Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 20 March 2016

MISA YA KUMBUKUMBU YA JAMES LUHANGA JR, BALTIMORE, MARYLAND NCHINI MAREKANI


Padri Honest Munishi akiongoza misa ya kumbukumbu ya marehemu James Luhanga Jr iliyofanyika siku ya Jumamosi March 19, 2016 katika kanisa la Mt. Edward Baltimore, Maryland nchini Marekani. Marehemu James Luhanga Jr alifariki Februari 3, 2016 mkoani Iringa. Picha na Vijimambo Blog/ kwanza Production.
Ndugu wa marehemu wakipeleka matoleo ya sadaka ya misa ya kumbukumbu ya mpendwa wao James Luhanga Jr.
Wanafamilia wakifuatilia misa ya kumbukumbu ya mpendwa wao marehemu James Luhanga Jr. iliyofanyika siku ya Jumamosi March 19, 2016 Baltimore, Maryland nchini Marekani.
Wanafamilia wakifuatilia misa ya kumbukumbu ya mpendwa wao marehemu James Luhanga Jr. iliyofanyika siku ya Jumamosi March 19, 2016 Baltimore, Maryland nchini Marekani.
 
Pamela (kushoto) na Eliza Madada wa marehemu James Luhanga Jr. wakiwa katika picha ya pamoja kama kumbukumbu ya misa ya kumkumbuka mdogo wao aliyefariki Februari 3, 2016 mkoni Iringa. 
Wakati wa kupata chakula.
Katika picha toka kushoto ni Pamela Luhanga, James Luhanga Sr na Eliza Luhanga.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Thursday 17 March 2016

TANZANIA RED CARPET YAFANA SEATTLE, WASHINGTON STATE


Mama mitindo Asya Idarous Khamsini (kati) akiwa katika picha ya pamoja na mashabiki wake wa mitindo kwenye usiku wa Tanzania Red Carpet uliofanyika siku ya Jumamosi March 12, 2016 mjini Seattle jimbo la Washington na kuhudhuriwa na Watanzania wanaoishi jimbo hilo na marafiki zao.
Mama mitindo Asya Idarous Khamsini akipata ukodak moment.
Wavaaji nguo za mitindo wakipata picha ya pamoja na mama mitindo Asya Idarous Khamsini.

Tuesday 15 March 2016

Ujumbe wa JWTZ watembelea Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Washington, DC (11 Machi, 2016)

Mhe. Wilson M. Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Washington, DC alikutana na Ujumbe wa JWTZ ulioongozwa na Mkuu wa Tiba Jeshini, Brigedia Jenerali (Dkt.) Denis Raphael Janga, aliyekuwa amefuatana na Mkuu wa Chuo cha Kikeshi cha Tiba - Lugalo, Brigedia Jenerali (Dkt) Robinson Mboni Mwanjela. Wengine ni Mkurugenzi wa Kinga Jeshini, Luteni Kanali Charles Emilio Mwanziva pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wauguzi, Luteni Kanali Lawrence Tia Banda. Ujumbe huo ulikwa na ziara ya Kikazi ya wiki moja hapa Marekani, katika kuendeleza mahusiano baina na JWTZ na majeshi ya Marekani.
 Pichani kutoka kushoto: Col. Adolph Mutta (DA), Brig. Gen. (Dkt) Denis R. Janga, Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi, Brig. Gen. (Dkt) Robinson M. Mwanjela, Lt. Col. (Dkt) Charles E. Mwanziva na Lt. Col. Lawerence T. Banda



HARAMBEE YA KUMCHANGIA MARIAM HUSSEIN YAFANYIKA DMV




Mariamu Hussein akihudhuria harambe ya kumchangia iliyofanyika siku ya Jumamosi Silver Spring, Maryland nchini Marekani na kuhudhuriwa na WanaDMV na marafiki zao. Mariam Hussein nasumbuliwa na ugonjwa wa saratani.


Vitu mbalimbali vilivyoletwa na WanaDMV kwa ajili ya kuvipiga mnada kwenye harambee iliyofanyika siku ya Jumamosi March 12, 2016 Silver Spring, Maryland nchini Marekani.

WanaDMV na marafiki zao waliohudhuria harambee ya Mariam Hussein (wanne toka kushoto) iliyofanyika siku ya Jumamosi March 12, 2016 Silver Spring, Maryland nchini Marekani.
Baadhi ya WanDMV wakiendelea kupata mapochopocho  kwenye harambee ya kumchangia Mariam Hussein (hayupo pichani) iliyofanyika siku ya Jumamosi March 12, 2016 Silver Spring, Maryland nchini Marekani.
Mariam Hussein (kati) akiwa na familia yake kwenye harambee ya kumchangia fedha za matibabu ya saratani iliyofanyika siku ya Jumamosi March 12, 2016
Mnada ukiendelea 
Vitu mbalimbali vilivyoletwa katika mnada wa harambee ya Mariam Hussein uliofanyika siku ya Jumamosi March 12, 2016 Silver Spring, maryland nchini Marekani.
Mariam Hussein (kati) akifuatilia Harambee ya mnada wa kuwezesha kupatikana kwa fedha za matibabu ya Saratani siku ya Jumamosi March 12, 2016 Silver Spring, maryland nchini Marekani.
Picha ya pamoja
Picha ya pamoja
Picha ya pamoja

Sunday 13 March 2016

Wapendwa Natumaini Jumapili ni Njema;Burudani-Anchor - Hillsong Live,My God is Awesome - Charles Jenkins,Break Every Chain (Live) - Tasha Cobbs,


Wapendwa;Ni Jumapili nyingine tena Mungu ametupa kibali cha kuwa pamoja tena....
Natumai wote wazima na jumapili ilikuwa/inaendelea vyema..
Tumshukuru Mungu kwa kila jambo,Hakuna na hatokuwepo kama yeye..

 "Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake."
Neno La Leo;Wagatia:6:1-18
Tuvumiliane na kusaidiana
1Ndugu, kama mkimwona mtu fulani amekosea, basi, nyinyi mnaoongozwa na Roho mwonyeni mtu huyo ajirekebishe; lakini fanyeni hivyo kwa upole, mkiwa na tahadhari msije nanyi wenyewe mkajaribiwa. 2Saidianeni kubeba mizigo yenu na hivyo mtatimiza sheria ya Kristo.3
                      3Mtu akijiona kuwa ni kitu, na kumbe si kitu, huyo anajidanganya mwenyewe. 4Lakini kila mmoja na aupime vizuri mwenendo wake mwenyewe. Ukiwa mwema, basi, anaweza kuona fahari juu ya alichofanya bila kuwa na sababu ya kujilinganisha na mtu mwingine. 5Maana kila mmoja anapaswa kuubeba mzigo wake mwenyewe.
                        Mwenye kufundishwa neno la Mungu na amshirikishe mwalimu wake riziki zake.
7Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna. 8Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu; lakini akipanda katika Roho, atavuna kutoka kwa Roho uhai wa milele. 9Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake. 10Kwa hiyo, tukiwa bado na wakati, tuwatendee watu wote mema, na hasa ndugu wa imani yetu.
                           Mawaidha ya mwisho na salamu
11Tazameni jinsi nilivyoandika kwa herufi kubwa, kwa mkono wangu mwenyewe. 12Wale wanaotaka kuonekana wazuri kwa mambo ya mwili ndio wanaotaka kuwalazimisha nyinyi mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu moja tu: Kusudi wao wenyewe wasije wakadhulumiwa kwa sababu ya msalaba wa Kristo.13Maana, hao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki sheria; huwataka nyinyi mtahiriwe wapate kujivunia alama hiyo mwilini mwenu. 14Lakini mimi sitajivunia kamwe chochote isipokuwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo; maana kwa njia ya msalaba huo ulimwengu umesulubiwa kwangu, nami nimesulubiwa kwa ulimwengu

        15Kutahiriwa au kutotahiriwa si kitu; cha maana ni kuwa kiumbe kipya.16Wanaoufuata mwongozo huo nawatakia amani na huruma; amani na huruma kwa Israeli – watu wa Mungu.
17Basi, sasa mtu yeyote asinisumbue tena, maana alama nilizo nazo mwilini mwangu ni zile za Yesu.
18Ndugu, neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amina.










"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.