Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 26 March 2016

Mgombea uwakilishi Marekani William Jawando ahojiwa Kilimanjaro Studio, azungumza na Diaspora


Mgombea uwakilishi katika Bunge la Marekani William Jawando, leo alihojiwa katika studio za Kilimanjaro zilizopo Beltsville, Maryland nchini Marekani ambapo alizungumzia kuhusu mikakati yake katika kuisaidia diaspora ya Afrika katika eneo lake na Marekani kwa ujumla.

Will, ambaye akishinda atakuwa ni mtu wa pili aliyezaliwa na Baba aliyetoka Afrika kuingia bungeni humo (baada ya Rais Obama) ameeleza mambo mengi ikiwa ni pamoja na namna ambavyo uchaguzi mkuu wa mwaka huu ni muhimu Zaidi nchini Marekani, na hasa kwa wakazi wenye asili ya Afrika waishio vitongoji vya Washington DC.

Ikumbukwe kwamba, inakadiriwa kuwa mmoja kati ya wazaliwa kumi wa Afrika walipo nchini Marekani, anaishi eneo hili, na nusu yao, wameingia nchini baada ya mwaka 2000. Hivyo amefafanua namna ambavyo kuwa na mtu mwenye kuelewa na kuwakilisha vema jamii hiyo, ni muhimu kwa jamii hiyo.

Aligusia pia namna ambavyo asili yake na makuzi yake yamechangia yeye kuingia katika kazi za kuihudumia jamii, akaeleza vipaumbele vyake kwenye uongozi wake ujao na pia wito alionao kwa jamii ya waAfrika walioko Marekani.

Uchaguzi wa kuteuliwa kugombea kupitia chama cha Democrat utafanyika Aprili 26, lakini kura za mapema zitapigwa kati ya Aprili 14 na 21.

Kujua mengi kuhusu Will Jawando, maisha yake, kampeni na mipango yake, tembelea willjawando.com

Anagombea kiti kilichoachwa wazi na mwakilishi Chris Van Hollen ambaye ameamua kugombea kiti cha Seneti kinachoachwa wazi na Seneta Barbara Mikulski anayestaafu

Mahojiano kamili na Will Jawando yatakujia hivi karibuni

Baada ya mahojiano, Will alipata nafasi ya kuzungumza na baadhi ya wanaDiaspora wa Afrika waliokuwa ndani ya jengo ilipo studio.

Mgombea uwakilishi kutoka jimbo la Maryland, Will Jawando akipata picha na Mubelwa Bandio baada ya mahojiano
Mgombea uwakilishi kutoka jimbo la Maryland, Will Jawando akizungumza na baadhi ya waAfrika waliohudhuria "Meet & Greet"



Michelle Jawando, mke wa mgombea uwakilishi kutoka jimbo la Maryland, Will Jawando akizungumza machache kuhusu umuhimu wa uchaguzi wa mwaka huu

Mubelwa Bandio akiendelea na maandalizi ya mwisho ya mahojiano na Will Jawando
Mmoja wa wadau wa Kilimanjaro Studio Harieth Shangarai akimpatia maelezo machache Will Jawando
Mgombea uwakilishi kutoka jimbo la Maryland, Will Jawando akiuliza maswali kuhusu uendeshaji wa Kilimanjaro studio
Mubelwa Bandio akitoa maelekezo kwa Will Jawando
Mahojiano yanaendelea

Friday 25 March 2016

Tanzania: Journalists on Gender equality in media



Pili, a journalist at a community radio station, and Saumu, newspaper journalist at Dar-es-Salaam, share their experiences as women working in the media. In an interesting and intimate discussion, the two journalists share their professional path and the obstacles they face every day as women working in the media and come up with potential solutions directly inspired by their own issues.

This interview takes part in the framework of the UNESCO project “Empowering Local Radios with ICTs”, supported by Sweden, aims to strengthen the capacities of local radio stations to improve the quality and variety of their programmes and broadcasts by increasing the use of information and communication technology (ICT) in order to provide poor populations and marginalized groups – in particular women and girls - with access to quality information on issues of local concern and foster their participation in the public debate by increasing the number of women working as journalist or interviewed as sources and experts.

Shukrani/Thanks;UNESCO 

WANAFUNZI WA FEZA BOYS HIGH SCHOOL WATEMBELEA VIRGINIA INTERNATIONAL UNIVERSITY


Wanafunzi wa Feza Boys High School kutoka jijini Dar es Salaam wakipata picha ya pamoja walipokua Virginia International University iliyopo jimbo la Virginia siku ya Alhamisi March 24, 2016, wanafunzi hao wapo kwa ziara maalum ya kuangalia uwezekano wa kujiunga na chuo hicho katika masomo ya juu.
 Makamu Rais wa Chuo hicho Dr. Suleyman Bahceci (kulia) akiwaeleza wanafunzi hao taratibu za kufuata kwa ajili ya kujiunga na VIU
Kushoto ni Alex Luketa Mtanzania anayefanyakazi chuoni hapo kwa ajili ya kusajili wanafunzi kutoka Afrika Mashariki akiwa pamoja na wanafunzi wa Feza Boys High School wakimsikiliza Makamu Rais wa chuo (hayupo pichani) alipokua akielezea wanafunzi hao utaratibu wa kujiunga na masomo VIU.
Wanafunzi wa Feza Boys wakipata mulo.
Mazungumuzo yakiendelea.
 Picha ya pamoja

Thursday 24 March 2016

Jikoni Leo; Mandazi ya kusokota ,Mapishi ya biscuit za karanga,na Sophie's Kitchen...

Wapendwa/Waungwana natumaini mnaendelea nyema na maandalizi ya Pasaka..
Ni Jikoni Leo na mapishi haya yatawasadia kuongezea kwenye maakuli ya Pasaka..
Mapishi haya kutoka kwa "da'Sophie"...

Basi nisiwachoshe na maneno meengi...

Twende sote sasa....






Shukrani;Sophie Kitchen...Zaidi;jitukumbuka63

"Swahili Na Waswahili"Muwe na wakati mwema.




Sunday 20 March 2016

MISA YA KUMBUKUMBU YA JAMES LUHANGA JR, BALTIMORE, MARYLAND NCHINI MAREKANI


Padri Honest Munishi akiongoza misa ya kumbukumbu ya marehemu James Luhanga Jr iliyofanyika siku ya Jumamosi March 19, 2016 katika kanisa la Mt. Edward Baltimore, Maryland nchini Marekani. Marehemu James Luhanga Jr alifariki Februari 3, 2016 mkoani Iringa. Picha na Vijimambo Blog/ kwanza Production.
Ndugu wa marehemu wakipeleka matoleo ya sadaka ya misa ya kumbukumbu ya mpendwa wao James Luhanga Jr.
Wanafamilia wakifuatilia misa ya kumbukumbu ya mpendwa wao marehemu James Luhanga Jr. iliyofanyika siku ya Jumamosi March 19, 2016 Baltimore, Maryland nchini Marekani.
Wanafamilia wakifuatilia misa ya kumbukumbu ya mpendwa wao marehemu James Luhanga Jr. iliyofanyika siku ya Jumamosi March 19, 2016 Baltimore, Maryland nchini Marekani.
 
Pamela (kushoto) na Eliza Madada wa marehemu James Luhanga Jr. wakiwa katika picha ya pamoja kama kumbukumbu ya misa ya kumkumbuka mdogo wao aliyefariki Februari 3, 2016 mkoni Iringa. 
Wakati wa kupata chakula.
Katika picha toka kushoto ni Pamela Luhanga, James Luhanga Sr na Eliza Luhanga.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA