Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 29 December 2015

Kipindi cha JUKWAA LANGU Dec 28 2015 (FULL)


Photo Credits: govtech.com

Kipindi hiki hukujia kila JUMATATU, kujadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu Tanzania ya sasa na ile tuitakayo.
Wiki hii ni ya mwisho kwa mwaka 2015, hivyo kipindi hiki kimeangaza baadhi ya yaliyotokea katika siasa za Tanzania.
Studioni alikuwepo Dj Luke Joe, Said Mwamende na Mama Jessica Mushala.
Na kama kawaida, kwa njia ya simu tukaungana na wasikilizaji wengi ndani na nje ya Marekani
KARIBU

Monday 28 December 2015

Mahojiano na msanii Hashim Kambi Washington DC


Hashim Kambi ni msanii wa filamu nchini Tanzania.
Alikuwa mkarimu sana kupita studio zetu za Kilimanjaro hapa Beltsville Maryland na kuzungumza nasi


Friday 25 December 2015

Nawatakia Christmas Njema;Burudani-Boney M. Christmas Album FULL 1981,Baba Gaston - Kakolele Viva Christmas

Nawatakia  Christmas Njema Iwe yenye Heri,Baraka,Furaha na Aamani.

"I wish everyone a  Merry Christmas" 
 







"Swahili Na Waswahili"Muwe na Wakati mwema.

Tuesday 22 December 2015

Kipindi cha Jukwaa Langu Dec 21 2015 (FULL)


Kipindi hiki hukujia kila jumatatu kuanzia saa 11 jioni kwa saa za
Marekani ya Mashariki kuijadili Tanzania ya sasa na ile tuitakayo.

Kuna mengi tuliyogusia pamoja na wasikilizaji wetu

KARIBU

 

Tuesday 8 December 2015

Mahojiano na DC Paul Makonda katika kipindi cha JUKWAA LANGU Dec 7 2015




Kipindi cha JUKWAA LANGU hukujia kila Jumatatu kuanzia saa 11 jioni kwa saa za Marekani ya Mashariki kuijadili Tanzania ya sasa na ile tuitakayo

Katika kipindi hiki, tumeungana na Mhe Paul Makonda. Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni jiji Dar Es Salaam ambaye mbali na mambo mengine, ameeleza "ya moyoni" kuhusu tofauti iliyopo kati ya utendaji wa Rais wa awamu ya nne Mhe Jakaya Kikwete (aliyemteua katika wadhifa huo) na Rais wa sasa Dk John Magufuli. Kabla ya hapo aligusia namna alivyoteuliwa kuwa mkuu wa Wilaya, na kwanini anaamini inastahili kuwepo namna nzuri zaidi ya kuteua watu katika nafasi kama yake.

Na kabla ya hayo yote, alizungumzia migogoro mbalimbali inayoendelea wilayani mwake kama wa kiwanda cha Urafiki, kubomolewa kwa nyumba za thamani, mgogoro wa Coco Beach nk.

Na kama ilivyo desturi, akapokea maswali na ushauri toka kwa wasikilizaji wetu

KARIBU