Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 31 October 2011

COVENTRY NA EID PARTY!!!!!!!!


EID PARTY EID PARTY EID PARTY COVENTRY, U.K.!!!
KARIBUNI SANA WASWAHILI WOTE KATIKA KUSHEHEREKEA EID!!
Party hii ni ya kina MAMA na  WATOTO tuu.


Tarehe  12.11. Itakuwa jumamosi,Itaanza saa 9:00 Mchana [3:00.pm],Mpaka saa 3:00 za Usiku[9:00.pm].

Mahali ni; Moat House Leisure and Neighbourhood Centre,
                  Winston  Avenue,Coventry,Cv2 1EA.

Tiketi zimesha anza kuuzwa!!Wahi Tiketi yako Mapema!!
Bei £5 kwa Mtu mmoja.Watoto chini ya mwaka mmoja wataingia Bure!!Chakula Bure!!Kinywaji 50p.
Pia kutakuwa na michezo  ya Watoto,kama Bouncy Castle na Mingine Mingiiii!!

Kwa Maelezo zaidi na manunuzi ya Tiketi
Wasiliana na;Bi ZAYANA Kwa namba 07889257308.

UKIPATA UJUMBE HUU WAJULISHE NA WENGINE.
KARIBUNI SANA!!!!!!.

Friday 28 October 2011

Mama mkwe Kuvunja Nyumba/Ndoa,ni Mapenzi kwa Mwanawe?Kwani ni Yeye Mama!!

 Wapendwa, hivi kwa nini MAMA MKWE/WAKWE;Hasa  Mama wa MUME.Mara nyingi wanapenda kuiingilia nyumba/Ndoa za watoto wao, Mpaka wengine kufanikiwa kuvunja/kuharibu Mahusiano/Ndoa hizo.Je wanataka mke wanaompenda wao/ kukuchaguli wao au Mapenzi tuu ya Mtoto wake tangu mdogo mpaka Akioa ndiyo yanamfanya aone/waone WIVU?Na JE nini kifanyike ili hali hiyo isitokee?.

Mimi Rachel nasema;Kina mama wakwe watarajiwa na mliokuwa na wakwe tayari,Jamani Taratibu waacheni watoto wajinafasi,Bali pale watakapotaka Ushauri au inapobidi.
Haya nawe Mpenzi Msomaji unalipi la kuongezea au Ushauri,Maoni gani kwa mama Wakwe wa Aina hii?

Karibuni sana Wababa,Wamama,Wanawake na Wanaume,mliokuwa ndani ya ndoa na mliokuwa bado!!!!!!!.

PATA NA BURUDANI YA IJUMAA HII KUTOKA KWA KAKA; MRISHO MPOTO!.

Thursday 27 October 2011

ANGALIZO KWA WATANZANIA WOTE, UTAPELI HUU UNAANZA KUOTA MIZIZI.






KUNA TAARIFA ZA WANIGERIA AMBAO WAMEWEKA MASKANI MAENEO YA SINZA, SHUGHULI AMBAZO WANAFANYA WANAIGERIA HAWA BADO HAZIELEWEKI, NI TATA.
MUDA MWINGI HASA VIPINDI VYA JIONI WANAPENDA KUSHINDA KATIKA BAA KADHAA AMBAZO ZINA AMBAA AMBAA NA BARA BARA YA SHEKILANGO, KUANZIA MAENEO YA URAFIKI MPAKA BAMAGA.

HIVI KARIBUNI WATUMIAJI WENGI WA SIMU ZA KIGANJANI NA INTERNET WAMEKUWA WAKITUMIWA MESEJI MBALI MBALI ZA KUSHINDA ZAWADI FLANI, MFANO WATUMIAJI WA SIMU ZA KIGANJANI WAMEKUWA WAKIPATA MSG AMBAYO INAWAONYESHA WAMESHINDA ZAWADI KUTOKA KAMPUNI YA NOKIA, WAKATI UNAKUTA ULIOTUMIWA MSG HIYO MUDA HUO UNATUMIA SIMU YA MCHINA AMBAYO HAINA HATA JINA, NA WALE WATUMIAJI WA INTERNET WANAPATA EMAIL ZA KUTAKA WAINGIZE DETAIL ZAO ZA AKAUNTI ZAO ZA BENKI, HIYO EMAIL INAKUONYESHA KAMA VILE ULICHEZA BAHATI NASIBU FLANI.

WATANZANIA WOTE KAENI CHONJO, KAPINGAZ Blog BADO INAWAFUATILIA HAWA JAMAA ILI KUWEZA KUJUA UNDANI WAO, NA VILE VILE TUNAVIOMBA VYOMBO VYA USALAMA NAVYO VIWEZE KUJUA HAWA JAMAA WANAFANYA NINI, HOFU YETU INAWEZEKANA WAO NDIO WANAJIHUSISHA NA UTAPELI HUU AMBAO NAAMINI WATANZANIA WENGI BADO HAWAJAUJUA VIZURI WIZI HUU WA KUTUMIA MITANDAO.
  
  Habari hii nimetumiwa na Kapingaz Blog

Asante sana.

Tuesday 25 October 2011

Watoto wa Kike na Mitindo!!!!!!

                                 da'Nadia na poziiiii.
                              da'Nadia na Tabasam...
                                     da'Ester kapoziiii....
                                   da'Ester yupo makini....
                                         da'Miriam na poziiii....
                                 da'Naomi  dadalao kwa mitindo sijui Jina.....

Waungwana mnasemaje? Watoto wetu wakipendeza nasi pia roho nyeupeeeee!!!
Mpendwa wewe unapendelea watoto wakitoka vipi/wakivaa vipi?
Nini wewe ulikuwa Unapenda kutinga/kuvaa ulipokuwa mdogo?

Wengi enzi za Utoto kulikuwa na nguo maalum, yaani ya Kanisani/Jumapili, Hospitali,Siku Kuu,Yakutokea kwenda kwa ndugu na jamaaa na yaKushindia/ukiwa nyumbani au kuchezea Rede kama si mpira wa Miguuu!!!!Hahahahhha Tumetokambali mwehhhh.

Lakini Watoto wa Leo wengi wao hakuna Masharti sana kila wakati Wamependeza tuu.

Karibuni Sana Tukumbushane ya Utoto na kutoa Maoni/Mawazo yako kwani Yanathamani kwetu!!!









Sunday 23 October 2011

Mwanamke na Kujiamini!!!!

Wanawake Tufunguke,Tujitoe,Tuamke,Tushikamane,Tupendane,Tuelimishane,Tujifunze na Tujiamini,
Hakuna kitu rahisi, Lakini ukiamua na kujituma utafanikiwa, Hatua moja huanzisha na nyingine,Tusisite kuulizana na kuomba Ushauri pale unapoona umekwama.Pale ulipo na unaweza kufanya kitu ili kusaidiana na kina baba pamoja na Familia,Jamii. Kila mmoja anamuhitaji mwenzie kwanamna moja au nyingine,Kama wewe unafanya kazi na kuna mwingine anafanya biashara.Unaweza kutamani Vitumbua na pengine unajua kupika lakini umechoka au hujui basi kuna mama yupo nyumbani yeye anapika na akakuuzia nayeakapata pesa kidogo nawe umepata mlo,Binadamu kila mmoja anajua hiki na mwingine anajua kile.WANAWAKE TUSILALE.

Nawatakia Jumapili Njema!!!.


Wednesday 19 October 2011

Nimekumbuka Kwetu,Nyumbani ni Nyumbani!!!!!!!!!!!!

                Nimewakumbuka Rafiki Zangu.
               Nimewakumbuka wa kaka wa Mitaa ya Kwetu.
                           Nimewakumbuka Ndugu zangu.
          Nimewakumbuka Vijana wa Mitaa ya Kwetu.
      Nimekumbuka hata Usafiri Wetu.
Nimekumbuka  Maembe,Mabungo na Matunda yote na Wauzaji wake.Hasa Magenge ya Karibu!!!!!

Wapendwa mimi Leo nimekumbuka Kwetu/Nyumbani, yaani ukiniuliza sana machozi yanaweza kunitoka.
Nanimekumbuka meeeeengiiiiii yakwetu.

Zamani ikiwa Likizo tunapelekwa kwa bibi mzaa mama[bi' Mwalimu], sasa ukiona naanza kuandika majina ya ndugu zangu,marafiki na wazazi wangu ujue kumekucha, nikimaliza kuandika bibi ajiandae kunirudisha.Na kila j'Mosi tunapelekwa kwa bibi mzaa baba[bi'MwanaPenza],yeye alikuwa mzee kidogo hawezi kutuhudumia, Hatukai sana huko, nae akiona narudi rudi ndani kunywa maji ajiandae na maswali baba alisema atakuja saangapi?akizugazuga tuu nitamuangushia kilioooo mpaka atuja kwanini tulienda.

Duuhhhh sasa huku nilipo sasa na Ukubwa huu sijui nifanye nini??
Nimeimba leo kuanzia Nyimbo za mchakamchaka,za mwalimu Kachale,Kibuzi,Ukuti na zote za utoto,
Nikahamia Youtube na Cd zote za Nyumbani, lakini nikaona Haitoshi ngoja nishiriki nanyi.

Jee Mpendwa nawe kunasiku yanakukuta haya na je unafanya nini ili kusahau?au unajifariji vipi?

Karibuni sana kwa mchango wa mawazo na Ushauri!!!!!!!!!