Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Hallelujah Mungu yu mwema sana..
Tumshukuru katika yote..
Ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Ni kwa neema/rehema zake,ni kwa mapenzi yake Mungu Baba sisi kuwa hivi tulivyo,Si kwa nguvu zetu,si kwa akili zetu,si kwa uwezo wetu wala si kwa utashi wetu,si kwamba sisi ni wema sana wala si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwamba Sisi ni wazuri mno..
Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote..
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu..
Utukuzwe ee Baba wa Mbinguni,Usifiwe Mungu wetu,Uhimidiwe Yahweh,
Uabudiwe Jehovah,Unatosha Mungu wetu,Matendo yako ni makuu sana,Matendo yako ni ya ajabu mono..
Hakuna kama wewe Mungu wetu..
Sifa na utukufu tunakurudishia wewe Baba wa Mbinguni..!
Lakini nchi ile iliyokuwa imekumbwa na huzuni haitabaki daima katika giza hilo kuu. Hapo awali Mungu alizifedhehesha nchi za Zebuluni na Naftali, lakini siku za usoni ataifanikisha sehemu hii ya baharini na nchi iliyo ngambo ya Yordani na hata Galilaya wanamoishi watu wa mataifa. Watu waliotembea gizani wameona mwanga mkubwa. Watu walioishi katika nchi ya giza kuu, sasa mwanga umewaangazia. Wewe, ee Mungu, umelikuza taifa, umeiongeza furaha yake. Watu wanafurahi mbele yako, wana furaha kama wakati wa mavuno, kama wafurahivyo wanaogawana nyara. Maana nira nzito walizobeba, nira walizokuwa wamefungwa, na fimbo ya wanyapara wao, umezivunjavunja kama wakati wa Wamidiani. Viatu vyote vya washambulizi vitani na mavazi yote yenye madoa ya damu yatateketezwa kama kuni za kuwasha moto.
Mungu wetu tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako..
Yahweh tunaomba utusamehe Dhabi zetu zote tulizozifanya
kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Jehovah nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea..
Baba wa Mbinguni tunaomba utuepushe katika majaribu Yahweh tunaomba utuokoe na yule mwovu na Kazi zake zote...
Mungu wetu tunaomba ututakase miili yetu na akilil zetu Jehovah tunaomba utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..
Maana mtoto amezaliwa kwa ajili yetu, tumepewa mtoto wa kiume. Naye atapewa mamlaka ya kutawala. Ataitwa: “Mshauri wa Ajabu”. “Mungu Mwenye Nguvu”, “Baba wa Milele”, “Mfalme wa Amani”. Utawala wake utastawi daima, amani ya ufalme wake haitakoma. Atachukua wadhifa wa mfalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha, kwa haki na uadilifu, tangu sasa na hata milele. Hayo atayafanya Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
Yahweh tunaomba ukabariki Kazi za mikono yetu..
Mungu wetu tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika ufanyaji/utendaji Baba wa Mbinguni nasi tunaomba tukafanye kama inavyokupendeza wewe..
Mungu wetu tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo Yahweh
nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhutaji..
Mfalme wa amani tuyaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka..
Mungu wetu tunaomba ulinzi wako wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki,Yahweh tunaomba ukatamalaki na kutuatamia..
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako,Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote za maisha yetu..
Baba wa Mbinguni ukaonekane popote tupitapo Yahweh ukajulikane kwamba upo Baba wa Mbinguni..
Mungu wetu ukatufanye chombo chema nasi tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..
Mwenyezi-Mungu ametoa tamko dhidi ya Yakobo nalo litampata Israeli. Watu wote watatambua, ukoo wote wa Efraimu na wakazi wa Samaria. Kwa kiburi na majivuno wanasema: “Kuta za matofali zimeanguka lakini sisi tutazijenga kwa mawe yaliyochongwa! Nyumba za boriti za mikuyu zimeharibiwa lakini mahali pake tutajenga za mierezi.” Basi, Mwenyezi-Mungu atawaletea wapinzani na kuwachochea maadui zao. Waaramu upande wa mashariki, Wafilisti upande wa magharibi, wamepanua vinywa vyao kuimeza Israeli. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, bado ameunyosha mkono wake. Ingawa aliwaadhibu watu, hawakumrudia Mwenyezi-Mungu wa majeshi. Basi kwa muda wa siku moja tu, Mwenyezi-Mungu atakata katika Israeli vichwa na mikia, tawi la mtende na nyasi: Vichwa ndio wazee na waheshimiwa, mikia ndio manabii wafundishao uongo. Wale wanaoongoza watu hawa wamewapotosha, na hao wanaoongozwa nao wamepotoka. Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu hawahurumii vijana wao, hana huruma juu ya yatima na wajane wao; kwani hakuna hata mmoja amchaye Mungu, kila mtu husema uongo. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, bado ameunyosha mkono wake. Uovu huwaka kama moto uteketezao mbigili na miiba; huwaka kama moto msituni, na kutoa moshi mzito upandao angani juu. Kwa ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi nchi imechomwa moto, na watu ni kama kuni za kuuwasha. Hakuna mtu anayemhurumia ndugu yake; wananyanganya upande mmoja na hawatosheki; wanakula upande mwingine lakini hawashibi. Kila mmoja anamshambulia mwenzake. Manase dhidi ya Efraimu, Efraimu dhidi ya Manase na wote wawili dhidi ya Yuda. Hata hivyo, hasira ya Mwenyezi-Mungu haijatulia, bado ameunyosha mkono wake.
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba ukawavushe salama wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali..
Yahweh tunaomba ukawaweke huru wale walio Katika vifungo vya yule mwovu..
Mungu wetu tunaomba ukawatendee walio magerezani pasipo na hatia
Yahweh haki ikatendeke juu yao..
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawaponye wagonjwa na ukawape nguvu/uvumilivu wale wanaowauguza..
Yahweh tuaomba ukawalishe wenye njaa ukawape chakula cha kutosha na kuweka Akiba..
Jehovah tunaomba ukawe tumaini kwa walio kata tamaa,walio kataliwa
wenye tofu na mashaka Mungu wetu ukaonekane katika shida zao
Yahweh tunaomba ukawasamehe wale walio kwenda kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako nazo ziwaweke huru,Nuru yako ikaangaze katika maisha yao,Amani ikatawale..
Baba wa Mbinguni ukawatendee sawasawa na mapenzi yako..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!
Asanteni sana wapendwa/waungwana kwakuwa nami..
Mungu aendelee kuwabariki,amani ikatawale,upendo ukadumu..
Muwe na Christmas njema..
Nawapenda.
|