Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 25 April 2014

Maandalizi ya sherehe za Muungano Washington DC‏





Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico Mhe. Liberata Mulamula akizungumzia maandalizi ya sherehe za miaka 50 ya muungano ofisini kwake Washington Dc Jumatano, Aprili 23, 2014.
Photo: Sunday Shomari

Thursday 24 April 2014

Mswahili wetu Leo;Da'Faiza wa Fabuloustaa!!!!!!!

Mswahili wetu Leo ni  da'Faiza Omar.
Binti huyu ni Blogger na ana mambo meengi mazuri
Kumjua zaidi Karibu sana kwenye Blog yake.

Mtembelee hapa;http://fabulousfaa.blogspot.co.uk

Tuesday 22 April 2014

Mazungumzo na Dr Patrick Nhigula kuhusu Bunge maalum la Katiba‏





Karibu katika mazungumzo na Dr Patrick Nhigula kuhusu mwenendo wa Bunge Maalum la Katiba na mwenendo mzima wa nchi ya Tanzania.
Huu ni mfululizo wa mazungumzo na watu mbalimbali kuhusu suala hili muhimu kwa mustakabali wa nchi ya Tanzania.
Karibu

Kwa maoni, tafadhali wasiliana nasi kwa barua pepe kwanzaproduction at gmail dot com

Saturday 19 April 2014

Shukrani/Asanteni Wote na MUNGU awabariki Sana!!!!


Salaam Waungwana;

Tunamshukuru MUNGU mwenyeezi kwa yote.
Tunamshukuru MUNGU kwa maisha ya Mama/Bibi yetu mpendwa Khadija Mgaya Chuma[bibi Mwalimu].
Tunamshukuru MUNGU kwa kufanikisha vyema,Mazishi ya Mpendwa wetu.
Bi Khadija alifariki usiku wa Jumanne na Kuzikwa siku Alhamisi katika Makaburi ya Ilala Mchikichini.Dar.
Mama Kiwinga na Familia yake,Wanawashukuru sana Ndugu,Jamaa,Marafiki,Majirani na Wote walioshiriki kwa Michango,Muda,Upendo,Faraja, Sala/Dua na Mengineyo.
MUNGU azidi kuwabariki na kuwaongezea kila lililo jema kwenu.

Wenu Mama Kiwinga
Wa Ilala Sharifu/Shamba.

Asante Sana.


"Swahili Na Waswahili" Tunawashukuru wote katika yote.

Sunday 13 April 2014

Nawatakia JumaPili Njema;Burudani-Molimo na Nzambe yaka/Nitakushukuru,Mungu ni mwema/Kombo nayo ekumama ,Kutoka kwa- Feza Shamamba Hosseya

Wapendwa;Nawatakia JumaPili yenye Unyenyekevu,Upole,Uvumilivu,Upendo na Umoja....

Kwahiyo nawasihi,mimi niliye mfungwa katika BWANA,Mwenende kama  inavyoustahili wito wenu mlioitiwa;
Kwa unyenyekevu wote na upole,kwa uvumilivu,mkichukuliana katika upendo.

Neno La Leo;Waefeso:4:1-16
3.Na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4.Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.
5.BWANA mmoja,imani moja,ubatizo mmoja.
6.MUNGU mmoja,naye ni BABA wa wote,aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote.
7.Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo. 






"Swahili Na Waswahili"MUNGU Atubariki Sote.

Saturday 12 April 2014

[AUDIO]. DAKIKA 90 ZA DUNIA: Maadhimisho ya Kwibuka20, Washington DC‏


 Wiki
kama hii, miaka 20 iliyopita, nchi ya Rwanda ilishuhudia kuanza kwa
mauaji ambayo kwa siku 99 zilizofuata, yaliacha historia mbaya na ambayo
itaendelea kukumbukwa na vizazi vijavyo.
Ndani ya siku 100, watu wanaokadiriwa kufika milioni 1 waliuawa katika mauaji ya kimbari.
Miaka
20 baadaye (mwaka huu), dunia nzima imeungana na Rwanda kukumbuka kile
ambacho wengi wanaona kuwa kilitokea na kuachwa kuendelea kutokana na
Jumuiya ya kimataifa kutoingilia kati na kutoa msaada muafaka kwa wakati
muafaka.
Kumekuwa na matukio mbalimbali kukumbuka mauaji ya kimbari
ya Rwanda ambayo yamefanyika duniani kote, Kutoka Kigali Rwanda mpaka
hapa Dar-Es Salaam na hata huko Washington DC.



Hii ni sehemu ya
ripoti ya Kwanza Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA
kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam
Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).