Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 16 May 2014

Matembezi ya Mswahili Vijijini;Burudani-Nuta Jazz Band (Tanzania) - Pongezi Wakulima (60's Tanzanian Rumba!)

Waungwana;Nipatapo muda huwa napenda kuzunguka/Kutembea na kujifunza/kujione mambo yakoje...
Basi Leo niwapeleke Shamba /Vijijini kidogo.

Swali.....
Wakulima wa Ng'ambo wapi wanapatia na Wakulima wa Afrika wapi wanakosea?
Jee Mkulima ni Mtu Masikini/Fukara,Mnyonge,Kaishiwa na........?

Jee unapenda kuwa Mkulima?








Nuta....Pongezi kwa Wakulima...


"Swahili Na Waswahili" Muwe na Wakati Mwema.

Monday 12 May 2014

Boko Haram: Waonyesha wasichana waliotekwa


Wasichana ambao kundi la Boko Haram liliwateka nyara


Kiongozi wa kundi la Boko Haram Abubakar Shekahu amesema kuwa atawaachilia huru wasichana waliotekwa nyara iwapo tu wapiganaji wa kundi hilo wanaozuiliwa na serikali ya Nigeria wataachiliwa huru.
Katika kanda mpya iliyotolewa na kundi hilo, kiongozi huyo, amesema kuwa wasichana hao waliweza kusilimu katika kipindi cha wiki nne zilizopita tangu watekwe nyara.
Kanda hiyo inaonyesha zaidi ya wanawake miamoja wakiwa wamevalia hijabu na kuswali. Abubaka Shekau anasema kuwa wanawake hao ni wasichana waliotekwa nyara na kundi hilo.
Walitekwa nyara kutoka katika shule yao mjini Chibok, Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo
Rais wa Ufaransa amejitolea kuwa mwenyeji wa mkutano utakaotafuta njia za kupambana na Boko Haram.

Habari zaidi;http://www.bbc.co.uk/swahili/habari

Shukrani.

Sunday 11 May 2014

Nawatakia JumaPili Njema;Burudani-Umoja One SDA Church choir Volume 3 DVD



Wapendwa;Nawatakia JumaPili Njema,Amani,Baraka,Upendo,Utuwema,Kweli,Shukrani,Tumaini,Imani,Upole kiasi na Utukufu Turudishe kwa BWANA......


Sisi twatokana na MUNGU.Yeye amjuaye MUNGU atusikia;yeye asiyetokana na MUNGU hatusikii.Katika hili twamjua Roho wa kweli,na roho ya upotevu.........

Neno La Leo;Waraka wa Kwanza wa Yohana:4;1-21
Kuzipima Roho;1-6
MUNGU ni Pendo;7-21


Na amri hii tumepewa na yeye,ya kwamba yeye ampendaye MUNGU,Ampende na ndugu yake.


Mhhhhhh.......
 Asante/Shukrani;Umoja SDA

"Swahili Na Waswahili"MUNGU Atubariki Sote.

Sunday 4 May 2014

Nawatakia JumaPili Njema;Burudani,Kijitonyama-Twaokolewa kwa Neema Na Nyingine!!!!!!!!

Wapendwa nawatakia JumaPili Njema na Yenye Baraka,Amani,Upendo na Utukufu Turudishe kwake BWANA....

Mimi nitasimama katika zamu yangu,nitajiweka juu ya mnara,nitaangalia ili nione atakalo niambia, na jinsi nitakavyojibu katika habari ya kulalamika kwanngu.
Neno La Leo;Hababkuki;2:1-5.


BWANA akanijibu akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye apate kuisoma kama maji.





"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Monday 28 April 2014

Mhe Mwigulu Nchemba akizungumzia suala la uraia pacha Washington DC‏

Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba akihojiana na Mubelwa Bandio wa Kwanza Production Washington DC.

Photo Credits: Habari Kwanza blog
Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba, amesema kuwa anajivunia kiasi cha UZALENDO walichonacho waTanzania hapa nchini, jambo linalompa moyo kuendeleza harakati zake za kusaidia kupatikana kwa uraia pacha, ombi lililo kuu kwa waTanzania waishio nje ya nchi katika mabadiliko ya katiba mpya.

Mhe Nchemba, ambaye alikuwa mmoja wa wageni waalikwa kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanzania yaliyofanyika jijini Washington DC nchini Marekani, amesema kuwa ushiriki wa waTanzania na rafiki zao katika maadhimisho haya, umemdhihirishia nia na mapenzi yao kwa nchi yao, na hilo limemsukuma zaidi kusaidia kupitishwa kwa suala la uraia pacha kwenye katiba mpya.

Hii ni ripoti katika kipindi cha Morning Jam