Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 19 November 2012

Kisa Cha Leo na Mswahili Emu-3-Uchungu wa Mwana Aujuaye Mzazi;Sehemu ya 25!!!!!!



Kwa marejeo: Kais alipohisi kuwa huyo mwanaume, aliyemuona na yule mwanamke, ni askari wa mzee Hasim, alikimbia….., je alikimbilia wapi, na huko alipokwenda aliishia wapi, ukumbuke kuwa binti huyo alikuwa mja mzito, je ujauzito wake uliishia wapi….tuendelee sehemu hiyo ya Kaisi……..

Kais, alipozindukana alijikuta yupo kwenye kitanda, na wakati hupo tumbo lilikuwa likimuuma sana, na harufu aliyoisikia hakuwahi kusikia kabla, akageuza kichwa huku na kule, lakini hakuona mtu kwa upeo wa mcho yake. Akainua kichwa na , kwa mbali akaona watu wamevaa nguo nyeupe, moyoni akajua ni malaika, akakumbuka hadithi alizowahi kusimuliwa za malaika kuwa ni wao ni weupe, na kwasababu hawana dhambi, kila kitu chao ni cheupe.

‘Ina maana nimeshakufa nipo mbinguni,…nipo peponi na malaika’akawaza na kabla hajaweza kuinua kichwa vyema, mara akahisi kuna watu wameshikilia miguuni yake, na sauti zikawa zinaongea, mmoja akasema,;

‘Huyu tusipomfanyia upasuaji, tunaweza tusiwaokoe wote’

Kais akawaza hawa malaika wanataka kumfanya nini, kumfanyia upasuaji, haiwezekani, kwao hakuna kitu kama hicho, wanaamini kuzaa ni kwa njia ya kawaida tu, kuna dawa unakunywa, na haichukui muda kujifungua, na kabla hajajua nini kinachoendelea, akahisi tumbo likaanza kumuua, liliuma sana, maumivui ambayo hakuweza kuyavumilia akaanza kupiga ukulele.

Mmoja wa wale, watu ambao yeye aliwaona kama malaika, wakaja na kumshika vyema, na mmoja akawa kashika sindano,..Kais aliogopa sana, lakini hakuweza hata kujitetea, kwani mwili ulikuwa hauna nguvu hata ya kuinua mkono, kutokana nay ale maumivu, akapigwa sindano, ambayo ilimfanya atulie, na kuzama kwenye giza, …alipozindukana akasikia kitoto kikilia..

‘Mtoto wako mnzuri ana afya njema,..’ akaambiwa, na alipogeuza kichwa pembeni, akaona kitoto kimelazwa kwenye kitanda kidogo pembeni yake. Kilikuwa cheupe, kizuri, akatabasamu, na akainua mkono na kukishika. Baadaye aliwageukia wale watu ambao kipindi cha nyuma aliwaona kama malaika, lakini sasa akili ilikuwa imetulia, na ile hali ya mwanzo aliiona kama ndoto, akasema; kusoma zaidi ingiahttp://miram3.blogspot.co.uk/


"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima

Sunday 18 November 2012

Nawatakia J'Pili yenye Nuru;Burudani-Bahati Bukuku - Yehova na Nyingine Nyingiii!!!!!



Wapendwa;Nawatakia J'Pili yenye Nuru na Neema.

Ondoka,uangaze;kwa kuwa Nuru yako imekuja,Na utukufu wa BWANA umekuzukia.

Neno La Leo ISAYA:60:1-6;Maana tazama,giza litafunika Dunia,Na giza kuu litazifunika kabila za watu;Bali BWANA atakuzukia wewe,Na utukufu wake utaonekana juu yako.


"Swahili NA Waswahili" Mbarikiwe Woooote.

Friday 16 November 2012

Jikoni Leo;Tupike Pamoja-Mapishi ya Country salad - Recipe of (Swahili)!!!!!!

Waungwana;"Jikoni leo" si wengine ni "Tupike Pamoja," Walipotea kidogo lakini waswahili wanasema kinya kingi kina.............basi wamerudi tena kwa kishindo.

Nisiwachoshe kwa maneno meeengi.Fuatana nasi katika Pishi la Leo ni "Country Salad" ...

Haya mambo hayo...ukitaka kujua zaidi usisite ingiaTupike Pamoja au www.tupikepamoja.com            

"Swahili NA Waswahili"Karibuni Woote!!!
 

Thursday 15 November 2012

Wa-Afrika na Sherehe zao;Leo Ma-Arusi wa Leo wanavyo Jimwaga!!!!!

S n W
Waungwana; vipi Maarusi wa leo wanavyojimwaga/cheza,changamka? inapendeza au inachukiza? 

Ma-Arusi wa Leo wanafuraha sana na wanajimwaga vilivyo, yaani wanaonyesha furaha zao kabisa na ukichukulia siku kama hizi hazijirudii.
Unafikiri kwanini wanakuwa hivi jee, wamechaguana wenyewe,wanakwenda na wakati,hawana Aibu,wamengojea kwa muda mrefu kuwa MKE/MUME au............?

Vipi wa zamani ni kilio mtindo mmoja jee wengi wao wamelazishwa,Upweke wa kuwa mbali na familia,Furaha iliwazidi,Kutojuana/kuchaguliwa,wali-Olewa/Oa wakiwa wadogo  Au......?

"Swahili na Waswahili" Karibuni woooote!!!!!!

Monday 12 November 2012

Da'CHIKU ETUTU'S BABY SHOWER,Waalikwa[2]!!!!


                                          Da'Chiku MUNGU alikuingiza vyumba vyote....Mrembo mke wa Etutu!!

















Wapendwa mmetokelezea/Pendeza sana na MUNGU awape Moyo wa ushirikiano Daima na Mapenzi.
                                        Swahili na Waswahili Tunakutakia kila lililo Jema na Baraka.MUNGU azidi kuwabariki  katika Uzao wenu.
Bibi na Bwana ETUTU..Wanawashukuru Wooote.
         Picha na Mpiga wetu Bai mwana wa Mussa,Shukrani Mingi.

Mapenzi Na Wapenzi;Burudani-Ali Kiba-MAPENZI YANA RUN DUNIA - Diamond na KIZAIZAI!!!!

Waungwana;" Mapenzi na Wapenzi".Mapenzi ni Raha Karaha?  jee Unampenda uliye naye au Unajikaza tuu ili siku ziende?

 kwanini  baadhi ya Wanawake wengi wanalaumiwa na baadhi ya waume zao eti wakisha zaa/kupata mtoto Mapenzi yanapungua kwa MUME?

 Jee kuna ukweli au Wanaume wanawivu hata kwa Watoto wao?

Karibu sana kwa Maoni/Ushauri na kuelimishana kwa Upendo.

Diamond anasema.....Kizaizai oohh Mapenzi yanauma eee nyie Mapenzi karahaaa Kizaizai.........
Ali Kiba anatuambia
......aaa aEeehhh eeeooohh ....Unatema BIG kwa Karanga za Kuonjeshwaaaa..Mapenzi yana Run Duniaaaaaa..

Mhhhhhh wewe UNASEMAJEE........

 
"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima
.
S n W

Sunday 11 November 2012

Wanawake Waswahili Wa Coventry Wamtakia Kheri na Baraka;Mpendwa wao-Chiku Etutu's Baby Shower!!!!!![1]

           Mwenyewe da'Chiku katika pozi mwanana.



Pozi tofauti mama Kitumbo!

              Mikeki 
                  Kula baba kama si wewe nisingeitwa mama..
                        Kula mama kama si wewe nisingekuwa baba......






                      Zawadi na mkono wa kheri na baraka kutoka kwa Waungwana.....[Eeehh dada yangu unavisa wewee wapi Nana]hahahaaaa
k
Kamati ya Shughuli hii,Mnatishaaaa Cov Mamazzzzzzzz[WWWCUK]
              Picha na Mpiga Picha wetu BAI Mwana wa Mussa mamaaa ya Cov..

Usicheze mbali picha zitaendeleaa nani kavaa nini na nani alikuwepo nani katokelezeaaaaa?

       "Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.