Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 5 September 2015

Reggae Time ya Pride FM......Justin Kalikawe




Ni zaidi ya miaka 12 sasa tangu kuondokewa na mwanamuziki mahiri wa Reggae kutoka nchini Tanzania, Justine Kalikawe.

Kwangu
ni kumbukumbu “mbichi” ya kuondoka kwake, kwa kuwa alifariki tukiwa
kwenye mkakati wa kufufua hamasa na umuhimu wa muziki wa reggae nchini.

Nakumbuka
ilikuwa ni mwaka 2003. Mwaka ambao ulikuwa na mambo mengi saana kwangu.
Ndio mwaka ambao nikiwa na Dj Fax (wakati huo sote tukiwa 100.5 Times
Fm) tulipanga mikakati ya kuwa na kipindi bora zaidi cha Reggae jijini
Dar (ambako radio hiyo ilikuwa ikisikika).

Na nakumbuka tulipanga
kukutana na kushauriana na wadau mbalimbali wa Reggae nchini kuhusu
namna tunavyoweza kushirikiana kuunyanyua muziki huo uliolenga katika
KUELIMISHA, KUBURUDISHA na KUIKOMBOA AKILI YA JAMII ya wanyonywaji. Ni
katika harakati hizo nilipoweza kuonana na kufanya mahojiano na wasanii
kama Jah Kimbute, Ras Inno na nikakosa nafasi kuonana na Justine
Kalikawe ambaye alikuwa akikosekana kutokana na ratiba yake ya kurekodi.
Hivyo nikawa "namvizia" ili kujua muda ambao hashiriki kurekodi nimpate
naye aweze kuizungumzia tasnia ya Reggae nchini Tanzania.

Bahati
mbaya Justine aliondoka na kwenda nje ya nchi kwa zaiara ya kimuziki na
aliporejea hakukaa muda mrefu akakutwa na mauti. Huo ndio ukawa mwisho
wa ushiriki wake katika mkakati huo.

Lakini wakati anafariki,
nilikuwa likizo Bukoba, hivyo siku hiyohiyo nilipata taarifa
zilizonishtua sana, lakini nikazikubali na kuanza mikakati ya kushiriki
mazishi yake, jambo ambalo nililifanikisha.

Lakini….

Justin Kalikawe ni nani?

No comments: