Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 23 October 2013

Tuesday 22 October 2013

MAENDELEO YA MSIBA WA BI MARTHA SHANI WASHINGTON DMV


                                          Marehemu Martha Shani[1976-2013]
Marehemu Bi Martha akiwa na mumewe Alex Pamoja na watoto wao Jose naChris 
                                         
                                   
NDUGU YETU ALEX KASSUWI BADO ANAHITAJI MSAADA WETU WA HALI NA MALI ILI KUWEZESHA KUSAFIRISHA MWILI WA MPENDWA MKE WAKE ALIYEFARIKI GHAFLA SIKU YA JUMAMOSI OCT 19, 2013.

KUTOA NI MOYO NA CHOCHOTE UTAKACHOWEZA KITASAIDIA NA HATIMAE KUWEZESHA SAFARI HII NDEFU YA KUMPELEKA MAREHEMU KATIKA MAPUMZIKO KWENYE NYUMBA YAKE YA MILELE TANZANIA

GHARAMA ZA MSIBA KUSAFIRISHA MAREHEMU NA FAMILIA YAKE NI $19,500

FEDHA ZILIZOPATIKANA HADI SASA NI $4,300
ZILIZOBAKI $ 15,200

TAFADHALI TUMA RAMBI RAMBI ZAKO KUPITIA ACCOUNT IFUATAYO :-
# 446030759150 BANK OF AMERICA,MD
ROUTING # 052001633
MAJINA KWENYE ACCOUNT NI ALEX KASSUWI & FAITH ISINGO

CHEKI ZINAWEZWA ANDIKWA KWA ALEX KASSUWI AU FAITH ISINGO.

PIA UNAWEZA KUTOA RAMBIRAMBI ZAKO KWA KUFIKA NYUMBANI KWA MAREHEMU AMBAKO NDIKO MSIBA UPO
ADDRESS NI

482 ARWELL CT
FREDERICK, MD,21703

AU WAWEZA WASILIANA NA MMOJA YA WANAKAMATI HAPO CHINI NA KUMUELEKEZA UPO WAPI ILI AWEZE KUKUSANYA MCHANGO WAKO

Tino Malinda -240-565-7133
Dickson Mkama - 301-661-6207
Mariam Mtunguja - 240-422-1852
Quizella Ntagazwa - 240-602-5011
MV Mtunguja- 240-593-0575
Victor Marwa - 240-515-6436
Faith Isingo - 240-705-1055
Julius Manase-240-393-8445

UKISOMA UJUMBE HUU TAFADHALI MTAARIFU NA MWENZIO, MZIGO HUU NI WETU SOTE NA KWA PAMOJA TUNAWEZA

HAKUNA KIDOGO PALIPO NA NIA. NA HAKUNA KIKUBWA PALIPO NA UMOJA.

Sunday 20 October 2013

Tumalizie J'Pili hii Vyema;Burudani- The Whispers Band-Nina Baba yangu asiyeshindwa kamwe na Nyingine!!!

Wapendwa muendelee na J'Pili kwa Amani,Furaha na Bidii....
Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake?

Neno La Leo;Mithali:22:29 na Muhubiri:9:10






"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

TAHADHARI: UTAPELI MWINGINE WAINGIA NCHINI; Sasa wanatumia mitandao ya Internet ya Kuomba ajira, TAFADHALI soma taarifa hii usije ukalizwa.



Kuna UTAPELI mpya umeingia Nchini, kuna watu ambao wanajifanya wana makampuni na wanatafuta watu wa kazi namaanisha wanatangaza nafasi za kazi, nafasi hizo za kazi huzitangaza kupitia mitandao ya Internet ambayo huwa ina maeneo ya kutangaza nafasi za ajira, nitashindwa kuitaja mitandao hiyo kwa kuwa sio utaratibu ila wewe ambaye unajua kuwa kuna mitandao ambayo inatangaza ajira kupitia njia ya Internet ujue ndio hiyo ambayo tunaiongelea hapa.

Matukio yenyewe yanakuwaje: Watu hao hutangaza nafasi za kazi mbali mbali kupitia mitandao hiyo kwa kuandika wana makampuni na wanatafuta watu kwa nafasi mbambali kwenye makampuni yao feki, kwa kutambua watanzania wengi wana shida ya ajira hutangaza nafasi ambazo wanaamini wengi wataziomba na kuweka vigezo vya chini sana hasa eneo la Elimu na uzoefu kwa kuamini wengi wataomba, baada ya hapo, wewe mwenye shida ya ajira ukishatuma CV yako ambayo itakuwa pia inaonyesha mawasiliano yako, wao hutumia mwanya huo kukutumia ujumbe mfupi (SMS) na kujifanya wao ni wafanyakazi wa kampuni husika ambayo imetangaza nafasi hiyo na kujidai  wanaweza kukusaidia kuipata kazi hiyo na kukutaka uwatumie hela ili wakufanyie mpango na kukutumia maswali ambayo utaulizwa kwenye INTERVIEW na majibu yake, hawa jamaa kwa kutambua shida ya Watanzania hawasemi wanataka kiasi kikubwa huwa wanataka kiasi cha Elfu kumi hadi Hamsini, wanafanya hivyo kwa kutambua wewe mtafuta ajira unaweza ukakipata kiasi hicho.

Matapeli hao hudiriki kukwambia na kiasi cha mshahara ambao utalipwa kwenye kazi hiyo ili kukutamanisha utume hiyo hela, simu hiyo ambayo imekutumia ujumbe huo ukiipigia huwa haipatikani na ikipatikana haipokelewi na wanakua wameziregister kwa majina ambayo wanakuaminisha ni yao kumbe ni majina ya uongo ya kutapelia watu.

Mpaka sasa wameshawaliza watu wengi sana kwa hiyo wewe mdau kuwa makini sana wakati unaomba ajira kupitia mitandao mbalimbali ya Internet, ukiona unaombwa hela baada ya kuomba ajira kupitia mitandao hiyo ujue ndio hao matapeli.

KUWA MAKINI EWE MTANZANIA

IMETOLEWA NA:
MDAU MPENDA HAKI

Saturday 19 October 2013

Kukamatwa kwa mtuhumiwa wa mauaji ya Omar Sykes Washington DC‏


Eneo la tukio Washington DC ambapo Omar Sykes (picha ya ndani) aliuawa.
Photo Credits: National Review Online


Jumanne wiki hii, idara ya Polisi Washington DC (Metropolitan Police Department) ilitangaza kukamatwa kwa mtuhumiwa mmoja kati ya wawili waliokuwa wakitafutwa kwa mauaji ya mwanafunzi mTanzania aliyekuwa akisoma katika chuo kikuu cha Howard hapa jijini.

Omar Sykes (22) aliuawa usiku wa Julai 4 mwaka huu nje kidogo ya maeneo ya chuo hicho alipokuwa pamoja na mwenzake.

Wakiwa mtaa mmoja toka chuoni, wanafunzi hao walivamiwa na watu wenye silaha waliotaka kuwapora, na katika harakati hizo, Omar alipigwa risasi
kifuani na kufariki.


Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).



Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es
Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC


Hii ilikuwa ripoti ya Oktoba 19, 2013



--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"


Tuesday 15 October 2013

Mahojiano na wadau wa darasa la Kiswahili Washington DC‏

Photo Credits: Panafricanvisions.com
Kiswahili inaaminika kuwa lugha asili ya Afrika inayozungumzwa na watu wengi kusini mwa jangwa la sahara.

Kama
tunavyojua, ni lugha ya taifa kwa nchi za Tanzania naKenya, na pia
yazungumzwa kwenye nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Burundi,
Rwanda, Uganda na visiwa vya Comoro.

Ikizungumzwa na watu
wanaokadiriwa kufikia milioni 100 hivi sasa, Kiswahili ndio lugha pekee
ya kiAfrika iliyo miongoni mwa lugha rasmi za Umoja wa Afrika. Na
inaaminika kuwa lugha ya saba kwa watumiaji wengi duniani

Na matumizi
yake kama lugha inayozungumzwa na wengi wenye lugha tofauti katika
ukanda wa Afrika Mashariki na Kati unaifanya lugha hii kuwa muhimu zaidi
kwa watu wengi walio na mahusiano na / ama wanaotaka kujishughulisha na
biashara, kazi ama diplomasia katika ukanda huo.

Kiswahili sasa
kinafunzwa katika vyuo visivyopungua 50 hapa nchini Marekani, lakini pia
inafundishwa kwenye vyuo vikuu mbalimbali Ulaya na hata bara Asia.

Kiswahili
ni lugha muhimu katika habari, shule, kazi za kiofisi, kidiplomasia na
hata usalama miongoni mwa mataifa na naamini ndio sababu hata jumuiya ya
waTanzania hapa Washington DC wakaona ni jambo la busara kuanzisha
darasa la kufunza Kiswahili kwa watoto hapa DMV.

Na leo,
wawakilishi wa wahusika wa mpango huo, Rais wa Jumuiya ya waTanzania DMV
(Washington DC, Maryland na Virginia) Idd Sandaly pamoja na walimu Asha
Nyang'anyi na Bernadeta Kaiza wamekuwa wakarimu sana kujiunga nami
katika studio za JAMII PRODUCTION hapa Washington DC.

KARIBU UUNGANE NASI

Rais wa Jumuiya ya waTanzania DMV (Washington DC, Maryland na Virginia) Iddi Sandaly akishiriki kipindi ndani ya studio za Jamii Production
Mmoja wa walimu wa darasa la Kiswahili hapa Washington DC Bernadeta Kaiza ndani ya studio za Jamii Production
Mmoja wa walimu wa darasa la Kiswahili hapa Washington DC Asha Nyang'anyi akishiriki kipindi ndani ya studio za Jamii Production
Twawapenda....Tukutane juma lijalo kwa kipindi kingine cha HUYU NA YULE tutakapohojiana na wadau wengine juu ya jambo jingine MUHIMU kwa jamii yetu

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Mahojiano ya Jamii Production na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Dr Charles Kimei‏

Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Dkt. Charles Kimei (kulia) akizungumza na Jamii Production  ndani ya ofisi ya Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nchi za Marekani na Mexico uliopo Jijini Washington DC

Jumatano ya Oktoba 9, 2013, Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRBD Dr Charles Kimei akiambatana na Mkurugenzi wa Masoko wa (CRDB) Tully Mwambapa, Bw. Mkurugenzi wa Hazina (CRDB) Alex Ngusaru na Msaidizi wa Dk.Kimei , Kenneth Kasigila walikuwa jijini Washington DC (pamoja na mambo mengine) kueleza mipango ambayo CRDB inayo katika kuboresha huduma za akaunti ya Tanzanite pamoja na kutambulisha huduma mpya ya JIJENGE.

Jamii Production ilipata fursa ya kuhojiana na Dr Kimei ambaye amefafanua mengi kuhusu huduma hizo.

KARIBU UUNGANE NASI





Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt. Charles Kimei na akipata picha na mpiga picha mkuu wa Jamii Production Abou Shatry baada ya mahojiano.

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"