Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 18 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 57....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki
Nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Nitachochea upepo wa kuangamiza dhidi ya Babuloni, dhidi ya wakazi wa Kaldayo. Nitawapeleka wapepetaji Babuloni, nao watampepeta; watamaliza kila kitu katika nchi yake watakapofika kuishambulia toka kila upande wakati wa maangamizi yake.” Usiwape nafasi wapiga mshale wa Babuloni; usiwaache wavute upinde, wala kuvaa mavazi yao ya vita. Usiwahurumie vijana wake; liangamize kabisa jeshi lake.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Wataanguka na kuuawa katika nchi ya Wakaldayo, watajeruhiwa katika barabara zake. Lakini Israeli na Yuda hawakuachwa na Mungu wao Mwenyezi-Mungu wa majeshi, ingawa nchi yao imejaa hatia mbele yake yeye Mtakatifu wa Israeli. Kimbieni kutoka Babuloni, kila mtu na ayaokoe maisha yake! Msiangamizwe katika adhabu yake, maana huu ndio wakati wa Mungu wa kulipa kisasi, anaiadhibu Babuloni kama inavyostahili.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Babuloni ilikuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Mwenyezi-Mungu, ambacho kiliilewesha dunia nzima. Mataifa yalikunywa divai yake, hata yakapatwa wazimu. Ghafla Babuloni imeanguka na kuvunjikavunjika; ombolezeni kwa ajili yake! Leteni dawa kutuliza maumivu yake; labda utaweza kuponywa.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Onyo dhidi ya ibada za sanamu
1Mtu mwadilifu akifa,
hakuna mtu anayejali;
mtu mwema akifariki,
hakuna mtu anayefikiri na kusema:
“Mtu huyo mwema ameondolewa asipatwe na maafa,
2ili apate kuingia kwenye amani.”
Watu wanaofuata njia ya haki,
watakuwa na amani na kupumzika.
3Lakini Mwenyezi-Mungu asema:
“Njoni hapa nyinyi wana wa wachawi;
nyinyi wazawa wa wachawi, wazinzi na malaya.
4Je, mnadhani mnamdhihaki nani?
Mnamfyonya nani na kumtolea ulimi?
Nyinyi wenyewe ni wahalifu tangu mwanzo,
nyinyi ni kizazi kidanganyifu.
5Nyinyi mnawaka tamaa kwenye miti ya mialoni,
na katika kila mti wa majani mabichi.
Mnawachinja watoto wenu
na kuwatambika katika mabonde na nyufa za majabali.
6Mnachagua mawe laini mabondeni,
na kuyafanya kitovu cha maisha yenu.
Mnayamiminia tambiko ya kinywaji
na kuyapelekea tambiko ya nafaka!
Je, mimi nitaridhishwa kwa vitu hivyo?
7Mmeweka vitanda vyenu juu ya milima mikubwa,
na kwenda huko kutoa tambiko.
8Nyuma ya milango na miimo
mmetundika kinyago chenu.
Nyinyi mnaniacha mimi
na kutandika na kuvipanua vitanda vyenu.
Mnafanya mapatano na hao mliopenda vitanda vyao.
Humo mnazitosheleza tamaa zenu mbaya,
huku mnakodolea macho kinyago chenu.57:8 huku … chenu: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
9Mnajitia marashi na manukato kwa wingi
kisha mnakwenda kumwabudu Moleki.57:9 Moleki: Au Mfalme.
Mnawatuma wajumbe wenu huko na huko,
kujitafutia miungu ya kuabudu;
hata kuzimu walifika.
10Mlichoshwa na safari zenu ndefu,
hata hivyo hamkukata tamaa;
mlijipatia nguvu mpya,
ndiyo maana hamkuzimia.
11“Mlimwogopa na kutishwa na nani
hata mkasema uongo,
mkaacha kunikumbuka mimi
na kuacha kabisa kunifikiria?
Mimi sikuwaambia kitu kwa muda mrefu;
ndio maana labda mkaacha kuniheshimu!
12Mnafikiri mnafanya sawa,
lakini nitayafichua matendo yenu,
nayo miungu yenu haitawafaa kitu.
13Mtakapolia kuomba msaada,
rundo la vinyago vyenu na liwaokoe!
Upepo utavipeperushia mbali;
naam, pumzi itavitupilia mbali.
Lakini watakaokimbilia usalama kwangu,
wataimiliki nchi,
mlima wangu mtakatifu utakuwa mali yao.”
Huruma ya Mungu
14Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Jengeni! Jengeni! Tayarisheni njia!
Ondoeni vikwazo vyote njiani mwa watu wangu!”
15Hivi ndivyo asemavyo Mungu aliye juu kabisa,
aishiye milele na ambaye jina lake ni “Mtakatifu”:
“Mimi nakaa huko juu, mahali patakatifu,
nakaa pia na wenye majuto na wanyenyekevu.
Mimi nitawatia moyo walio wanyenyekevu
na kuwapa nguvu wenye majuto.
16Maana sitaendelea kuwalaumu
wala kuwakasirikia daima.
La sivyo hao niliowaumba watadhoofika mbele yangu,
nami ndiye niliyewapa pumzi yangu ya uhai.
17Niliwakasirikia kwa sababu ya uovu na tamaa zao;
niliwaadhibu, nikauficha uso wangu na kukasirika.
Lakini wao waliendelea kufuata njia zao wenyewe.
18Niliiona mienendo yao, lakini nitawaponya;
nitawaongoza na kuwapa faraja,
nitawatuliza hao wanaoomboleza.
19Mimi nitawapa amani,
amani kwa walio mbali na walio karibu!
Mimi nitawaponya.
20Lakini waovu ni kama bahari iliyochafuka,
ambayo haiwezi kutulia;
mawimbi yake hutupa tope na takataka.”
21Mungu wangu asema hivi:
“Watu waovu sitawapa amani.”



Isaya57;1-21

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: