Sunday, 8 July 2012

Siku kama ya Leo da'Rukia.H.Penza Alizaliwa,Burudani-Tuselebuke!!!!!!!!!!

Mwenyewe Wifi/da'Rukia
Bibi na Bwana Penza
 
hehehee kaka wa mimi hachezi mbali, hapo chini kaweka mkia wa Taa, nasikia alirithi kwa ba'Mkubwa!!

Waungwana Siku kama ya Leo miaka Kadhaa iliyopita, Bibi na Bwana Haidari walipata mtoto wa kike na Wakamwita Rukia.
Kwanza tunawapongeza Wazazi/Walezi kwa yoote.
Asante pia kwa kumzalia Mke kaka Mashaka!!!!!

Wifi/da'Rukia Tunakutakia kila lililojema leo na siku zote Maishani .
Mungu azidi kukubariki na kukulinda na Akupe Miaka Mingi ili ufanikishe Malengo yako.Uwe Baraka kwa Watu wooote.

Swali:Waungwana;Eti ni kweli kuolewa na mume mwenye dada wengi ni karaha na si Raha?
 Anapo penda kaka ni hapo tuu.........Endelea na Tuselebuke aeeee ......mimi nakuja.......
"SWAHILI na WASWAHILI"Pamoja sana!!


8 comments: