za Pekee zimwendee Mwenyekiti wa Watoto da'Mija na Kamati Yake.
Mungu awabariki wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine.
Familia tunasema Asanteni sana kwa Moyo wenu na Mungu awe nanyi daima.


WENU KATIKA YOTE NA TUNAWAPENDA SANA.



         NASI SWAHILI NA WASWAHILI TUNAMTAKIA ARIANNA MAISHA MEMA YENYE AMANI NA FURAHA TELEEEEEEE.





Tuesday 18 October 2011

YUSTA MSOKA, MWANASHERIA ALIYEFANIKIWA KUTIMIZA MOJA YA NDOTO ZAKE.




Advocate Yusta Msoka

Yusta Msoka akiwa amesimama nyuma, mbele ya dirisha la pili upande wa kulia, akiwa katika picha ya pamoja na Wanasheria wenzake baada ya kula kiapo cha kuwa Advocate (Wakili)

KAPINGAZ Blog inapenda kumpongeza sana Dada Yusta kwa kufanikiwa kufika hapo alipofikia, vile vile inamshauri asiishie hapo aendelee zaidi mpaka aweze kufikia level ambayo ni ya kimataifa.

Kwa kutambua uhaba mkubwa wa Mawakili katika Taifa letu tunapenda kuwapongeza wale wote walioweza kufanikiwa kuwa Mawakili, tunawaomba wakafanye kazi zao kwa uadilifu na kuliletea sifa na mafanikio mazuri taifa letu, hasa hasa kuwa makini katika mikataba mikubwa ambayo taifa letu sasa linaangamia kutokana na mikataba hiyo.
                                                                             Habari hii nimetumiwa na Kapingaz Blog
                                                              Hongera da' Yusta.

Tuesday 11 October 2011

Da'Tamara-Sibusisiwe Atimiza mwaka 1!!!!!!!!!

                    Da'Tamara kama anaota vile!!!!!!
  Duhhhh sasa nimetimiza mwaka, Hawa wazazi sijui watanipeleka Boarding..?
                            Mwenyewe mama Tamara!!
Baba Tamara [kaka Manyanya] naona  kajibebea Tamara wake.


Hongera da'Tamara kwa siku yako hii Muhimu, Mungu akubariki katika yote.
Baba na Mama Tamara; Hongereni  sana na Mungu awe nanyi daima katika malezi ya da'Tamara
na Maisha yenu.


Zaidi kuhusu Tamara na Wazazi wake na menginemengiiiii!!! Ingia http://ninaewapenda.blogspot.co

Saturday 1 October 2011

Siku kama ya Leo dada Rabia,Nyembo Alizaliwa!!!!

Familia ya Bibi na Bwana A.Jumaa wa Dar-es-salaam,Siku kama ya leo walipata mtoto wa kike na Wakamwita  RABIA.






Ujumbe kutoka kwa Rabia.J.Nyembo;Anapenda kuwashukuru sana wazazi wake kwa malezi mema naya upendo waliyompa, mpaka pale alipoolewa.
Shukrani kwako Mume wangu kipenzi bwana Nyembo,na Mungu atubariki siku zote za maisha yetu,pia Asante  Mungu kwa kunijalia watoto wazuri,Naomi na Nadia.
Namshukuru sana Mungu kwakunifikisha hapa.
Mungu Tubariki Sote.


:Swahili na Waswahili wanakutakia kila lililo jema kwako na Familia pia.
 Mungu akuongezee miaka mingine mingiiiiiiiii.


Monday 26 September 2011

Kaka Joel Atimiza Miaka 5!!!!!!!!

             Mwenyewe kaka Joel.
             Kaka Joel akiwaza juu ya miaka 5.
            Akikata keki na da'Tracey akishuhudia.
            Kaka Vin ndiye aliyetuongozea sala ya Chakula.
           da'Manjula akiwa kwenye Sala.
             Hakukuwa na Shani leo ni juisi.
         Kama kawaida ya da'Damari yupo makini kwa watoto.
            da'Damari akihakikisha kila mmoja hakosi keki.
        Mwenyekiti na msimamizi mkuu wa watoto wa Swahili Fellowship, da'Mija Mwanamke wa Shoka.
   da'Josephine ,Mdhungu Mswahili mwenye vituko alikuwepo.
    Wamama waliwakilishwa na Mke wa Mwenyekiti wa Swahili Felloship da'Edna.


Familia ya Bwana Godfrey[Mzee wa Fellowship] na bibi Mellanie wa Coventry,U.k.
Wanamshuru sana Mungu kwa kumtunza mtoto wao Joel na Mungu azidi kumsimamia katika makuzi yake,
Awe baraka kwao na kwa Jamii pia.
Shukrani za pekee ziwaendee Watoto wote wa Coventry Swahili Fellowship,Mwenyekiti da'Mija na msaidizi wake da'Damari, Bila kuwasahau Wazazi/Walezi na wote waliofanikisha sherehe ya kaka Joel.
Mungu awabariki sana na wanawapenda sana.

Familia ya Isaac na Cuthbert wa Coventry nao wanamtakia kila lililojema kaka Joel na Mungu awenawe daima,Pia wanasema asanteni sana Familia ya Godfrey kwa yoteeeee!!!Mungu awaongezee kila inapoitwa Leo.


Mengineyo; Kaka Joel anapenda sana Magari na kuyajua mnoo,Mpaka ananishinda mimi jamani, kila aonapo Gari  alipendalo atakwenda kumwambia Mjomba Isaac na Wazazi wake, kutwa anatafuta Magari kwenye Computer, kama uonavyo hapo kwenye keki alikosa Gari kapachika ka'Pikipiki.


Swali; je kupenda huku ni kwasababu ni mtoto wa kiume,akikua anaweza kufanya kazi ya Udereva au zinazohusiana na Magari au ni Utoto tuu akikuwa ataacha?.

Wewe mpendwa kunakitu ulikuwa unapenda wakati wa Utoto na mpaka Leo unakipenda/kukifanya?
Karibuni sana!!!














Sunday 18 September 2011

Siku kama ya Leo dada Levina Alizaliwa!!!!!!!

Leo ni Siku muhimu kwa  da'Levina Kimwaga.
Siku kama ya Leo familia ya Bibi na Bwana Kimwaga, Walipata mtoto wa kike na Wakamwita LEVINA!!!


Tunakutakia kila la kheri,Baraka na Mafanikio kila inapoitwa Leo.


Mungu awe nawe daima.
Karibuni Waungwana Tuduwage pamoja.





Saturday 20 August 2011

Miriam Atimiza Miaka 3!!!!!!!!!

                      Da'Miriam katika poziii.

                                    Keki zote za Miriam.


                       Akijaribu kuzima huku akiogopa.
                               Miriam akisaidiwa kukata keki.
                        Nakupenda sana mama chukua hii,wapambe wakishuhudia.
                            Miriam, Nami nakupenda sana mwanangu nawe kula eehh.
                        Huyu alilishwa kwa niaba ya watoto wa kiume.
                               Na kwaniaba ya watoto wa kike naye alilishwa huyu.
   Mwenyekiti wa wanaume wa Coventry Swahili Christian Fellowship,Alihakikisha kila mtoto anapata keki.
 Mwenyekiti wa watoto wa Coventry Swahili Christian Fellowship,Akishughulika.
                       Watoto wa Kiswahili wakipata chakula.


    Mama hapo akishushia na maji ,Watoto wakifurahi kwa kumaliza vyema na walifungashiwa.
Da'Miriam na mama yake wanasema Asanteni sana kwa kuungana nao katikasiku hii Muhimu kwao.
Pia Shukrani za pekee ziwaendee wana Coventry Swahili Christian Fellowship na Wageni wote.
Anawapenda sana na Mungu awabariki.


Nasi Swahili naWaswahili,Tunakutakia maisha mema na yenye Amani siku zote!!!!!!!