Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 4 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Yoel 3...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Mwenyezi-Mungu asema, “Kwa hiyo, mimi nitawalaumu nyinyi, na nitawalaumu wazawa wenu. Haya, vukeni bahari hadi Kupro mkaone, au tumeni watu huko Kedari wakachunguze, kama jambo kama hili limewahi kutokea:
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kwamba kuna taifa lililowahi kubadilisha miungu yake ingawa miungu hiyo si miungu! Lakini watu wangu wameniacha mimi, utukufu wao, wakafuata miungu isiyofaa kitu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Shangaeni enyi mbingu, juu ya jambo hili, mkastaajabu na kufadhaika kabisa. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema. Maana, watu wangu wametenda maovu mawili; wameniacha mimi niliye chemchemi ya maji ya uhai, wakajichimbia visima vyao wenyewe, visima vyenye nyufa, visivyoweza kuhifadhi maji.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Mungu atayahukumu mataifa
1“Wakati huo na siku hizo
nitakapoirekebisha hali ya Yuda na Yerusalemu,
2nitayakusanya mataifa yote,
niyapeleke katika bonde liitwalo,
‘Mwenyezi-Mungu Ahukumu.
Huko nitayahukumu mataifa hayo,
kwa mambo yaliyowatendea watu wangu Israeli,
hao walio mali yangu mimi mwenyewe.
Maana waliwatawanya miongoni mwa mataifa,
waligawa nchi yangu
3na kugawana watu wangu kwa kura.
Waliwauza wavulana ili kulipia malaya,
na wasichana ili kulipia divai.
4“Mnataka kunifanya nini enyi Tiro na Sidoni na maeneo yote ya Filistia? Je, mna kisasi nami mnachotaka kulipiza? Kama mnalipiza kisasi, mimi nitawalipizeni mara moja! 5Mmechukua fedha na dhahabu yangu, na kuvibeba vitu vyangu vya thamani hadi kwenye mahekalu yenu. 6Mmewapeleka watu wa Yuda na Yerusalemu mbali na nchi yao, mkawauza kwa Wagiriki. 7Sasa, nitawarudisha watu wangu kutoka huko mlikowauza. Nitawalipizeni kisasi kwa yote mliyowatendea. 8Watoto wenu wa kiume na wa kike nitawafanya wauzwe kwa watu wa Yuda, nao watawauzia Washeba, watu wa taifa la mbali kabisa. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
9“Watangazieni watu wa mataifa jambo hili:
Jitayarisheni kwa vita,
waiteni mashujaa wenu;
askari wote na wakusanyike,
waende mbele.
10 Taz Isa 2:4; Mika 4:3 Majembe yenu yafueni yawe mapanga,
miundu yenu ya kupogolea iwe mikuki.
Hata aliye dhaifu na aseme:
‘Mimi pia ni shujaa’.
11Njoni haraka, enyi mataifa yote jirani,
kusanyikeni huko bondeni.”
Ee Mwenyezi-Mungu!
Teremsha askari wako dhidi yao!
12“Haya mataifa na yajiweke tayari;
yaje kwenye bonde liitwalo:
‘Mwenyezi-Mungu Ahukumu’.
Huko, mimi Mwenyezi-Mungu,
nitaketi kuyahukumu mataifa yote ya jirani.
13 Taz Ufu. 14:14-16, 19-20 Haya! Chukueni mundu wa kuvuna,
kwani sasa ni wakati wa mavuno.
Ingieni! Wapondeni kama zabibu
ambazo zimejaza shinikizo.
Uovu wao umepita kiasi
kama mapipa yanayofurika.”
14Wanafika makundi kwa makundi
kwenye bonde la Hukumu,
maana siku ya Mwenyezi-Mungu imekaribia.
15Jua na mwezi vinatiwa giza,
na nyota zimeacha kuangaza.
Mungu atawabariki watu wake
16Mwenyezi-Mungu ananguruma huko Siyoni;
sauti yake inavuma kutoka Yerusalemu;
mbingu na dunia vinatetemeka.
Lakini Mwenyezi-Mungu ni kimbilio la watu wake,
ni ngome ya usalama kwa Waisraeli.
17“Hapo, ewe Israeli,
utajua kwamba mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,
nakaa Siyoni, mlima wangu mtakatifu,
Yerusalemu utakuwa mji mtakatifu;
na wageni hawatapita tena humo.
18“Wakati huo, milima itatiririka divai mpya,
na vilima vitatiririka maziwa.
Vijito vyote vya Yuda vitajaa maji;
chemchemi itatokea nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu,
na kulinywesha bonde la Shitimu.3:18 Shitimu: Kiebrania; au Mgunga.
19“Misri itakuwa mahame,
Edomu itakuwa jangwa tupu,
kwa sababu waliwashambulia watu wa Yuda
wakawaua watu wasio na hatia.
20Bali Yuda itakaliwa milele,
na Yerusalemu kizazi hata kizazi.
21Nitawaadhibu waliomwaga damu ya watu wa Yuda
wala sitawaachia wenye hatia.
Mimi, Mwenyezi-Mungu nakaa Siyoni.”

Yoeli3;1-21

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Wednesday 3 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Yoel 2...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Hawakujiuliza: ‘Yuko wapi Mwenyezi-Mungu aliyetutoa nchini Misri, aliyetuongoza nyikani katika nchi ya jangwa na makorongo, nchi kame na yenye giza nene, nchi isiyopitiwa na mtu yeyote, wala kukaliwa na binadamu?’
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Niliwaleta katika nchi yenye rutuba, muyafurahie mazao yake na mema yake mengine. Lakini mlipofika tu mliichafua nchi yangu, mkaifanya chukizo nchi niliyowapa iwe yenu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Nao makuhani hawakujiuliza: ‘Yuko wapi Mwenyezi-Mungu?’ Wataalamu wa sheria hawakunijua, viongozi wa watu waliniasi; manabii nao walitabiri kwa jina la Baali na kuabudu sanamu zisizo na faida yoyote.”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Nzige: Onyo juu ya siku ya Mwenyezi-Mungu
1Pigeni tarumbeta huko Siyoni;
pigeni baragumu juu ya mlima mtakatifu!
Tetemekeni enyi wakazi wa Yuda,
maana siku ya Mwenyezi-Mungu inakuja,
naam, siku hiyo iko karibu!
2Hiyo ni siku ya giza na huzuni;
siku ya mawingu na giza nene.
Jeshi kubwa la nzige linakaribia
kama giza linalotanda milimani.
Namna hiyo haijapata kuweko kamwe
wala haitaonekana tena
katika vizazi vyote vijavyo.
3Kama vile moto uteketezavyo
jeshi hilo laharibu kila kitu mbele yake
na kuacha nyuma kila kitu kinateketezwa;
kabla hawajapita, nchi ni kama bustani ya Edeni,
lakini wakisha pita, ni jangwa tupu.
Hakuna kiwezacho kuwaepa!
4 Taz Ufu 9:7-9 Wanaonekana kama farasi,
wanashambulia kama farasi wa vita,
5Wanaporukaruka kwenye vilele vya milima,
wanarindima kama magari ya farasi,
wanavuma kama mabua makavu motoni.
Wamejipanga kama jeshi kubwa
tayari kabisa kufanya vita.
6Wakaribiapo, watu hujaa hofu,
nyuso zao zinawaiva.
7Wanashambulia kama mashujaa wa vita;
kuta wanazipanda kama wanajeshi.
Wote wanakwenda mbele moja kwa moja,
bila hata mmoja wao kubadilisha njia.
8Hakuna amsukumaye mwenziwe;
kila mmoja anafuata mkondo wake.
Wanapita kati ya vizuizi vya silaha,
wala hakuna kiwezacho kuwazuia.
9Wanauvamia mji,
wanapiga mbio ukutani;
wanaziparamia nyumba na kuingia,
wanapenya madirishani kama wezi.
10Nchi inatetemeka mbele yao,
mbingu zinatikisika.
Jua na mwezi vyatiwa giza,
nazo nyota zinaacha kuangaza.
11Mwenyezi-Mungu anaamuru jeshi lake kwa sauti;
askari wake ni wengi mno,
wanaomtii hawahesabiki.
2Siku ya Mwenyezi-Mungu kweli ni kuu na ya kutisha sana!
Nani atakayeweza kuistahimili?
Wito wa toba
12“Lakini hata sasa,”
nasema mimi Mwenyezi-Mungu,
“Nirudieni kwa moyo wote,
kwa kufunga, kulia na kuomboleza.
13Msirarue mavazi yenu kuonesha huzuni
bali nirudieni kwa moyo wa toba.”
Mrudieni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu;
yeye amejaa neema na huruma;
hakasiriki upesi, ni mwingi wa fadhili;
