Thursday, 12 July 2012
Wednesday, 11 July 2012
FELISTA MSOKA AAPISHWA RASMI KUWA WAKILI WA KUJITEGEMEA NA JAJI MKUU OTHMAN CHANDE.!!!
Wakili Felista Msoka
Wakili Felista Msoka akiwa na Mawakili wenzake siku ambayo aliapishwa kuwa Wakili wa kujitegemea.
Wakili Felista Msoka wa katikati na kushoto ni kaka yake Gilbert Msoka na kulia ni rafiki na ndugu wa karibu wa familia ya Msoka ambaye alisoma na kaka yake.
Wakili Felista Msoka akiwa na pacha wake wa kuzaliwa ambaye pia ni Wakili Bi. Yusta Msoka, kwa pamoja wakiwa na furaha kwa kuwa Mawakili.
Wakili Felista Msoka aliapishwa tarehe 6/07/2012 na Jaji Mkuu Othman Chande pamoja na mawakili wengine 286 akiwemo na Waziri wa sheria na Katiba Mh. Mathias Chikawe na kufanya idadi ya mawakili nchini kufikia 2602.
Mtandao huu unapenda kumpongeza kwa mafanikio hayo.
HONGERA SANA.
Tuesday, 10 July 2012
Mswahili Wetu Leo; Da'EMMY KOSGEI,Ameanzia Wapi na Anaendeleaje,Msikileze!!!
Waungwana Mswahili Wetu Leo ni Emmy.
Yeye anatumia Lugha ya kikuyu kwenye kuimba nyimbo zake,
Pia Mavazi yake Zaidi ni ya Ki Afrika.
Mimi ananivutia sanaaa na da'Emmy
Nimetokea sana kupenda midundo,Mirindimo, Sauti na..... Lakini KIKUYU IMEPIGA CHENGA!!!
Vipi wewe Muungwana Emmy anakuvutia? Zaidi nini?
Ebu Tumsikilize kidogo yeye ni Nani na Ameanzia wapi na Anafanyaje!!!!!
Swahili NA Waswahili Pamoja Sana!!!!
Shukrani; Africanacts na k24Tv
Wimbo Alio upatia Tunzo Ololo!!!!
Emmy akiwa Uk.
Sunday, 8 July 2012
Siku kama ya Leo da'Rukia.H.Penza Alizaliwa,Burudani-Tuselebuke!!!!!!!!!!
![]() |
| Mwenyewe Wifi/da'Rukia |
Nawatakia J'Pili Njema;Burudani - Taunet Nelel,Hakuna Mungu kama wewe na Mapambio Meengiii!!!
Wapendwa Nawatakia J'Pili yenye Baraka, Amani na Upendo!!!!
Neno la Leo;Zaburi:67;1-7;
Mungu na Atufadhili na kutubariki,Na Kutuangazia uso wake.Endelea..........
Saturday, 7 July 2012
Chaguo la Mswahili Leo-Mafikizolo - ndihamba nawe na nyingine nyingiii!!!!!!
Waungwana; Leo ngoja tuwaangalie Hawa "Mafikizolo",
Jee wewe wanakubamba/Unawapenda?
Nini zaidi kina kuvutia katika Muziki wao?.
Sina Mengi zaidi Nakusikiliza wewe.Twende sote sasa!!
"Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana.
EXTRA BONGO WAFUNIKA MBAYA KATIKA UZINDUZI WA UKUMBI WAO MPYA NEW WHITE HOUSE A.K.A BONGO RESORT KIMARA KOROGWE NDANI YA JIJI LA DAR ES SALAAM.!!!
Rais wa bendi ya Extra Bongo Ally Choki akiimba mbele ya wapenzi na washabiki wa bendi yake ndani ya ukumbi wao mpya New White House aka Bongo Resort Kimara Korogwe jana.
Rogert Hegga Katapila akiimba mbele ya washabiki wao katika ukumbi wao mpya uliopo Kimara Korogwe Dar es salaam.
Ally Choki na Henry
Mnenguaji mahiri wa Extra bongo akiwapagawisha washabiki wao ndani ya Kimara Korogwe.
Wakata nyonga wa kiume wa Extra Bongo wakiwakimbiza washabiki wao ndani ya ukumbi wao mpya Bongo Resort Kimara Korogwe.
la Extra Bongo Banza Stone A.K.A Makaveli, Generale akipagawisha wapenzi wao ndani ya White Inn Kimara Korogwe.Jembe
Mwanamuziki wa BAIKOKO akiimba mbele ya washabiki wa Extra Bongo ndani ya Kimara Korogwe.
Tunda Man naye hakuwa nyuma katika kuwaburudisha mashabiki wa Extra Bongo.
Mwanamuzi wa Kizazi kipya Bongo Fleva Sheta akiwakimbiza washabiki wake ndani ya ukumbi mpya wa Extra Bongo katika uzinduzi wa ukumbi huo.
Extra Bongo jana walizindua ukumbi wao mpya New White House a.k.a Bongo resort uliopo kimara Korogwe. Uzinduzi huo ulisindikizwa na kundi la bendi ya taarabu Coast modern Taarab chini ya omary tego na Maua Tego, Tunda Man, Cheta na kundi maarufu la BAIKOKO ambalo linapiga muziki wenye maadhi ya utamaduni wa makabila ya watu kutoka Mkoa wa Tanga.
Subscribe to:
Comments (Atom)















