Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 9 October 2017

Kikombe Cha Asubuhi Kumbukumbu la Sheria 34 (Kumbukumbu la Torati katika tafsiri nyingine)




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah..!Haleluyah..!Haleluyah..!Mungu wetu yu mwema sana..
Tumshukuru Mungu wetu katika yote..
Mtakatifu..!Mtakatifu..!Mtakatifu..!Baba wa Mbinguni..
Mungu wetu,Muumba wetu,Muumba wa Mbingu na Nchi na vyote vinavyoonekana na visivyo onekana..
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..!
Muweza wa yote,Hakuna kama wewe,Unastahili sifa,
Unastahili kuabudiwa,Unasthahili kutukuzwa,unastahili ee Mungu..!
Uhimidiwe Jehovah,Unatosha Baba wa Mbinguni,
Matendo yako ni makuu sana,matendo yako ni
 ya ajabu,wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Alfa na Omega..!


“Sikiliza!” Asema Yesu, “Naja upesi pamoja na tuzo nitakalompa kila mmoja kufuatana na matendo yake. Mimi ni Alfa na Omega, wa kwanza na wa mwisho, mwanzo na mwisho.” Heri yao wale wanaoosha mavazi yao, wapate kuwa na haki ya kula tunda la mti wa uhai, na haki ya kuingia mjini kwa kupitia milango yake. Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji. “Mimi, Yesu, nimemtuma malaika wangu awathibitishieni mambo haya katika makanisa. Mimi ni mzawa wa ukoo wa Daudi. Mimi ni nyota angavu ya asubuhi!” Roho na Bibi arusi waseme, “Njoo!” Kila mtu asikiaye hili, na aseme, “Njoo!” Aliye na kiu na aje; anayependa, na achukue maji ya uhai bila malipo.

Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwa ulinzi wako kwetu  wakati wote..
Asante kwa kutuchagua na kutupa kibali cha kuendelea
kuiona leo hii Mungu wetu..
Asante kwa pumzi/uzima na ukatufanye tayari kwa majukumu yetu na kujiandaa kwa yajayo..


“Lakini, juu ya siku au saa hiyo, hakuna mtu ajuaye itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana; Baba peke yake ndiye ajuaye. Kwa maana kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu. Maana nyakati hizo, kabla ya gharika kuu, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka Noa alipoingia ndani ya ile safina. Hawakujua kuna nini mpaka ile gharika ilipotokea, ikawakumba wote. Ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Mtu atakapokuja. Wakati huo watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa. Kina mama wawili watakuwa wanasaga nafaka, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa. Basi, kesheni, kwa maana hamjui siku atakayokuja Bwana wenu. Lakini kumbukeni jambo hili: Kama mwenye nyumba angejua siku mwizi atakapofika, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe. Kwa hiyo, nanyi pia muwe tayari, kwa maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”

Si kwamba sisi ni wema sana,si kwa nguvu zetu wala utashi wetu
sisi kuwa hivi tulivyo leo hii Yahweh ni kwa mapenzi yako
ni kwa neema/rehema zako Mungu wetu sisi kuwa hivi tulivyo
Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe Mungu wetu..

Yahweh tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza, tukijishusha na tukijiachilia mikononi mwako Mungu wetu..
Tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya..
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea..
Mungu wetu tunaomba utuepushe katika majaribu Baba 
utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote..
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu 
Baba utufunike kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana
na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti...
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..


“Kweli nawaambieni, yeyote yule asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia mlangoni, bali hupenya na kuingia kwa njia nyingine, huyo ni mwizi na mnyanganyi. Lakini anayeingia kwa kupitia mlangoni, huyo ndiye mchungaji wa kondoo. Mngojamlango wa zizi humfungulia, na kondoo husikia sauti yake; naye huwaita kondoo wake kila mmoja kwa jina lake, na kuwaongoza nje. Akisha watoa nje huwatangulia mbele, nao kondoo humfuata, kwani wanaijua sauti yake. Kondoo hao hawawezi kumfuata mgeni, bali watamkimbia kwa sababu hawaijui sauti yake.” Yesu aliwaambia mfano huo, lakini wao hawakuelewa alichotaka kuwaambia.


Jehovah tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu,Biashara,Masomo na vyote tunavyenda kugusa kutumia Mungu wetu tunaomba ukavitakase na kuvifunika kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..
Mungu wetu vyote tunavyoenda kufanya/kutenda   tukatende kama inavyokupendeza wewe..

Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo 
Mungu wetu nasi tunaomba utupe neema ya kuweza 
kuwabariki wenye kuhitaji,Mungu wetu tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbingu tunaomba utupe sawasawana mapenzi yako..

