Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday, 9 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 14...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

“Mimi siwezi kufanya kitu kwa uwezo wangu mwenyewe. Mimi ninahukumu kama ninavyosikia kutoka kwa Baba, nayo hukumu yangu ni ya haki. Nia yangu si kufanya nipendavyo mwenyewe, bali apendavyo yule aliyenituma.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Nikijishuhudia mimi mwenyewe, ushahidi wangu hauwezi kukubaliwa kuwa wa kweli. Lakini yuko mwingine ambaye hutoa ushahidi juu yangu, nami najua kwamba yote anayosema juu yangu ni ya kweli.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Nyinyi mlituma ujumbe kwa Yohane naye aliushuhudia ukweli. Si kwamba mimi nautegemea ushahidi wa wanadamu, lakini nasema mambo haya ili mpate kuokolewa.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake,
lakini mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2Mwenye mwenendo mnyofu humcha Mwenyezi-Mungu,
lakini mpotovu humdharau Mungu.
3Mpumbavu hujiadhibu mwenyewe kwa kuropoka kwake,
lakini mwenye hekima hulindwa na maneno yake.
4Bila ng'ombe wa kulima ghala za mtu ni tupu,
mavuno mengi hupatikana kwa nguvu ya ng'ombe wa kulima.
5Shahidi mwaminifu hasemi uongo,
lakini asiyeaminika hububujika uongo.
6Mwenye dharau hutafuta hekima bure,
lakini mwenye busara hupata maarifa kwa urahisi.
7Ondoka mahali alipo mpumbavu,
maana hapo alipo hamna maneno ya hekima.
8Hekima ya mwenye busara humwonesha njia yake,
lakini upumbavu wa wapumbavu huwadanganya wenyewe.
9Wapumbavu huchekelea dhambi,
bali wanyofu hupata fadhili kwa Mungu.14:9 aya ya 9 makala ya Kiebrania si dhahiri.
10Moyo waujua uchungu wake wenyewe,
wala mgeni hawezi kushiriki furaha yake.
11Nyumba ya mtu mwovu itabomolewa,
lakini hema ya wanyofu itaimarishwa.
12 Taz Meth 16:25 Njia unayodhani kuwa ni sawa,
mwishoni yaweza kukuongoza kwenye kifo.
13Huzuni yaweza kufichika katika kicheko;
baada ya furaha huja majonzi.
14Mtu mpotovu atavuna matunda ya mwenendo wake,
naye mtu mwema atapata tuzo la matendo yake.
15Mjinga huamini kila kitu anachoambiwa,
lakini mwenye busara huwa na tahadhari.
16Mwenye hekima ni mwangalifu na huepa uovu,
lakini mpumbavu hajizuii wala hana uangalifu.
17Mwenye kuwaka hasira haraka hutenda kipumbavu,
lakini mwenye busara ana uvumilivu.
18Wajinga hurithi upumbavu,
lakini wenye busara hutuzwa taji ya maarifa.
19Waovu watapiga magoti mbele ya watu wema,
watu wabaya mlangoni mwa waadilifu.
20Maskini huchukiwa hata na jirani yake,
lakini tajiri ana marafiki wengi.
21Anayemdharau jirani yake ni mwenye dhambi,
bali ana heri aliye mwema kwa maskini.
22Anayepanga maovu kweli anakosea!
Wanaopanga kutenda mema hufadhiliwa.
23Bidii katika kila kazi huleta faida,
lakini maneno matupu huleta umaskini.
24Mali ni taji ya fahari ya wenye hekima,
lakini ujinga ni shada la wapumbavu.
25Shahidi wa kweli huokoa maisha,
lakini msema uongo ni msaliti.
26Amchaye Mwenyezi-Mungu ana tumaini imara,
na watoto wake watapata kimbilio salama.
27Kumcha Mwenyezi-Mungu ni chemchemi ya uhai;
humwezesha mtu kuepa mitego ya kifo.
28Fahari ya mfalme ni wingi wa watu wake,
lakini bila watu mtawala huangamia.
29Mtu asiye mwepesi wa hasira ana busara kubwa,
lakini akasirikaye upesi hukuza upumbavu.
30Amani rohoni humpa mtu afya,
lakini tamaa huozesha mifupa.
31Anayemdhulumu maskini anamtukana Muumba wake,
lakini amwoneaye huruma mhitaji anamtukuza Mungu.
32Mwovu huangamizwa kwa matendo yake maovu,
lakini mwadilifu hupata usalama kwa unyofu wake.14:32 kwa unyofu wake: Kiebrania; katika kifo chake.
33Hekima imo moyoni mwa mtu mwenye busara;
haipatikani kamwe mioyoni mwa wapumbavu.
34Uadilifu hukuza taifa,
lakini dhambi ni balaa kwa taifa lolote.
35Mfalme humfadhili mtumishi atendaye kwa hekima,
lakini hasira yake huwakumba watendao yasiyofaa.

Methali14;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday, 8 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 13...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!



Baba hamhukumu mtu yeyote; shughuli yote ya hukumu amemkabidhi Mwana, ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba ambaye amemtuma.

Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...
“Kweli nawaambieni, anayesikia neno langu, na kumwamini yule aliyenituma, anao uhai wa milele. Hatahukumiwa kamwe, bali amekwisha pita kutoka kifoni na kuingia katika uhai. Kweli nawaambieni, wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wafu wataisikia sauti ya Mwana wa Mungu, nao watakaoisikia, wataishi.

Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kama vile Baba alivyo asili ya uhai, ndivyo pia alivyomjalia Mwanae kuwa asili ya uhai. Tena amempa mamlaka ya kuhukumu kwa sababu yeye ni Mwana wa Mtu. Msistaajabie jambo hili; maana wakati unakuja ambapo wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake, nao watafufuka: Wale waliotenda mema watafufuka na kuishi, na wale waliotenda maovu watafufuka na kuhukumiwa.

Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

1Mtoto mwenye hekima husikia maagizo ya baba yake,
lakini mwenye dharau hasikilizi maonyo.
2Mtu mwema hupata mema kutokana na maneno yake,
lakini wadanganyifu huishi kwa ukatili.
3Achungaye mdomo wake huyahifadhi maisha yake,
anayeropoka ovyo hujiletea maangamizi.
4Mvivu hutamani lakini hapati chochote,
hali mwenye bidii hujaliwa riziki kwa wingi.
5Mwadilifu huuchukia uongo,
lakini mwovu hutenda kwa aibu na fedheha.
6Uadilifu huwalinda wenye mwenendo mnyofu,
lakini dhambi huwaangusha waovu.
7Baadhi hujidai kuwa matajiri kumbe hawana kitu;
wengine hujiona kuwa maskini hali wana mali tele.
8Fidia ya mtu ni mali yake,
lakini maskini hana cha kutishwa.
9Mwadilifu hungaa kama taa iwakayo vizuri,
lakini waovu ni kama taa inayozimika.
10Kiburi husababisha tu ugomvi,
lakini kwa wanaokubali shauri jema mna hekima.
11Mali ya harakaharaka hutoweka,
lakini akusanyaye kidogokidogo ataiongeza.
12Tumaini la kungojangoja huumiza moyo,
lakini tazamio linalotimia ni mti wa uhai.
13Anayedharau mawaidha anajiletea maangamizi,
lakini anayetii amri atapewa tuzo.
14Mafundisho ya wenye hekima ni chemchemi ya uhai;
humwezesha mtu kuiepa mitego ya kifo.
15Kuwa na akili huleta fadhili,
lakini njia ya waovu ni ya taabu13:15 aya ya 15 Kiebrania si dhahiri.
16Mwenye busara hutenda kila kitu kwa akili,
lakini mpumbavu hutembeza upumbavu wake.
17Mjumbe mbaya huwatumbukiza watu taabuni,13:17 huwatumbukiza watu taabuni: Au huanguka taabuni.
lakini mjumbe mwaminifu huleta nafuu.
18Umaskini na fedheha humpata asiyejali mafundisho,
lakini mwenye kusikia maonyo huheshimiwa.
19Inafurahisha upatapo kile unachotaka,
kwa hiyo wapumbavu huchukia kuepa uovu.
20Anayeandamana na wenye hekima hupata hekima,
lakini anayejiunga na wapumbavu atapata madhara.
21Watendao dhambi huandamwa na balaa,
lakini waadilifu watatuzwa mema.
22Mtu mwema huwaachia urithi uzao wake,
lakini mali ya mwenye dhambi imerundikiwa waadilifu.
23Shamba la maskini hutoa mazao mengi,
lakini bila haki hunyakuliwa.13:23 aya 23 Kiebrania si dhahiri.
24Asiyemwadhibu mtoto wake hampendi;
lakini ampendaye mwanawe humrudi mapema.
25Mwadilifu anacho chakula cha kumtosheleza,
lakini tumbo la waovu hutaabika kwa njaa.


Methali13;1-25

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday, 5 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 12...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, Mwana hawezi kufanya kitu peke yake; anaweza tu kufanya kile anachomwona Baba akikifanya. Maana kile anachofanya Baba, Mwana hukifanya vilevile.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Baba ampenda Mwana, na humwonesha kila kitu anachokifanya yeye mwenyewe, tena atamwonesha mambo makuu kuliko haya, nanyi mtastaajabu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Kama vile Baba huwafufua wafu na kuwapa uhai, vivyo hivyo naye Mwana huwapa uhai wale anaopenda.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

1Apendaye nidhamu hupenda maarifa,
bali asiyependa kuonywa ni mjinga.
2Mtu mwema hufadhiliwa na Mwenyezi-Mungu,
lakini mwenye nia mbaya hulaaniwa na Mungu.
3Mtu hawi imara kwa kutenda maovu,
lakini hakuna kiwezacho kumngoa mtu mwadilifu.
4Mke mwema ni taji ya fahari kwa mumewe;
amwaibishaye mumewe ni kama kidonda mifupani mwake.
5Mawazo ya mwadilifu ni ya haki;
mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.
6Maneno ya waovu lengo lake ni kuua,
lakini maneno ya waadilifu huwaokoa wanaotishwa.
7Waovu huangamizwa na kutoweka kabisa,
lakini jamaa ya waadilifu hudumishwa.
8Mtu husifiwa kadiri ya hekima yake,
lakini mtu wa fikira mbaya hudharauliwa.
9Afadhali mtu wa chini anayejitegemea,
kuliko ajitakiaye makuu na kukosa chakula.
10Mtu mwadilifu huwajali wanyama wake,
lakini huruma ya mwovu ni ukatili.
11Mkulima mwenye bidii ana chakula tele,
lakini afuataye mambo yasiyofaa hana akili.
12Waovu hutamani faida isiyo halali,
lakini mtu mwadilifu husimama imara.12:12 aya ya 12 makala ya Kiebrania si dhahiri na tafsiri yake si hakika.
13Mtu mwovu hunaswa kwa uongo wake mwenyewe,
lakini mwadilifu hutoka katika taabu.
14Mtu hufanikiwa kutokana na maneno yake
kama apatavyo matokeo ya kazi za mikono yake.
15Mpumbavu huiona njia yake kuwa sawa,
lakini mwenye hekima husikiliza shauri.
16Udhia wa mpumbavu hujulikana mara,
lakini mwerevu huyapuuza matukano.
17Msema kweli hutoa ushahidi wa kweli,
lakini shahidi wa uongo hutamka udanganyifu.
18Maneno ya ovyo hujeruhi kama upanga,
lakini asemayo mwenye hekima huponesha kidonda.
19Ukweli hudumu milele,
lakini uongo ni wa kitambo tu.
20Wanaopanga maovu wamejaa udanganyifu moyoni,
lakini wanaonuia mema hupata furaha.
21Waadilifu hawapatwi na jambo lolote baya,
lakini waovu wamejaa dhiki.
22Midomo isemayo uongo ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,
lakini watu waaminifu ni furaha yake.
23Mwenye busara huficha maarifa yake,
lakini wapumbavu hutangaza upumbavu wao.
24Kuwa na bidii kutampa mtu cheo,
lakini uvivu utamfanya mtumwa.
25Wasiwasi moyoni humkosesha mtu raha,
lakini neno jema humchangamsha.
26Mtu mwadilifu huuepa uovu,12:26 Mtu mwadilifu … uovu: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
lakini njia ya waovu huwapotosha wenyewe.
27Mwindaji mvivu hatapata anachowinda,
lakini mwenye bidii atafanikiwa.12:27 aya ya 27, makala ya Kiebrania si dhahiri.
28Uadilifu ni njia ya uhai,
lakini uovu huongoza katika mauti.


Methali12;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday, 4 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 11...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kwa vile Yesu alifanya jambo hilo siku ya Sabato, Wayahudi walianza kumdhulumu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, Yesu akawaambia, “Baba yangu anafanya kazi daima, nami pia nafanya kazi.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kwa sababu ya maneno haya, viongozi wa Wayahudi walizidi kutafuta njia ya kumuua Yesu; si kwa kuwa aliivunja Sheria ya Sabato tu, bali pia kwa kuwa alisema kwamba Mungu ni Baba yake, na hivyo akajifanya sawa na Mungu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,
lakini matumizi ya kipimo halali ni furaha kwake.
2Kiburi huandamana na fedheha,
lakini kwa watu wanyenyekevu mna hekima.
3Unyofu wa watu wema huwaongoza,
upotovu wa wenye hila huwaangamiza.
4Utajiri haufai kitu siku ya ghadhabu,
lakini uadilifu huokoa kutoka kifo.
5Uadilifu wa watu wanyofu huinyosha njia yao,
lakini waovu huanguka kwa uovu wao wenyewe.
6Uadilifu wa wanyofu huwaokoa na hatari,
lakini wafitini hunaswa kwa tamaa zao wenyewe.
7Mwovu akifa tumaini lake nalo hutoweka;
tazamio la asiyemcha Mungu huishia patupu.
8Mtu mnyofu huokolewa katika shida,
na mwovu huingia humo badala yake.
9Asiyemcha Mungu huangamiza wengine kwa mdomo wake,
lakini mwadilifu huokolewa kwa maarifa yake.
10Waadilifu wakipata fanaka mji hushangilia,
na waovu wakiangamia watu hupiga vigelegele.
11Mji hufanikishwa kwa baraka za wanyofu,
lakini huangamizwa kwa mdomo wa waovu.
12Anayemdharau jirani yake hana akili,
mtu mwenye busara hukaa kimya.
13Apitapitaye akichongea hutoa siri,
lakini anayeaminika rohoni huficha siri.
14Pasipo na uongozi taifa huanguka,
penye washauri wengi pana usalama.
15Anayemdhamini mgeni atakuja juta,
lakini anayechukia mambo ya dhamana yu salama.
16Mwanamke mwema huheshimiwa,
mwanamume mwenye bidii hutajirika.
17Mtu mkarimu hufaidika yeye mwenyewe,
lakini mtu mkatili hujiumiza mwenyewe.
18Faida anayopata mwovu ni ya uongo,
lakini atendaye mema hakika atapata faida ya kweli.
19Mtu anayepania kuwa mwadilifu ataishi,
lakini anayechagua kutenda maovu atakufa.
20Wenye nia mbaya ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,
lakini wenye mwenendo mwema ni furaha yake.
21Hakika mwovu hataepa kuadhibiwa,
lakini waadilifu wataokolewa.
22Mwanamke mzuri asiye na akili,
ni kama pete ya dhahabu puani mwa nguruwe.
23Matazamio ya waadilifu yana matokeo mema;
tamaa za waovu huishia katika ghadhabu.
24Atoaye kwa ukarimu huzidi kutajirika;
lakini bahili huzidi kudidimia katika umaskini.
25Mtu mkarimu atafanikishwa,
amnyweshaye mwingine maji naye atanyweshwa.
26Watu humlaani afichaye nafaka,11:26 Hapa yahusu wanaoficha nafaka kungojea waiuze kwa bei kubwa wakati wa shida.
lakini humtakia baraka mwenye kuiuza.
27Atafutaye kutenda mema hupata fadhili,
lakini atafutaye kutenda maovu atapatwa na maovu.
28Anayetegemea mali zake ataanguka,
lakini mwadilifu atastawi kama jani bichi.
29Anayeivunja nyumba yake ataambua upepo.
Mpumbavu atakuwa mtumwa wa wenye hekima.
30Matendo ya mwadilifu huleta uhai,
lakini uhalifu huuondoa uhai.
31 Taz 1Pet 4:18 Ikiwa mwadilifu hupata tuzo hapa duniani,
hakika mwovu na mwenye dhambi atapatilizwa.


Methali11;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.