Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 16 November 2011

Kuna Siku za Furaha na Siku za Vilio,Yote ni MaishaTusikate Tamaa!!!

                 Siku Ndugu zangu walipokuwa na Furaha.
                                        Mshumaa ulio Zimika.
                                            Mshumaa ulioZimika

Mungu awatie Nguvu katika wakati huu Mgumu na Sikuzote,Zaidi tudumishe Upendo,Umoja,Ushirikiano na Tusikate Tamaa,Wakati kama huu ndiyo utamjua Rafiki,Ndugu wa Kweli na Mengi Mema kwa Mabaya unaweza kuyasikia.Na niwakati kwa Waliopoteza Wazazi/Wapendwa wao Kuwakumbuka na Kulia tena,Nimeamini wanaosema Kilio hakiishi Utalia kila unapokumbuka.Nilitamani niwe nanyi lakini Mungu aliye nanyi ni Zaidi yetu sisi Tuliyo mbali.Mungu awalaze Mahali Pema Peponi Nduguzangu na Rafiki zangu,Jirani zangu na Wote waliotangulia.Sina Mengi ya Kusema bali nasema Asante Mungu.Wenu MWANAPENZA.

Monday 14 November 2011

Wanawake Waswahili wa Coventry wanakutakia,Kila la kheri da'May!!!!!!!!

                                        Mwenyewe da'May.
                                           Kekiiiii
                                               Kata mwanangu kataaa Keki
             May akilishwa na dada yake Esther,dada huyu ndiyo chanzo cha shughuli hii
                       May akimlisha dada yake kwa Furaha
             Da'May baada ya kumlisha dada yake wakaangaliana,May akasema Asante dada yangu
                   May na Mswahili wa Congo
                Mama mwenye nyumbaaa alilishwa pia
                    dada akisogea kutoa Nasaha zake mambo ya Tanga hayo
                           Heheheheee da'Stellah Akitoa Nasaha zake
                   Weshuuu!! da'Tina akitoa Nasaha zake
                           Wamama wakifuatilia Nasaha mbalimbali
                        Waswahili kutoka Milton nao walikuwepo
                          Da'Edna alikuwa MC siku hiyo, Yupo sambamba na mwali
                           Da'Asha mwenye furaha akifuatilia mapango mzima wa Nasaha
                              Wamama hawa wameguswa na Nasaha
                          Da'Bai yupo makini na kamera yake,lakini sikio lipowazi Kusikiliza Nasaha
                     Da'Sarah,Mamie na Stellah,Shughuli ilikamalika
                                 Da'Tinna alikuwepo
                        Dadazzzz walikuwepo,Neema,Maggie na Vick
                           Penye Wanawake Waswahili hakukosi Mila babuu Mtu kwako yakheeee
                         Haya funga Vibwebwe jamaniiiii!!!!Twende sasa!!
                                Hahhahahha Mwali kakuaaaaaaaaaaa,Swahili na Waswahili Wapendwaaaa


                         Nyanyuka sasa Mdogo wangu ya Coventry yameisha Subiri ya Dar na  Tangaaa

                    Mpango mzima wa muziki na Ngoma ulisababishwa na da'Chikuuuu huyo wa Mwisho


Shughuli hii ndogo ya Kumtakia Ndoa Njema dada May,Iliandaliwa na da'Esther,yeye ni dada wa bi Arusi mtarajiwa, Wanawake Waswahili wa Coventry U.K,[WWCU]Walikuwa bega kwa bega na da'Esther kufanikisha jambo hili.
Wanawake Coventry mpo juu na Mungu awabariki sana!!!


Dada May anatarajia kufunga Ndoa hivi karibuni,Ndoa hiyo itakuwa Nyumbani Tanzania[Bongo].
Kwaniaba ya Wanawake wenzangu;Da'May Tunakutakia Safari njema,Ndoa njema yenye baraka na Mungu akutangulie kwa kila jambo wewe na Mume wako Mtarajiwa pamoja na Familia na Wote watakaofanikisha.
Mengi yalishasemwa  pale kwenye sherehe,Hatuna la zaidi sisi TUNAKUPENDA SANA!!!!!!!






Wednesday 9 November 2011

DR. REGINA KAPINGA AIPEPERUSHA VEMA BENDERA YA TANZANIA NDANI YA BILL AND MELINDA GATE FOUNDATION.



DR. Regina Kapinga

Mama Regina (Program Officer of Bill & Melinda Gate Foundation) ni Mtanzania wa kwanza kuchaguliwa kuwa Staff wa Bill and Melinda Gate Foundation.

kutokana na Elimu na uzoefu aliokuwa nao katika kufanya kazi kwenye Taasisi za kimataifa, Taasisi ya kimataifa inayomilikiwa na Tajiri mkubwa Duniani Bill Gate ambaye ni mmiliki wa kampuni kubwa ya technolojia ya Microsoft ikaona imtumie katika kuweza kusimamia shughuli zote zinazohusu misaada mbali mbali katika mabara maskini Duniani, yaani Afrika na Asia.

Watanzania tunakutakia afya njema ili uweze kuitangaza zaidi Nchi yetu, tunaamini kupitia wewe Taifa letu litafaidika na misaada mbali mbali kutoka kwenye Foundation hiyo.
        
Habari hii nimetumiwa na KapingaZ Blog
Asante sana.

Monday 7 November 2011

Da'Arianna Atimiza Miaka 3!!!!!!!

                     da'Arianna  kasimama tayari.
                           Kitu  cha kekiii.
              Mwenyekiti da'Mija akiandaa kekii.
                                 Arianna na mama'ke wakifurahia.
                          Mama Arianna akimsaidia kukata keki.
                              Kula mwanangu weee.
                                Dadazzzzz wakitabasamu.
               watoto wakibadilishana mawazo.
                  dada unajua mchezo huu?
                 Watoto wa Swahili Fellowship, wakisubiri kekii.
                  wametulia wenyewe.
                                    Watoto wanatabasamu naona mambo yalianza kusogea.
                       Watoto waliitikia mwaliko.
                        Mama kula eehhh,mama alikula mwishoni baada ya kuhakikisha watoto wote wamepata keki.

Familia ya bibi na bwana  Jonathan Mbwambo wa Coventry U.K.
Wanamshukuru sana Mungu kwa Mema mengi aliyo watendea, Moja  kati ya hayo ni kumlinda mtoto wao mpendwa da'Ariann mpaka leo Ametimiza miaka 3, Mungu ni Mwema sana.
Pia wanapenda kutoa Shukrani kwa Wazazi  na Watoto wa Coventry Christian Swahili Fellowship,na Wote waliojumuika nao.Shukrani za Pekee zimwendee Mwenyekiti wa Watoto da'Mija na Kamati Yake.
Mungu awabariki wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine.
Familia tunasema Asanteni sana kwa Moyo wenu na Mungu awe nanyi daima.


WENU KATIKA YOTE NA TUNAWAPENDA SANA.



         NASI SWAHILI NA WASWAHILI TUNAMTAKIA ARIANNA MAISHA MEMA YENYE AMANI NA FURAHA TELEEEEEEE.





Sunday 6 November 2011

ALFEO SILUNGWE AKIITANGAZA TANZANIA KATIKA MOJA YA PRESENTATION ZAKE INDIA.




Alfeo Silungwe Mtanzania anaye piga Nondo ya Masters of Statistic ndani ya Nchi ya India akiwa anafanya presentation katika moja ya kozi anayo isomea chuoni hapo.





                                                   Habari hii nimetumiwa na KapingaZ Blog.
                          Asante sana.
                                  


Trehe:5/11 NI SIKU ALIYOFARIKI BIBI TITI MOHAMED, MMOJA WA WANAWAKE WALIOKUWA WANAHARAKATI WA UKOMBOZI WA TAIFA LETU.


Bibi Titi Mohamed enzi za uhai wake.



Hapa akiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Bibi Titi Mohammed (1926 - 5 Novemba, 2000) alikuwa mmoja wa wanawake wa kwanza kushika nafasi za ubunge na uwaziri nchini Tanzania. Pia alikuwa kati ya wanawake wa kwanza kujiunga na harakati za kugombea uhuru wa Tanganyika.
Mwaka 1969 Bibi Titi Mohammed alikamatwa na mwaka uliofuata alifikishwa mahakamani kwa kosa la kula njama ya kutaka kupindua serikali. Katika kesi hiyo, Bibi Titi alikuwa ni mwanamke pekee katika washtakiwa 7. Baada ya kesi hiyo kusikilizwa alipatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo cha maisha. Hata hivyo, mwaka 1972 alisamehewa na rais Julius Nyerere.

Juu ya kutolewa kwake, Mohammed aliongoza maisha yake akiwa mpweke. Mume wake alimtelekeza wakati wa kesi, ushirika wake wa kisiasa ukanyang'anywa, na marafiki zake wengi wakamlani.
Mnamo mwaka wa 1991, wakati Tanzania ikisherekea miaka 30 ya uhuru, Bibi Titi ameonekana kwenye makaratasi ya chama tawala kama "Shujaa wa Kike Aliyepigania Uhuru".
Mnamo tar. 5 Novemba, 2000 Mohammed amekufa kwenye hospitali ya Net Care Hospital mjini Johannesburg ambapo alikuwa akitibiwa.
Moja kati ya mabarabara makubwa ya mjini Dar es Salaam yamepewa jina la Mohammed kwa heshima ya mafaniko makubwa aliyoyafanya wakati wa mbio za kutafuta uhuru wa Mtanzania.


Habari hii nimetumiwa na Kabipingaz Blog
Asante sana.