Mfalme wa Amani tunaomba Amani na Upendo vikatawale katika Nyumba/ndoa zetu,watoto,wazazi wetu,famila/ndugu na wote wanaotuzunguka,Mungu wetu tunaomba ulinzi wako wakati wote
Baba wa Mbimnguni tunaomba utamalaki na kutuatamia..
Yahweh tunaomba uwe nasi katika yote,Mungu wetu tunaomba mkono wako wenye nguvu ukatuguse ,ukatutakase na kutufunika kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo,Mungu wetu ukatupe neema ya kuweza kusimamia Neno lako Amri na Sheria zako siku zote za maisha yetu ,Ukatufanye chombo chema Baba nasi
tukatumike kama inavyokupendeza wewe...
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe
na kiasi..


Basi, akasema tena, “Kweli nawaambieni, mimi ni mlango wa kondoo. Wale wengine wote waliokuja kabla yangu ni wezi na wanyanganyi, nao kondoo hawakuwasikiliza. Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na kupata malisho. Mwizi huja kwa shabaha ya kuiba, kuua na kuharibu. Mimi nimekuja mpate kuwa na uhai – uhai kamili. “Mimi ni mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo wake. Mtu wa kuajiriwa ambaye si mchungaji, na wala kondoo si mali yake, anapoona mbwamwitu anakuja, huwaacha kondoo na kukimbia, kisha mbwamwitu huwakamata na kuwatawanya. Yeye hajali kitu juu ya kondoo kwa sababu yeye ni mtu wa mshahara tu. Mimi ni mchungaji mwema. Nawajua walio wangu, nao walio wangu wananijua mimi, kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Mimi nayatoa maisha yangu kwa ajili yao.
Baba wa Mbinguni tazama wenye shida/tabu,wagonjwa,wenye njaa waliokata tamaa,waliokatawaliwa,walioumizwa,walio katika
vifungo vya yule mwovu,wote wataabikao,
wanaopitia magumu/majaribu mbali mbali,Mungu wetu tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu,Baba ukawape uponyajiwa mwili na roho pia, Mungu wetu ukawasimamishe wote walioanguka,
 Mungu wetu ukasikie kulia kwao Baba ukawafute
machozi ya watoto wako,Mungu wetu ukawape neema ya kuweza kujiombea na kufuata njia zako nazo ziwaweke huru..
Baba wa Mbinguni ukawape msamaha wale wote waliokwenda kinyume nawe,Mungu wetu wakuombapo kwa imani Baba ukawape Amani na kupokea sala/maombi yao..




Tena ninao kondoo wengine ambao hawamo zizini humu. Inanibidi kuwaleta hao pia, nao wataisikia sauti yangu, na kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja. “Baba ananipenda kwani nautoa uhai wangu ili nipate kuupokea tena. Hakuna mtu anayeninyanganya uhai wangu; mimi nautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa na uwezo wa kuuchukua tena. Hivi ndivyo Baba alivyoniamuru nifanye.” Kukawa tena na mafarakano kati ya Wayahudi kwa sababu ya maneno haya. Wengi wao wakasema, “Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?” Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mwenye pepo. Je, pepo anaweza kuyafumbua macho ya vipofu?”

Asante Mungu wetu yote tunayaweka mikononi mwako..
Tukiamini na kushukuru daima..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!!

Asanteni sana wapendwa katika Bwana..
Mungu wetu aendelee kuonekana kwa kila jambo
mfanyalo,naye akawape Baraka na kuwaongezea zaidi
ya mnapojitoa,msipungukiwe katika mahitaji yenu 
Baba wa Mbinguni  akawape kama inavyompendeza yeye..

Nawapenda.


Kifo cha Mose

1Basi, Mose akaondoka kwenye tambarare ya Moabu, akaenda mlimani Nebo, akapanda kilele cha Pisga kilicho mkabala wa Yeriko. Hapo Mwenyezi-Mungu akamwonesha nchi yote: Toka Gileadi mpaka Dani; 2eneo lote la Naftali, eneo la Efraimu na Manase, eneo lote la Yuda mpaka Bahari ya Mediteranea; 3nyika ya Negebu na eneo la nyika ya bonde la Yeriko, mji wa mitende, mpaka Soari. 4Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Hii ndiyo nchi ile niliyomwapia Abrahamu, Isaka na Yakobo kwamba nitawapa wazawa wao. Nimekuonesha uione kwa macho yako mwenyewe, lakini hutafika huko.”
5Basi, Mose mtumishi wa Mwenyezi-Mungu akafariki huko nchini Moabu, kama Mwenyezi-Mungu alivyokuwa amemesema. 6Mwenyezi-Mungu akamzika34:6 akamzika: Kufuatana na baadhi ya hati za Kigiriki; Kiebrania: Akazika. katika bonde la Moabu, mkabala na mji wa Beth-peori; lakini mpaka leo, hakuna mtu ajuaye mahali alipozikwa. 7Mose alikuwa na umri wa miaka 120 alipofariki; macho yake yalikuwa hayajafifia, na alikuwa timamu na mwenye nguvu. 8Waisraeli waliomboleza kifo chake kwa muda wa siku thelathini kwenye nchi tambarare ya Moabu. Kisha siku za matanga na maombolezo ya kifo chake zikaisha.
9Yoshua mwana wa Nuni alijaa roho ya hekima, kwa kuwa Mose alikuwa amemwekea mikono yake. Hivyo Waisraeli walimtii Yoshua na kufuata amri ambazo Mwenyezi-Mungu alimpa Mose.
10Hapajatokea tena nabii katika Israeli kama Mose, ambaye Mwenyezi-Mungu aliongea naye ana kwa ana. 11Hakuna nabii mwingine ambaye alifanya ishara na miujiza kama ile ambayo Mwenyezi-Mungu aliyomtuma Mose afanye juu ya mfalme wa Misri, wakuu wake na nchi yake yote. 12Hakuna nabii mwingine ambaye amefanya mambo makuu na ya kutisha kama alivyofanya Mose mbele ya Waisraeli wote.



