Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 24 April 2016

CLOUDS MEDIA GROUP IKIONGOZWA NA MD JOE KUSAGA YATEMBELEA NYUMBANI KWA BALOZI MANONGI, NEW YORK


Mwakilishi wa kudumu wa Ubalozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa Mhe. Balozi Tovako Manongi akimkaribisha Mkurugenzi wa Clouds Media Group Joseph Kusaga nyumbani kwake siku ya Jumamosi April 23, 2016.
Mkurugenzi huyo alitembelea nyumbani kwa Balozi jijini New York akiongozana na baadhi ya wafanyakzi wake ambao walikuja nchini Marekani kwa ajili ya tamasha la Radio lililofanyika jijini Las Vegas. Picha na Vijimambo New York.
Mhe. Balozi Tuvako Manongi akiwatambulisha maafisa na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa kwa Mkurugenzi wa Clouds Media Group, Bwn, Joseph Kusaga (hayupo pichani) siku ya Jumamosi April 23, 2016.
Mkurugenzi wa Clouds Media Group Bwn. Joseph Kusaga akitambulisha timu yake kwa Mhe. Balozi Tuvako Manongi.
Mhe. Balozi Tuvako Manongi, mwakilishi wa kudumu wa Ubalozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa, New York akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Clouds Media Group, Bwn. Joseph Kusaga.
Mkurugenzi wa Clouds Medea Group, Bwn. Joseph Kusaga akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Tuvako Manongi na mkewe.
Timu nzima ya Clouds Media Group iliyohudhuria Tamasha la Radio nchini Marekani ikiwa katika picha ya pamoja na Balozi Tuvako Manongi na mkewe.
Kutoka kushoto ni Saleh Mohammed, Daudu Lembuya, Dj Venture, Mhe. Balozi Tuvako Manongi, Mkurugenzi Joseph Kusaga, Mama Manongi, Dj Peter Moe na Jackson Joseph.
Kushoto ni Brightus Titus, Getrude Clement na NY Ebra wakiwa katika picha ya pamoja.

Siku hiyo pia lilifanyika kusanyiko la maDJ mbalimbali wa zamani waishio nchini Marekani ambao walikutana kwa nyama choma na kubadilishana mawazo. MaDj hawa ni wachache miongoni mwa wengi wanaounda kundi la Tanzania Djs Worldwide ambalo limeanza miezi mitatu iliyopita, na mpaka sasa lina wanachama wapatao 70. Kusanyiko lao la kwanza lilifanyika Escape One March 24 (lirejee hapa)




Saturday 23 April 2016

FRANK LYIMO APEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA MAREKANI, ASHINDA MR. VIRGINIA INTERNATIONAL UNIVERSITY




Frank Lyimo (mwenye vazi la kimasai) mmoja ya Watanzania wanaosoma katika chuo cha kimataifa cha Virginia, ameshinda kwenye shindano la vivazi lililofanyika siku ya Alhamisi April 21, 2016. Vazi lililompa taji hilo ni vazi la kimasai.
Frank Lyimo akiwa katika picha ya pamoja na miss District of Columbia mara tu alipovikwa taji na kuwa Mr. Virginia International University.
Frank Lyimo akiwa katika picha ya pamoja na wanachuo wenzake wa Kitanzania wakipeperusha bendera ya Tanzania chuoni hapo katika kusherehekea ushindi.
Frank Lyimo (kati) akiwa na washiriki wengine.


Monday 18 April 2016

MWILI WA MAREHEMU HENRY KIHERILE WAAGWA HOUSTON, TEXAS


Jioni ya jana Jumamosi (16/04) Jumuiya ya Watanzania waishio katika jiji la Houston na miji mingine ya karibu ilifanya Ibada Takatifu katika kanisa la Umoja kumuaga mpendwa wao Henry Kiherile aliyefariki wiki moja na nusu iliyopita baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana. Ibada hiyo ilihudhuriwa na idadi kubwa ya watu waliokuwa na huzuni kubwa juu ya kifo hicho kilichogusa mioyo ya watu wengi. Mwili wa marehemu Henry unatarajiwa kusafirishwa jioni ya leo kuelekea nyumbani Tanzania kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam siku ya Ijumaa tarehe 22/04/2016. Pata picha za Misa hiyo hapa chini.

Marehemu Henry Kiherile enzi za uhai wake
Gari lililobeba mwili wa Henry likiingia kanisani


Wachungaji wakiwa nje ya kanisa kabla ya ibada


Jeneza lililobeba mwili wa Henry likiingizwa kanisani
Dada  Lulu  ( mdogo wa Marehemu Henry ) akimuaga kwa uchungu kaka yake
Mr. & Mrs. Tenende ( Baba na Mama mkubwa wa marehemu ) wakiwa kanisani
Waombolezaji wakilia kwa uchungu
Rafiki wa Henry kutoka Cameroon
Waombolezaji