Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 1 November 2012

Wanawake Waswahili wa Coventry,U.K.[WWWCU]Wamtakia Kheri na Baraka da'Maggie[2]!!!!!!


wakimuingiza mpendwa wao








Tukicheza ngoma za Asili






Wakifatilia Matukio







Keki








Wamama/waalikwa







Chakula
Nasaha

Shangwe!!!!!!!!
Shukrani na MUNGU awabariki wooote mliofanikisha jambo  hili.

Wednesday 31 October 2012

Mpendwa Wetu da'Mamie Msuya Amefiwa na Mama Yake!!!!!


Da'Mamie Msuya Pichani.
Amefiwa na MAMA yake Mzazi Afrika.
Dada Mamie anajiandaa na safari, Ataondoka kesho kwenda Afrika.
Tuungane nae katika wakati huu mgumu kwake. Hapa U.K. Msiba upo Nyumbani kwake.
Address;3C THOMAS KING HOUSE,
WELLINGTON ST,
CV1 5SJ.
COVENTRY.
Asanteni.

Tuesday 30 October 2012

Wanawake Waswahili Wa Coventry,U.K.[WWWCU]Wamtakia Kheri na Baraka da'Maggie!!!!!!!














Watu wa Mapambo[Zay&Rachel]
Kina kaka/Baba wa Covenrty na da'Esther wakiweka sawa mambo ya Burudani.
Kina mama wa Coventry wakiandaa chakula



Wapiga picha wakiongozwa na Mwanamke wa shoka da'Mija [Mrs Manju]kutoka MI-RA COMPANY
Maombi yaliongozwa na da'Elina[Mrs Ademisoye]
Neno lilitolewa na da'Rachel-siwa [ muke ya Mubena]
kupambwa na kuhakikisha da'Maggie amefika na kuondoka yalisimamiwa na da'Lina[Wifi la Wabongo]

Mpendwa wetu da'Maggie. 
yeye ndiye aliyetukutanisha  hapo.Ndugu yangu Maggie watu wote hawa wametoa Muda,Hali na Mali kwa sababu yaMshikamano, Umoja,Utuwema, Fadhili na Upendo wa Kweli............
MUNGU  na Azidi kutuongoza.

Picha Zitaendelea usicheze mbaaali.

"Swahili na Waswhili" na "Wanawake wa Shoka"[MI-RA]
Pamoja Daima.....


Sunday 28 October 2012

Siku kama ya Leo da'Jestina George Alizaliwa!!!!!!


Siku kama ya Leo miaka kadhaa iliyopita Mpendwa wetu Da'Jestina[mamake na Imani] Alizaliwa.
Da'Jestina Tunakutakia kila lililo Jema,Baraka,Amani,Fadhili na Uishi Miaka Mingi na Utimize Malengo Yako.

MUNGU azidi kukutendea na kukulinda kila iitwapo Leo.

Ukitaka kujua mengi kuhusu dada huyu ingiahttp://www.jestina-george.com/

Tumalize J'Pili kwa Amani na Upendo;Burudani-Atta Boafo - Double Double na Nyingine Nyingii!!!!

Wapendwa; Tumalize J'Pili hii Vyema,Tuwe na Amani,Upendo,Umoja,Msamaha,Uvumilivu na Shukrani.
Neno la Leo.Mithali;29:7-9 Mambo haya mawili nimekuomba;Usininyime[matatu]kabla sijafa.Uniondelee ubatili na Uongo;Usinipe umasikini wala Utajiri;Unilishe chakula kilicho kadiri yangu.............

"Swahili NA Waswahili" MUNGU Atubariki Soooote

Thursday 25 October 2012

TANZIA!!!!!



FAMILIA YA  MAREHEMU MCHUNGAJI MWAKIPUNDA WA NGAMANGA IPINDA KYELA WANASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MZEE NSUBISI SAMUEL MWAKIPUNDA (MKURUGENZI WA ZAMANI WA IDARA YA MAELEZO)  KILICHOTOKEA SIKU YA JUMATANO TAREHE 24/10/2012.

MIPANGO YA MAZISHI INAFANYIKA NYUMBANI KWA MAREHEMU PUGU KINYEMWEZI DAR ES SALAAM.
HABARI ZIWAFIKIE NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI POPOTE PALE WALIPO.

KWA MAWASILIANO ZAIDI
+255655994499
BWANA AMETOA BWANA, AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE

AMEN