Kumbukumbu la Sheria 34:1-12


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 6 October 2017

Kikombe Cha Asubuhi Kumbukumbu la Sheria 33 (Kumbukumbu la Torati katika tafsiri nyingine)



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu kwa Mema mengi aliyotutendea/anayotutendea

Mtakatifu Baba wa Mbinguni,Mungu wetu ,Baba yetu..
Muumba wetu,Muumba wa vyote,Mwenyezi-Mungu shujaa vitani
Mwenyezi-Mungu muweza wa yote,Mwenyezi-Mungu mwenye huruma,Mwenyezi-Mungu ndiye mponyaji,Mwenyezi-Mungu ndiyo jina lake..



Neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Yeremia mara nyingine, wakati alipokuwa bado amefungwa katika ukumbi wa walinzi: Mwenyezi-Mungu aliyeiumba dunia, Mwenyezi-Mungu aliyeifanya na kuiimarisha dunia, ambaye jina lake ni Mwenyezi-Mungu, aliniambia, “Niite, nami nitakujibu na kukuambia mambo makubwa yaliyofichika ambayo hujapata kuyajua. Maana, mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, nasema kwamba nyumba za mji wa Yerusalemu na nyumba za wafalme wa Yuda zitabomolewa kwa sababu ya kuzingirwa na kwa sababu ya mashambulizi. Watu watajaribu kuwakabili Wakaldayo lakini hiyo itakuwa bure, maana mahandaki yatajaa maiti za watu ambao nitawaua kwa hasira na ghadhabu yangu. Kwa vile wamefanya uovu huo wote, mimi nitauacha mji huu. “Hata hivyo, mimi nitauponya mji huu na kuwapa watu wake afya; nitawajalia ustawi mwingi na usalama. Nitawastawisha tena watu wa Yuda na watu wa Israeli; nitawaimarisha kama walivyokuwa hapo awali. Nitawatakasa dhambi zao zote na kuwasamehe uovu wao na uasi walionitendea. Nao mji huu utakuwa sababu ya furaha kwangu, mji wa sifa na fahari mbele ya mataifa yote duniani ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na fanaka nitakazouletea mji huu wa Yerusalemu.” Mwenyezi-Mungu asema: “Katika mji huu ambao mnasema umekuwa ukiwa bila watu wala wanyama, naam, katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu ambazo ni tupu, bila watu wala wanyama, humo kutasikika tena sauti za vicheko, sauti za furaha, sauti za harusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wakileta tambiko za shukrani katika nyumba ya Mwenyezi-Mungu: ‘Mshukuruni Mwenyezi-Mungu wa majeshi kwa kuwa Mwenyezi-Mungu ni mwema, kwa maana fadhili zake zadumu milele.’ Nitairudishia nchi hii fanaka yake ya awali. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”


Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwa ulinzi wako wakati wote..
Asante kwakutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Utukuzwe Mungu wetu,Uhimidiwe Baba wa Mbinguni..
Unastahili sifa,Unastahili kuabudiwa Mwenyezi-Mungu..
Baba wa Upendo,Baba wa baraka,Baba wa yatima,Mume wa wajane..
Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe..



Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: “Mahali hapa ambapo ni jangwa bila watu wala wanyama, na katika miji yake yote, patakuwa na malisho ambayo wachungaji watalisha makundi yao ya kondoo. Katika miji ya nchi yenye milima, katika miji ya Shefela na katika miji ya jangwa la Negebu, katika nchi ya Benyamini, kandokando ya mji wa Yerusalemu na katika miji ya Yuda, watu watahesabu tena kondoo wao. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.” Mwenyezi-Mungu asema: “Siku zaja ambapo nitatimiza ahadi yangu niliyofanya na watu wa Israeli na watu wa Yuda. Katika siku hizo, naam, wakati huo, nitachipusha chipukizi mwadilifu wa uzao wa Daudi. Chipukizi huyo atatekeleza haki na uadilifu katika nchi. Wakati huo nchi ya Yuda itaokolewa na mji wa Yerusalemu utakuwa salama. Na mji huo utaitwa ‘Mwenyezi-Mungu ni Ukombozi Wetu’. Maana mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Hapatakosekana kamwe mzawa wa Daudi atakayetawala Israeli. Kadhalika nao makuhani wa ukoo wa Lawi watakuwapo daima kunihudumia wakinitolea sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka na kunitolea tambiko milele.”

Yahweh tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na tukijiachilia mikononi mwako Mungu wetu..
Tunaomba utusamehe makosa yetu yote tuliyoyafanya
kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Mfalme wa Amani nasi tunaomba utupe neema ya kuweza
 kuwasamehe wale wote waliotukosea..
Mungu wetu utuepushe katika majaribu na utuokoe
 na yule mwovu na kazi zake zote..
Baba wa Mbinguni tunaomba ututakase miili yetu
 na akili zetu Jehovah utufunike kwa Damu ya Bwana wetu
Yesu Kristo wa Nazareti,yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..

Mwenyezi-Mungu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Biashara,masomo na vyote tunavyoenda kufanya/kutenda 
Baba wa Mbinguni tukatende kama inavyokupendeza wewe..
Jehovah tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba utupe neema ya kuweza
 kuwabariki wenye kuhitaji..
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu..
Jehovah ukatupe sawasawa na mapenzi yako..


Neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Yeremia: “Kama vile hamwezi kutangua agano langu nililoweka kuhusu usiku na mchana hivyo kwamba usiku na mchana visiweko kama nilivyopanga, vivyo hivyo hamwezi kutangua agano langu nililofanya na mtumishi wangu Daudi. Nilifanya agano na Daudi kwamba daima atakuwa na mzawa wa kutawala mahali pake; vilevile kutakuwako daima makuhani wa ukoo wa Lawi watakaonitumikia. Kama vile nyota angani na mchanga wa pwani visivyohesabika, ndivyo nitakavyoongeza idadi ya wazawa wa mtumishi wangu Daudi na idadi ya makuhani wa ukoo wa Lawi.”
Mfalme wa Amani tunaomba amani yako ikatawale katika 
Nyumba/ndoa zetu,watoto,wazazi wetu,familia/ndugu 
na wote wanaotuzunguka..
Mungu wetu tunaomba ulinzi wako wakati wote tuingiapo/tutokapo
Baba wa Mbinguni ukabariki na kuvibariki vyote tunavyoenda
kugusa/kutumi Yahweh ukavitakase na kuvifunika kwa 
Damu ya Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Mungu wetu ukawaguse wote walio katika shida/tabu
wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali..
Mungu wetu ukawaponye kimwili na kiroho na ukawarudishe wale waliopote,Mungu wetu ukatupe neema ya kusimamia
Neno lako Amri na Sheria zako siku zote za maisha yetu
Baba wa Mbinguni tukawe barua njema na tukasomeke
kama inavyokupendaza wewe..

Neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Yeremia: “Je, hujasikia wasemayo watu hawa, kwamba mimi Mwenyezi-Mungu nimewatupilia mbali watu wa Israeli na watu wa Yuda, jamaa mbili nilizoziteua? Wamewadharau watu wangu, hata kuwaona kwamba wao si taifa. Lakini mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Mimi niliweka agano kuhusu mchana na usiku na kuweka sheria za mbingu na dunia. Basi, ndivyo ilivyo pia: Sitawatupa wazawa wa Yakobo na Daudi, mtumishi wangu; nitamteua mmoja wa wazawa wake atawale wazawa wa Abrahamu, Isaka na Yakobo. Kwa maana nitawarudishia fanaka yao na kuwahurumia.”

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tuwe na hekima
busara,wanyenyekevu, upole na kiasi..
Ee Mungu wetu tunaomba ukapokee sala/maombi yetu...
Mwenyezi-Mungu Mungu wetu tunakushukuru na
 kuamini kwama wewe ni Mungu wetu leo,kesho na hata milele
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!
Asanteni sana wapendwa katika Bwana kwakuwa nami
Mwenyezi-Mungu Mungu wa Rehema na Baraka
akawe nanyi daima Amani yake ikatawale katika maisha yenu..
Nawapenda.



Mose anayabariki makabila ya Israeli

1Hii ndiyo baraka ambayo Mose, mtu wa Mungu aliwatakia Waisraeli kabla ya kufariki kwake. Alisema:
2Mwenyezi-Mungu alikuja kutoka mlima Sinai,
alitutokea kutoka mlima Seiri;
aliiangaza kutoka mlima Parani.
Alitokea kati ya maelfu ya malaika,
na moto uwakao katika mkono wake wa kulia.
3Mwenyezi-Mungu aliwapenda watu wake;
na huwalinda watakatifu wake wote.
Hivyo, malaika wake walifuata nyayo zake,
na kupata maagizo kutoka kwake.
4Mose alituamuru tutii sheria;
kitu cha thamani kuu cha taifa letu.
5Mwenyezi-Mungu akawa mfalme wa Israeli,
wakati viongozi wao walipokutana,
na makabila yote yalipokusanyika.
6Mose alisema juu ya kabila la Reubeni:
“Reubeni aishi wala asife,
na watu wake wasiwe wachache.”
7Juu ya kabila la Yuda alisema:
“Ee Mwenyezi-Mungu usikilize kilio cha kabila la Yuda;
umrudishe tena kwa watu wale wengine.
Upigane kwa mikono yako kwa ajili yake,
ulisaidie kabila la Yuda dhidi ya adui zake.”
8Juu ya kabila la Lawi, alisema:
“Ee Mwenyezi-Mungu ulipatie Lawi kauli yako ya Urimu,
kauli yako ya thumimu33:8 kauli yako … kauli yako: Kiebrania: Urimu, Thumimu. Taz Kut 28:30 kwa hao waaminifu wako,
ambao uliwajaribu huko Masa.
9Ulishindana nao kwenye maji ya Meriba.
Walawi walioamua kuwaacha wazee wao,
wakawasahau jamaa zao,
wasiwatambue hata watoto wao
maana walizingatia amri zako,
na kushika agano lako.
10Na wawafundishe wazawa wa Yakobo maagizo yako;
wawafundishe watu wa Israeli sheria yako.
Walawi na wafukize ubani mbele yako,
sadaka nzima za kuteketezwa madhabahuni pako.
11Ee Mwenyezi-Mungu, uzibariki nguvu zao,
uzikubali kazi za mikono yao;
uzivunjilie mbali nguvu za maadui zao,
nguvu za wanaowachukia hata wasiinuke tena.”
12Juu ya kabila la Benyamini alisema:
“Hili ni kabila alipendalo Mwenyezi-Mungu,
nalo hukaa salama karibu naye.
Yeye hulilinda mchana kutwa,
na kukaa kati ya milima33:12 milima: Neno kwa neno: Mabega. yake.”
13Juu ya kabila la Yosefu alisema:
“Mwenyezi-Mungu na aibariki nchi yake,
kwa baraka nzuri kabisa kutoka juu,
14ibarikiwe kwa matunda bora yalioiva kwa jua,
kwa matunda ya kila mwezi;
15kwa mazao bora ya milima ya kale,
na mazao tele ya milima ya kale,
16Nchi yake ijae yote yaliyo mema,
ibarikiwe kwa wema wa Mwenyezi-Mungu,
ambaye alitokea katika kichaka.
Baraka hizi ziwashukie watu wa kabila la Yosefu,
aliyekuwa mkuu miongoni mwa ndugu zake.
17Fahari yake ni fahari ya fahali wa kwanza,
pembe zake ni za nyati dume.
Atazitumia kuyasukuma mataifa;
yote atayasukuma mpaka miisho ya dunia.
Efraimu atakuwa na pembe hizo 10,000
na Manase kwa maelfu.”
18Juu ya kabila la Zebuluni na kabila la Isakari, alisema,
“Zebuluni, furahi katika safari zako;
nawe Isakari, furahi katika mahema yako.
19Watawaalika wageni kwenye milima yao,
na huko watu watatoa sadaka zinazotakiwa.
Maana wao watapata utajiri wao kutoka baharini
na hazina zao katika mchanga wa pwani.”
20Juu ya kabila la Gadi, alisema:
“Atukuzwe Mungu ampatiaye Gadi sehemu kubwa.
Gadi hunyemelea kama simba
akwanyue mkono na utosi wa kichwa.
21Alijichagulia eneo zuri kuliko yote,
mahali ilipotengwa sehemu ya kiongozi.
Aliwaongoza watu na kumtii Mwenyezi-Mungu,
alitekeleza mpango wa Mungu kwa Israeli.”
22Juu ya kabila la Dani alisema hivi:
“Dani ni mwanasimba
arukaye kutoka Bashani.”
23Juu ya kabila la Naftali alisema:
“Ee Naftali fadhili,
uliyejaa baraka za Mwenyezi-Mungu,
nchi yako ni kusini kwenye ziwa Kinerethi.”
24Juu ya kabila la Asheri alisema:
“Asheri abarikiwe kuliko watoto wote wa Yakobo,
na upendelewe na ndugu zako wote;
na achovye mguu wake katika mafuta.
25Miji yako ni ngome za chuma na shaba.
Usalama wako utadumu maisha yako yote!”
26Mose akamalizia kwa kusema,
“Ee Israeli, hakuna aliye kama Mungu wako,
yeye hupita mbinguni kuja kukusaidia,
hupita juu angani katika utukufu wake.
27Mungu wa milele ndiye kimbilio lenu;
nguvu yake yaonekana duniani.
Aliwafukuza maadui mbele yenu;
aliwaamuru: ‘Waangamizeni.’
28Kwa hiyo, watu wa Israeli wakakaa salama,
wazawa wa Yakobo peke yao,
katika nchi iliyojaa nafaka na divai,
nchi ambayo anga lake hudondosha umande.
29Heri yenu nyinyi Waisraeli.
Nani aliye kama nyinyi, watu mliookolewa na Mwenyezi-Mungu,
ambaye ndiye ngao ya msaada wenu,
na upanga unaowaletea ushindi!
Adui zenu watakuja wananyenyekea mbele yenu,
nanyi mtawakanyaga chini.”


Kumbukumbu la Sheria 33:1-29


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.


Thursday 5 October 2017

Kikombe Cha Asubuhi Kumbukumbu la Sheria 32 (Kumbukumbu la Torati katika tafsiri nyingine)



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote..
Mungu wetu,Baba yetu,Muumba wetu na Muumba wa vyote...
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..
Baba wa upendo,Baba wa Baraka,Mfalme wa Amani..
Yahweh,Jehovah,El shaddai,Elo him,El Olam,El Qanna,Emanuel..
Mungu pamoja nasi..!!
Utukuzwe Jehovah,Uhimidiwe Yahweh,Usifiwe Mungu wetu..
Uabudiwe Baba wa Mbinguni,Hakuna kama wewe..
wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Alfa na Omega..
Unatosha Mungu wetu,Matendo yako ni ya ajabu...
Matendo yako ni makuu mno...!!



Sasa, ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni, nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake. Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure. Mimi niliwakabidhi nyinyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: Kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu; kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kufuatana na Maandiko Matakatifu; kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili. Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya 500 kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa. Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote. Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati. Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume, na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu. Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo, na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami. Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachohubiri, na hiki ndicho mnachoamini.

Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwa ulinzi wako wakati wote..
Asante kwakutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea
kuiona leo hii..
Si kwamba sisi ni wema sana,wala si kwamba sisi ni wazuri mno
Si kwa nguvu zetu wala uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo..
Ni kwa mapenzi yako,nikwa Neema na rehema zako Mungu wetu

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na tukijiachilia mikononi mwako Mungu wetu..
Baba tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya..
kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Jehovah nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe
wale wote waliotukosea..
Baba wa Mbinguni tunaomba utuepushe katika majaribu
 na utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote...
Mungu wetu tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
na utufunike kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..




Sasa, maadamu inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu? Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka; na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana. Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka kwa wafu na kumbe yeye hakumfufua – kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi. Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka. Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu. Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa. Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani. Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, wa kwanza wa wale waliolala katika kifo. Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka kwa wafu kumesababishwa na mtu mmoja. Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo. Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza; halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja. Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba ufalme, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu. Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda maadui zake wote na kuwaweka chini ya miguu yake. Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo. Maana, Maandiko yasema: “Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini, Maandiko yanaposema: “Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale” ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo. Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote. Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao? Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa? Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili. Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, “Tule na tunywe, maana kesho tutakufa.” Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema. Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!



Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu,Biashara,
Masomo na yote tunayoenda kufanya/kutenda tukatende
sawasawa na mapenzi yako..
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo,Mungu wetu nasi tunaomba utupe neema
ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji..
Jehovah tusipungukiwe katika mahitaji yetu..
Yahweh ukatupe sawasawa na mapenzi yako..

Mfalme wa Amani tuyaweka maisha yetu mikononi mwako..
Nyumba/Ndoa zetu,watoto,wazazi,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka..
Mungu wetu tunaomba ulinzi wako,Furaha,Amani yako ikatawale..
Upendo ulio wako,hekima,busara na tukanene yaliyo yako..
Tukasimamie Neno lako Amri na Sheria zako siku zote za maisha yetu
Ukatufanye chombo chema nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..



Lakini mtu anaweza kuuliza: “Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani?” Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota. Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye. Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee. Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine. Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine. Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri. Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika. Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu. Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho. Maana Maandiko yasema: “Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;” lakini Adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uhai. Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida, kisha ule mwili wa kiroho. Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni. Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni. Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyo aliyetoka mbinguni.

Yahweh tazama wenye shida/tabu,wagonjwa,wenye njaa..
waliokata tamaa,waliokataliwa,wenye mashaka/hofu..
walioanguka na kuelemewa na mizigo,walio katika vifungo vya 
yule mwovu na wote wenye kuhitaji..
Mungu wetu tunaomba unyooshe mkono wako wenye nguvu...
ukawaguse na kuwaponya kimwili na kiroho pia..
Baba wa Mbinguni ukawafungue na wakapate kuwa huru..
Yahweh ukawasimamishe na kuwasamehe wale waliokwenda kinyume nawe..
Baba wa Mbimnguni ukawape neema ya kujiombea ,Mfalme wa Amani Nuru yako ikaangaze katika maisha ya watoto wako..
Baba ukasikie kulia kwao Jehovah ukawafute machozi yao
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yao..
Yahweh ukawape neema ya kukujua wewe na kusimamia
Neno lako na wakafuate njia zako nao wakapate kuwa huru..
Wafiwa ukawe mfariji wao..



Basi, ndugu, nasema hivi: Kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika. Sikilizeni, nawaambieni siri: Sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa, wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana tarumbeta ya mwisho itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa. Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa. Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: “Kifo kimeangamizwa; ushindi umekamilika!” “Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?” Kifo hupata sumu yake katika dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika sheria. Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo. Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.

Jehovah tunayaweka haya yote mikononi mwako..
Tukishukuru na kuamini wewe ndiye Mungu wetu..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!!
Wapendwa/waungwana asanteni sana kwakuwa nami..
Baba wa faraja,upendo,Amani awe nanyi 
Nuru yake ikaangaze katika maisha yenu..
Nawapenda.


1“Tegeni masikio enyi mbingu:
Sikiliza, ee dunia, maneno ninayosema.
2Mafundisho yangu na yatone kama mvua,
maneno yangu yadondoke kama umande,
kama manyunyu kwenye mimea michanga,
kama mvua nyepesi katika majani mabichi.
3Maana nitalitangaza jina la Mwenyezi-Mungu,
nanyi mseme, ‘Mungu wetu ni Mkuu’.
4“Mwenyezi-Mungu ni Mwamba wa usalama;
kazi zake ni kamilifu,
njia zake zote ni za haki.
Yeye ni Mungu mwaminifu asiye na kosa,
yeye hufanya mambo ya uadilifu na ya haki.
5Lakini nyinyi mmekosa uaminifu kwake,
nyinyi sio watoto wake tena kwa sababu ya uovu,
nyinyi ni kizazi kiovu na kipotovu.
6Mnawezaje kumlipa hivyo Mwenyezi-Mungu,
enyi watu wapumbavu na msio na akili?
Je, yeye siye Baba yenu aliyewaumba,
aliyewafanya na kuwaimarisha?
7Kumbukeni siku zilizopita,
fikirieni miaka ya vizazi vingi;
waulizeni baba zenu nao watawajulisha,
waulizeni wakubwa wenu nao watawaeleza.
8Mungu Mkuu alipoyagawia mataifa mali yao,
alipowagawa wanadamu,
kila taifa alilipatia mipaka yake,
9kulingana na idadi ya watoto wa Mungu,32:9 watoto wa Mungu: Tafsiri kadiri ya hati ya Kumrani. Kiebrania: Watoto wa Israeli.
lakini alijiwekea watu wa Yakobo kuwa wake,
hao alijichagulia kuwa mali yake.
10Aliwakuta katika nchi ya jangwa,
nyika tupu zenye upepo mkali.
Aliwalinda na kuwatunza,
aliwafanya kama mboni ya jicho lake.
11Kama tai alindaye kiota chake,
na kurukaruka juu ya makinda yake,
akitandaza mabawa yake ili kuwashikilia,
na kuwabeba juu ya mabawa yake.
12Yeye Mwenyezi-Mungu mwenyewe aliwaongoza
na hapakuwa na mungu mwingine wa kumsaidia.
13Aliwapitisha katika nyanda za juu za nchi,
nao wakala mazao ya mashambani.
Akawapa asali miambani waonje
na mafuta kutoka mwamba mgumu.
14Aliwapa siagi na maziwa ya mifugo,
mafuta ya wanakondoo na kondoo madume,
makundi ya mifugo ya Bashani na mbuzi.
Aliwapa ngano nzuri kabisa na divai mpya wakanywa.
15Watu wa Israeli walinona na kupiga mateke;
walinenepa, wakawa na kitambi na kunawiri;
kisha wakamwacha Mungu aliyewaumba,
wakamdharau Mwamba wa wokovu wao.
16Walimfanya aone wivu mkali kwa miungu yao,
walimchochea akasirike kwa matendo yao ya kuchukiza.
17Walitambikia majini ambayo hayakuwa miungu,
waliiendea miungu ambayo hawakuijua kamwe,
miungu mipya iliyotokea siku za karibuni,
ambayo wazee wao hawakuiheshimu kamwe.
18Hamkumjali Mwamba aliyewapa uhai,
mlimsahau Mungu aliyewazaa nyinyi.
19Mwenyezi-Mungu aliona jambo hilo akawaacha;
aliwakataa watoto wake, waume kwa wake.
20Akasema, ‘Nitawaficha uso wangu
nione mwisho wao utakuwaje!
Maana wao ni kizazi kipotovu,
watoto wasio na uaminifu wowote.
21Wamenichochea kuona wivu kwa kitu kisicho mungu,
wamenikasirisha kwa sanamu zao.
Hivyo nitawafanya waone wivu kwa kisicho watu,
nitawakasirisha kwa kutumia taifa la wapumbavu.
22Hasira yangu imewaka moto,
inachoma mpaka chini kuzimu,
itateketeza dunia na vilivyomo,
itaunguza misingi ya milima.
23Nitarundika maafa chungu nzima juu yao,
nitawamalizia mishale yangu.
24Watakonda kwa njaa,
wataangamizwa kwa homa kali.
Nitapeleka wanyama wenye meno makali kuwashambulia,
na nyoka wenye sumu wanaotambaa mavumbini.
25Vita vitasababisha vifo vingi nje
na majumbani hofu itawatawala,
vijana wa kiume na wa kike watauawa
hata wanyonyao na wazee wenye mvi.
26Nilisema, ningaliwaangamiza kabisa
na kuwafanya wasikumbukwe tena na mtu yeyote,
27ila tu kwa sababu ya majivuno ya maadui zao
ili maadui zao wasije wakafikiria vingine;
wasije wakasema, wamefaulu kuwaangamiza,
nami Mwenyezi-Mungu sihusiki katika mambo haya!’
28“Israeli ni taifa lisilo na akili,
watu wake hawana busara ndani yao.
29Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa,
wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwaje.
30Mtu mmoja anawezaje kuwashinda watu 1,000,
au watu wawili wanawezaje kuwashinda watu 10,000,
isipokuwa kama Mwamba wao amewatupa,
Mwenyezi-Mungu wao amewaacha?
31Hata adui zetu wenyewe wamekiri wazi,
mwamba wao hauna nguvu kama mwamba wetu.
32Maana mizabibu yao ni miche ya Sodoma
zimetoka katika konde za Gomora;
zabibu zake ni zabibu zenye sumu,
vishada vyake ni vichungu.
33Divai yao ni kama sumu ya nyoka,
ina sumu kali ya majoka.
34“Je sina njia ya kuwaadhibu?
Silaha zangu ninazo mkononi.
35Kisasi ni juu yangu,
mimi nitalipiza,
wakati miguu yao itakapoteleza;
maana siku yao ya maafa imewadia,
mwisho wao u karibu sana.
36Mwenyezi-Mungu atawatetea watu wake,
na kuwahurumia watumishi wake,
wakati atakapoona nguvu zao zimeishia,
wala hakuna aliyebaki, mfungwa au mtu huru.
37Ndipo Mwenyezi-Mungu atakapowauliza watu wake,
‘Iko wapi ile miungu yenu,
mwamba mlioukimbilia usalama?’
38Iko wapi hiyo miungu iliyokula matoleo yenu
na kunywa divai na tambiko zenu za kinywaji?
Basi na iinuke, iwasaidieni;
acheni hiyo iwe kinga yenu sasa!
39Oneni kuwa mimi ndimi Mungu
na wala hakuna mwingine ila mimi.
Mimi huua na kuweka hai;
hujeruhi na kuponya,
na hakuna awezaye kumwokoa yeyote mikononi mwangu.
40Nanyosha mkono wangu mbinguni,
na kuapa, kwa uhai wangu wa milele,
41kama mkiuona upanga wangu umeremetao,
na kunyosha mkono kutoa hukumu,
nitawalipiza kisasi maadui zangu,
nitawaadhibu wale wanaonichukia.
42Mishale yangu nitailevya kwa damu,
upanga wangu utashiba nyama,
utalowa damu ya majeruhi na mateka
na adui wenye nywele ndefu.
43“Enyi mataifa washangilieni watu wake,
maana yeye hulipiza kisasi damu ya watumishi wake,
huwalipiza kisasi wapinzani wake,
na kuitakasa nchi ya watu wake.”
44Mose alikuja mbele ya Yoshua, mwana wa Nuni, wakakariri maneno ya wimbo huu, ili Waisraeli wote wausikie.

Wosia wa Mose

45Mose alipomaliza kuwaambia watu wa Israeli maneno haya yote, 46aliwaambia, “Yawekeni mioyoni mwenu maneno yote ambayo ninawapeni leo. Lazima muwaamuru watoto wenu ili wafuate kwa uaminifu maneno yote ya sheria hii. 47Maana sheria hii si maneno matupu bali ni uhai wenu; kwa sheria hii mtaishi maisha marefu katika nchi mnayokwenda kuimiliki, ngambo ya mto Yordani.”
48Siku hiyohiyo, Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 49“Panda mlima huu wa Abarimu, mlima Nebo katika nchi ya Moabu, mkabala wa mji Yeriko, ukaiangalie nchi ya Kanaani ninayowapa Waisraeli waimiliki. 50Kisha ufariki hukohuko mlimani kama kaka yako Aroni alivyofariki katika mlima Hori, 51kwa sababu nyote wawili mlivunja uaminifu wenu kwangu mbele ya Waisraeli mlipokuwa kwenye maji ya Meriba, karibu na mji wa Kadeshi, katika jangwa la Sini, mkakosa kuuthibitisha utakatifu wangu kati ya Waisraeli. 52Utaiona nchi iliyo mbele yako, lakini hutaingia katika nchi hiyo ninayowapa Waisraeli.”



Kumbukumbu la Sheria 32:1-52

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.