Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 22 May 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Hosea 8..

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Basi, tuzingatie kwa makini imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka mbinguni; Yesu, Mwana wa Mungu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Huyu Kuhani Mkuu wetu anaelewa kabisa unyonge wetu; yeye mwenyewe alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu mwenye neema, tupokee huruma na neema ya kutusaidia wakati wa shida.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Makosa makuu ya Israeli
1“Pigeni baragumu!
Adui anakuja kama tai
kuivamia nyumba ya Mwenyezi-Mungu,
kwa kuwa wamelivunja agano langu
na kuiasi sheria yangu.
2Waisraeli hunililia wakisema:
‘Mungu wetu, sisi tunakujua.’
3Lakini Israeli amepuuza mambo mema,
kwa hiyo, sasa adui watamfuatia.
4“Walijiwekea wafalme bila kibali changu,
walijiteulia viongozi ambao sikuwatambua.
Wamejitengenezea miungu ya fedha na dhahabu,
jambo ambalo litawaangamiza.
5Watu wa Samaria, naichukia sanamu yenu ya ndama.
Hasira yangu inawaka dhidi yenu.
Mtaendelea mpaka lini kuwa na hatia?
6Nanyi Waisraeli ni hivyohivyo!8:6 Nanyi … hivyohivyo: Labda iwe hivyo. Kiebrania: Tena kutoka Israeli.
Na sanamu yenu hiyo fundi ndiye aliyeitengeneza.
Yenyewe si Mungu hata kidogo.
Naam! Sanamu ya ndama ya Samaria itavunjwavunjwa!
7“Wanapanda upepo, watavuna kimbunga!
Mimea yao ya nafaka iliyo mashambani
haitatoa nafaka yoyote.
Na hata kama ikizaa,
mazao yake yataliwa na wageni.
8Waisraeli wamemezwa;
sasa wamo kati ya mataifa mengine,
kama chombo kisicho na faida yoyote;
9kwa kuwa wamekwenda kuomba msaada Ashuru.
Efraimu ni punda anayetangatanga peke yake;
Efraimu amekodisha wapenzi wake.
10Wametafuta wapenzi kati ya watu wa mataifa,
lakini mimi nitawakusanya mara.
Na hapo watasikia uzito wa mzigo,
ambao mfalme wa wakuu8:10 Mfalme wa wakuu: Jina lingine la mfalme wa Ashuru. aliwatwika.
11“Watu wa Efraimu wamejijengea madhabahu nyingi,
na madhabahu hizo zimewazidishia dhambi.
12Hata kama ningewaandikia sheria zangu mara nyingi,
wao wangeziona kuwa kitu cha kigeni tu.
13Wanapenda kutoa tambiko,
na kula nyama yake;
lakini mimi Mwenyezi-Mungu sipendezwi hata kidogo.
Mimi nayakumbuka makosa yao;
nitawaadhibu kwa dhambi zao;
nitawarudisha utumwani Misri.
14Waisraeli wamemsahau Muumba wao,
wakajijengea majumba ya fahari;
watu wa Yuda wamejiongezea miji ya ngome,
lakini mimi nitaipelekea moto miji hiyo,
na kuziteketeza ngome zao.”

Hosea8;1-14

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Thursday 21 May 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Hosea 7..


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, tujitahidi kuingia katika pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwetu atakayekataa kutii kama walivyofanya wao.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na uboho. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake yeye ambaye kwake tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

1Kila nikitaka kuwarekebisha watu wangu,
ninapotaka kuwaponya Waisraeli,
uovu wa watu wa Efraimu hufunuliwa,
matendo mabaya ya Samaria hujitokeza.
Wao huongozwa na udanganyifu,
kwenye nyumba wezi huvunja
nje barabarani wanyang'anyi huvamia.
2Hawafikiri hata kidogo kwamba mimi
nayakumbuka maovu yao yote.
Sasa maovu yao yamewabana.
Yote waliyotenda yako mbele yangu.
Uhaini katika ikulu
3“Wanamfurahisha mfalme kwa maovu yao
wanawafurahisha wakuu kwa uhaini wao.
4Wote ni wazinzi;
wao ni kama tanuri iliyowashwa moto
ambao mwokaji hauchochei tangu akande unga
mpaka mkate utakapoumuka.
5Kwenye sikukuu ya mfalme,
waliwalewesha sana maofisa wake;
naye mfalme akashirikiana na wahuni.
6Kama tanuri iwakavyo,
mioyo yao huwaka kwa hila;
usiku kucha hasira yao hufuka moshi,
ifikapo asubuhi, hulipuka kama miali ya moto.
7Wote wamewaka hasira kama tanuri,
na wanawaangamiza watawala wao.
Wafalme wao wote wameanguka,
wala hakuna anayeniomba msaada.
Israeli anategemea mataifa mengine
8“Efraimu amechanganyika na watu wa mataifa.
Anaonekana kama mkate ambao haukugeuzwa.
9Wageni wamezinyonya nguvu zake,
wala yeye mwenyewe hajui;
mvi zimetapakaa kichwani mwake,
lakini mwenyewe hana habari.
10Kiburi cha Waisraeli chashuhudia dhidi yao,
hawanirudii mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao;
wala hawanitafuti kwa matukio hayo yote.
11Efraimu ni kama njiwa, mjinga asiye na akili;
mara yuko Misri, mara Ashuru kuomba.
12Watakapokwenda nitatandaza wavu wangu niwanase,
nitawaangusha chini kama ndege wa angani;
nitamwaadhibu kadiri ya ripoti ya maovu yao.
13Ole wao kwa kuwa wameniacha!
Maangamizi na yawapate, maana wameniasi.
Nilitaka kuwakomboa,
lakini wanazua uongo dhidi yangu.
14“Wananililia, lakini si kwa moyo.
Wanagaagaa na kujikatakata vitandani mwao,
kusudi nisikilize dua zao za nafaka na divai;
lakini wanabaki waasi dhidi yangu.
15Mimi ndimi niliyeiimarisha mikono yao,
lakini wanafikiria maovu dhidi yangu.
16Wanaigeukia miungu batili,
wako kama uta uliolegea.
Viongozi wao watakufa kwa upanga,
kwa sababu ya maneno yao ya kiburi.
Kwa hiyo, watadharauliwa nchini Misri.

Hosea7;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Wednesday 20 May 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Hosea 6..

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Tena jambo hili lasemwa pia: “Hawataingia mahali pangu pa pumziko.” Basi, hiyo ahadi ya kuingia bado ipo, maana wale waliohubiriwa Habari Njema pale awali walishindwa kuingia humo kwa sababu walikosa kutii.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa “Leo,” akasema baadaye kwa njia ya Daudi maneno yaliyokwisha tajwa: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiwe wakaidi.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kama Yoshua angekuwa amewapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine. Kwa hiyo, basi, bado kuna kupumzika kwa watu wa Mungu. Maana, kila aingiaye mahali pa pumziko la Mungu atapumzika kutoka katika kazi yake kama vile pia Mungu alivyopumzika kutoka kazi yake.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Toba isiyo ya kweli
1“ ‘Twendeni, tukamrudie Mwenyezi-Mungu!
Yeye mwenyewe ameturarua,
lakini yeye mwenyewe atatuponya.
Yeye mwenyewe ametujeruhi,
lakini yeye mwenyewe atatibu majeraha yetu.
2Baada ya siku mbili, atatupa uhai tena,
naam, siku ya tatu atatufufua
ili tuweze kuishi pamoja naye.
3Basi tumtambue,
tujitahidi kumjua Mwenyezi-Mungu.
Kuja kwake ni hakika kama alfajiri,
yeye atatujia kama manyunyu,
kama mvua za masika ziinyweshayo ardhi.’”
4Lakini Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Nitakutendea nini ee Efraimu?
Nikufanyie nini ee Yuda?
Upendo wenu kwangu ni kama ukungu wa asubuhi,
kama umande unaotoweka upesi.
5Ndiyo maana nimewavamia kwa njia ya manabii,
nimewaangamiza kwa maneno yangu,
hukumu yangu huchomoza kama pambazuko.
6Maana ninachotaka kwenu ni upendo na si tambiko,
Kumjua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa.
Uhalifu umeenea kote nchini
7“Lakini mlilivunja agano langu
kama mlivyofanya mjini Adamu;
huko walinikosea uaminifu.
8Gileadi ni mji wa waovu,
umetapakaa damu.
9Kama wanyang'anyi wamwoteavyo mtu njiani,
ndivyo na makuhani walivyojikusanya na kuvizia.
Wanaua watu njiani kuelekea Shekemu,
naam, wanatenda uovu kupindukia.
10Nimeona jambo la kuchukiza sana
miongoni mwa Waisraeli:
Watu wa Efraimu wanakimbilia miungu mingine
naam, Waisraeli wamejitia unajisi.
11Nawe Yuda hali kadhalika,
nimekupangia wakati utakapovuna adhabu.



Hosea6;1-11

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Tuesday 19 May 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Hosea 5..


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, kwa vile ahadi ya kuingia mahali pa pumziko bado ipo, na tuogope ili yeyote kati yenu asije akashindwa kupata pumziko hilo. Maana Habari Njema imehubiriwa kwetu kama vile ilivyohubiriwa kwa hao watu wa kale. Lakini ujumbe huo haukuwafaa chochote, maana waliusikia lakini hawakuupokea kwa imani.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, sisi tunaoamini tunapata pumziko hilo aliloahidi Mungu. Kama alivyosema: “Nilikasirika, nikaapa: ‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko.’” Mungu alisema hayo ingawa kazi yake ilikuwa imekwisha malizika tangu alipoumba ulimwengu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Maana Maandiko yasema mahali fulani kuhusu siku ya saba: “Mungu alipumzika siku ya saba, akaacha kazi zake zote.”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Wakufunzi wabaya wa Israeli
1“Haya! Sikilizeni enyi makuhani!
Tegeni sikio, enyi Waisraeli!
Sikilizeni enyi ukoo wa kifalme!
Nyinyi mlipaswa kuzingatia haki,
badala yake mmekuwa mtego huko Mizpa,
mmekuwa wavu wa kuwanasa huko Tabori.
2Mmechimba shimo refu la kuwanasa huko Shitimu.
Lakini mimi nitawaadhibuni nyote.
3Nawajua watu wa Efraimu,
Waisraeli hawakufichika kwangu.
Nyinyi watu wa Efraimu mmefanya uzinzi,
watu wote wa Israeli wamejitia najisi.
Hosea aonya dhidi ya ibada za miungu
4“Matendo yao yanawazuia wasimrudie Mungu wao.
Mioyoni mwao wamejaa uzinzi;
hawanijui mimi Mwenyezi-Mungu.
5Kiburi cha Waisraeli chaonekana wazi;
watu wa Efraimu watajikwaa katika hatia yao,
nao watu wa Yuda watajikwaa pamoja nao.
6Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng'ombe,
kumtafuta Mwenyezi-Mungu;
lakini hawataweza kumpata,
kwa sababu amejitenga nao.
7Wamevunja uaminifu kwa Mwenyezi-Mungu,
wamezaa watoto walio haramu.
Mwezi mwandamo utawaangamiza,
pamoja na mashamba yao.
Vita kati ya Yuda na Israeli
8“Pigeni baragumu huko Gibea,
na tarumbeta huko Rama.
Pigeni king'ora huko Beth-aveni.
Enyi watu wa Benyamini, adui yenu yuko nyuma!
9Siku nitakapotoa adhabu
Efraimu itakuwa kama jangwa!
Ninachotangaza miongoni mwa makabila ya Israeli,
ni jambo litakalotukia kwa hakika.
10Viongozi wa Yuda wamekuwa
wenye kubadili mipaka ya ardhi.
Mimi nitawamwagia hasira yangu kama maji.
11Efraimu ameteswa,
haki zake zimetwaliwa;
kwani alipania kufuata upuuzi.
12Hivyo mimi Mungu niko kama nondo kwa Efraimu,
kama donda baya kwa watu wa Yuda.
13Watu wa Efraimu walipogundua ugonjwa wao,
naam, watu wa Yuda walipogundua donda lao,
watu wa Efraimu walikwenda Ashuru
kuomba msaada kwa mfalme mkuu;
lakini yeye hakuweza kuwatibu,
hakuweza kuponya donda lenu.
14Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efraimu,
kama mwanasimba kwa watu wa Yuda.
Mimi mwenyewe nitawararua na kuondoka,
nitawachukua na hakuna atakayewaokoa.
15Nitarudi mahali pangu na kujitenga nao
mpaka wakiri kosa lao na kunirudia.
Taabu zao zitawafundisha wanitafute, wakisema:



Hosea5;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Monday 18 May 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Hosea 4..


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki/nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Nilipitia karibu na shamba la mvivu; shamba la mzabibu la mtu mpumbavu. Nilishangaa kuona limemea miiba, magugu yamefunika eneo lake lote, na ukuta wake wa mawe umebomoka.
Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona


Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Nilitazama, nikawaza, mwishowe nikapata funzo: Lala tu kidogo; sinzia tu kidogo! Kunja mikono yako tu upumzike!
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu


Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Lakini kumbuka kwamba uwapo usingizini, umaskini utakuvamia kama mnyanganyi, ufukara kama mtu mwenye silaha.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Mungu awalaumu watu wake
1Msikilizeni Mwenyezi-Mungu,
enyi Waisraeli.
Mwenyezi-Mungu anawashutumu wakazi wa nchi hii.
“Hamna tena uaminifu wala wema nchini;
hamna anayemjua Mungu katika nchi hii.
2Kuapa, uongo, mauaji, wizi na uzinzi huzuka humo.
Umwagaji damu hufuatana mfululizo.
3Kwa hiyo, nchi yote ni kame,
wakazi wake wote wanaangamia
pamoja na wanyama wa porini na ndege;
hata samaki wa baharini wanaangamizwa.
Mungu anawashutumu makuhani
4“Lakini watu wasilaumiwe, wasishutumiwe;
maana mimi nakushutumu wewe kuhani.
5Wewe utajikwaa mchana,
naye nabii atajikwaa pamoja nawe usiku.
Nitamwangamiza mama yako Israeli.
6Watu wangu wameangamia kwa kutonijua,
maana wewe kuhani umekataa mafundisho.
Nimekukataa kuwa kuhani wangu.
Kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako,
nami pia nitawasahau watoto wako.
7“Kadiri makuhani walivyoongezeka,
ndivyo wote walivyozidi kuniasi.
Basi, nitaigeuza fahari yao kuwa aibu.
8Wanajishibisha kwa sadaka za watu wangu wenye dhambi.
Wana hamu sana ya kuwaona wametenda dhambi.
9Lakini yatakayowapata watu yatawapata makuhani;
nitawaadhibu kwa sababu ya mwenendo wao,
nitawalipiza matendo yao wenyewe.
10Watakula, lakini hawatashiba;
watazini, lakini hawatapata watoto,
kwa sababu wameniacha mimi Mwenyezi-Mungu,
na kufuata miungu mingine.
Mungu alaani ibada za miungu
11“Divai mpya na ya zamani
huondoa maarifa.
12Watu wangu huomba shauri kutoka kwa mti;
kijiti chao cha ramli ndicho kinachowapa kauli.
Nia ya kufanya uzinzi imewapotosha;
wamefanya uzinzi kwa kufuata miungu mingine,
wakaniacha mimi Mungu wao.
13Wanatambikia kwenye vilele vya milima;
naam, wanatoa tambiko vilimani,
chini ya mialoni, migude na mikwaju,
maana kivuli chao ni kizuri.
“Kwa hiyo binti zenu hufanya uzinzi,
na bibiarusi wenu hufanya uasherati.
14Lakini sitawaadhibu binti zenu wanapofanya uzinzi,
wala bibi arusi wenu wanapofanya uasherati,
maana, wanaume wenyewe ndio wanaofuatana na wazinzi,
na kutambikia pamoja nao katika ibada za uzinzi.
Watu hawa watovu wa akili hakika wataangamia!
15“Ama kweli nyinyi Waisraeli ni wazinzi!
Lakini, msiwafanye watu wa Yuda wawe na hatia!
Msiende mahali patakatifu huko Gilgali,
wala msiende kule Beth-aveni.4:15 Beth-aveni: Neno kwa neno: Nyumba ya ukaidi; labda mahali pa Betheli, yaani “Nyumba ya Mungu”.
Wala msiape mkisema,
‘Kama Mwenyezi-Mungu aishivyo!’”
16Waisraeli ni wakaidi kama punda.
Kwa nini basi Mungu ashughulike kuwachunga,
kama kondoo kwenye malisho mapana?
17“Watu wa Efraimu4:17 Efraimu: Utawala wa kaskazini au Israeli. wamejifunga na sanamu.
Haya! Waache waendelee tu!
18Kama vile genge la walevi,
wanajitosa wenyewe katika uzinzi;
wanapendelea aibu kuliko heshima yao.
19Basi, kimbunga kitawapeperusha,
na watayaonea aibu matambiko yao kwa miungu ya uongo.


Hosea4;1-19

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe