Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 14 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 32....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Tunakushukuru, ee Mungu, tunakushukuru! Tunatangaza ukuu wa jina lako na kusimulia juu ya matendo yako makuu.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Mungu asema: “Mimi nimeweka wakati maalumu! Wakati huo nitahukumu kwa haki. Nchi ikitetemeka na vyote vilivyomo, mimi ndiye ninayeitegemeza misingi yake. Nawaambia wenye kiburi: ‘Acheni kujigamba’; na waovu: ‘Msioteshe pembe za kiburi! Msijione kuwa watu wa maana sana, wala kusema maneno ya majivuno.’”
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Hukumu haitoki mashariki au magharibi; wala haitoki nyikani au mlimani. Mungu mwenyewe ndiye hakimu; humshusha mmoja na kumkweza mwingine. Mwenyezi-Mungu, anashika kikombe mkononi, kimejaa divai kali ya hasira yake; anaimimina na waovu wote wanainywa; naam, wanainywa mpaka tone la mwisho. Lakini mimi nitafurahi milele, nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo. Atavunja nguvu zote za watu waovu; lakini nguvu za waadilifu ataziimarisha.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Mfalme mwadilifu
1Kutatokea mfalme atakayetawala kwa uadilifu,
nao viongozi wataongoza kwa kufuata haki.
2Kila mmoja atakuwa kama mahali pa kujikinga na upepo,
kama mahali pa kujificha wakati wa tufani.
Watakuwa kama vijito vya maji katika nchi kame,
kama kivuli cha mwamba mkubwa jangwani.
3Macho hayatafumbwa tena,
masikio yatabaki wazi.
4Wafanyao mambo kwa hamaki wataamua kwa busara,
wenye kigugumizi wataongea sawasawa.
5Wapumbavu hawataitwa tena waungwana,
wala walaghai hawataitwa tena waheshimiwa.
6Wapumbavu hunena upumbavu,
na fikira zao hupanga kutenda uovu,
kutenda mambo yasiyo mema,
kusema mambo ya kumkufuru Mwenyezi-Mungu.
Huwaacha wenye njaa bila chakula,
na wenye kiu huwanyima kinywaji.
7Ulaghai wa walaghai ni mbaya;
hao huzua visa viovu,
na kumwangamiza maskini kwa maneno ya uongo,
hata kama madai ya maskini ni halali.
8Lakini waungwana hutenda kiungwana,
nao hutetea mambo ya kiungwana.
Mawaidha kwa wanawake wa Yerusalemu
9Inukeni, enyi wanawake mnaostarehe, mnisikilize;
sikilizeni ninayosema enyi mabinti mlioridhika.
10Katika mwaka mmoja hivi mtatetemeka nyinyi mliotosheka;
maana hamtapata mavuno yoyote,
na mavuno ya zabibu yatatoweka.
11Tetemekeni kwa woga, enyi mnaojikalia tu;
tetemekeni kwa hofu, enyi mnaostarehe!
Vueni nguo zenu, mbaki uchi,
mjifunge vazi la gunia viunoni mwenu.
12Jipigeni vifua kwa huzuni,
ombolezeni, kwa sababu ya bustani zilizokuwa nzuri,
kwa mizabibu iliyokuwa ikizaa sana,
13kwa ardhi ya watu wangu inayoota miiba na mbigili,
kwa nyumba zote zilizojaa watu wenye furaha,
kwa mji uliokuwa na shangwe.
14Maana ikulu ya mfalme itaachwa mahame,
mji huo wa watu wengi utahamwa.
Mlima na mnara wa ulinzi utakuwa mapango milele,
pundamwitu watapitapita huko kwa furaha,
kondoo watapata malisho yao humo.
Nyakati za amani
15Hali itaendelea kuwa hivyo
mpaka tumiminiwe roho ya Mungu kutoka juu.
Hapo jangwa litakuwa shamba la rutuba tena,
na mashamba ya rutuba yatakuwa msitu.
16Haki itadumu katika nchi iliyokuwa nyika,
uadilifu utatawala katika mashamba yenye rutuba.
17Kutokana na uadilifu watu watapata amani,
utulivu na usalama utadumu milele.
18Watu wangu watakaa katika makao ya amani,
katika maskani salama na mazingira matulivu.
19Msitu wa adui utatoweka kabisa,32:19 Msitu … utatoweka kabisa: Au Patanyesha mvua ya mawe msitu utakapoanguka.
na mji wake utaangamizwa.
20Lakini heri yenu nyinyi:
Mtapanda mbegu zenu popote penye maji,
ng'ombe na punda wenu watatembeatembea watakavyo.


Isaya32;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: