Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 17 August 2012

Kisa cha Leo ni Emu-Three na Mbio za Sakafuni,Huishia Ukingoni!!!!


Mbio za sakafuni,huishia ukingoni 4

Waungwana leo nimewaletea Mswahili; Emu-Three na Diary Yangu[Yake]
ANASEMA;Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za maisha 
(diaries), 
visa na matukio na yale unayopenda kuchangia na wenzako (mijadala),
 maneno ya hekima,
 kusaidiana na pia kutoa dukuduku lako (kilio chako). 
Soma na uchangie chochote kwa 
kutoa maoni (comments) yako,
 au tutumie kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

Tupitie Kisa hiki kidogo, hii ni Sehemu ya 4:Kila mfanyakazi tunayemchukua hakai hapa nyumbani, sasa nimechoka kabisa kutafuta mfanyakazi wa nyumbani, naona ni heri nijifanyie kazi zangu mwenyewe, kwanza nililelewa kama mfanyakzia wa nyumbani…’akasema mke wangu.

Kipindi hicho maisha yetu yapo juu, tuna kila kitu, …lakini maisha ya ndani yalikuwa na mitihani yake, na ilionyesha wazi kuwa tulihitaji msaidizi, ili na yeye apate muda wa kufuatilia miradi yetu.Niliinuakichwa na kumtizama kwa macho ya huruma,maanaalikuwa mtu wa pilikapilika, shughuli zandani, shughuli zamiradi, shughuli za kijamii, zote alikuwa akijitahidi kujumuika nazo.

Nilimwangalia na kutabasamu, na hapo nikakumbuka siku za nyuma, wakati akiwa binti, wakati nampigania kumpata, ilikuwa kama kampeni za siasa ambazo nilikuwa nikipambana nazo, na hata siku anaingia kwangu kama mke wangu sikuamini.
‘Unanikumbusha mbali sana mke wangu, sijui kama ningekukosa ingelikwuaje…’nikasema.Inaendelea;kuanzia Sehemu ya 1-hii ya 4 na Kuendelea na Kisa hiki ingia;http://miram3.blogspot.co.uk
Mpendwa Unalolote la kuongezea kwa mwandishi huyu?Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.Karibu sana.


Hongera sana Emu-Three kwa Kazi zako,Mungu Azidi kukubariki sana sana kwa Kazi za Mikono yako na kila lililo Jema.Tunakutakia Swaumu Njema!!!!!

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Thursday 16 August 2012

FFU wa Ngoma Africa band na Mashambulizi yao Tubingen,Ujerumani!!!!!













FFU wa Ngoma Africa band  imewasha moto,TUBINGEN
  
Wamechukua Tuzo ya "IDA-International Diaspora Award"

Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya,Ngoma Africa Band
Siku ya Jumamosi 11.8 .2012 walishambuli jukwaa na la
International Africa Festival 2012,Tubingen,Ujerumani,
na kuhakikishia washabiki kuwa FFU ni tishio la kimataifa !
Kiongozi wa bendi Ras Makunja alikabidhiwa Tuzo ya kimataifa ya
"International Diaspora Award" kwa niaba ya bendi hiyo.

The Ngoma Africa Band

Wednesday 15 August 2012

Jikoni Leo; Mswahili alilifuata Mtaani;Burudani-MIRIAM MAKEBA - Pata, Pata!!!

  Huu ulikuwa Mchanganyiko[Msetoo], Mchele,spaghetti,Karoti naaaNjegere yaani kama Biliyani,Pilau. haa hhaaaaaa [Mchanyatooo]

 Huyu alipika Nyama iliyochanganywa na Majani siyajui, Ndizi na vingine vingi kama Tulavyo Waswahili lakini Michanganyo yake tofauti kidogo.[Jamaica]


 Hawa waliandaa OLIVE Kwa radha Tofauti, hii mimi nilitaka kurudisha Chenji[sikuweza kumeza]

 Hii ni Nazi, hiyo Nyeupe kabla haija Okwa, hii ya chini imeOkwa nilipenda sana.

 Hawa walitengeneza/kupika kutumia Tambi[Noodles]Ngano na Viungo vya kwao....


 Hawa walitumia Ngano zaidi.Mmmhhh Ngano ina mambo meeengi sana!!

 Waungwana;"JIKONI  LEO"Lilikuwa Mitaani kuona,kujifunza,kuonja tusivyovijua/Mapishi ya watu wa Nchi Mbalimbali.
Kulikuwa na mambo meengi, Leo tuanze na Jikoni.Kuonja ilikuwa Bureeeee ,Duhh nilionja mpaka nilichoka Mmmmhh vingine havionjeki. Nafikiri ni Mazoea ya Vyakula.
Nazi ilitengenezwa kivingine,Ngano ambayo mimi nimezoea kwa Maandazi,Chapati na vitu vichache vya Kiswahili, nayo ilipikwa kivingine.
Duuhh sijui nianzie wapi niishie wapi,wewe kula kwa picha tuu.MCHELE MMOJA Mapishi Mbali mbali..........

Yote tisa Chakula cha Waswahili Hakikuwepo,Sikujua kwa nini labda hawakuwa na Taarifa au Mwezi Mtukufu waliona walaji Wachacheeeee!!
Katika Kutembea watoto wakaniita Mama tumeona Banda la ZANZIBAR!!!!!!Lakini Tumemsalimia kwa KISWAHILI Amecheka tuu,Tukamsalimia kwa Kiinglishi[ENGLISH] Ametujibu.Nilipofika hapo nikakutana na Muhindi Amezaliwa KENYA naye anamuuliza kama ametokea TANZANIA?Kwa KISWAHILI,Duhhh kaka Muuzaji alichekaaaaa.Akasema hajui hiyo Lugha yeye anajua hiyo kitu ZANZIBAR na MASAI Tuu.Baada ya kuongea Nae Akasema yeye ni MJAMAIKA[JAMAICAN] Hupenda kujifunza Mapishi na Mambo ya Nchi Tofauti.

Mimi nikamsalimia MUHINDI Tuka chapa SWAHILI YETU  na TUKAFURAHI.

Jee Unalolote la Kuongezea kuhusu kwanini WASWAHILI Kutokuwepo/Kutokuwa na Banda hapo?
Uoga,Kutojiamini,Hatupendi kujitangaza,Hatuna Muda/Nafasi ,Mwezi Mtukufu,Hatufuatilii nini kinaendelea Sehemu Tunayo Ishi ...AU?
Karibuni sana kwa Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

 Hii ilikuwa; COVENTRY.U.K.
 "Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.


Tuesday 14 August 2012

Siku kama ya Leo da'Leyla Kiwinga Alizaliwa;Burudani-Lady Jaydee - Shamba!!!!!




 Siku kama ya Leo,Familia ya Bibi na Bwana M.S.Kiwinga Walipata Mtoto wa kike na Wakamwita LEYLA.
Naye ndiye Funga Dimba[Mtoto wa Mwisho] wa Familia hiyo.
Da'Leyla Tunakutakia kila lililo Jema Maishani.MUNGU Azidi kukubariki na kukulinda kila iitwapo Leo.Akupe sawaswa na Mapenzi Yake,Uwe baraka kwa Watu Woote.

Pamoja Sana. MUNGU NI PENDO



Sunday 12 August 2012

Nawatakia J'Pili Njema,Burudani;Usinipite Mwokozi -Lydiah Joy Kaimuri;Sarah k-Niinue;Unibariki-Hellen Ken!!!!

Wapendwa Nawatakia J'Pili yenye Upendo,Amani na Furaha.

Nanyi mkiwa katika kusali,msipayuke-payuke,kama watu wa mataifa,maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa Mengi.

Neno la Leo;Mathayo Mtakatifu:6;7-13.

MUNGU Atubariki Sote.

Saturday 11 August 2012

Chaguo la Mswahili Leo;[Mambo ya Pwani]Top in Town -Khadija Koppa,Omar Koppa;Nifagilieni na Kitchen Party!!!


Malkia wa Mipasho,Khadija Koppa.

Waungwana;
 "Chaguo la Mswahili Leo"Mambo ya Pwani,Taarab/Rusha Roho!!Mmmmhh lakini usitoe Roho.Sina Maneno Meeengi Sikiliza mwenye mambo yao.
Mnasema ToT Kimeo Mbona Mnachezaaa?Pisha Njia pisha Njiaaa....Tarararar eehh Tararaa Wacha weeeeh...tehthetheteh

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Thursday 9 August 2012

Mapishi ya Chicken and pinneaple salad with pink sauce na Mapishi ya Chicken with avocado Sauce- Recipe of (Swahili]!!

Waungwana "JIKONI LEO" SI Wengine ni "da'SOPHI" na "Tupike Pamojaa".
Leo Mapishi ni kuku kwa Nananasi NA Kuku kwa Parachichi.Mmmmmhhh Tamu Saaaana.

Hivi vitu tunavyo sana Nyumbani lakin jee wote tulikuwa tunajua jinsi ya Matumizi Tofauti  AU Ulikuwa unajua ni MaTunda tuu?

Una Swali au Maoni?Usisite kumuuliza. Kujua Zaidi usiache kutembelea.Tupike Pamoja.

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daimaaaa!!!!!!