Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 24 March 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo47...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa Leo hii.Baba wa Mbinguni,Mfalme wa Amani,
Muumba wetu,Muumba Mbingu Na Nchi,Mungu usiyelala wala kunsinzia,Mungu unayejibu na Kubariki,Mungu unayesamehe,wewe ni Apha na Omega...
Tazama Baba Jana imepita Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine Mfalme wa Amani..Tunajinyenyekeza mbele zako Muumba wetu ,Tunakushukuru na kukutukuza Baba.. Tunasema asante Jehovah kwa Kibali ulichotupa Baba cha kuiona Leo hii,Tunaomba ukatuongoze na Kuibariki siku hii na Tuanze nawe Baba katika yote..Tuingiapo/Tutokapo,Vilaji/Vinywaji,Vyombo vya usafiri na tutembeapo,Hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!!
Ukabariki kazi zetu Baba, Biashara,Masomo,Vyote tunavyoenda Kugusa/Kutumia tunaomba ukavitakase kwa Damu Ya Mwokozi wetu Bwana wetu Yesu Kristo iliyomwagika ili sisi tupate kupona..
Ukatutakase Miili yetu na Akili zetu Baba..
Ukabariki Ridhiki zetu ziingiapo na zitokapo,Ukatufanye chombo chema na tukatumike sawasawa na Mapenzi yako Baba Mungu..
Utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Baba..
Nasi ukatupe Neema ya kusameheana..
Ukawaguse na kuwaponya wote Wanaopitia Magumu/Majaribu,Shida/Tabu..Wagonjwa,Waliokata tamaa,Waliokataliwa na Wafiwa wakawe mfariji wao..


Tena jambo hili lasemwa pia: “Hawataingia mahali pangu pa pumziko.” Basi, hiyo ahadi ya kuingia bado ipo, maana wale waliohubiriwa Habari Njema pale awali walishindwa kuingia humo kwa sababu walikosa kutii. Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa “Leo,” akasema baadaye kwa njia ya Daudi maneno yaliyokwisha tajwa: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiwe wakaidi.” Kama Yoshua angekuwa amewapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine. Kwa hiyo, basi, bado kuna kupumzika kwa watu wa Mungu. Maana, kila aingiaye mahali pa pumziko la Mungu atapumzika kutoka katika kazi yake kama vile pia Mungu alivyopumzika kutoka kazi yake. Basi, tujitahidi kuingia katika pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwetu atakayekataa kutii kama walivyofanya wao. Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na uboho. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu. Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake yeye ambaye kwake tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu. Basi, tuzingatie kwa makini imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka mbinguni; Yesu, Mwana wa Mungu. Huyu Kuhani Mkuu wetu anaelewa kabisa unyonge wetu; yeye mwenyewe alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi. Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu mwenye neema, tupokee huruma na neema ya kutusaidia wakati wa shida.


Asante Mungu kwa hapa tulipo tunaomba Baba ukaibariki hii Nchi na Mfalme wa Amani ukatawale hapa tulipo...Baba ukaibariki na kutawala Tanzania,Afrika na Dunia yote..Amani yako na mkono wako ukawaguse na kuwaongoza wanaotuongoza wapate kutuongoza katika haki na kweli..Upendo,Fadhili,Umoja,Kweli, Hekima na Busara zinatoka kwako...
Utupe Neema ya kutambua/kujitambua,Roho mtakatifu akatuongoze kwenye Kunena/Kutenda...

Mwenyezi-Mungu asipoijenga nyumba, waijengao wanajisumbua bure. Mwenyezi-Mungu asipoulinda mji, waulindao wanakesha bure.[Zaburi 127:1]

Tunajiachili mikononi mwako Baba,Sifa na Utukufu ni kwako Baba..Tunashukuru na kuamini wewe ni Bwana na Mwokozi wetu ...
Amina...!!!!
Mungu awabariki.

1Basi, Yosefu akaenda kwa Farao, akamwambia, “Baba yangu na ndugu zangu pamoja na kondoo, ng'ombe na mali yao yote, wamefika kutoka nchi ya Kanaani. Sasa wako katika eneo la Gosheni.” 2Yosefu alikuwa amewachukua ndugu zake watano, akawajulisha kwa Farao. 3Farao akawauliza, “Kazi yenu ni nini?” Wakamjibu, “Bwana, sisi watumishi wako ni wachungaji, kama walivyokuwa babu zetu.” 4Kisha wakamwambia Farao, “Sisi watumishi wako tumekuja kukaa kama wageni humu nchini kwa kuwa njaa ni kali huko Kanaani na hakuna tena malisho kwa mifugo yetu. Hivyo, bwana, tunakuomba, sisi watumishi wako, uturuhusu kukaa katika eneo la Gosheni.” 5Farao akamwambia Yosefu, “Baba yako na ndugu zako wamekujia wewe. 6Nchi yote ya Misri iko chini yako; wape baba yako na ndugu zako sehemu bora ya nchi hii. Waache wakae katika eneo la Gosheni. Na iwapo unawafahamu watu stadi miongoni mwao, wateue wawe waangalizi wa mifugo yangu.”
7Kisha, Yosefu akamleta baba yake Yakobo kumwamkia Farao; naye Yakobo akampa Farao baraka zake. 8Farao akamwuliza Yakobo, “Umri wako ni miaka mingapi?” 9Yakobo akamjibu, “Umri niliojaliwa kama msafiri ni miaka 130. Miaka hiyo imekuwa michache na iliyojaa mateso, tena haijafikia idadi ya miaka waliyoishi wazee wangu kama wasafiri.” 10Kisha Yakobo akambariki Farao, akaondoka. 11Basi, Yosefu akawapa baba yake na ndugu zake eneo la Ramesesi lililo bora kabisa katika nchi ya Misri, liwe makao yao, nao wakalimiliki kama alivyoagiza Farao. 12Yosefu akawa anawapatia chakula baba yake, ndugu zake na jamaa yote ya baba yake kulingana na idadi ya watu waliowategemea.

