Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 18 January 2013

Watoto na Shangwe;Leo ndani ya Coventry ipo hivi!!!!!!!













Waungwana;Leo hali ya hewa Coventry ipo hivi...Lakini watoto wanafurahi sana....
Kwetu Bongo tunacheza kwenye Mchanga.....huku wacheza kwenye Snow!!!!!!!!
Baadhi ya Shule zilifungwa  mapema Leo.

Swali la Kizushi;Kule Nyumbani nilikuwa nasikia kuna Ugonjwa wa Ngiri kwa wanaume, Wakati wa Mvua/Baridi hasa Pwani.Jee waliokuwa wanaumwa huko Nyumbani Wakija huku wanapona?

"Swahili NA Waswahili" Pamoja sana.

Thursday 17 January 2013

SIMANZI KUBWA; JUDITH CHIKAKA AWALIZA CHUO KIKUU CHA ARDHI, WAFANYAKAZI WENZAKE WIZARA YA ARDHI, WANA CCM TEMEKE, CHAMA CHA WANARIADHA TANZANIA, MUMEWE ERASTO MAPUNDA NA WANAMICHEZO KWA UJUMLA.



Marehemu Judith Chikaka Mapunda enzi za uhai wake.


Mwili wa Judith Chikaka ukiwa umelazwa ndani ya Jeneza Pamoja na mwili wa marehemu Mtoto wake mchanga.
Marehemu Judith Chikaka alifariki siku ya Jumapili  ya tarehe 13/01/2012 katika Hospitali ya Mwananyamala wakati alipofikishwa hapo kwa ajili ya kujifungua, kwa bahati mbaya na mapenzi yake muumba alifariki kabla ya kujifungua.


Mume wa Marehemu Judith, Bwana Erasto Mapunda akiwa amembeba mtoto wake wa kwanza aliyezaa na mkewe.
Baba mzazi wa marehemu Judith, Mzee Chikaka

Mama mzazi wa marehemu Mama Chikaka sakiwana majonzi makubwa baada ya kumpoteza mtoto wake kipenzi

Padre kutoka Parokia ya Kigamboni akiendesha Ibada ya misa takatifu ya kumwombea Judith alale kwa amani. Ibada hiyo ilifanyika nyumbani kwa Marehemu Judith maeneo ya Kigamboni Kibada.
Baadhi ya viongozi wa CCM Temeke wakitoa rambi rambi zao.
Spika wa Bunge la wanafunzi wa chuo cha Ardhi akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya wanafunzi wenzake.
Rais wa Chama cha Riadha Tanzania Bwana S. Nyambui akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya wanachama na chama chao kwa ujumla.
Mume wa marehemu Judith akiweka Shada la maua katika nyumba ya milele ya mkewe
Kushoto ni mwakilishi wa Familia ya marehemu akipokea rambi rambi kutoka kwa wafanyakazi wenzake wa marehemu kutoka wizara ya Ardhi
Mwakilishi kutoka Wizara ya Ardhi upande wa michezo akitoa salamu zake kwa niaba ya wanamichezo wenzake.

Hii ndio nyuma ya milele ya marehemu Judith Chikaka Mapunda.

Marehemu Judith  alizikwa jana katika makaburi ya Kibada maeneo ya Kigamboni, ameacha Mume na Mtoto mmoja.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEME MAHALI PEMA PEPONI.
AMIN.


"Swahili NA Waswahili" Inawapa pole wafiwa na wote walioguswa na Msiba huu.

Wednesday 16 January 2013

Siku Kama Ya Leo Kaka Simon kitururu Alizaliwa!!!!

Kitururu na Utaifa..
Kitururu utotoni na wazazi..
Mtoto  Max ....ni Zawadi Kubwa kwake..... kitururu 
Kitururru..Baba Max na Ulezi..
Kitururu Mawazoni...Ametulia......

Kitururu na Mapishi....
Simon wa Kitururu Mitaani...


Waungwana;Siku kama ya Leo,Kaka Simon Kitururu,Babake Max....Muzee wa Yeah...kaka Kadoda.......duuhh Majina mengine atakuja kumalizia kaka  Ihayabuyaga Chacha O' Wambura.

Tunakutakia kila la kheri na Baraka Maishani mwako.Uwe na Wakati Mzuri Leo na Siku zote!!!!!

Swali La Kizushi...Unamfahamu /Kufikiri  ni Mtu wa Aina Gani  kaka Simon Kitururu? 

kujua zaidi kuhusu kaka huyu ingia;http://simon-kitururu.blogspot.co.uk/


"Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana.

Watoto Na Malezi;Child Prostitution - South Africa!!!!







Waungwana;Watoto wetu ni Wapendwa wetu!!!!..Janga la Dunia...Nani wa kulaumiwa?

Mtoto wa mwenzio ni Wako au Mtoto wa mwenzio mkubwa Mwenzio?

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana.


Monday 14 January 2013

Siku kama Ya Leo Kaka Isaac Alizaliwa!!!!!!

Siku kama ya Leo miaka kadhaa ilitopita, kaka ISAAC, babake Sandra na Tracey,Mume ya Madame Rachel.... Alizaliwa!!!!!

Tunakutakia kila lililojema Maishani, MUNGU azidi kukulinda na kukubariki kila iitwapo Leo.Akujaalie miaka mingi  yenye Amani,Furaha,Upendo na Upole Kiasi.. Ufanikishe Malengo yako na Uzidi kuwa Baraka kwetu na kwa Jamii.

 Na Iwe kama Tulivyo NENA.
AMEEEEEN!!!!!!!!!!!

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.



Sunday 13 January 2013

Tumalizie J'Pili Vyema na Amani;Burudani-Solomon Mukubwa na Ambassadors of Christ!!!!




Wapendwa Natumaini mlikuwa na J'Pili Njema..kama kuna iliyokuwa na vikwazo,shida na Tabu..Mtegeemee MUNGU!!
Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake,Aliwaambia Enyi wazao wa nyoka,ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?

Neno La Leo;Mathayo Mtakatifu:3:1-17:Na tazama,sauti kutoka mbinguni ikisema,Huyu ni Mwanangu,mpendwa wangu,ninayependezwa naye.

   "Swahili NA Waswahili" Neema na Baraka za MUNGU  ziwe Nanyi Daima.

Saturday 12 January 2013

Chaguo la Mswahili Leo;Kutoka kwa Mdau -Image Profession;Burudani-Question:J.Kassam Ft. Ivan!!!!!!

 Mwimbo mwingine wa mwanamuziki chipukizi Juma Kassam akisindikizwa na Ivan ,anakuja kivingine 

akiuliza swali"Question",ni zaidi ya ubunifu.


Muelekeo mpya zaidi ya vile tulivyozoea ya nyimbo zenye ujumbe wa mapenzi.





"Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana.