Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 20 March 2015

Maisha na Malezi;Mama Mtumwa Wa Mapenzi..!!!


MAMA MALKIA WA UPENDO        💎
                                
💞MAMA MTUMWA WA MAPENZI💞          💎

🌾🍃Mwanadamu ulizaliwa katika hisia za kulia  ukiwa kichanga mwenye uchafu Asili ya upendo ipo kwa mama ulipofumbua macho ulikutana na tabasamu la mama.

🌾🍃Mama alitabasamu wakati unalia mama alijifanya uchizi ili kukufurahisha ghafla ungetokea kuwaona mtoto anapocheza na mama yake ungelidhani wote ni watoto kwa mapenzi ya mama.

🌾🍃Mwanadamu tambua unaweza umizwa na wengi lakini upendo wa mama ukakufanya utulie na hakuna mapenzi ya kweli kwa mtu kama mapenzi ya mama.

🌾🍃Mama juu yako baya likikukuta mama hulia mama yupo tayari kudanganya ulimwengu kukukomboa katika matatizo yako.

🌾🍃Alificha chakula wakati ukicheza udogoni na uliporejea ukamkuta amelala lakini aliacha maagizo utakuta wapo wa kukupashia yote mapenzi.

🌾🍃Mama alipoamka mwanzo alikuulizia ameshakula? Ima umekula atafurahi ima hujala atapita majumba ya watu kukuulizia hata kama atatoka miguu peku yote mapenzi tu.

🌾🍃Ulipoumwa usiku halali atataabika kwa kukaa na wewe ukiwa mikononi mwake huku akilalila ukuta pembeni mwa kitanda huku akitarajia pakikucha shingo limuume kwa kukesha na wewe yote mapenzi hayo.

🌾🍃Mtu yoyote akikupenda watu watamshangaa kwanini anakupenda sana? Lakini mapenzi ya mama hayaulizwi kwanini anampenda yote ni nguvu za hisia za upendo toka kwa mama.

🌾🍃Umekuwa sasa huenda hayupo tena mama amekuacha katika dunia ya mihangaiko na wala tambua hakuna tena kiumbe kitachokupenda kama alivokuwa mama.

🌾🍃Na ukiwa umebarikiwa upendo ulio hai kwako namaanisha uhai wa mama basi huenda amechokaa na anatembea kama mtoto sasa rudisha upendo wako kwa kumfanya nae afurahi japo hutoweza kulipiza yote.

🌾🍃Mama utamkumbuka utapomkosa utatamani kuita mama na hata ukipata wa kuwaita upendo hautatoka moyoni.

🌾🍃Wakati ulipotoka alitabasamu basi na wewe hakikisha wakati anakukimbia duniani mfanye atabasamu hata kama atatokwa na machozi .

🌾🍃Mtumie ujumbe huu Mama na kama hunae tena muombe kwa MOLA upatapo ujumbe huu watumie wenzako huenda wakafufua hisia kwa Mama.

🌾🍃HUYU NDIO MAMA MALIKIA WA UPENDO. 

 🌴🐪KISIWA CHA IMANI🐪🌴


Nimetumiwa na Rafiki Nami nimeileta hapa tujifunze sote.

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Saima.

Wednesday 18 March 2015

Niambie Live Show....Ep1‏


Omby Nyongole, Salma Moshi na Queen Mkelemi
Karibu kwenye kipindi hiki cha NIAMBIE LIVE

Kipindi kinachozungumzia mambo mbalimbali yaliyochukua nafasi za juu kwenye mitandao ya kijamii. Pia kupata Tip ya siku / wiki kusaidia kuboresha maisha yako.

Ni Niambie Live....

KARIBU

Tuesday 17 March 2015

Monday 16 March 2015

NesiWangu Show...Albinism


Karibu katika kipindi cha NesiWangu.

Katika kipindi hiki, Harriet Shangarai amezungumza na wanaharakati wa masuala ya Albinism. Sehemu ya kwanza ni mazungumzo na Daisy Makwaia wa Albino Charity Organization na sehemu ya pili ni mazungumzo yao na mwanaharakati mwenye Albinism Babu Sikare wa Afrobino Ltd

Karibu


Sunday 15 March 2015

Tumalizie Jumapili hii vyema;"Happy Mother's Day"Burudani-Upendo NkoneUpendo wa Yesu..!!!!

Wapendwa;Tumalizie Jumapili hii vyema.
"Happy Mother's Day" mama Rachel-siwa[mama'k]
 na Wamama wote wanao jua majukumu yao kama MAMA.
Mungu awape Busara,Hemakima,Maarifa,Upendo,Furaha,Amani na Maisha marefu.
Pole kwa wenzetu waliopoteza/kufiwa na MAMA ..MUNGU awape uvumilivu ,msiache kufuata  yale yote mema MAMA aliyo waachia.
Wale wanaotafuta Watoto MUNGU akaonekane na awabariki nanyi mpate watoto.
MUNGU azidi kutubariki katika malezi.


1Je, maisha yenu katika Kristo yanawapeni nguvu? Je, upendo wake unawafarijini? Je, mnao umoja na Roho Mtakatifu na kuoneana huruma na kusikitikiana nyinyi kwa nyinyi? 2Basi, ikamilisheni furaha yangu kwa kuwa na fikira moja, upendo mmoja, moyo mmoja na nia moja.

Neno La Leo;Wafilipi 2:1-30

Unyenyekevu na ukuu wa Kristo

1Je, maisha yenu katika Kristo yanawapeni nguvu? Je, upendo wake unawafarijini? Je, mnao umoja na Roho Mtakatifu na kuoneana huruma na kusikitikiana nyinyi kwa nyinyi? 2Basi, ikamilisheni furaha yangu kwa kuwa na fikira moja, upendo mmoja, moyo mmoja na nia moja. 3Msifanye chochote kwa moyo wa fitina au kwa majivuno ya bure; muwe na unyenyekevu nyinyi kwa nyinyi, na kila mmoja amwone mwenzake kuwa bora kuliko yeye mwenyewe.4Pasiwe na mtu anayetafuta faida yake mwenyewe tu bali faida ya mwenzake. 5Muwe na msimamo uleule aliokuwa nao Kristo Yesu:  6Yeye, kwa asili alikuwa daima Mungu;lakini hakufikiri kwamba kule kuwa sawa na Munguni kitu cha kungangania kwa nguvu.7Bali, kwa hiari yake mwenyewe,aliachilia hayo yote, akajitwalia hali ya mtumishi,akawa sawa na wanadamu,akaonekana kama wanadamu.8Alijinyenyekesha na kutii mpaka kufa,hata kufa msalabani.9Kwa sababu hiyo Mungu alimkweza juu kabisa,akampa jina lililo kuu kuliko majina yote.10Ili kwa heshima ya jina la Yesu,viumbe vyote mbinguni, duniani na kuzimu,vipige magoti mbele yake,11na kila mtu akiri kwamba Yesu Kristo ni Bwana,kwa utukufu wa Mungu Baba.




"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Saturday 14 March 2015

PAZI REUNION HOUSTON, TEXAS LEO KUWAKA MOTO WACHEZAJI WENGI NDANI YA NYUMBA‏



 Timu ya Pazi wanaume wakipata picha ya pamoja na mashabiki wao walipokua nyumbani kwa madikodiko ambaye pia ni mmoja wa waratimu wa tamasha hili la kumbukumbu ya timu hiyo iliyowika miaka mingi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Tamasha hili lililobeba jina la Pazi Reunion litafikia tamati leo Jumamosi March 14, 2015 kwa mechi kadhaa na kuakumbuka na kuaenzi viongozi na wachezaji wa timu hiyo waliotangulia mbele ya haki.
 Pazi Queens wakiwa katika picha ya pamoja leo patakua hapatoshi.
Patrick Mwigula kutoka South Carolina na Atiki Matata kutoka Uingereza wachezaji wa Pazi waliowika miaka ya nyuma wakijadili mchezo wa leo kama walivyokutwa na kamera ya Vijimambo.
 Atiki Matata na Richard Kasesela wakipata picha ya pamoja.
Kulia ni Masawe shabiki wa Pazi wa miaka mingi si mazoezi si mechi alikua hakosekani uwanjani hapa akisalimiana na Richard Kasesela mara tu walipoonana baada ya kupoteana kwa miaka mingi.
Kutoka kushoto ni Emmanuel, Patrick na Kasesela wakikumbushana enzi zao za Pazi.
Wachezaji wa Pazi toka shoto ni Vitalis Gunda toka Maryland, Richard Kasesela toka Tanzania na Willy Crrusa toka Houston, Texas wakikumbushana enzi zao.
Kwa picha zaidi Bofya HAPA