Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 12 February 2017

Natumaini Jumapili ilikuwa/Inaendelea Vyema;Burudani-Your Presence Is Heaven,Victor's Crown by Darlene Zschech from REVEALING JESUS

Wapendwa/Waungwana Natumaini Jumapili ilikuwa Njema/Inaendelea Vyema kabisa..
Hapa kwetu ilikuwa nzuri kabisa Tunamshukuru Mungu kwa siku hii kwetu..
Waliokwenda Nyumbani mwa Bwana ninaimani hawakuondoka hivihivi na walichobeba kitawasaidia
wao, Familia na wengine pia..
Kama ulishindwa kufika nyumbani mwa Bwana kwa sababu iliyokuwa nje ya uwezo wako pole sana na Bwana atafanya njia
na upate kufika wakatimwingine..
Kama ni Uvivu,Uzembe au kifungo chochote Mungu akakuamshe na kukukumbusha wakati mwingine usikose
nawe jibidishe/jitahidi kumshinda mwovu na kuungana na wengine nyumbani mwa Bwana..
Mungu aendelee kuwabariki katika yote na tukumbushane kwa Upendo...



“Basi, acheni uovu wote; uongo, unafiki, wivu na maneno ya kashfa visiweko tena. Kama vile watoto wachanga wanavyotamani maziwa, nanyi pia mnapaswa kuwa na hamu ya maziwa halisi ya kiroho, ili kwa nguvu yake mpate kukua na kukombolewa. 

Jiwe kuu
“Basi, acheni uovu wote; uongo, unafiki, wivu na maneno ya kashfa visiweko tena. Kama vile watoto wachanga wanavyotamani maziwa, nanyi pia mnapaswa kuwa na hamu ya maziwa halisi ya kiroho, ili kwa nguvu yake mpate kukua na kukombolewa. Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mmegundua kwamba Bwana ni mwema.” Basi, mwendeeni Bwana! Yeye ndiye jiwe hai lililokataliwa na watu; lakini mbele ya Mungu ni jiwe teule na la thamani kubwa. Mwendeeni yeye kama mawe hai mkajengeke na kuwa nyumba ya kiroho ambamo mtatumikia kama makuhani watakatifu, kutolea tambiko za kiroho zenye kumpendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo. Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Tazama! Naweka jiwe huko Siyoni, jiwe la msingi, teule na la thamani. Mtu atakayemwamini huyo hataaibishwa.” Kwenu nyinyi mnaoamini, jiwe hilo ni la thamani kubwa; lakini kwa wale wasioamini, “Jiwe walilolikataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi.” Tena Maandiko yasema: “Jiwe hilo ni jiwe la kujikwaa, mwamba wa kuwaangusha watu.” Watu hujikwaa kwa sababu hawauamini ule ujumbe; na ndivyo walivyopangiwa tangu mwanzo. Lakini nyinyi ni ukoo mteule, makuhani wa Mfalme, taifa takatifu; watu wake Mungu mwenyewe, mlioteuliwa kutangaza matendo makuu ya Mungu aliyewaiteni kutoka gizani, akawaingizeni katika mwanga wake mkuu. Wakati mmoja nyinyi hamkuwa watu wa Mungu, lakini sasa nyinyi ni watu wake; wakati mmoja hamkupewa huruma ya Mungu, lakini sasa mmepokea huruma.”
‭‭1 Petro‬ ‭2:1-10‬ ‭BHND‬‬
http://bible.com/393/1pe.2.1-10.bhnd






"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

No comments: