Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 24 February 2017

Jikoni Leo; Na Da'Farhat- Chicken And Vegetable Spring Rolls In Kiswahili Na Best Homemade Whole Fried Fish In kiswahili


Haya Wapendwa/Waungwana ni siku nyingi kidogo tumekosa "Jikoni Leo"
Tuanze na Dada huyu na mapishi yake haya...

Karibuni...





Kama unayako mapishi unapenda nawengine wajifunze na kukufuatilia..usisite kututumi/kutujuulisha
Email;Rasca@hotmail.co.uk au unaweza kuni Inbox kwa mitandao ya kijamii, Natumia Rachelsiwa..


Zaidi;Farhat Yummy

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo27....

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana,Yeye awezaye yote,Mfalme wa Amani,Mungu ni pendo apenda watu,Anayefanya njia pasipo na njia,
Akisema atakubariki na atafanya hivyo,Unastahili kuabudiwa,Kutukuzwa Baba wa mbinguni,Wewe Uliyetuumba,wewe ni habari njema,wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Kuamka wazima na wenye Afya ni kwa Neema/Rehema ya Mungu tuu na si kwa uwezo,Nguvu/Utashi na uelewa wetu,Mungu wetu si mtu hata aseme uongo,Ahadi zake ni Amina na kweli..


Mwachie Mwenyezi-Mungu mzigo wako naye atakutegemeza,Kamwe hamwachi mwadilifu ashindwe.{Zaburi55;22]
Mkabidhi Mwenyezi-Mungu maisha yako,Mtumainiye yeye naye atafanya kitu.{Zaburi37:5}
Sasa ndugu yangu mpendwa yanini kutangatanga,Kujibebesha mizigo isiyo yako na usiyoiweza?Mpe leo maisha yako Mungu ukiamini na yeye anatosha, na kufuata njia zake kamwe hatokuacha, Furaha ipo kwakwe,Tumaini ni yeye,Upendo wa kweli unapatikana kwakwe,Faraja ya kweli ipo kwa Mungu...
Mtumainiye Mqwenyezi-Mungu na kutenda mema,Upate kuishi katika nchi na kuwa salama{Zaburi37:3}
Mungu akatubariki kuingiakwetu/Kutoka kwetu,Vyombo vya usafiri na Tutembeapo,Vilaji/Vinywaji,Kazi,Biashara,Elimu na vyote tunavyoenda kutumia/kugusa Mungu akavitakase na kuvifunika na damu ya Mwokozi..


Lakini tukiishi katika mwanga, kama naye alivyo katika mwanga, basi, tutakuwa na umoja sisi kwa sisi, nadamu yake Yesu Kristo, Mwanae, inatutakasa dhambi zote.{1Yohane 1:7}

Tunajiachilia Mikononi mwako Baba wa Mbingu,Tukishukuru na Kuamini wewe ni Bwana na Mwokozi wetu..
                                      Amina..!!
                                       Mungu akaonekane kwenye Maisha yenu.
                                    


Isaka anambariki Yakobo

1Isaka alikuwa amezeeka na macho yake yalikuwa hayaoni. Basi, alimwita Esau mwanawe mkubwa, akamwambia, “Mwanangu!” Naye akaitika “Naam baba, nasikiliza!” 2Isaka akasema, “Tazama, mimi ni mzee, wala siku ya kufa kwangu siijui. 3Basi, chukua silaha zako, yaani podo na upinde wako, uende porini ukaniwindie mnyama. 4Halafu unitengenezee chakula kitamu, kile nipendacho, uniletee ili nile, nipate kukubariki kabla ya kufa kwangu.”
5Kumbe, wakati huo Isaka alipokuwa akiongea na Esau mwanawe, Rebeka alikuwa anasikiliza. Kwa hiyo, Esau alipokwenda porini kuwinda, 6Rebeka alimwambia mwanawe Yakobo, “Nimemsikia baba yako akimwambia kaka yako Esau, 7amwindie mnyama na kumtengenezea chakula kitamu, ili ale, apate kumbariki mbele ya Mwenyezi-Mungu kabla ya kufa kwake. 8Sasa mwanangu, sikiliza maneno yangu na utii ninayokuagiza. 9Nenda kwenye kundi la mbuzi uniletee wanambuzi wawili wazuri, nimtengenezee baba yako chakula kitamu, kile apendacho. 10Kisha utampelekea baba yako ale, apate kukubariki kabla hajafa.”
11Lakini Yakobo akamwambia mama yake Rebeka, “Kumbuka kaka yangu Esau amejaa nywele mwilini, hali mimi sina. 12Labda baba atataka kunipapasa, nami nitaonekana kama ninamdhihaki, kwa hiyo nitajiletea laana badala ya baraka.” 13Mama yake akamwambia, “Laana yako na inipate mimi, mwanangu; wewe fanya ninavyokuagiza: Nenda ukaniletee hao wanambuzi.”
14Basi, Yakobo akaenda, akachukua wanambuzi wawili, akamletea mama yake; naye akatayarisha chakula kitamu, kile apendacho Isaka baba yake. 15Kisha Rebeka akatwaa mavazi bora ya Esau, mwanawe mkubwa, aliyokuwa nayo nyumbani, akamvika Yakobo, mwanawe mdogo. 16Akamvika pia ngozi za wale wanambuzi mikononi na kwenye sehemu laini shingoni mwake. 17Kisha akampa kile chakula kitamu na mkate aliokuwa ametayarisha.
18Basi, Yakobo akaingia ndani kwa baba yake, akamwita, “Baba!” Naye akaitika, “Naam! Ni nani wewe mwanangu?” 19Yakobo akamjibu baba yake, “Ni mimi Esau, mzaliwa wako wa kwanza. Nimefanya kama ulivyoniagiza. Tafadhali baba, kaa kitako ule mawindo yangu ili upate kunibariki.” 20Lakini Isaka akamwuliza, “Imekuwaje umepata mawindo upesi hivyo, mwanangu?” Yakobo akamjibu, “Mwenyezi-Mungu, Mungu wako, amenifanikisha.”
21Ndipo Isaka akamwambia Yakobo, “Basi, mwanangu, karibia nipate kukupapasa ili nijue kweli kama wewe ndiwe mwanangu Esau au la.” 22Yakobo akamkaribia baba yake Isaka, naye akampapasa na kusema, “Sauti ni sauti ya Yakobo, lakini mikono ni mikono ya Esau.” 23Hakumtambua kwa sababu mikono yake ilikuwa yenye nywele nyingi kama ya Esau kaka yake; kwa hiyo akambariki. 24Akamwuliza tena, “Kweli wewe ndiwe mwanangu Esau?” Naye akamjibu, “Ndiyo.” 25Basi, baba yake akasema, “Niletee hiyo nyama nile mawindo yako mwanangu, nikubariki.” Hapo Yakobo akampelekea chakula, naye akala; akampelekea divai pia, akanywa. 26Ndipo baba yake Isaka, akamwambia, “Sogea karibu, mwanangu, unibusu.” 27Basi, Yakobo akamkaribia baba yake na kumbusu, na baba yake aliposikia harufu ya mavazi yake, akambariki akisema,
“Tazama, harufu nzuri ya mwanangu
ni kama harufu ya shamba alilobariki Mwenyezi-Mungu!
28Mungu akumiminie umande wa mbinguni;
akupe ardhi yenye rutuba,
nafaka na divai kwa wingi.
29Jamii za watu zikutumikie,
na mataifa yakuinamie kwa heshima.
Uwe mtawala wa ndugu zako,
watoto wa kiume wa mama yako wakuinamie kwa heshima.
Kila akulaaniye na alaaniwe,
kila akubarikiye na abarikiwe!”

Esau anaomba baraka

30Isaka alipokwisha kumbariki Yakobo, naye Yakobo alipokuwa ndio tu ametoka mbele ya baba yake Isaka, Esau kaka yake Yakobo, akarudi kutoka mawindoni. 31Esau pia akatengeneza chakula kitamu, akampelekea baba yake, akamwambia, “Haya baba, inuka ule mawindo yangu mimi mwanao, ili upate kunibariki!” 32Isaka akauliza, “Wewe ni nani?” Naye akamjibu, “Ni mimi mwanao Esau, mzaliwa wako wa kwanza.” 33Hapo Isaka akatetemeka mno, akasema, “Ni nani basi yule aliyewinda na kuniletea mawindo, nami nimekwisha kula kabla hujaja? Tena nimekwisha mbariki; naam, amekwisha barikiwa!”
34Esau alipoyasikia maneno ya baba yake, akaangua kilio cha uchungu. Kisha akamwambia baba yake, “Ee baba yangu, nibariki na mimi, tafadhali!” 35Lakini Isaka akasema, “Ndugu yako alikuja kwa hila, naye amechukua baraka yako.” 36Esau akasema, “Ndio maana anaitwa Yakobo! Amechukua nafasi yangu mara mbili. Kwanza alichukua haki yangu ya mzaliwa wa kwanza, na sasa amechukua baraka Zangu.” Kisha akamwuliza baba yake, “Je, hukunibakizia baraka yoyote?” 37Isaka akamjibu, “Nimekwisha mfanya Yakobo kuwa mtawala wako, na kumpa ndugu zake wote kuwa watumishi wake. Nimempatia nafaka na divai. Nikufanyie nini sasa, wewe mwanangu?” 38Esau akamwambia baba yake, “Baba, kwani una baraka moja tu? Nibariki hata mimi, ee baba!” Hapo Esau akalia kwa sauti kubwa. 39Ndipo Isaka, baba yake, akamwambia,
“Makao yako yatakuwa mbali na ardhi yenye rutuba,
na mbali na umande wa mbinguni.
40Utaishi kwa upanga wako,
na utamtumikia ndugu yako;
lakini utakapoasi
utaivunja kongwa yake shingoni mwako.”
41Basi, Esau akamchukia Yakobo kwa sababu ya baraka aliyokuwa amepewa na baba yake. Esau akawaza, “Siku za matanga ya baba zitakapokwisha, ndipo nitakapomuua ndugu yangu Yakobo.” 42Lakini Rebeka alipojua nia ya mwanawe mkubwa, akamwita mwanawe mdogo Yakobo, akamwambia, “Jihadhari, ndugu yako Esau anajifariji kwa kupanga kukuua. 43Kwa hiyo, mwanangu, sikiliza maneno yangu. Ondoka ukimbilie kwa kaka yangu Labani kule Harani. 44Kaa naye kwa muda, mpaka ghadhabu ya nduguyo itakapopoa. 45Ghadhabu yake itakapopoa, naye atakapokuwa amesahau uliyomtendea, nitatuma mtu akurudishe. Kwa nini nifiwe na nyinyi wote wawili siku moja?”

Yakobo anatumwa kwa Labani

46Rebeka akamwambia Isaka, “Sina raha kabisa maishani kwa sababu ya hawa wanawake wa Esau Wahiti. Ikiwa Yakobo ataoa mmojawapo wa wanawake hawa Wahiti, maisha yangu yana faida gani?”
Mwanzo27;1-46

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN):
Jifunze zaidi

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 23 February 2017

Chaguo La Mswahili Leo;Tina Campbell featuring Teddy Campbell SPEAK THE WORD

Tina na Mume wake Teddy..wimbo umenigusa/nimeupenda...
Swali..wewe Mke/Mume kipi mnafanya pamoja ukiacha kulala pamoja?


"Speak The Word".....Twende pamoja.



"Swahili Na Waswahili"Burudika.

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo26..

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Nimatumaini yangu mmeanza siku hii vyema na Mungu yu pamoja nanyi..
Asante Mungu wetu kwa kutupa kibali cha kuiona leo hii..Tunaomba Baba ukaibariki siku hii na Kutuongoza kwa kila jambo..Ikawe yenye Baraka,Amani na Imani..Ukatamalaki Mungu Baba katika Maisha yetu,Kazi,Biashara,Elimu,Familia na vyote tunavyoenda kutumia/kugusa Baba ukavitakase na ukavifunike na Damu yako ..Ukabariki kuingia/kutoka kwetu,Vyombo vya usafiri na tutembeapo,vilaji/vinywaji...
Roho mtakatifu akatuongoze kwenye kunena na kutenda.. ukatufanye chombo chako Baba wa mbingu na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Ukawaguse na kuwaponya wanaopitia Magumu/Majaribu, Vifungo mbalimbali vya mwovu,Shida/Tabu,Wagonjwa walio mahospitalini/majumbani,walio magerezani pasipo na hatia..
Wafiwa ukawe mfariji wao,Waliokata tamaa wakapate Tumaini.
Hakuna linaloshindika mbele zako Mfalme wa Amani,Ukatawale na kuibariki Nchi hii tunayoishi,Ukabariki Tanzania,Afrika na Dunia yote Mfalime wa Amani ukatawale na kuwaongoza vyema wanaotuongoza wakatuongoze kwa haki na kweli.
Tunakwenda kinyume na mwovu..
Tunakuja mbele zako na kujiachilia mikononi mwako Baba wa Mbinguni..
Tukishukuru na kuamini kwamba wewe ni Bwana na Mwokozi wetu.
Amina...!!!

Amani ya Bwana ikae nanyi Daima.


Isaka anahamia Gerari

1Baadaye palitokea njaa nchini humo, njaa tofauti na ile ya hapo awali wakati wa uhai wa Abrahamu. Isaka akaenda Gerari kwa Abimeleki mfalme wa Wafilisti. 2Mwenyezi-Mungu akamtokea Isaka na kumwambia, “Usiende Misri, bali kaa katika nchi nitakayokuambia. 3Kaa ugenini katika nchi hiyo, nami nitakuwa nawe na kukubariki. Nitatimiza ahadi niliyompa baba yako Abrahamu, kwani nitakupa wewe na wazawa wako nchi hizi zote. 4Nitawazidisha wazawa wako wawe kama nyota za mbinguni na kuwapa nchi hizi zote. Kutokana na wazawa wako, mataifa yote duniani yatabarikiwa, 5kwa sababu Abrahamu alinitii mimi, akazingatia maagizo yangu, amri zangu, masharti yangu na sheria zangu.”
6Basi, Isaka akakaa huko Gerari. 7Watu wa huko walipomwuliza habari za mkewe, yeye alijibu, “Huyu ni dada yangu.” Aliogopa kusema kwamba ni mke wake kwa kuogopa kwamba wakazi wa nchi wangemuua kwa sababu ya Rebeka, maana Rebeka alikuwa mzuri sana. 8Baada ya kukaa huko kwa muda mrefu, Abimeleki mfalme wa Wafilisti alichungulia dirishani akamwona Isaka akimkumbatia mkewe Rebeka. 9Abimeleki akamwita Isaka na kumwambia, “Kumbe huyo ni mke wako! Mbona ulisema ni dada yako?” Isaka akajibu, “Kwa kuwa niliogopa kwamba ningeuawa kwa sababu yake.”
10Abimeleki akamwuliza, “Ni jambo gani hili ulilotutendea? Mmoja wa watu wangu angaliweza kulala na mkeo bila wasiwasi, nawe ungekuwa umetutia hatiani.” 11Ndipo Abimeleki akawaonya watu wote akisema, “Yeyote atakayemgusa mtu huyu au mke wake, atauawa.”
12Mwaka huo Isaka alipanda mbegu katika nchi ile, akavuna mara mia zaidi, maana Mwenyezi-Mungu alimbariki, 13naye akatajirika. Alizidi kupata mali hadi akawa tajiri sana. 14Alikuwa na makundi ya kondoo, ng'ombe na watumwa wengi, hata Wafilisti wakamwonea wivu. 15Wafilisti walikuwa wamevifukia visima vyote vya maji ambavyo watumishi wa Abrahamu, baba yake, walikuwa wamechimba wakati alipokuwa bado hai. 16Ndipo Abimeleki akamwambia Isaka, “Ondoka kwetu, kwani wewe umetuzidi nguvu.”
17Basi, Isaka akaondoka huko, akapiga kambi yake katika bonde la Gerari, akakaa huko. 18Isaka akavichimbua vile visima vilivyokuwa vimechimbwa wakati Abrahamu baba yake alipokuwa hai, visima ambavyo Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kifo cha Abrahamu. Akavipa majina yaleyale aliyovipa baba yake. 19Lakini watumishi wa Isaka walipochimba katika lile bonde na kupata kisima cha maji yanayobubujika, 20wachungaji wa hapo Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaka wakisema, “Maji haya ni yetu.” Hivyo Isaka akakiita kisima hicho Eseki, kwa sababu waligombana naye. 21Halafu wakachimba kisima kingine, nacho pia wakakigombania; hivyo Isaka akakiita kisima hicho Sitna. 22Kisha Isaka akaenda mahali pengine na kuchimba kisima kingine. Lakini hicho hawakukigombania; hivyo Isaka akakiita Rehobothi akisema, “Sasa Mwenyezi-Mungu ametuachia nafasi, nasi tutastawi katika nchi hii.”
23Kutoka huko, Isaka alikwenda Beer-sheba. 24Usiku huohuo Mwenyezi-Mungu alimtokea na kumwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako Abrahamu. Usiogope kwa kuwa niko pamoja nawe; nitakubariki na kuwazidisha wazawa wako kwa ajili ya Abrahamu, mtumishi wangu.” 25Kwa hiyo, Isaka akajenga huko madhabahu, akamwabudu Mwenyezi-Mungu. Akapiga kambi huko; na watumishi wake wakachimba kisima.

Isaka na Abimeleki wanapatana

26Abimeleki alitoka Gerari akiwa pamoja na Ahuzathi, mshauri wake, na Fikoli mkuu wa jeshi lake, akamwendea Isaka. 27Isaka akawauliza, “Kwa nini mmekuja kwangu hali mnanichukia na mlinifukuza kwenu?” 28Wao wakamjibu, “Tumeona wazi kwamba Mwenyezi-Mungu yuko pamoja nawe. Kwa hiyo, tunafikiri inafaa tule kiapo pamoja nawe na kufanya agano, 29kwamba hutatudhuru, nasi kadhalika hatutakudhuru. Tulikutendea mema, tukakuacha uende zako kwa amani, bila kukutendea baya lolote lile. Na sasa wewe ni mbarikiwa wa Mwenyezi-Mungu.” 30Basi, Isaka akawafanyia karamu, nao wakala na kunywa. 31Kesho yake wakaamka asubuhi na mapema na kula kiapo. Kisha Isaka akawasindikiza na kuagana nao kwa amani. 32Siku ileile watumishi wa Isaka walimjia na kumpasha habari za kile kisima walichokuwa wamechimba, wakasema, “Tumepata maji!” 33Basi, Isaka akakiita kisima hicho Shiba; kwa hiyo jina la mji huo ni Beer-sheba hata leo.

Wake za Esau

34Esau alipokuwa na umri wa miaka arubaini, alioa wake wawili Wahiti: Yudithi bintiye Beeri, na Basemathi bintiye Eloni. 35Wanawake hao waliyafanya maisha ya Isaka na Rebeka kuwa machungu.
Mwanzo26;1-35
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN):
Jifunze zaidi

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 22 February 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo25..

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Asante Mungu Baba kwa Mapenzi yako na kutupa kibali cha kuiona siku hii.
Wengi walitamani kuiona lakini imeshindikana, Sisi si kwamba ni wema sana,Wajuaji,wenyenguvu/Utashi hapana ni kwa Neema/Rehema yako Baba wa Mbinguni,Baba wa Mbinguni Ukatamalaki katika Nyumba zetu,Ndoazetu, Watoto/Familia zetu,Elimu,Kazizetu,Biashara na Maisha yetu.Mfalme wa Amani ukawaguse na kuwaponya wanaopitia Magumu/Majaribu, Shida/Tabu,Vifungo mbalimbali..
Mungu Baba ukavibariki na kuvitakasa vyote tunavyoenda kutumia/kugusa.
Roho mtakatifu akatuongoze kwenye kunena na Kutenda,Kutambua/kujitambua.
Baba ukatupe na kutuongezea Upendo,Amani,Furaha,Msamaha/kusamehe,kuchukuliana na kueleweshana/kukumbushana kwa wema.
Tunakwenda kinyume na mwovu,Tunajiachilia mikononi mwako Baba wa mbingu na nchi..
Tunashukuru na kuamini wewe ni Bwana na mwokozi wetu..
Amina..!!
Upendo wa Mungu Ukatamalaki kwa kila mmoja wetu.


Wazawa wengine wa Abrahamu

(1Nya 1:32-33)
1Abrahamu alioa mke mwingine, jina lake Ketura. 2Ketura alimzalia Abrahamu: Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua. 3Yokshani alimzaa Sheba na Dedani; wazawa wa Dedani walikuwa Waashuru, Waletushi na Waleumi. 4Watoto wa Midiani walikuwa Efa, Eferi, Henoki, Abida na Eldaa. Wote hao walikuwa wazawa wa Ketura.
5Abrahamu alimrithisha Isaka mali yake yote. 6Lakini watoto wa kiume wa masuria wake akawapa zawadi, na wakati alipokuwa bado hai, aliwapeleka katika nchi ya mashariki, mbali na Isaka mwanawe.

Kifo cha Abrahamu

7Abrahamu aliishi miaka 175. 8Alifariki baada ya kuishi maisha marefu na ya fanaka, akajiunga na wazee wake waliomtangulia. 9Isaka na Ishmaeli, wanawe Abrahamu, wakamzika baba yao katika pango la Makpela, mashariki ya Mamre kwenye shamba lililokuwa la Efroni, mwana wa Sohari, Mhiti. 10Abrahamu alikuwa amenunua shamba hilo kwa Wahiti. Huko ndiko alikozikwa Abrahamu na mkewe Sara. 11Baada ya kifo cha Abrahamu, Mungu alimbariki Isaka mwanawe. Naye Isaka akawa anaishi karibu na kisima cha Beer-lahai-roi.

Wazawa wa Ishmaeli
(1Nya 1:28-31)
12Hawa ndio wazawa wa Ishmaeli mwanawe Abrahamu ambaye Hagari Mmisri, aliyekuwa mjakazi wa Sara, alimzalia Abrahamu. 13Hii ni orodha yao kufuatana na kuzaliwa kwao: Nebayothi, mzaliwa wa kwanza, Kedari, Adbeeli, Mibsamu, 14Mishma, Duma, Masa, 15Hadadi, Tema, Yeturi, Nafishi na Kedema. 16Hao ndio watoto wa kiume wa Ishmaeli, waliokuwa asili ya makabila kumi na mawili; makazi na vijiji vyao vilijulikana kwa majina yao. 17Ishmaeli alikuwa na umri wa miaka 137 alipofariki, akajiunga na wazee wake waliotangulia. 18Wazawa wa Ishmaeli walikaa katika eneo lililo kati ya Hawila na Shuri, mashariki ya Misri, kuelekea Ashuru. Walikaa kwa utengano na wazawa wengine wa Abrahamu.

Kuzaliwa kwa Esau na Yakobo

19Hawa ndio wazawa wa Isaka mwana wa Abrahamu. 20Isaka alipokuwa na umri wa miaka arubaini alimwoa Rebeka, binti Bethueli, Mwaramu wa Padan-aramu. Rebeka alikuwa dada yake Labani. 21Rebeka alikuwa tasa, kwa hiyo Isaka akamwomba Mwenyezi-Mungu. Naye Mwenyezi-Mungu akakubali ombi lake, Rebeka akapata mimba. 22Mimba hiyo ilikuwa ya mapacha. Watoto hao wakashindana tumboni mwake Rebeka, naye akasema, “Kama hivi ndivyo mambo yalivyo, ya nini kuishi?” Basi, akaenda kumwuliza Mwenyezi-Mungu. 23Mwenyezi-Mungu akamwambia,
“Mataifa mawili yamo tumboni mwako;
makabila mawili yatakayozaliwa nawe, yatafarakana.
Moja litakuwa lenye nguvu kuliko lingine;
mkubwa atamtumikia mdogo.”
24Siku zake za kujifungua zilipotimia, Rebeka alijifungua mapacha. 25Wa kwanza alikuwa mwekundu, mwenye nywele mwili wote; hivyo wakamwita Esau. 26Wa pili alizaliwa akiwa amemshika Esau kisigino, hivyo wakampa jina Yakobo. Isaka alikuwa na umri wa miaka sitini wakati Esau na Yakobo walipozaliwa.
Esau anauza haki yake
27Watoto hao wakakua; Esau akawa mwindaji hodari, mpenda maisha ya mbugani, na Yakobo akawa mtu mtulivu, mpenda maisha ya nyumbani. 28Basi, Isaka akampenda Esau kwa sababu alipenda kula mawindo yake, lakini Rebeka akampenda Yakobo.
29Siku moja, Yakobo alipokuwa anapika dengu, Esau alirudi nyumbani kutoka mawindoni ana njaa sana. 30Kwa hiyo akamwambia Yakobo, “Nafa njaa; tafadhali, nigawie chakula hicho chekundu nile.” (Ndiyo maana walimpanga jina Edomu yaani mwekundu). 31Yakobo akajibu, “Kwanza niuzie haki yako ya mzaliwa wa kwanza.” 32Esau akasema, “Sawa! Niko karibu kufa; haki yangu ya mzaliwa wa kwanza itanifaa nini?” 33Yakobo akamwambia, “Niapie kwanza.” Basi, Esau akamwapia na kumwuzia Yakobo haki yake ya mzaliwa wa kwanza. 34Ndipo Yakobo akampa Esau mkate na dengu kiasi. Esau akala, akanywa, kisha akaondoka, akaenda zake. Hivyo ndivyo Esau alivyoidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.
Mwanzo25;1-34

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN):
Jifunze zaidi

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 21 February 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo24....

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Nimatumaini yangu mmeanza siku hii na Mungu..
Tumshukuru sana Mungu kwa Pumzi/Uzima,Afya na kutupa kibali cha kuiona leo hii..Ikawe yenye Baraka,Amani,Upendo,Furaha na Kumpendeza Mungu wetu muumba wa vyote..
Akatubariki Kuingia/Kutoka kwetu,Kazi,Biashara,Elimu,Vilaji/Vinywaji, Vyombo vya usafiri na tutembeapo Baba wa mbinguni awe nasi na kuvitakasa vyote tunavyoenda kugusa/kutumia..
Roho mtakatifu akatuongoze kwenye kunena na kutenda,Mungu baba aka
tupe na ukutuongezea Hekima,Busara,Uvumilivu,Utambuzi/kujitambua na kuheshimiana.
Mfalme wa Amani ukawafariji wafiwa,Ukawaponye na kuwaokoa Wenye Shida/Tabu,Wagonjwa,waliokata tamaa, wenyevifungombalimbali na wote wanaopitia Magumu/Majaribu yoyote.
Mfalme wa Amani ukatawale maisha yetu na ukatupe sawasawa na Mapenzi yako..
Tunajikabidhi mikononi mwako Baba wa mbinguni,Tukishukuru na kuamini kwamba wewe ni Bwana na mwokozi wetu..
Amina...!!
Muwe na Imani na Amani.


Isaka anaoa
1Sasa Abrahamu alikuwa mzee wa miaka mingi, naye Mwenyezi-Mungu alikuwa amembariki katika kila hali. 2Siku moja Abrahamu akamwambia mtumishi wake aliyekuwa mzee kuliko wengine na msimamizi wa mali yake yote, “Weka mkono wako mapajani mwangu, 3nami nitakuapisha kwa jina la Mwenyezi-Mungu, Mungu wa mbingu na dunia, kwamba hutamwoza mwanangu msichana yeyote miongoni mwa binti za Wakanaani ninaoishi nao. 4Niapie kwamba utakwenda mpaka katika nchi yangu, kwa jamaa zangu, umtafutie mwanangu Isaka mke.” 5Mtumishi akamwambia, “Huenda mwanamke huyo atakataa kufuatana nami kuja huku, ikiwa hivyo, je, ni lazima nimrudishe mwanao nchini ulikotoka?” 6Abrahamu akamwambia, “La! Angalia sana usimrudishe mwanangu huko. 7Mwenyezi-Mungu, Mungu wa mbingu, aliyenitoa nyumbani kwa baba yangu na kutoka katika nchi nilimozaliwa, na ambaye alisema nami, aliniapia kwamba atawapa wazawa wangu nchi hii. Yeye atamtuma malaika wake mbele yako ili umletee mwanangu mke kutoka huko. 8Iwapo mwanamke huyo hatapenda kufuatana nawe hadi huku, basi kiapo changu hakitakufunga, lakini kwa vyovyote vile usimrudishe mwanangu huko.” 9Basi, mtumishi huyo akaweka mkono wake mapajani mwa Abrahamu, bwana wake, akaapa kuhusu jambo hilo.
10Kisha, huyo mtumishi akachukua ngamia kumi wa bwana wake akaondoka akiwa na zawadi nzuri za kila aina. Akasafiri kwenda katika mji alimokaa Nahori, nchini Mesopotamia. 11Alipowasili, aliwapigisha magoti ngamia wake kando ya kisima kilichokuwa nje ya mji. Ilikuwa jioni wakati ambapo wanawake huenda kisimani kuteka maji. 12Naye akaomba, “Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, nakuomba unijalie nifaulu leo na umfadhili Abrahamu bwana wangu. 13Niko hapa kando ya kisima ambapo binti za wenyeji wa mji huja kuteka maji. 14Basi, msichana nitakayemwambia atue mtungi wake wa maji anipatie maji ninywe, naye akanipa mimi pamoja na kuwanywesha ngamia wangu, na awe ndiye uliyemchagulia mtumishi wako Isaka. Jambo hilo litanionesha kwamba umemfadhili bwana wangu.”
15Kabla hajamaliza kuomba, mara Rebeka, binti Bethueli, mwana wa Milka, mkewe Nahori, ndugu yake Abrahamu, akafika amebeba mtungi wake begani. 16Msichana huyo alikuwa na sura ya kuvutia sana, na bikira ambaye hakuwa amelala na mwanamume yeyote. Basi, akateremka kisimani, akaujaza mtungi wake maji na kupanda. 17Ndipo yule mtumishi akaharakisha kukutana naye, akamwambia, “Tafadhali, nipatie maji ya kunywa kutoka mtungi wako.” 18Msichana akamjibu, “Haya kunywa bwana wangu.” Na papo hapo akautua mtungi wake, akiushikilia ili amnyweshe. 19Alipokwisha kumpatia maji, akamwambia, “Nitawatekea maji ngamia wako pia, wanywe mpaka watosheke.” 20Basi, akafanya haraka, akawamiminia ngamia maji ya mtungi wake katika hori, akakimbia kisimani kuteka maji mengine na kuwanywesha ngamia wake wote. 21Yule mtu akawa anamtazama kwa makini bila kusema lolote, apate kufahamu kama Mwenyezi-Mungu ameifanikisha safari yake au sivyo.
22Ngamia walipotosheka kunywa maji, yule mtu akampa huyo msichana pete ya dhahabu yenye uzito upatao gramu sita, na bangili mbili za dhahabu za gramu kumi kila moja. 23Akamwuliza, “Niambie tafadhali: Wewe ni binti nani? Je, kuna nafasi ya kulala nyumbani kwenu?” 24Rebeka akajibu, “Mimi ni binti Bethueli, mwana wa Milka, mkewe Nahori. 25Kwetu kuna majani na malisho ya kutosha na mahali pa kulala wageni.” 26Ndipo yule mtu akainamisha kichwa chake, akamwabudu Mwenyezi-Mungu 27akisema, “Atukuzwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hajasahau fadhili zake na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mwenyezi-Mungu ameniongoza mimi mwenyewe moja kwa moja hadi kwa jamaa ya bwana wangu!”
28Kisha yule msichana akakimbia kwenda kuwapa habari jamaa za mama yake. 29Rebeka alikuwa na kaka yake aitwaye Labani. Labani akatoka mbio kukutana na yule mtu kisimani. 30Labani alikuwa ameiona ile pete na bangili mikononi mwa dada yake, na kusikia mambo Rebeka aliyoambiwa na huyo mtu. Labani alimkuta yule mtu amesimama karibu na ngamia wake kando ya kisima. 31Labani akamwambia, “Karibu kwetu wewe uliyebarikiwa na Mwenyezi-Mungu. Mbona unasimama nje? Mimi mwenyewe nimekwisha tayarisha nyumba na mahali kwa ajili ya hawa ngamia wako!” 32Basi, mtumishi huyo wa Abrahamu akaingia nyumbani. Labani akawafungua ngamia na kuwapatia majani ngamia wake, akampa yeye na watu wake maji ya kunawa miguu. 33Basi, wakamwandalia chakula, lakini yeye akasema, “Sitakula mpaka nimesema ninachotaka kusema.” Labani akamwambia, “Haya, tuambie.”
34Yule mtu akasema, “Mimi ni mtumishi wa Abrahamu. 35Mwenyezi-Mungu amembariki sana bwana wangu, naye amekuwa mtu maarufu. Amempa makundi ya kondoo na mifugo mingi, fedha na dhahabu, watumishi wa kiume na wa kike, ngamia na punda! 36Sara, mke wa bwana wangu katika uzee wake, alimzalia bwana wangu mtoto; na bwana wangu amempa huyo mtoto mali yake yote. 37Bwana wangu aliniapisha mimi akisema, ‘Hutamwoza mwanangu msichana yeyote miongoni mwa binti za Wakanaani ambao ninaishi katika nchi yao. 38Bali utakwenda mpaka nchi yangu, kwa jamaa zangu, ili umtafutie mwanangu Isaka mke.’ 39Nami nikamwambia bwana wangu, ‘Huenda mwanamke huyo akakataa kufuatana nami kuja huku.’ 40Lakini yeye akasema, ‘Mwenyezi-Mungu aniongozaye maishani mwangu, atamtuma malaika wake aende pamoja nawe na kukufanikisha katika safari yako; nawe utamtwalia mwanangu mke kutoka kwa jamaa yangu na nyumba ya baba yangu. 41Kama utakapofika kwa jamaa zangu hawatakupa huyo msichana, basi, hutafungwa na kiapo changu.’
42“Leo nilipofika kisimani nimeomba, ‘Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, nakuomba nifaulu leo katika safari yangu na umfadhili Abrahamu bwana wangu. 43Niko hapa kando ya kisima. Msichana atakayekuja kuteka maji ambaye nitamwomba anipatie maji kidogo ya kunywa kutoka mtungi wake, 44naye akanipa na kuwatekea maji ngamia wangu, basi huyo na awe ndiye uliyemchagua kuwa mke wa mwana wa bwana wangu.’
45“Kabla sijamaliza kuomba moyoni mwangu, mara Rebeka alifika na mtungi wake wa maji begani, akateremka kisimani na kuteka maji. Nami nikamwambia, ‘Tafadhali nipe maji ya kunywa.’ 46Naye akautua mtungi wake haraka kutoka begani mwake, akasema, ‘Haya, kunywa bwana wangu. Nitawatekea maji ngamia wako pia.’ Basi mimi nikanywa na ngamia wangu pia akawapa maji. 47Ndipo nilipomwuliza, ‘Je, wewe ni binti wa nani?’ Akaniambia, ‘Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Milka, mkewe Nahori.’ Ndipo nilipompa pete na kumvisha bangili mikononi. 48Kisha nikainama na kumwabudu Mwenyezi-Mungu; nikamtukuza Mwenyezi-Mungu, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye ameniongoza moja kwa moja kwa binti wa ukoo wa bwana wangu kwa ajili ya mwanawe. 49Sasa, basi, niambieni kama mko tayari kumtendea bwana wangu kwa uaminifu na haki; kama sivyo, basi semeni, nami nitajua cha kufanya.”
50Baada ya kusikia hayo, Labani na Bethueli wakamjibu, “Jambo hili limetoka kwa Mwenyezi-Mungu, sisi hatuwezi kuamua lolote. 51Rebeka huyu hapa; mchukue uende. Na awe mke wa mwana wa bwana wako kama Mwenyezi-Mungu alivyosema.” 52Mtumishi wa Abrahamu aliposikia maneno hayo, alimsujudia Mwenyezi-Mungu. 53Kisha akatoa vito vya fedha na dhahabu na nguo, akampa Rebeka. Pia aliwapa ndugu na mama yake Rebeka mapambo ya thamani kubwa.
54Mtumishi wa Abrahamu na watu aliokuja nao wakala, wakanywa na kulala huko. Walipoamka asubuhi, mtumishi yule akasema, “Naomba kurudi kwa bwana wangu.” 55Lakini ndugu na mama yake Rebeka wakasema, “Mwache msichana akae nasi muda mfupi, kama siku kumi hivi; kisha anaweza kwenda.” 56Lakini yeye akasema, “Tafadhali, msinicheleweshe, kwa kuwa Mwenyezi-Mungu amekwisha fanikisha safari yangu; naomba mniruhusu kurudi kwa bwana wangu.” 57Nao wakasema, “Basi, tumwite msichana mwenyewe, tumwulize.” 58Wakamwita Rebeka na kumwuliza, “Je, utakwenda na mtu huyu?” Naye akajibu, “Nitakwenda.” 59Basi, wakamwacha Rebeka na yaya wake aende na mtumishi wa Abrahamu na watu wake. Yaya wake Rebeka pia aliandamana naye. 60Basi, wakambariki Rebeka wakisema,
“Ewe dada yetu!
Uwe mama wa maelfu kwa maelfu;
wazawa wako waimiliki miji ya adui zao.”
61Kisha, Rebeka na wajakazi wake wakapanda ngamia na kumfuata huyo mtumishi wa Abrahamu; nao wote wakaondoka.
62Wakati huo, Isaka alikuwa ameondoka Beer-lahai-roi, akawa anakaa huko pande za Negebu. 63Siku moja jioni, Isaka alikwenda mashambani kutafakari. Basi, akatazama akaona ngamia wanakuja. 64Naye Rebeka alipotazama na kumwona Isaka, alishuka chini 65na kumwuliza mtumishi wa Abrahamu, “Ni nani yule mtu anayetembea kule shambani, anakuja kutulaki?” Yule mtumishi akasema, “Ni bwana wangu.” Basi, Rebeka akatwaa shela yake, akajifunika uso. 66Yule mtumishi akamsimulia Isaka yote aliyokuwa ameyafanya. 67Basi, Isaka akamchukua Rebeka ndani ya hema iliyokuwa ya Sara mama yake, akawa mke wake. Isaka akampenda Rebeka na kupata faraja baada ya kifo cha mama yake.
Mwanzo24;1-67
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN):
Jifunze zaidi

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 20 February 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo23...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana, Anastahili kusifiwa,Anastahili kuabudiwa,Ahimidiwe,Mungu wetu asiyelala,Mungu wetu aponyae,Mungu wetu afanyae njia pasipo na njia,Yeye ni Alpha na Omega..!!
Tunamshukuru sana  kwa Neema/Rehema  ya kuiona leo hii,
Asante Baba wa Mbinguni kwa kutupa kibali cha kuendelea kuwepo leo hii..
Sisi si kwamba ni wema sana,Wazuri sana,Wajuaji, wenyenguvu/Utashi..Hapana ni kwa mapenzi yako tuu wewe uliyetuumba, na kuumba Mbingu na nchi na vyoote vilivyopo..
Ukaibariki siku hii Baba wa Mbinguni, Tuingiapo/Tutokapo,Vyombo vya Usafiri,Tutembeapo,Vilaji/Vinywaji,Kazi,Biashara,Elimu na vyote tunavyoenda kutumia/kugusa Mfalme wa Amani ukavitakase..
kuwaguse na kuwaponya wote wanaopitia Magumu/Majaribu,Vifungo mbalimbali vya mwovu,Wagonjwa,Wafiwa,Waliokata tamaa,wenyeshida/Tabu mbalimbali..
Mfalme wa Amani ukatawale katika maisha yetu, Ukatawale na kuwaongoza wanaotuongoza wakaongoze kwa haki na kweli,Ukaibariki nchi hii tunayoishi Baba,Ukaibariki Tanzani,Afrika na Dunia yote Mfalme wa Amani ukatawale..
Tunakwenda kinyume na Mwovu, Tunajiachilia mikononi mwako Bwana Mungu wetu, Tunashukuru na Tukiamini wewe ni Bwana na Mwokozi wetu..
Amina..!!!!!!
Tuanze wiki na Mungu yeye atosha..
Mbarikiwe.


Kifo cha Sara
1Sara aliishi miaka 127. Hiyo ndiyo iliyokuwa miaka ya maisha yake Sara. 2Alifia huko Kiriath-arba, yaani Hebroni, katika nchi ya Kanaani. Abrahamu akaomboleza na kumfanyia matanga Sara mkewe. 3Abrahamu akaiacha maiti ya mkewe, akatoka kwenda kuzungumza na Wahiti, akawaambia, 4 “Mimi ninaishi kama mgeni miongoni mwenu. Nipatieni sehemu ya ardhi ya kaburi, ili nipate kumzika marehemu mke wangu.” 5Wahiti wakamjibu, 6“Ee bwana wetu, tusikilize; wewe ni kiongozi maarufu miongoni mwetu. Mzike marehemu mkeo katika kaburi lolote utakalojichagulia; hakuna yeyote miongoni mwetu atakayekunyima kaburi lake, wala kukuzuia kumzika marehemu mkeo.” 7Hapo Abrahamu akasimama na kuinama kwa heshima mbele ya wananchi Wahiti, 8akawaambia, “Ikiwa mnaniruhusu nimzike marehemu mke wangu, tafadhali mwombeni Efroni mwana wa Sohari, kwa niaba yangu, 9aniuzie lile pango lake la Makpela lililo mpakani mwa shamba lake. Msihini aniuzie nilifanye makaburi yangu; anipatie kwa bei ya haki papa hapa mbele yenu.”
10Efroni mwenyewe alikuwa miongoni mwa Wahiti hao waliokuwa wamekutanika penye lango la mji. Basi, Efroni Mhiti, akamjibu Abrahamu, mbele ya Wahiti wote hapo langoni, 11“La, bwana; tafadhali unisikilize. Ninakupa shamba lote na pango lililomo humo; tena ninakupa mbele ya wananchi wenzangu. Mzike humo marehemu mkeo.”
12Abrahamu akainama tena kwa heshima mbele ya wananchi, 13akamwambia Efroni, wananchi wote wakisikia, “Nakuomba, tafadhali unisikilize. Nitakulipa bei kamili ya shamba lako, na ninakuomba upokee malipo haya, ili nipate kumzika humo marehemu mke wangu.” 14Efroni akamjibu Abrahamu, “Bwana, nisikilize; 15shamba lenye thamani ya shekeli 400 tu za fedha ni nini kati yako na mimi? Mzike marehemu mke wako.” 16Abrahamu akakubaliana na Efroni, akampimia kiasi cha fedha alichotaja mbele ya Wahiti wote, fedha shekeli 400, kadiri ya vipimo vya wafanyabiashara wa wakati huo.
17Basi, shamba la Efroni lililoko huko Makpela, mashariki ya Mamre, pango na miti yote iliyokuwamo pamoja na eneo zima, likawa lake 18Abrahamu mbele ya Wahiti wote waliokutanika penye lango la mji. 19Baada ya hayo, Abrahamu akamzika Sara mkewe katika pango hilo lililokuwamo katika shamba la Makpela, mashariki ya Mamre (yaani Hebroni) katika nchi ya Kanaani. 20Shamba na pango lililokuwamo humo lilithibitishwa na Wahiti liwe mali yake Abrahamu apate kuzika humo wafu wake.
Mwanzo23;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (BHN):
Jifunze zaidi
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.