Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 28 June 2018

UZINDUZI WA JUMUIYA YA WATANZANIA UINGEREZA MJINI READING , JUNI 2018


Picha na Habari za Freddy Macha

Kwa miaka mingi imesikika mikutano ya vyama na vilivyodai kushirikisha Watanzania Uingereza. Ila mwaka huu Jumuiya mpya iliyoundwa (ATUK-" Association of Tanzania United Kingdom")- imeahidi kuweka chombo tofauti.


Akizindua hafla hiyo mjini Reading (tamka “redding”) Balozi Asha Rose Migiro, alisifu jitihada hasa za kitengo cha vijana waliosukuma kuelewana. Akahimiza kuwa serikali nzima kuanzia Mheshimiwa Rais, Wizara ya Mambo ya Nje na Ubalozi wako bega moja na ATUK.

Baadaye Joseph Warioba alieleza kuwa kitendo hiki kimefikiwa baada ya utafiti na mazungumzo ya muda mrefu kuhakikisha hakuna tena migongano. Tofauti ya sasa na zamani ni nini? Warioba alihimiza kuwa zamani wahusika waliendekeza maslahi binafsi na ulafi. ATUK tunaelezwa, inashirikisha Watanzania wa kila namna wakiwemo wataalamu, wafanyabiashara, wasomi, wasanii nk. Shughuli iliofanyika Jumamosi 23 Juni, 2018 – ulikusanya zaidi ya Watanzania, ndugu na marafiki zao zaidi ya 300 –kiasi kikubwa kinachodokeza matumaini makubwa.

1- BLOGA- Balozi Migiro akihutubia- pic by F Macha 2018Balozi Migiro akihutubia Watanzania Reading, Jumamosi 23 2018. Kulia kwake ni mwakilishi wa muda wa ATUK, Joseph Warioba na kushoto, Rose Kutandula, Afisa Utawala, Ubalozini.

2-BLOGA- Dk Hamidu Hassan akizungumza kuh wasomi- pic by F Macha 2018Dokta Hassan Hamidu akielezea umuhimu wa wasomi na wataalamu kujiunga kushirikiana kutekeleza ujenzi Nyumbani na Ughaibuni.

3-BLOGA- Mseto wa wageni na wananchi wakisikiliza- pic by F Macha 2018.jpgMseto wa wananchi na wageni wakisikiliza wazungumzaji wa sekta, taaluma na kanda mbalimbali za Uingereza

4-BLOGA- Mjasiria mali Hamidu Mbaga wa All Things African- pic by F Macha 2018.jpgMjasiria mali, Hamida Mbaga, mwenye kampuni ya “All Things African”, akionesha baadhi ya mavazi na bidhaa za Kitanzania anazozisambaza kila ncha ya Uingereza miaka mingi sasa.

5-BLOGA- Balozi Migiro akiwa na mpinzani wa adha ya UKEKETAJI - Devota Haule- pic by F Macha 2018Balozi Migiro (kulia) na mpigania haki za wanawake na adha ya UKEKETAJI, Devota Haule anayeishi Uingereza. Bi Haule ni piamjumbe wa Jumuiya ya wana afya (“health practitioners”) wa Kitanzania Uingereza, yenye zaidi ya wanachama hamsini.

6-BLOGA- Wataalamu mbalimbali - pic by F Macha 2018.jpgWataalamu mseto waliojumuika. Dokta Hassan Hamza, mwanamuziki Fab Moses (WASATU), Dokta Gideon Mlawa (aliyebobea masuala ya Kisukari) Saidi Kanda (WASATU) na Ammy Ninje- kocha wa muda wa Timu ya Taifa Stars. Nyuma yao kabisa, Dk Kazare Nakyoma, mganga wa wenye ulemavu wa akili.

7-BLOGA- Balozi akisalimiana na mmoja wa wageni waliohudhuria- pic by F Macha 2018.jpgBalozi akisalimiana na baadhi ya wageni waliohudhuria

8-BLOGA- Zuhura Mkwawa na Pauline Nzengula- pic by F Macha 2018.jpgWatanzania wengi walisafiri toka majimbo ya mbali Uingereza. Hapa ni Zuhura Mkwawa, mwakilishi Leicester na katibu wake, Pauline Nzengula.

9-BLOGA-Keki ya Ishara- pic by F Macha 2018Keki ya Ishara ya Uzinduzi baada ya kukatwa

10- BLOGA- Waganga na Wanadiplomasia- pic by F Macha 2018Dokta Hamza Hassan, Msaidizi Utawala Ubalozini, Husna Hemed, Balozi Migiro na Dokta Gideon Mlawa

11-BLOGA- Watoto waliotumbuiza - pic by S Mzuwanda 2018.jpgWatoto waliotumbuiza. Picha na Simon Mzuwanda

12-BLOGA-Mwanahabari wa ATUK- Simon Mzuwanda- pic by F Macha 2018.jpgMwanahabari mkuu wa ATUK- Simon Mzuwanda na kamera yake.

Tazama mahojiano na habari zaidi BAADHI YA WALIOSHIRIKI - “Kwa Simu Toka London” ( KSTL)


  1. MAHOJIANO NA JOE WARIOBA
https://www.youtube.com/watch?v=KRPAGkI2WvQ
  1. MAHOJIANO NA DEVOTA HAULE KUHUSU UKEKETAJI
https://www.youtube.com/watch?v=HBgL9IJ75oI&t=23s
  1. MAHOJIANO NA DOKTA GIDEON MLAWA –MTAALAMU WA KISUKARI
https://www.youtube.com/watch?v=uszuASkrSDQ&t=47s
  1. MJASIRIA MALI HAMISA MBAGA AKIZUNGUMZIA KUHUSU BIDHAA ZA KITANZANIA ULAYA
https://www.youtube.com/watch?v=YdiT9x0yguw&t=5s

5. NDOGO NDOGO ZA KIJANA EDWARD “HUNGAZ” CHACHA KUHUSU UMOJA WA WATZ

https://www.youtube.com/watch?v=TWmuDqP3MIM

6. TATHMINI YA MJUMBE WA ATUK- MOHAMMED MWAUPETE

https://www.youtube.com/watch?v=w_HJjmaTbGU











No comments: