Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 23 October 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 21...





Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..
Yahweh..!Jehovah..! Adonai..!Elohim..!El Olam..!El Qanna..!
El Elyon..!El shaddai..!Emanueli...!-Mungu pamoja nasi...
Unastahili sifa Mungu wetu,Unastahili kuabudiwa Jehovah,
Unastahili kuhimidiwa Yahweh,Unastahili Kutukuzwa Baba wa Mbinguni....!



Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!



Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, “Mahali hapa ni nyikani, na saa za mchana zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula.” Yesu akawaambia, “Si lazima waende, wapeni nyinyi chakula.” Lakini wao wakamwambia, “Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili.” Yesu akawaambia, “Nileteeni hapa.” Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha Yesu akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akavibariki. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu. Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili. Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao 5,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ngambo ya ziwa wakati yeye anayaaga makundi ya watu. Baada ya kuwaaga watu, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake, na wakati huo ile mashua ilikwisha fika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikumbwa na taabu kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga. Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji. Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliogopa sana, wakasema, “Ni mzimu!” Wakapiga yowe kwa hofu. Mara, Yesu akasema nao, “Tulieni, ni mimi. Msiogope!” Petro akamwambia, “Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako.” Yesu akasema, “Haya, njoo.” Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu. Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, “Bwana, niokoe!” Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, “Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?” Kisha wakapanda mashuani, na upepo ukatulia. Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, “Hakika wewe ni Mwana wa Mungu.”

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji

Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti. Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote, wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake. Nao wote waliomgusa walipona.

Tazama watoto wako wanaokutafuta/kukuomba kwa bidii na imani, Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea
Kufuata njia zako nazo zikawaweke huru
Ukawape macho ya rohoni ee Mungu wetu na masikio ya kusikia
sauti yako,Ukawaokoe na kuwalinda,ukawaponye kimwili na kiroho
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao,Amani ikatawale katika maisha yao,Upendo ukadumu kati yao
 

Baba wa Mbinguni tunayaweke haya yote mikono mwako
tukiamini Mungu wetu utawatendea sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!



Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu
kwakuwanami/kunisoma Mungu Baba aendelee
kuwabariki na kuwatendea kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na Upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima
Nawapenda. 




Jibu la Yobu

1Kisha Yobu akajibu:
2“Sikilizeni kwa makini maneno yangu;
na hiyo iwe ndiyo faraja yenu.
3Nivumilieni, nami nitasema,
na nikisha sema endeleeni kunidhihaki.
4Je, mimi namlalamikia binadamu?
Ya nini basi, nikose uvumilivu?
5Niangalieni, nanyi mshangae,
fumbeni mdomo kwa mkono.
6Nikifikiri yaliyonipata nafadhaika
nafa ganzi mwilini kwa hofu.
7Kwa nini basi waovu wanaishi bado?
Mbona nguvu zao zaongezeka hata uzeeni?
8Huwaona watoto wao wakifanikiwa;
na wazawa wao wakipata nguvu.
9Kwao kila kitu ni salama bila hofu;
wala kiboko cha Mungu hakiwafikii.
10Naam, ng'ombe wao wote huongezeka,
huzaa bila matatizo yoyote.
11Watoto wao wachanga huwatembeza kama kundi;
na watoto wao hucheza ngoma;
12hucheza muziki wa ngoma na vinubi,
na kufurahia sauti ya filimbi.
13Huishi maisha ya fanaka
kisha hushuka kwa amani kuzimu.
14Humwambia Mungu, ‘Usitusumbue!
Hatutaki kujua matakwa yako.
15Mungu Mwenye Nguvu ni nini hata tumtumikie?
Tunapata faida gani tukimwomba dua?’
16Kufanikiwa kwao si kuko mikononi mwao,
wakiwa wamemweka Mungu mbali na mipango yao?21:16 tafsiri inayolingana na Septuaginta. Kiebrania: Shauri la waovu liko mbali nami.
17“Mara ngapi umepata kuona mwanga wa maisha ya mwovu umezimwa,
wakapata kukumbwa na maafa,
au Mungu amewahi kuwaangamiza kwa hasira yake?
18Hata hivyo, na wapeperushwe kama majani makavu,
wawe kama makapi yanayochukuliwa na dhoruba!
19“Nyinyi mwasema, ‘Mungu amewawekea watoto wao
adhabu ya watu hao waovu.’
Kwa nini hawalipizi wao wenyewe, wapate kutambua!
20Waone wao wenyewe wakiangamia;
waone wenyewe ghadhabu ya Mungu mwenye nguvu.
21Maana wakifa watajali nini juu ya wazawa wao,
wakati siku zao zitakapokuwa zimefika mwisho?
22Je, binadamu aweza kumfunza Mungu maarifa,
Mungu ambaye huwahukumu wakazi wa mbinguni?
23“Mtu hufa katika kilele cha ufanisi wake,
akiwa katika raha mustarehe na salama;
24amejaa mafuta tele mwilini,
na mifupa yake ikiwa bado na nguvu.
25Mwingine hufa na huzuni kubwa moyoni,
akiwa hajawahi kuonja lolote jema.
26Hata hivyo, wote hufa na kuzikwa,
wote hufunikwa na mabuu.
27“Sikilizeni! Mimi nayajua mawazo yenu yote,
na mipango yenu ya kunidharau.
28Eti mwauliza, ‘Iko wapi nyumba ya mkuu?
Iko wapi nyumba alimoishi mwovu?’
29“Je, hamjawauliza wapita njia,
mkakubaliana na ripoti yao?
30Mwovu husalimishwa siku ya maafa,
huokolewa siku ya ghadhabu!
31Ni nani atakayemshutumu mtu mwovu,
au atakayemlipa kwa yote aliyotenda?
32Anapochukuliwa kupelekwa kaburini,
kaburi lake huwekewa ulinzi.
33Watu wengi humfuata nyuma
na wengine wengi sana humtangulia.
Anapozikwa, udongo huteremshwa taratibu.
34Mtawezaje basi, kunifariji kwa maneno matupu?
majibu yenu hayana chochote ila uongo.”



Yobu21;1-34

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 22 October 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 20...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua
na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!




Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu. Basi, akawaambia watumishi wake, “Mtu huyu ni Yohane Mbatizaji, amefufuka kutoka kwa wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake.” Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Kisa ni kwamba Yohane alikuwa amemwambia Herode, “Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!” Herode alitaka kumuua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.


Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine

Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa, hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba. Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, “Nipe papa hapa katika sinia kichwa cha Yohane Mbatizaji.” Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe. Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane. Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake. Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini. Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.

Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.



Hoja ya tatu ya Sofari

1Kisha Sofari, Mnaamathi, akajibu:
2“Fikira zangu zanifanya nikujibu,
wala siwezi kujizuia tena.
3Nasikia maonyo nisiyoweza kuvumilia,
lakini akili yangu yanisukuma nijibu.
4“Wewe labda umesahau jambo hili:
Kwamba tangu zamani Mungu alipomuumba mtu duniani,
5mwovu atajiona ameshinda kwa muda tu,
furaha yake asiyemcha Mungu ni ya muda mfupi tu!
6Mwovu aweza kufana hata kufikia mbingu,
kichwa chake kikafika kwenye mawingu,
7lakini atatupiliwa mbali kama mavi yake.
Waliopata kumjua watajiuliza: ‘Yuko wapi?’
8 Taz Hek 5:14 Atatoweka kama ndoto, asionekane tena,
atafutika kama maono ya usiku.
9Aliyemwona, hatamwona tena,
wala pale alipoishi hapatatambuliwa tena.
10Yeye mwenyewe itambidi kurudisha mali yake yote,
watoto wake wataomba huruma kwa maskini.
11Japo alijisikia amejaa nguvu za ujana,
lakini zote zitalala pamoja naye mavumbini.
12“Mdomoni mwake uovu ni mtamu kama sukari,
anauficha chini ya ulimi wake;
13hataki kabisa kuuachilia,
bali anaushikilia kinywani mwake.
14Lakini ufikapo tumboni huwa mchungu,
mkali kama sumu ya nyoka.
15Mwovu humeza mali haramu na kuitapika;
Mungu huitoa tumboni mwake.
16Anachonyonya mtu mwovu ni sumu ya nyoka;
atauawa kwa kuumwa na nyoka.
17Hataishi kuiona mitiririko ya fanaka,
wala vijito vya mafanikio na utajiri.
18Matunda ya jasho lake atayaachilia,
hatakuwa na uwezo wa kuyaonja,
19kwa sababu amewaangamiza maskini na kuwaacha,
amenyakua nyumba ambazo hakuzijenga.
20“Kwa vile ulafi wake hauna mwisho,
hataweza kuokoa chochote anachothamini.
21Baada ya kula hakuacha hata makombo,
kwa hiyo fanaka yake yote haitadumu.
22Kileleni mwa fanaka dhiki itamvamia,
balaa itamkumba kwa nguvu zote.
23Akiwa anajishughulisha kushibisha tumbo,
Mungu atamletea ghadhabu yake
imtiririkie kama chakula chake.
24Labda ataweza kuepa upanga wa chuma,
kumbe atachomwa na upanga wa shaba.
25Mshale utachomolewa kutoka mwilini mwake;
ncha yake itatolewa mgongoni mwake ikingaa,
vitisho vya kifo vitamvamia.
26Hazina zake zitaharibiwa,
moto wa ajabu utamteketeza;
kilichobaki nyumbani mwake kitateketezwa.
27Mbingu zitaufichua uovu wake,
dunia itajitokeza kumshutumu.
28Mali zake zitanyakuliwa
katika siku ya ghadhabu ya Mungu.
29Hicho ndicho apewacho mtu mwovu kutoka kwa Mungu,
ndicho mwovu alichopangiwa na Mungu.”



Yobu20;1-29

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 19 October 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 19...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante

 kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Jehovah  Jireh..!Jehovah Nissi..!Jehovah Raah..!
Jehovah Rapha..!Jehovah Shammah..!Jehovah Shamlom..!
Emanuel-Mungu pamohja nasi..!!
Neema yako yatutosha Baba wa Mbinguni..!

“Sikiliza!” Asema Yesu, “Naja upesi pamoja na tuzo nitakalompa kila mmoja kufuatana na matendo yake. Mimi ni Alfa na Omega, wa kwanza na wa mwisho, mwanzo na mwisho.” Heri yao wale wanaoosha mavazi yao, wapate kuwa na haki ya kula tunda la mti wa uhai, na haki ya kuingia mjini kwa kupitia milango yake. Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona...



“Mimi, Yesu, nimemtuma malaika wangu awathibitishieni mambo haya katika makanisa. Mimi ni mzawa wa ukoo wa Daudi. Mimi ni nyota angavu ya asubuhi!” Roho na Bibi arusi waseme, “Njoo!” Kila mtu asikiaye hili, na aseme, “Njoo!” Aliye na kiu na aje; anayependa, na achukue maji ya uhai bila malipo.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu tunaomba ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya Baba wa Mbinguni ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo Mungu wetu

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Mimi Yohane nawapa onyo wote wanaosikia maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki: Mtu yeyote akiongeza chochote katika mambo haya, Mungu atamwongezea mabaa yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Na mtu yeyote akipunguza chochote katika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, Mungu atamnyang'anya sehemu yake katika ule mti wa uhai, na sehemu yake katika mji mtakatifu, ambavyo vimeelezwa katika kitabu hiki. Naye anayetoa ushahidi wake juu ya mambo haya asema: “Kweli naja upesi.” Amina. Njoo Bwana Yesu! Nawatakieni nyote neema ya Bwana Yesu. Amina.

Tazama wenye shida/tabu,watoto wako wanaokutafuta kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
Yahweh tunaomba  ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu  unajua haja za mioyo ya kila mmoja
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Jehovah ukaonekane katika maisha yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.





Jibu la Yobu

1Kisha Yobu akajibu:
2“Mtaendelea kunitesa mpaka lini,
na kunivunjavunja kwa maneno?
3Mara hizi zote kumi mmenishutumu.
Je, hamwoni aibu kunitendea vibaya?
4Hata kama ingekuwa nimekosa kweli,
kosa langu lanihusu mimi mwenyewe.
5Mnaishusha hadhi yangu mpate kujikuza;
mnanilaumu kwa kunyenyekezwa kwangu.
6Jueni kwamba Mungu amenitendea vibaya,
na kuninasa katika wavu wake.
7Tazama napiga yowe: ‘Dhuluma!’
Lakini sijibiwi.
Naita kwa sauti kubwa,
lakini sipati haki yangu.
8Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipite
amezitia giza njia zangu.
9Amenivua fahari yangu;
ameiondoa taji yangu kichwani.
10Amenivunja pande zote, nami nimekwisha;
tumaini langu amelingoa kama mti.
11Ameichochea ghadhabu yake dhidi yangu;
ameniona kuwa kama adui yake.
12Majeshi yake yanijia kwa pamoja;
yametengeneza njia ya kuja kwangu,
yamepiga kambi kuizunguka nyumba yangu.
13Mungu amewaweka ndugu zangu mbali nami;
rafiki zangu wakuu wamenitoroka kabisa.
14Jamaa zangu na marafiki hawanisaidii tena.
15Wageni nyumbani mwangu wamenisahau;
watumishi wangu wa kike waniona kuwa mgeni.
Mimi nimekuwa kwao mtu wasiyemjua.
16Namwita mtumishi wangu lakini haitikii,
ninalazimika kumsihi sana kwa maneno.
17Nimekuwa kinyaa kwa mke wangu;
chukizo kwa ndugu zangu mwenyewe.
18Hata watoto wadogo hunidharau,
mara ninapojitokeza wao hunizomea.
19 Taz Sir 6:8 “Rafiki zangu wakuu wanachukizwa nami,
wale niliokuwa nikiwapenda wamenipa kisogo.
20Mwili wangu umebakia tu mifupa na ngozi,
nimeponea chupuchupu baada ya kupoteza yote.
21Nioneeni huruma,
nioneeni huruma enyi rafiki zangu;
maana mkono wa Mungu umenifinya.
22Kwa nini mnanifuatia kama Mungu?
Mbona hamtosheki na mwili wangu?
23“Laiti maneno yangu yangeandikwa!
Laiti yangeandikwa kitabuni!
24Laiti yangechorwa kwa chuma na risasi
juu ya jiwe ili yadumu!
25Najua wazi Mkombozi wangu anaishi,
mwishowe yeye atanipa haki yangu hapahapa duniani.
26Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivyo,
nitamwona Mungu kwa macho yangu mwenyewe.19:26 kwa macho yangu mwenyewe: Au Katika mwili huu.
27Mimi mwenyewe nitakutana naye;
mimi mwenyewe na si mwingine nitamwona kwa macho.
28“Nyinyi mwaweza kujisemea:
‘Tutamfuatia namna gani?
29Tutapataje kwake kisa cha kumshtaki?’
Lakini tahadharini na adhabu.
Chuki yenu yaweza kuwaletea kifo!
Mnapaswa kujua: Mungu peke yake ndiye hakimu.”



Yobu19;1-29

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 18 October 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 18...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana..
Tumshukuru Mungu wetu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Baba wa Upendo,Baba wa faraja,Baba wa huruma,Baba wa Baraka
Mungu mwenye nguvu,Mungu mwenye kuponya
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo,Muweza wa yote
Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Alfa na Omega...!!


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe ee Mungu wetu....!!

Kisha malaika akanionesha mto wa maji ya uhai maangavu kama kioo, yakitoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu na Mwanakondoo. Mto huo ulitiririka kupitia katikati ya barabara kuu ya mji. Kandokando ya mto huo kulikuwa na mti wa uhai unaozaa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, yaani kila mwezi; na majani yake ni dawa ya kuwaponya watu wa mataifa. Hapana kitu chochote kilicholaaniwa kitakachokuwa katika mji huo. Kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwanakondoo kitakuwa katika mji huo, na watumishi wake watamwabudu. Watauona uso wake, na jina lake litaandikwa juu ya paji za nyuso zao. Usiku hautakuwako tena, wala hawatahitaji mwanga wa taa au wa jua, maana Bwana Mungu atawaangazia, nao watatawala milele na milele.

Tazama Jana imepita ee Mungu wetu Leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingineJehovah...
Yahweh tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha

na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti

yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona 


Kisha malaika akaniambia, “Maneno haya ni ya kweli na ya kuaminika. Bwana Mungu ambaye huwapa manabii Roho wake, alimtuma malaika wake awaoneshe watumishi wake mambo ambayo lazima yatukie punde. “Sikiliza! Naja upesi. Heri yake anayeyazingatia maneno ya unabii yaliyo katika kitabu hiki.”

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii

 Mungu wetu ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu

Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Tukawe barua njema  ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Mimi Yohane, niliyaona na kusikia mambo haya. Nilipokwisha sikia na kuona, nikajitupa chini mbele ya miguu ya huyo malaika aliyenionesha mambo hayo, nikataka kumwabudu. Lakini yeye akaniambia, “Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako manabii na wote wanaoyatii maagizo yaliyomo katika kitabu hiki. Mwabudu Mungu!” Tena akaniambia, “Usiyafiche kama siri maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, maana wakati wa kutimizwa kwake umekaribia. Kwa sasa anayetenda mabaya na aendelee kutenda mabaya, na aliye mchafu aendelee kuwa mchafu. Mwenye kutenda mema na azidi kutenda mema, na aliye mtakatifu na azidi kuwa mtakatifu.”

Mungu Baba tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabuwote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.




Hoja ya pili ya Bildadi

1Kisha Bildadi, Mshuhi, akajibu:
2“Utawinda maneno ya kusema hadi lini?
Tafakari vizuri nasi tutasema.
3Kwa nini unatufanya kama ng'ombe?
Mbona unatuona sisi kuwa wapumbavu?
4Wewe unajirarua mwenyewe kwa hasira zako.
Kwani, dunia itaachwa tupu kwa ajili yako
au miamba ihamishwe toka mahali pake?
5 Taz Yobu 21:17 “Naam, mwanga wa mtu mwovu utazimishwa;
mwali wa moto wake hautangaa.
6Nyumbani kwake mwanga ni giza,
taa inayomwangazia itazimwa.
7Hatua zake ndefu zitafupishwa;
mipango yake itamwangusha chini.
8Nyayo zake mwenyewe zitamtia mtegoni;
kila akitembea anakumbana na shimo.
9Mtego humkamata kisiginoni,
tanzi humbana kabisa.
10Amefichiwa kitanzi ardhini;
ametegewa mtego njiani mwake.
11Hofu kuu humtisha kila upande,
humfuata katika kila hatua yake.
12Alikuwa na nguvu, lakini sasa njaa imembana;
maafa yako tayari kumwangusha.
13“Ugonjwa mbaya unakula ngozi yake,
maradhi ya kifo18:13 maradhi ya kifo: Neno kwa neno mzaliwa wa kwanza wa kifo. hula viungo vyake.
14Anangolewa katika nyumba aliyoitegemea,
na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
15Nyumba yake tupu, wengine wataishi humo;
madini ya kiberiti yametawanywa katika makao yake.
16Yeye ni kama mti uliokauka mizizi,
matawi yake juu yamenyauka.
17Nchini hakuna atakayemkumbuka;
jina lake halitatamkwa tena barabarani.
18Ameondolewa mwangani akatupwa gizani;
amefukuzwa mbali kutoka duniani.
19Hana watoto wala wajukuu;
hakuna aliyesalia katika makao yake.
20Watu wa magharibi wameshangazwa na yaliyompata,
hofu imewakumba watu wa mashariki.
21Hayo ndio yanayowapata wasiomjali Mungu;
hapo ndipo mahali pa wasiomjua Mungu.”



Yobu18;1-21

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.