Usimamizi wa Yosefu

13Baadaye chakula kiliadimika kabisa nchini kote. Njaa ilikuwa kali sana hata ikawafanya watu wote katika nchi ya Misri na ya Kanaani kudhoofika. 14Yosefu akakusanya fedha yote ya nchi ya Misri na Kanaani kutokana na nafaka waliyonunua, akaipeleka fedha hiyo ikulu kwa Farao. 15Baada ya watu wote wa nchi ya Misri na Kanaani kutumia fedha yao yote Wamisri wote walimjia Yosefu na kumwambia, “Tupe chakula! Kwa nini tufe mbele ya macho yako? Tazama, sasa fedha yetu imekwisha!” 16Yosefu akawaambia, “Kama fedha yenu imekwisha, basi nipeni mifugo yenu, nami nitawapa nafaka.” 17Ndipo wakamletea Yosefu mifugo yao: Farasi, ng'ombe, kondoo, mbuzi na punda, naye akawapa chakula. Mwaka huo Yosefu akawa anawapa chakula kwa kubadilishana na mifugo yao yote.
18Mwaka uliofuata wakamjia tena na kumwambia, “Bwana, ukweli ni kwamba fedha yetu yote imekwisha, na wanyama wetu wamekuwa mali yako. Sasa, bwana, sisi watumishi wako hatuna chochote tunachoweza kukupa isipokuwa miili yetu na mashamba yetu. 19Ya nini sisi tufe mbele ya macho yako na mashamba yetu yaharibike? Utununue sisi pamoja na mashamba yetu, tuwe watumwa wa Farao, mradi tu utupe chakula. Tupe nafaka, tusije tukafa; utupe na mbegu kwa ajili ya mashamba yetu.”
20Hivyo Yosefu akainunua nchi yote ya Misri iwe mali ya Farao. Kila Mmisri alilazimika kuuza shamba lake, kwa jinsi njaa ilivyokuwa kali. Nchi yote ikawa mali ya Farao, 21na Yosefu akawafanya watu kuwa watumwa,47:21 akawafanya … watumwa: Kiebrania na Septuaginta “akawahamishia mijini”. kutoka pembe moja hadi pembe nyingine ya nchi ya Misri. 22Ardhi ambayo Yosefu hakuinunua ni ile iliyomilikiwa na makuhani. Hao hawakulazimika kuiuza ardhi yao kwani waliishi kwa posho maalumu waliyopewa na Farao. 23Kisha Yosefu akawaambia watu, “Tazameni, nimekwisha wanunua nyinyi nyote na mashamba yenu kuwa mali ya Farao. Mtapewa mbegu nanyi mtapanda mashamba yenu. 24Wakati wa mavuno, sehemu moja ya tano mtampa Farao. Sehemu nne zitakazobaki zitakuwa mbegu na chakula kwa ajili yenu na jamaa zenu na watoto wenu.” 25Wakamjibu, “Bwana, umeyaokoa maisha yetu! Kwa vile umetuonesha wema wako, sisi tutakuwa watumwa wa Farao.” 26Ndivyo Yosefu alivyotangaza sheria moja ambayo iko mpaka leo nchini Misri: Kila raia lazima atoe sehemu moja ya tano ya mavuno yake kwa Farao. Ardhi ya makuhani tu ndiyo haikununuliwa na kufanywa mali ya Farao.

Wosia wa Yakobo

27Basi, watu wa Israeli wakakaa katika eneo la Gosheni nchini Misri. Wakiwa huko, wakachuma mali nyingi, wakazaana na kuongezeka sana. 28Yakobo alikaa katika nchi ya Misri kwa muda wa miaka kumi na saba, hadi alipofikia umri wa miaka 147.
29Wakati wa kufa kwake ulipokaribia, Yakobo akamwita mwanawe Yosefu, akamwambia, “Sasa, kama kweli unanipenda, weka mkono wako mapajani mwangu, uniahidi kwamba utanitendea kwa heshima na haki. Usinizike huku Misri, 30ila unilaze pamoja na babu zangu. Nichukue kutoka Misri, ukanizike katika makaburi yao.” Yosefu akamjibu, “Nitafanya kama ulivyosema.” 31Yakobo akamwambia, “Niapie!” Yosefu akamwapia. Kisha Israeli akainamia upande wa kichwa cha kitanda chake.Mwanzo47;1-31

Bible Society of Tanzania

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 23 March 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo46...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tuende Mbele za Mungu kwa Shukrani na Utukufu..
Mtakatifu,Mtakatifu, Mtakatifu Baba wa Mbinguni, Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi, Baba yetu ,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo, Yeye ni mwanzo na yeye ni mwisho,Hakuna wa kufanana naye..
Muweza wa Yote..Sifa na Utukufu ni kwako Daima..
Asante Baba kwa kutupa nafasi hii ya kuendelea kuiona leo hii..
Jana imepita Baba Leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Mfalme wa Amani Tunaomba Utubariki katika Kazi zetu,Biashara,Masomo.Tuingiapo/Tutokapo,Vyombo vya usafiri na tutembeapo,Hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!!
Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda na maamuzi/kuamua Baba Ukabariki Vilaji/vinywaji na Ukavitakase na Damu ya Bwana wetu Mwokozi wetu Yesu Kristo vyote tunavyoenda kugusa/kutumia,ukatutakase Akili na Miili yetu Jehovah..
Utusamehe pale tulipoenda kinyume nawe Baba wa Mbinguni..
Nasi utupe Neema ya kuweza kusameheana Mfalme wa Mbingu..
Baba ukawaguse na kuwaponya wote wanaopitia Magumu/majaribu,Wenye Shida/Tabu, Wagonjwa,Wafiwa ukawe mfariji wao..Waliovifungoni Baba ukawaweke huru na kuwaokoa Baba..
Utupe Ridhiki zetu sawasawa na Mapenzi yako Baba wa Mbinguni Uzibariki ziingiapo/zitokapo...
Utukufu ni wako,Sifa na Fadhili zako zadumu Milele..

Tunajiachilia Mikononi Mwako Baba wa Mbinguni,Tukishukuru na Kuamini wewe ni Bwana na Mwokozi wetu..
Amina..!!!
Solomoni alipomaliza kusema sala hiyo yote na ombi lake kwa Mwenyezi-Mungu aliinuka kutoka pale mbele ya madhabahu ya Mwenyezi-Mungu, mahali alipokuwa amepiga magoti akiinua mikono yake juu. Alisimama, akawabariki Waisraeli wote waliokuwa wamekusanyika hapo, akisema kwa sauti kubwa, “Atukuzwe Mwenyezi-Mungu ambaye amewapatia starehe watu wake Israeli, kulingana na ahadi yake. Ametimiza ahadi zake zote njema alizozitoa kupitia kwa mtumishi wake Mose. Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, awe nasi, kama alivyokuwa na babu zetu; tunaomba asituache, wala asitutupe. Yeye aelekeze mioyo yetu kwake, ili tufuate njia zake, tukishika amri zake, maongozi yake na maagizo yake aliyowapa babu zetu. Basi, maneno yangu haya ambayo ni ombi langu mbele ya Mwenyezi-Mungu, yawe karibu na Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, mchana na usiku, naye amjalie mtumishi wake, na watu wake Israeli, ili wafanikiwe katika haja zao za kila siku. Nayo mataifa yote ulimwenguni yatajua kwamba kweli Mwenyezi-Mungu ndiye Mungu; wala hakuna mwingine. Nanyi, muwe waaminifu kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, mkifuata masharti yake na kutii amri zake zote kama mnavyofanya hivi leo.”
Mungu awabariki katika yote.


Yakobo anasafiri kwenda Misri


1Basi, Israeli akaanza safari yake pamoja na mali yake yote. Alipofika Beer-sheba, akamtolea tambiko Mungu wa Isaka, baba yake. 2Mungu akaongea na Israeli katika maono usiku, akamwita, “Yakobo! Yakobo!” Yakobo akaitika, “Naam nasikiliza.” 3Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu, Mungu wa baba yako. Usiogope kwenda Misri; utakapokuwa huko, nitakufanya uwe taifa kubwa. 4Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe huko Misri na kukurudisha huku. Utakapofariki, mkono wa Yosefu ndio utakaoyafumba macho yako.”
5Basi, Yakobo akaondoka Beer-sheba. Wanawe wakamchukua yeye, watoto wao wachanga pamoja na wake zao katika magari ambayo Farao alipeleka kumchukua. 6Walichukua pia mifugo na mali yao yote waliyokuwa wamechuma katika nchi ya Kanaani, wakaenda Misri. Yakobo aliwachukua wazawa wake wote: 7Wanawe, wajukuu wake wa kiume na wa kike, wote akawaleta Misri.
8Wazawa wa Israeli ambao walikwenda Misri pamoja naye walikuwa Reubeni, mzaliwa wake wa kwanza, 9pamoja na wana wa Reubeni: Henoki, Palu, Hesroni na Karmi. 10Simeoni na wanawe: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli, aliyezaliwa na mwanamke Mkanaani. 11Lawi na wanawe: Gershoni, Kohathi na Merari. 12Yuda na wanawe: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera. (Lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi walikuwa Hesroni na Hamuli. 13Isakari na wanawe: Tola, Puva, Yashubu46:13 Yashubu: Au Yobu. na Shimroni. 14Zebuluni na wanawe: Seredi, Eloni na Yaleeli. 15Hao ndio wana ambao Lea alimzalia Yakobo kule Padan-aramu, pamoja na Dina binti yake. Jumla ya wanawe, binti zake na wajukuu wake walikuwa watu thelathini na watatu.
16Gadi na wanawe: Sifioni, Hagi, Shuni, Esboni, Eri, Arodi na Areli. 17Asheri na wanawe: Imna, Ishva, Ishvi, Beria na Sera, dada yao. Beria na wanawe: Heberi na Malkieli. 18Hawa kumi na sita ni watoto na wajukuu wa Yakobo na Zilpa, mjakazi ambaye Labani alimpa Lea, binti yake.
19Raheli alimzalia Yakobo wana wawili: Yosefu na Benyamini. 20Huko Misri, Asenathi, binti Potifera, aliyekuwa kuhani wa mji wa Oni, alimzalia Yosefu wana wawili: Manase na Efraimu. 21Wana wa Benyamini walikuwa Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu na Ardi. 22Watu hao kumi na wanne ni watoto na wajukuu wa Yakobo na Raheli, mkewe.
23Dani na Hushimu, mwanawe. 24Naftali na wanawe: Yaseeli, Guni, Yeseri na Shilemu. 25Hao saba ni watoto na wajukuu wa Yakobo na Bilha, mjakazi ambaye Labani alimpa binti yake Raheli.
26Jumla ya wazawa wa Yakobo aliokwenda nao Misri, bila kuwahesabu wake za wanawe, ilikuwa watu sitini na sita. 27Huko nchini Misri Yosefu alikuwa amepata wana wawili. Kwa hiyo watu wote wa jamaa ya Yakobo walioingia Misri walikuwa sabini.

Yakobo anafika Misri

28Yakobo akamtanguliza Yu
da kwa Yosefu kumwomba waonane huko Gosheni; nao wakafika katika eneo la Gosheni. 29Yosefu akapanda gari lake la farasi, akaenda kumlaki Israeli, baba yake, huko Gosheni. Alipomfikia baba yake, alimkumbatia na kulia kwa kitambo kirefu. 30Israeli akamwambia Yosefu, “Hata nikifa sasa si kitu kwa kuwa nimeuona uso wako na kujua kwamba wewe u hai!” 31Yosefu akawaambia ndugu zake na jamaa yote ya baba yake, “Nakwenda kumwarifu Farao kwamba ndugu zangu na jamaa yote ya baba yangu waliokuwa katika nchi ya Kanaani wamekuja kwangu. 32Nitamweleza kwamba nyinyi ni wachungaji kwani mmekuwa mkichunga mifugo, na kwamba mmewasili pamoja na mbuzi, kondoo, ng'ombe na mali yenu yote. 33Basi, Farao akiwaita na kuwaulizeni, ‘Kazi yenu ni nini?’ 34Semeni: ‘Bwana, sisi watumishi wako, ni wafugaji wa mifugo tangu utoto wetu mpaka leo, kwani ndivyo walivyokuwa babu zetu’; semeni hivyo ili mruhusiwe kukaa katika eneo la Gosheni.” Yosefu alisema hivyo kwa sababu kwa Wamisri wachungaji wote wa kondoo ni chukizo.
Mwanzo46;1-34

Bible Society of Tanzania

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 22 March 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo45...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa Mema aliyotutendea/anayoendelea kututundea..

Tumkaribie Mungu

19Basi, ndugu, kwa damu ya Yesu tunapewa moyo thabiti wa kuingia Mahali Patakatifu. 20Yeye ametufungulia njia mpya, njia ya uhai, kupitia lile pazia, yaani mwili wake mwenyewe. 21Basi, tunaye kuhani maarufu aliye na mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. 22Kwa hiyo tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu na imani timilifu, kwa mioyo iliyotakaswa kutokana na dhamiri mbaya, na kwa miili iliyosafishwa kwa maji safi. 23Tuzingatie kabisa tumaini letu tunalokiri, maana Mungu aliyefanya ahadi zake ni mwaminifu. 24Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema. 25Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, siku ile ya Bwana inakaribia.[Waebrania 10:19-25]
Asante Mungu wetu, Muumba mbingu na Nchi, Bwana wetu na Mwokozi wetu,Mfalme wa Amani,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..
Bwana wa Majeshi,Muweza wa yote..
Asante kwa kutuchagua na kutupa kibali cha kuiona leo hii Baba..
Si kwa Uwezo wetu,Nguvu/utashi wetu..Si kwamba sisi ni wema sana Baba hapana..Ni kwa Neema /Rehema zako Muumba wetu...
Mtakatifu Baba wa Mbinguni tunaiweka siku hii mikononi mwako..Ukatuongoze na kutubariki Baba.. Tuingiapo/Tutokapo,Vilaji/Vinywaji,Hatua zetu ziwe nawe Baba..Vyombo vya usafri na tutembeapo Baba wa Mbingu usituache..
Tunaomba ubariki kazi zetu,Biashara,Masomo, na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba ukavitakase..
Ukabariki Ridhiki zetu Baba zinazoingia na zinazotoka..zikawe na ulinzi wako..Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda tukatende sawasawa na mapenzi yako..Utufanye chombo chema Baba nasi tukatumike sawaswa na mapenzi yako..
Utusamehe dhambi zetu Baba wa Mbinguni, tulizokosa kwa kuwaza/kutenda..kwa makusudi/kutokukusudia,Tunazozijua/kutojua..
Nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Bariki Yatima na Wajane Baba, Wenye Shida/Tabu na wote wanaopitia Magumu/Majaribu Baba ukawaponye na kuwaweka huru..
Sifa na utukufu ni zako Baba wa Mbinguni..
Tunashukuru na kuamini wewe ni Bwana na Mwokozi wetu..
Amina....!!

37Maana kama yasemavyo Maandiko:
“Bado kidogo tu,
na yule anayekuja, atakuja,
wala hatakawia.
38Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi;
walakini akirudi nyuma,
mimi sitapendezwa naye.”

39Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tumo na wale wanaoamini na kuokolewa.[Waebrania 10:37-39]


Yosefu anajitambulisha

1Hapo Yosefu akashindwa kujizuia mbele ya wote walioandamana naye, akawaamuru watoke nje. Hivyo Yosefu alikuwa peke yake alipojitambulisha kwa ndugu zake. 2Lakini alilia kwa sauti kubwa hata Wamisri wakamsikia, hali kadhalika na watu wa jamaa ya Farao nao wakamsikia. 3Yosefu akawaambia ndugu zake, “Mimi ni Yosefu. Je, baba yangu angali hai?” Lakini ndugu zake wakapigwa na bumbuazi mbele yake, hata wakashindwa kumjibu. 4Yosefu akawaambia ndugu zake, “Tafadhali, sogeeni karibu nami.” Walipomkaribia, akawaambia, “Mimi ndiye ndugu yenu Yosefu, mliyemwuza Misri. 5Lakini sasa msifadhaike wala kujilaumu kwa kuniuza. Mungu ndiye aliyenileta huku niwatangulie, ili niyaokoe maisha ya watu. 6Huu ni mwaka wa pili tu wa njaa nchini, na bado kuna miaka mitano zaidi ambapo watu hawataweza kulima wala kuvuna mavuno. 7Mungu alinileta huku niwatangulie, ili kusalimisha maisha yenu mbaki hai nchini na kuwakomboa kwa ukombozi mkubwa. 8Kwa hiyo, si nyinyi mlionileta huku, bali ni Mungu. Ndiye aliyenifanya kama baba kwa Farao, msimamizi wa nyumba yake yote na mtawala wa nchi yote ya Misri. 9Basi, fanyeni haraka, mwende kwa baba na kumwambia, ‘Yosefu, mwana wako, anasema: Mungu amenifanya kuwa mkuu wa nchi yote ya Misri. Basi, usikawie kuja kwangu. 10Utakaa karibu nami katika eneo la Gosheni: Wewe, wana wako na wajukuu wako, mifugo yako na mali yako yote. 11Utakapokuwa Gosheni, mimi nitakutunza wewe, jamaa yako pamoja na mifugo yako ili msije mkafa njaa, kwani bado miaka mitano zaidi ya njaa.’” 12Kisha Yosefu akasema, “Nyinyi wenyewe mmeona kwa macho yenu na hata ndugu yangu Benyamini ameona kwa macho yake kwamba ni mimi mwenyewe Yosefu ninayezungumza nanyi. 13Ni lazima kumwambia baba yangu juu ya fahari yangu huku Misri na yote mliyoyaona. Basi, fanyeni haraka, mkamlete baba yangu huku.” 14Kisha Yosefu akamkumbatia Benyamini, nduguye, akalia; Benyamini naye akalia, huku wamekumbatiana. 15Akiwa bado analia, Yosefu akawakumbatia ndugu zake na kuwabusu. Hapo ndipo ndugu zake walipoweza kuzungumza naye.

Farao anamwalika Yakobo aje Misri

16Habari hizo zilipofika ikulu ya mfalme, kwamba ndugu za Yosefu wamekuja, zikamfurahisha sana Farao na watumishi wake. 17Kwa hiyo, Farao akamwambia Yosefu, “Waambie ndugu zako wawapakie punda wao mizigo, warudi nchini Kanaani, 18wamlete hapa baba yao na jamaa zao wote. Mimi nitawapa sehemu nzuri kabisa ya nchi ya Misri, ambako wataweza kufurahia matunda yote ya nchi hii. 19Waambie pia wachukue kutoka hapa magari ya kukokotwa ya kuwaleta watoto wao wachanga na wake zao na wala wasikose kumleta baba yao. 20Waambie wasijali juu ya mali zao maana sehemu nzuri kuliko zote katika nchi ya Misri itakuwa yao.”
21Basi, wana wa Israeli wakafanya kama walivyoagizwa. Yosefu akawapa magari kulingana na maagizo ya Farao na chakula cha njiani. 22Aliwapa kila mmoja wao mavazi ya kubadili, lakini akampa Benyamini vipande 300 vya fedha na mavazi matano ya kubadili. 23Tena alimpelekea baba yake zawadi hizi kwa ajili ya safari yake: Punda kumi waliobeba bidhaa bora za Misri, punda jike kumi waliobeba nafaka, mikate na vyakula vingine. 24Basi, Yosefu akaagana na ndugu zake. Walipokuwa wanaondoka aliwaonya akisema, “Msigombane njiani!”
25Basi, wakatoka Misri na kurudi nyumbani kwa baba yao Yakobo, nchini Kanaani. 26Wakamwambia baba yao, “Yosefu yu hai! Yeye ndiye mtawala wa nchi yote ya Misri!” Hapo baba yao akapigwa na bumbuazi, kwani hakuweza kuyasadiki maneno yao. 27Lakini, walipomsimulia yote waliyoagizwa na Yosefu na alipoyaona magari aliyopelekewa na Yosefu kumchukua, moyo wake ukajaa furaha kupita kiasi. 28Israeli akasema, “Sasa nimeridhika; mwanangu Yosefu yu hai! Nitakwenda nimwone kabla sijafa.”
Mwanzo45;1-28

Bible Society of Tanzania


"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 21 March 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo44...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Ni siku nyingine tena Mungu ametupa Kibali na kutuchagua kuiona siku hii,Kwa Neema/Rehema zake Mungu yeye ametufanya kuwa hivi tulivyo na kuendelea kuishi,Kwabaraka zake Mungu ametuamsha salama..
Kwa uwezo wake yeye Mungu ametupa wakati huu nasi tuutumie vyema katika maisha yetu haya..Wengi walitamani kuiona siku hii lakini kwa Mapenzi yake Mungu haikuwezekana..Wengine wanatamani kusimama lakini hawawezi,Wengine wanatamani wapate walau kauli na kutubu na kumtukuza Mungu lakini hawawezi.. si kwamba ni waovu sana ..
nasi si kwamba ni wema sana, Wenye nguvu na utashi,wenyekujua sana ..Hapana ni kwa mapenzi yake Baba Mungu muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi..yeye ndiye muamuzi wa haya..Yeye akisema ndiyo hakuna wakusema hapana...Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo..
Tunaomba Baba ukatubariki tuingiapo/tutokapo,kwenye vyombo vya usafiri na tutembeapo,Hatua zetu ziwe nawe Baba..
Baba tunaomba ukabariki kazi zetu,Biashara,masomo,vilaji/vinywaji na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba ukavitakase na Damu ya Bwana wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo..
Ukawaguse/kuwaponya Wagonjwa,wenye shida/tabu, wanaopitia magumu/mapito,wenye vifungo mbalimbali baba ukawafungue kwenye minyororo ya mwovu tunaomba ukawaweke huru..wafiwa wakawe mfariji wao..
Mfalme wa Amani ukatawale maisha yetu...

Utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Baba wa Mbinguni nasi ukatupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Tunajiachilia mikononi mwako Baba wa mbinguni,Tukisifu na kushukuru..
Tunaamini wewe ni Bwana na Mwokozi wetu..
Amina..!!!


11Mwenyezi-Mungu na awape watu wake nguvu!
Mwenyezi-Mungu na awabariki watu wake kwa amani!
[Zaburi 29;11]



Kikombe chapatikana kwa Benyamini

1Kisha Yosefu alimwagiza msimamizi wa nyumba yake akisema, “Yajaze magunia ya watu hawa nafaka kiasi watakachoweza kuchukua. Halafu, weka fedha ya kila mmoja wao mdomoni mwa gunia lake. 2Katika gunia la yule mdogo kabisa, kiweke kile kikombe changu cha fedha, pamoja na fedha yake.” Huyo msimamizi akafanya kama alivyoamriwa na Yosefu. 3Kulipopambazuka wakaruhusiwa kuondoka pamoja na punda wao. 4Walipokuwa wamesafiri mwendo mfupi tu kutoka mjini, Yosefu alimwambia msimamizi wa nyumba yake, “Haraka! Wafuate wale watu, na utakapowakuta, uwaulize, ‘Kwa nini mmelipa mema mliyotendewa kwa maovu? Kwa nini mmeiba kikombe cha bwana wangu ambacho 5yeye hunywa nacho na kukitumia kupiga ramli? Mmekosa sana kwa kufanya hivyo!’”
6Yule msimamizi alipowakuta akawaambia maneno haya. 7Lakini wao wakamwuliza, “Bwana, una maana gani kutuambia maneno kama hayo? Sisi watumishi wako kamwe hatuwezi kufanya jambo kama hilo! 8Kumbuka, bwana, fedha tuliyokuta katika midomo ya magunia yetu tuliirudisha kutoka katika nchi ya Kanaani. Itawezekanaje tena tuibe fedha au dhahabu nyumbani mwa bwana wako? 9Basi, kama akipatikana mmoja wetu ana kikombe hicho, na auawe, na sisi wengine wote tutakuwa watumwa wako.”
10Huyo msimamizi akasema, “Sawa; na iwe kama mlivyosema. Yeyote atakayepatikana na kikombe hicho, atakuwa mtumwa wangu, lakini wengine wote hamtakuwa na lawama.” 11Basi, kila mmoja akashusha gunia lake chini haraka na kulifungua. 12Yule msimamizi akayapekua magunia yote, akianzia la mkubwa wao na kumalizia na la mdogo kabisa. Kikombe kikapatikana katika gunia la Benyamini. 13Hapo wakayararua mavazi yao kwa huzuni. Kila mmoja wao akambebesha punda wake mzigo wake, wakarudi mjini.
14Yuda na nduguze wakafika nyumbani kwa Yosefu naye Yosefu alikuwapo bado nyumbani. Basi, wakamwinamia kwa heshima, 15naye Yosefu akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivyo? Je hamjui kwamba mtu kama mimi ninao uwezo wa kubashiri?” 16Yuda akamjibu, “Tukuambie nini bwana? Tuseme nini kuonesha kwamba hatuna hatia? Mungu ameyafichua makosa yetu, sisi watumishi wako. Sasa sote tu watumwa wako, sisi pamoja na yule aliyepatikana na kikombe chako.” 17Lakini Yosefu akasema, “La! Mimi siwezi kufanya hivyo! Yule tu aliyepatikana na kikombe changu ndiye atakayekuwa mtumwa wangu. Nyinyi wengine wote rudini kwa amani kwa baba yenu.”

Yuda anamtetea Benyamini

18Ndipo Yuda akamkaribia Yosefu na kumwambia, “Bwana, nakuomba uniruhusu mimi mtumishi wako, nijitetee mbele yako kwa maneno machache; ninakusihi usinikasirikie, kwani wewe ni kama Farao mwenyewe. 19Bwana, wewe ulituuliza kama tuna baba au ndugu, 20nasi tukakueleza kwamba tunaye baba, naye ni mzee, na kwamba tunaye ndugu mwingine mdogo aliyezaliwa wakati wa uzee wa baba yetu. Kaka yake huyo kijana amekwisha fariki, na huyo mdogo ndiye peke yake aliyebaki wa mama yake; na mzee wetu anampenda sana kijana huyo. 21Bwana, ulituagiza sisi watumishi wako kumleta huyo mdogo wetu upate kumwona. 22Tukakueleza kwamba huyo kijana hawezi kuachana na baba yake, kwa sababu akifanya hivyo baba yake atakufa. 23Lakini wewe bwana ukatuambia kwamba kama hatutakuja na ndugu yetu mdogo, hutatupokea tena.
24“Tuliporudi nyumbani kwa mtumishi wako, baba yetu, tulimwarifu ulivyotuagiza, bwana. 25Naye alipotuambia tuje tena huku kununua chakula, 26tulimwambia, ‘Hatuwezi kwenda, isipokuwa tu kama ndugu yetu mdogo atakwenda pamoja nasi; kama hatakwenda pamoja nasi hatuwezi kupokelewa na yule mtu.’ 27Basi, baba yetu, mtumishi wako, akatuambia, ‘Mnajua kwamba mke wangu Raheli alinizalia wana wawili: 28Mmoja alitoweka, nami nikasema, bila shaka ameraruliwa vipandevipande na mnyama wa porini, maana sijapata kumwona tena. 29Kama mtamchukua huyu pia kutoka kwangu, akipatwa na madhara basi, mtanishusha kuzimu nikiwa mzee mwenye huzuni.’ 30Kwa hiyo basi, bwana, nikimrudia baba yangu mtumishi wako bila kijana huyu, na hali uhai wa baba unategemea uhai wa kijana huyu, 31akiona kwamba kijana hayupo pamoja nasi, atakufa! Hivyo sisi watumishi wako, tutamuua baba yetu kwa huzuni. 32Zaidi ya hayo, mimi binafsi nilijitoa kuwa mdhamini wa huyu kijana kwa baba yangu, nikisema, ‘Nisipomrudisha Benyamini kwako, lawama na iwe juu yangu milele.’ 33Sasa, ee bwana, nakusihi, mimi mtumishi wako, nibaki, niwe mtumwa wako badala ya kijana huyu. Mwache yeye arudi nyumbani pamoja na ndugu zake. 34Nitawezaje kumrudia baba yangu bila kijana huyu? Siwezi kustahimili kuyaona madhara yatakayompata baba yangu.”
Mwanzo44;1-34
Bible Society of Tanzania
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 20 March 2017

Hekima,Busara na Amani.;Muwe na mchana Mwema..




Anayeonywa mara nyingi akawa mkaidi, ataangamia ghafla asipone tena. Waadilifu wakitawala watu hufurahi, lakini waovu wakitawala watu hulalamika. Apendaye hekima humfurahisha baba yake; lakini aandamanaye na malaya hufuja mali yake. Mfalme akitumia haki huipatia nchi uthabiti, lakini akipenda hongo taifa huangamia. Mwenye kumbembeleza jirani yake, anatega mtego wa kujinasa mwenyewe. Mtu mbaya hunaswa kwa kosa lake, lakini mtu mwadilifu huimba na kufurahi. Mwadilifu anajua haki za maskini, lakini mtu mwovu hajui mambo hayo. Wenye dharau huutia vurugu mji mzima, lakini wenye hekima hutuliza ghadhabu. Mwenye hekima akibishana na mpumbavu, mpumbavu huwaka hasira na kucheka bila kutulia. Wapendao kumwaga damu humchukia mtu asiye na hatia, lakini watu wema huyalinda maisha yake. Mpumbavu huonesha hasira yake wazi, lakini mwenye hekima huizuia na kuituliza. Mtawala akisikiliza mambo ya uongo, maofisa wake wote watakuwa waovu. Maskini na mkandamizaji wanafanana kwa kitu kimoja: Wote wawili wamepewa macho na Mwenyezi-Mungu. Mfalme anayewaamua maskini kwa haki, atauona utawala wake umeimarika milele. Adhabu na maonyo huleta hekima, lakini mtoto aliyeachwa afanye apendavyo humwaibisha mama yake. Waovu wakitawala maovu huongezeka, lakini waadilifu watashuhudia kuanguka kwao. Mpe nidhamu mwanao naye hatakupa wasiwasi; yeye ataufurahisha moyo wako. Pasipo maono ya kinabii watu hukosa nidhamu; heri mtu yule anayeshika sheria. Mtumwa haonyeki kwa maneno matupu, maana ingawa anayaelewa yeye hatayatii. Wamwona mtu apayukaye bila kufikiri? Mtu mpumbavu ni afadhali kuliko yeye. Ambembelezaye mtumwa wake tangu utoto, mwishowe mtumwa huyo atamrithi. Mwenye ghadhabu huchochea ugomvi, mtu wa hasira husababisha makosa mengi. Kiburi cha mtu humporomosha mwenyewe, lakini mnyenyekevu wa roho atapata heshima. Anayeshirikiana na mwizi anajidhuru mwenyewe; husikia laana ya aliyeonewa bila kusema neno. Kuwaogopa watu ni kujitega mwenyewe, lakini anayemtumaini Mwenyezi-Mungu yu salama. Wengi hupenda kujipendekeza kwa mtawala, hali mtu hupata haki yake kwa Mwenyezi-Mungu. Mdhalimu ni chukizo kwa mnyofu, naye mnyofu ni chukizo kwa mwovu.
Methali 29:1-27
"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo43...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa kibali cha kuiona siku hii tena..

Asante Baba yetu, Mungu wetu,Mwokozi,Muumba wetu,Muumba Mbingu na nchi,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..Asante kwa kutuchagua na kutupa nafasi hii tena ya kuendelea kuiona leo hii..si kwa wema wetu,nguvu/utashi,ujuzi wetu Baba bali ni kwa Neema/Rehema zako..
Jana imepita Baba Leo ni siku mpya na kesho ni sikunyingine Mfalme wa Amani tunaomba utawale katika maisha yetu,Roho mtakatifu atuongoze kwenye kunena/kutenda,Ukabariki kazi zetu,Biashara,Masomo Baba,Hatua zetu ziwe nawe,Vyombo vya usafiri na tutembeapo,Tuingiapo/Tutokapo Baba ukawe nasi...
ukatakase vyote tunavyoenda kugusa/kutumia..Ukatutakase Miili yetu,Akili zetu  kwa damu ya Bwana wetu,Mwokozi wetu Yesu Kristo iliyo mwagika kwa ajili yetu..
Baba utusaheme pale tulipokwenda kinyume nawe.. Nasi utupe Neema ya kuweza kusameheana..
Baba ukwaponye/kuwaokoa wote wanaopitia Magumu/mapito,Shida/Tabu,Ukawafungue waliokatika vifungo mbalimbali vya mwovu..ukawaguse na kuwaweka  huru kiroho na kimwili..
Mafalme wa Amani utawale na kuilinda Nchi hii tunayoishi,Baba ukatawale Tanzania,Afrika na Dunia yote..

Ukawaongoze wanaotuongoza wakaongoze katika haki na kweli..

tunarudisha Sifa na Utukufu ni kwako Baba wa Mbinguni..
Tunajiachilia Mikononi mwako Tukiamni wewe ni Bwana na mwokozi wetu
Amina...!!!

Utajiri, hekima na elimu ya Mungu ni kuu mno! Huruma zake hazichunguziki, na njia zake hazieleweki! Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Nani aliyepata kuyajua mawazo ya Bwana? Nani awezaye kuwa mshauri wake? Au, nani aliyempa yeye kitu kwanza hata aweze kulipwa tena kitu hicho?” Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, vyote vipo kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Utukufu na uwe kwake hata milele! Amina.
Tuanze siku/wiki na Mungu...
Mungu aendelee kuwabariki.


Benyamini aenda Misri

1Kisha njaa ilizidi kuwa kali katika nchi ya Kanaani. 2Baada ya kile chakula walichokuwa wamenunua kutoka Misri kumalizika, Yakobo akawaambia wanawe, “Nendeni tena Misri, mkatununulie chakula kidogo.” 3Lakini Yuda akamwambia baba yake, “Yule mtu alituonya vikali, akisema, ‘Sitawapokea msipokuja na ndugu yenu mdogo.’ 4Kama utakubali ndugu yetu kwenda pamoja nasi, basi, tutakwenda kukununulia chakula. 5Lakini iwapo hutakubali aende nasi, basi, hatutakwenda huko, kwani yule mtu alituambia waziwazi, ‘Hamtaniona msipokuja na ndugu yenu mdogo.’” 6Israeli akasema, “Kwa nini mkanitia taabuni kwa kumwambia huyo mtu kwamba mnaye ndugu mwingine?” 7Wakamjibu, “Yule mtu alituhoji kwa makini sana kuhusu mambo yetu na jamaa yetu akisema, ‘Je, baba yenu angali hai? Je, mnaye ndugu mwingine?’ Hivyo tulimjibu kulingana na maswali yake. Tungaliwezaje kujua kwamba atatuambia, ‘Mleteni ndugu yenu?’” 8Yuda akamwambia Israeli, baba yake, “Niruhusu mimi niende naye ili tuondoke mara moja, tuende tukanunue chakula, tusije tukafa njaa pamoja nawe na watoto wetu. 9Mimi mwenyewe nitakuwa mdhamini wake. Wewe utanidai mimi. Nisipomrudisha ukamwona kwa macho yako mwenyewe, lawama na iwe juu yangu milele. 10Kama tusingalikawia, tungalikuwa tumekwisha kwenda na kurudi mara mbili.”
11Hapo Israeli, baba yao, akawaambia, “Haya! Kwa vile ni lazima iwe hivyo basi, fanyeni hivi: Chukueni katika mifuko yenu baadhi ya mazao bora ya nchi yetu, mkampelekee zawadi huyo mkuu. Mchukulieni mafuta kidogo ya mkwaju, asali kidogo, ubani, manemane, kungu na lozi. 12Chukueni fedha mara mbili ya ile inayohitajika, kwa sababu ni lazima mrudishe fedha ile iliyowekwa midomoni mwa magunia yenu; pengine ilirudishwa kwa makosa. 13Mchukueni pia ndugu yenu mwende kwa huyo mtu. 14Mungu Mwenye Nguvu na awajalieni kupata huruma mbele ya mtu huyo, awaachieni yule ndugu yenu mwingine na Benyamini warudi pamoja nanyi. Kwa upande wangu, ikinipasa kufiwa na wanangu basi!”
15Hapo, wakachukua zile zawadi, na fedha mara mbili ya zile za awali, wakaenda Misri pamoja na ndugu yao Benyamini. Walipowasili, wakaenda na kusimama mbele ya Yosefu. 16Yosefu alipomwona Benyamini pamoja nao, akamwambia msimamizi wa nyumba yake, “Wapeleke watu hawa nyumbani, umchinje mnyama mmoja na kumtengeneza vizuri, maana watu hawa watakula nami chakula cha mchana.” 17Msimamizi huyo akafanya kama alivyoagizwa: Akawapeleka wale wageni nyumbani kwa Yosefu. 18Walipoona wamepelekwa nyumbani kwa Yosefu, wakashikwa na hofu, wakasema wao kwa wao, “Tumeletwa huku kwa sababu ya ile fedha tuliyorudishiwa katika magunia yetu tulipokuja safari ya kwanza ili apate kisingizio cha kutushambulia ghafla na kutunyanganya punda wetu na kutufanya watumwa wake.” 19Kwa hiyo wakamwendea yule msimamizi wa nyumba ya Yosefu wakaongea naye wakiwa mlangoni, 20wakamwambia, “Samahani, bwana! Sisi tulikuja hapa mara ya kwanza kununua chakula. 21Tulipofika mahali pa kulala wageni huko njiani, tulifungua magunia yetu, tukashangaa kukuta fedha ya kila mmoja wetu mdomoni mwa gunia lake bila kuguswa. Sasa tumeirudisha fedha hiyo. 22Tumeleta na fedha nyingine kununulia chakula. Hatujui ni nani aliyeweka fedha yetu katika magunia yetu.” 23Yule msimamizi akawajibu, “Msiwe na wasiwasi, wala msiogope. Bila shaka Mungu wenu, Mungu wa baba yenu, ndiye aliyewarudishieni fedha katika magunia yenu. Mimi nilipokea fedha yenu.” Kisha akawaletea Simeoni, ndugu yao. 24Huyo msimamizi alipowakaribisha nyumbani kwa Yosefu, akawapa maji ya kunawa miguu yao, na punda wao akawalisha. 25Nao wakatayarisha zawadi zao za kumpa Yosefu, kwa sababu walisikia kuwa watakula pamoja naye.
26Yosefu, aliporudi nyumbani, wakamletea zile zawadi walizokuwa nazo, wakamwinamia kwa heshima. 27Yosefu akawauliza habari zao na kusema, “Mlinisimulia habari za mzee, baba yenu. Je, hajambo? Angali hai?” 28Wakamjibu, “Mtumishi wako, baba yetu, hajambo na angali hai.” Kisha wakainama kwa heshima. 29Yosefu alipoinua macho yake na kumwona Benyamini, nduguye, mtoto wa mama yake, akasema, “Huyu ndiye ndugu yenu mdogo mliyeniambia habari zake? Mungu na akufadhili, mwanangu!” 30Ghafla, Yosefu akatoka mahali hapo, kwani machozi yalikuwa yanamlengalenga kwa shauku kubwa juu ya ndugu yake, akaingia chumbani mwake na kuangua kilio. 31Baada ya kunawa uso wake, alitoka huku akijikaza, akaamuru chakula kiletwe. 32Yosefu aliandaliwa chakula chake peke yake, na ndugu zake wakaandaliwa peke yao, hali kadhalika na Wamisri waliokula pamoja naye, wakaandaliwa peke yao, kwani ni chukizo kwa Wamisri kula chakula pamoja na Waebrania. 33Ndugu zake Yosefu waliketi mbele yake kulingana na umri wao, kuanzia wa kwanza hadi wa mwisho, wakawa wanaangaliana kwa mshangao. 34Chakula kilikuwa kikichukuliwa kutoka mezani pa Yosefu na kupelekwa kwao, lakini Benyamini alipewa mara tano zaidi ya kiasi walichopewa ndugu zake. Basi, wakanywa na kufurahi pamoja naye.
Mwanzo43;1-34

Bible Society of Tanzania

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.