daima yu tayari kuacha kuadhibu.
14Huenda Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, atabadili nia
na kuwapeni baraka ya mazao,
mkamtolea sadaka za nafaka na kinywaji.
15Pigeni tarumbeta huko Siyoni!
Toeni amri watu wafunge;
itisheni mkutano wa kidini.
16Wakusanyeni watu wote,
wawekeni watu wakfu.
Waleteni wazee,
wakusanyeni watoto,
hata watoto wanyonyao.
Bwana arusi na bibi arusi
na watoke vyumbani mwao.
17Kati ya madhabahu na lango la hekalu,
makuhani, wahudumu wa Mwenyezi-Mungu,
walie na kuomba wakisema:
“Wahurumie watu wako, ee Mwenyezi-Mungu.
Usiyaache mataifa mengine yatudharau
na kutudhihaki yakisema,
‘Yuko wapi basi Mungu wao?’”
Mungu ataifanikisha nchi
18Ndipo Mwenyezi-Mungu akaipenda nchi yake
akawahurumia watu wake.
19Alisikiliza, akajibu sala zao; akasema,
“Sasa nitawapeni tena nafaka,
sitawafanya mdharauliwe tena na mataifa.
20Nitawaondoa hao adui watokao kaskazini,
nitawafukuza mpaka jangwani;
askari wa mbele nitawatupa katika Bahari ya Chumvi
na wale wa nyuma katika Bahari ya Mediteranea.
Watatoa uvundo na harufu mbaya,
hao ambao wamefanya maovu makubwa.
21“Usiogope, ewe nchi,
bali furahi na kushangilia,
maana Mwenyezi-Mungu ametenda makuu.
22Msiogope, enyi wanyama.
malisho ya nyikani yamekuwa mazuri,
miti inazaa matunda yake,
mizabibu na mitini zinazaa kwa wingi.
23“Furahini, enyi watu wa Siyoni,
shangilieni kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,
maana amewapeni mvua za masika,2:23 mvua za masika: Au Mvua za masika kwa kuwa ni mwenye haki.
amewapeni mvua ya kutosha:
Mvua za masika na mvua za vuli kama hapo awali.
24Mahali pa kupuria patajaa nafaka,
mashinikizo yatafurika divai na mafuta.
25Nitawarudishia miaka ile iliyoliwa na nzige,
kila kitu kilicholiwa na tunutu, parare na matumatu,
hilo jeshi kubwa nililowaletea!
26Mtapata chakula kingi na kutosheka;
mtalisifu jina la Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,
aliyewatendea mambo ya ajabu.
Watu wangu, kamwe hawatadharauliwa tena.
27Mtatambua kwamba mimi nimo miongoni mwenu,
enyi Waisraeli;
kwamba mimi Mwenyezi-Mungu,
ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine.
Watu wangu, kamwe hawatadharauliwa tena.
Siku ya Mwenyezi-Mungu
28katika Kiebrania sura ya 3 yaanza hapa.“Kisha hapo baadaye
nitaimimina roho yangu juu ya binadamu wote.
Watoto wenu wa kike na wa kiume watatabiri,
wazee wenu wataota ndoto,
na vijana wenu wataona maono.
29Hata juu ya watumishi wa kiume na wa kike,
nitaimimina roho yangu wakati huo.
30“Nitatoa ishara mbinguni na duniani;
kutakuwa na damu, moto na minara ya moshi.
31Jua litatiwa giza,
na mwezi utakuwa mwekundu kama damu,
kabla ya kufika siku ya Mwenyezi-Mungu,
siku iliyo kuu na ya kutisha.
32Hapo watu wote watakaoomba kwa jina la Mwenyezi-Mungu wataokolewa.
Maana katika mlima Siyoni na Yerusalemu,
watakuwako watu watakaosalimika,
kama nilivyosema mimi Mwenyezi-Mungu.

Yoeli2;1-32

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Tuesday 2 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Tunamshukuru Mungu kwa kumaliza Kitabu cha Hosea,Leo Tunaanza Kitabu cha Yoeli..1


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tunamshukuru Mungu kwa kutupa kibali cha
 kupitia kitabu cha "HOSEA
"
Ni matumaini yangu kuna mengi tumejifunza/kufaidika
na kutupa mwanga/kuelewa kwenye kitabu hiki...

Leo tunapokwenda anza kupitia Kitabu cha"YOELI"tunamuomba Mungu wetu akatupe kibali,macho ya rohoni
 na akili ya kuelewa katika kujifunza NENO lake...
Ee Mungu  tunaomba ukatuongoze...!!
Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Neno la Mwenyezi-Mungu likanijia: “Nenda ukawatangazie waziwazi wakazi wote wa Yerusalemu kuwa mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Naukumbuka uaminifu wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama mchumba wako, ulivyonifuata jangwani kwenye nchi ambayo haikupandwa kitu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Israeli, wewe ulikuwa mtakatifu kwangu, ulikuwa matunda ya kwanza ya mavuno yangu. Wote waliokudhuru walikuwa na hatia, wakapatwa na maafa. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu, enyi wazawa wa Yakobo. Sikilizeni enyi jamaa zote za wazawa wa Israeli. Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Wazee wenu waliona kosa gani kwangu hata wakanigeuka na kuniacha, wakakimbilia miungu duni, hata nao wakawa watu duni?
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Neno la Mwenyezi-Mungu lililomjia Yoeli, mwana wa Pethueli:
Watu waombolezea mimea
2Sikilizeni kitu hiki enyi wazee;
tegeni sikio wakazi wote wa Yuda!
Je, jambo kama hili limewahi kutokea maishani mwenu,
au nyakati za wazee wenu?
3Wasimulieni watoto wenu jambo hili,
nao wawasimulie watoto wao,
na watoto wao wakisimulie kizazi kifuatacho.
4Nzige, makundi kwa makundi, wameivamia mimea;
kilichoachwa na nzige kimeliwa na tunutu,
kilichoachwa na tunutu kimeliwa na parare,
kilichoachwa na parare kimeliwa na matumatu.
5Enyi walevi, levukeni na kulia;
pigeni yowe, enyi walevi wa divai;
zabibu zote za kutengeneza divai mpya zimeharibiwa.
6 Taz Ufu 9:8 Jeshi la nzige limeivamia nchi yetu;
lina nguvu na ni kubwa ajabu;
meno yake ni kama ya simba,
na magego yake ni kama ya simba jike.
7Limeiharibu mizabibu yetu,
na kuitafuna mitini yetu.
Limeyabambua magamba yake na kuyatupa chini,
na matawi yake yameachwa meupe.
8Lieni kama msichana aliyevaa vazi la gunia
akiombolezea kifo cha mchumba wake.
9Sadaka za nafaka na kinywaji zimetoweka nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu.
Makuhani, wahudumu wa Mwenyezi-Mungu, wanaomboleza.
10Mashamba yamebaki matupu;
nchi inaomboleza,
maana nafaka imeharibiwa,
divai imetoweka,
mafuta yamekosekana.
11Ombolezeni enyi wakulima;
pigeni yowe enyi watunza mizabibu.
Ngano na shayiri zimeharibika,
mavuno yote shambani yameangamia.
12Mizabibu imenyauka;
mitini imedhoofika;
mikomamanga, mitende na mitofaa imekauka,
naam miti yote shambani imekauka.
Furaha imetoweka miongoni mwa watu.
13Enyi makuhani, jivikeni magunia kuomboleza,
lieni enyi wahudumu wa madhabahu.
Ingieni hekaluni mkaomboleze usiku kucha!
Sadaka za nafaka na kinywaji zimetoweka nyumbani kwa Mungu.
14Toeni amri watu wafunge;
itisheni mkutano wa kidini.
Kusanyeni wazee na wakazi wote wa nchi,
nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,
na humo mkamlilie Mwenyezi-Mungu.
15Ole wetu kwa ile siku ya Mwenyezi-Mungu,
siku hiyo ya Mwenyezi-Mungu inakaribia;
inakuja pamoja na maangamizi,
kutoka kwa Mungu Mkuu.
16Mazao yetu yameharibiwa huku tunatazama.
Furaha na kicheko vimetoweka nyumbani kwa Mungu wetu.
17Mbegu zinaoza udongoni;
ghala za nafaka ni ukiwa mtupu,
ghala zimeharibika,
kwa kukosa nafaka ya kuhifadhi.
18Tazama wanyama wanavyolia kwa huzuni!
Makundi ya ng'ombe yanahangaika,
kwa sababu yamekosa malisho;
hata makundi ya kondoo yanateseka.
19Ninakulilia wewe, ee Mwenyezi-Mungu,
moto umemaliza malisho nyikani,
miali ya moto imeteketeza miti mashambani.
20Hata wanyama wa porini wanakulilia wewe,
maana, vijito vya maji vimekauka,
moto umemaliza malisho nyikani.

Yoeli1;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Monday 1 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Hosea 14..


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki/Mwezi mwingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...
Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Ndipo mtakapoomba, nami Mwenyezi-Mungu nitawaitikia; mtalia kwa sauti kuomba msaada, nami nitajibu, ‘Niko hapa!’ “Kama mkiiondoa dhuluma kati yenu, mkiacha kudharau wengine na kusema maovu, mkiwapa chakula kwa ukarimu wenye njaa, mkitosheleza mahitaji ya wenye dhiki, mwanga utawaangazia nyakati za giza, giza lenu litakuwa kama mchana.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona

Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Mimi Mwenyezi-Mungu nitawaongozeni daima, nitatosheleza mahitaji yenu wakati wa shida. Nitawaimarisha mwilini, nanyi mtakuwa kama bustani iliyomwagiliwa maji, kama chemchemi ya maji ambayo maji yake hayakauki kamwe. Magofu yenu ya kale yatajengwa; mtajenga upya juu ya misingi iliyoachwa zamani. Nanyi mtaitwa watu waliotengeneza upya kuta, watu waliozifanya barabara za mji zipitike tena.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu

Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

“Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato, ukaacha shughuli zako siku yangu hiyo takatifu; kama ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha, ukaiheshimu siku hiyo takatifu ya Mwenyezi-Mungu, ukaacha na shughuli zako na kupiga domo, utapata furaha yako kwangu mimi Mwenyezi-Mungu, nitakupatia ushindi katika kila pingamizi nchini, nitakulisha mali ya Yakobo, babu yako. Mimi, Mwenyezi-Mungu, nimesema.”
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Kumrudia Mungu na hali mpya
1Enyi Waisraeli,
mrudieni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.
Mmejikwaa kwa sababu ya uovu wenu.
2Ombeni toba kwake,
mrudieni na kumwambia:
“Utusamehe uovu wote,
upokee zawadi zetu,
nasi tutakusifu kwa moyo.
3Ashuru haitatuokoa,
hatutategemea tena farasi wa vita.
Hatutaviita tena: ‘Mungu wetu’
hivyo vinyago tulivyochonga wenyewe.
Kwako ee Mungu yatima hupata huruma.”
4Mwenyezi-Mungu asema,
“Nitaponya utovu wao wa uaminifu;
nitawapenda tena kwa hiari yangu,
maana sitawakasirikia tena.
5Nitakuwa kama umande kwa Waisraeli
nao watachanua kama yungiyungi,
watakuwa na mizizi kama mwerezi wa Lebanoni.
6Chipukizi zao zitatanda na kuenea,
uzuri wao utakuwa kama mizeituni,
harufu yao nzuri kama maua ya Lebanoni.
7Watarudi na kuishi chini ya ulinzi wangu,
watastawi kama bustani nzuri.
Watachanua kama mzabibu,
harufu yao nzuri kama ya divai ya Lebanoni.
8Enyi watu wa Efraimu,
mna haja gani tena na sanamu?
Mimi ndiye ninayesikiliza sala zenu,
mimi ndiye ninayewatunzeni.
Mimi nitawapa kivuli kama mberoshi,
kutoka kwangu mtapata matunda yenu.
9Yeyote aliye na hekima ayaelewe mambo haya,
mtu aliye na busara ayatambue.
Maana njia za Mwenyezi-Mungu ni nyofu;
watu wanyofu huzifuata,
lakini wakosefu hujikwaa humo.”


Hosea14;1-9

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe